March 07, 2018

JOSEPH BOIMANDA: MTAJI WA MILIONI HAMSINI SERIKALI HAWANA MUDA WA KUKUFUATILIA

NA.HONORIUS MPANGALA
MAISHA popote unaweza kusema hivyo kwani waliofikiria katika hoja hii walikuwa na sababu za msingi zilizokuwa na maana kiuhalisia. Wakati kipato ndio sababu hasa zilizopelekea kukawa na maneno kama haya ambayo yanasadifu uhalisia wa maisha. Katika mazungumzo yangu na mmoja ya watanzania waishio nchini Afrika kusini ilinifanya nistaajabu kile anachonieleza ambacho ndio uhalisisa wa maisha ya huko.

Ni rafiki yangu na ndugu yangu Joseph Boimanda alinifanya nistaajabu pale aliposema mtaji wa milioni hamsini za kitanzania ukiwa Afrika Kusini sio lolote kwa serikali ya huko. Maisha yamekuwa yenye uhuru na amani ya kutosha kwa raia.
Wakati nataka kuyajua haya ananieleza kuwa mamlaka ya mapato ya huko haina muda wa kufuatilia mfanyabiashara wa kati.Kama inatokea mtu anataka kulipa mapato serikalini basi ni hiari yake,hii ni kwa wale wafanyabiashara wadogo na wa kati amabao mtaji yao ni kitu kidigo kwa serikali yao. 

Moja ya kauli yake ambayo inaingia katika masikio yangu na najikuta natumia akili nyingi kutafakari  ni pale aliposema kuwa siwezi kurejea haraka huko nyumbani. Ananieleza hakuwahi kufanya shughuli akiwa hapa nyumbani na akaweza kupata pesa ya kitanzania milioni moja na akaishika.Lakini anasema kama naweza kufanya shughuli zangu huku ugenini na niweza kupata kiasi cha milioni kumi za kitanzania zangu kwanini nirudi sasa.

Ukitafakari sana hoja za Boimanda unapata uhalisia wa wale wapambanaji wa maisha ambao wanafanya hivyo wakiwa mbali na nyumbani. Watu wenye malengo katika utafutaji siku zote wawapo ugenini jicho lao linakuwa katika kulinganisha kipato anachoweza kupata sehemu moja na akakitofautisha na sehemu nyingine.

Hiki ndicho ambacho kinanipa majibu ya kwanini kijana huyu aseme sitoweza kurejea sasa. Katika utafutaji maisha kitu namba moja tunaweza kukitaja mtu ambacho anapaswa kuwa nacho ni uthubutu ten ulio wa hali ya juu.Hiki ndicho ninachoweza kukisema kipo kwa wale ambao wamechagua njia Fulani ya maisha yenye utofauti na ujamaa tuliouzoea.

Nini kinakujia kichwani kwako raia wa nchi jirani anakuambia sina mpango wa kwenda nyumbani kwetu sasa kwani hapa natafuta kwa uhuru na pesa inapatikana sana. Hakika katika mtazamo wa haraka utaweza kujivunia moyoni kuwa mwenendo wa nchi yako umekuwa na kivutio kwa wageni kwani wenyewe wanakili  juu ya yale yanayoendelea hapa.
 
Boimanda hilo ndilo analoniambia kuwa Durban maisha yamekuwa kama anaishi nyumbani Nyasa. Anafanya yale yaliyompeleka kwa amani na uhuru kubwa. Anakiri changamoto hazikosekani popote duniani katika suala la utafutaji maisha lakini kile kinachoendelea kwake kinamfanya aamue kuisafirisha hadi familia yake kwenda huko aliko.
 
Licha ya kuwepo kwake mbali lakini amekuwa akifuatilia kila jambo la huku nyumbani Tanzania.Wakati mwingine yeye ndio amekuwa mtu wa kuniuliza juu nya jambo ambalo hata mimi niliyeko nchini sijasikia. Hii inatokana na yeye kuwa msikilizaji wa radio za kitanzania kwa njia za kimtandao na pia mtazamaji mkubwa wa vituo vetu vya luninga kwa njia hiyo ya kimtandao hivyo humfanya kuwa na kila taarifa ya yale yanayoendelea hapa nyumbani.
 
Hebu katika mtazamo wa kawaida unafanya biashara ambayo mtai wake ni kamafedha za kitanzania milioni hamsini halafu mamlaka ya mapato hawana habari na wewe nini kinajengeka kichwani kwako juu ya hili. Rand 100 ni sawa na pesa yetu ya kitanzania shilingi 17000 ina maana katika mtaji wa mfanyabiashara  wa milioni hamsini za kitanzania tulizosema ambazo hata mamlaka ya mapato hawakufuatilii na kutambua kama unaliingizia taifa kipato ni sawa na rand 294117.647.
 
Sasa anakuambia kiasi hicho unaweza kukikusanya kwa muda wa miezi kuanzia tisa hadi mwaka. Ananikumbusha moja ya simulizi la mchezaji aliyekuwa na asili ya Nigeria kuwa aliapa kutorejea kwao kama hana chochote.
Aliyaeleza haya akiwa anatafuta timu ya kuchezea soka nchini Israel hivyo alisema aheli nife nikiwa natafuta kuliko kurejea Nigeria nikiwa sina chochote.
Wenye mitazamo kama hii ni wachache na huenda wakawa na haya kutokana na sababu za kifamilia au uchumi wa nchi. 

Kama mjuavyo utulivu wa mahali popote ndipo panapoweza kufanya maendeleo yakafanyika kwa kiasi kikubwa na kwa kasi pia.Itazame Rwanda ya mwaka 1994 ndio hii ya leo? Yote yaliyotokea ni kwasababu ya utulivu kwa raia ambao hutoa mwanya wa wananchi kuwa na busy na shughuli zao za kila siku.
Vitisho kwa raia na kuwapo kwa hofu ndiko kunako fanya maisha ya mwanachi mmoja kuishi kifukara kwa hofu ya matukio ya kiujambazi au hata yale yanayoweza kutokea kwasababu kisiasa.

Kutokana na dunia kuwa kama kijiji hivyo binadamu wamebadilika sana kimitazamo. Mitazamo hiyo isiweze kuwafanya watu wakashindwa kuenzi yale ambayo yalizoeleka kufanyika kwa sisi kama jamii na badala yake hufanyika kwa hofu kwasababu ya maagizo wanayopewa watu.

Pale ambapo tuliamini ndio kimbilio la wasio na kwao dhana hii imekuwa ikibadilika kutokan nay ale yanayokuwa yakitokea. Tulikumbwa na tatizo la watu wasiojulikana katika wilaya ya mkuranga lakini askari wetu walikuwa makini hadi kuhakikisha hali ile inatulizwa na kuitokomeza kabisa.

Licha ya kufanikiwa katika hilo,upande wa pili wa kimtazamo mambo yamekuwa tofauti juu ya siasa za nchi hii. Hili nalo linaweza likawa sababu ya kuwafanya watu wakaona ni heli nikafie ugenini nikiwa natafuta kuliko kuwepo nyumbani ambapo tunasema pana kila kitu ila kilichopo mioyoni mwa watu ni hofu dhidi yali ya matukio yanayoendelea kufanyika na kutokea kama kutekwa na kupotea kwa watu.

Tuna kila sababu ya kuirejeshea hali ya kujiamini na kuondokana na hofu ambayo inazunguzka katika vichwa vya watanzania wengi. Hofu hii iko ndani na hata kwa wale wanao kaa nje kwani maswali ya kujiiuliza yamekuwa mengi na yakakosa majibu.

1 comment:

  1. Cerakote Titanium - Tantric Artworks - Titanium
    Cerakote Titanium. A Tantric titanium price per ounce artworks sculpture titanium knee replacement that contains copper and platinum. The painting titanium nail is based on the Tantric and titanium trimmer is of the highest does titanium set off metal detectors quality.

    ReplyDelete

Maoni yako