November 02, 2012

AMBROCE NKWERA, KIZAZI KIPYA CHA WILAYA YA NYASA NDANI YA MAHAKAMA

Miaka mingi sana imepita wazee wetu wazaliwa wa wilaya za Mkoa wa Ruvuma wemekuwa wakifanya kazi katika sekta mbalimbali, lakini hawana muda wa kutosha kufikiria kurudi nyumbani Nyasa na kufanya kazi karibu na wakazi wao. Lakini wapo vijana wenye tofauti kiasi kikubwa na wazee kama Prof. Nkoma (TCRA), Prof Mpangala (UDSM), Jaji Samatta(Mahakama Kuu), Mataka(ATC) na wengine wengi sana ambao waliozaliwa na kukulia wilaya Nyasa. Aidha, inapendeza pia kuona mzaliwa wa wilaya ya Nyasa James Zotto, akifanya utafiti wake wa masomo ya juu(Masters) katika suala la Utatuzi wa mgogoro wa mpaka wa Ziwa Nyasa baina ya Malawi na Tanzania. Zotto ni mzaliwa wa mji wa Liuli katika wilaya ya Nyasa.
                                      
                                        AMBROCE NKWERA KAZINI MAHAKAMANI
Hata hivyo kijana AMBROCE NKWERA yeye alisukumwa na nia ya kuwatumikia watu wa wilaya ya Nyasa, lakini amejikuta akipangiwa wilaya ya Mbinga ambayo zamani ilikuwa pamoja na Nyasa. Kwa hakika sio hatua mbaya, bali lengo lake liliongozwa na kuwatumikia watu wa ukanda wa Mkoa wa Ruvuma hususani wilaya za Songea, Tunduru, Mbinga na Nyasa au Ludewa(Iringa).
Baada ya serikali kutangaza nafasi za kazi ya Uhakimu kwa wilaya kadhaa za Nyasa, ndipo kijana huyu akachukua uamuzi wa kuomba nafasi hiyo. Na hadi sasa anaitumikia jamii ya Tanzania hususani wilaya ya Mbinga hivyo kukamilisha ujenzi wa Taifa. Labda swali hapa ni kwanini aliamua 'KURUDI NYUMBANI' ambayo ni sera yetu nami nikiwa mfuasi wake?
Sababu kubwa ni kwamba kuna wafanyakazi waliowahi kuajiriwa na kupangiwa wilaya ya Mbinga ama maeneo ya Wilaya za mkoa Ruvuma halafu hawaendi kufanya kazi vituo vya kazi. Hii ilikuwa ikimkera na kuona kuna haja wazaliwa wa maeneo hayo wenye sifa kuomba kazi ili warejee na kuwatumikia watu wa nyumbani kwao. 

                                          
                                                     AKITOKA KAZINI
Lengo hilo lilifanikiwa baada ya Mahakama kuu kumwajiri AMBROCE NKWERA na kumwapisha huko wilayani Lushoto mkoa wa Tanga. Kwa sasa yeye anatumikia taifa kupitia wilaya ya Mbinga ambayo ni jirani na nyumbani kwao wilaya ya Nyasa.  Yeye ni miongoni mwa walioshauri kuanzishwa mahakama maalumu ya kuwahukumu watu wote wanaoshtakiwa kwa kosa la Ufisadi ambayo anasema sawa na wahujumu uchumi (tutachapisha mahojiano yake siku zijazo).
Kwa hakika anastahili sifa na kupongezwa sababu uamuzi wake licha ya shahada yake ya sheria, akaona kuna haja ya kwenda kufanya kazi maeneo ambayo wengi hawataki kufanya kazi, maana huwa wanaripoti na kuondoka moja kwa moja, hawarudi tena. 
AKIFURAHIA MANDHARI YA MBINGA
Sasa, roho yake imetulia atakuwa HAKIMU mzuri sana, mikono yake itatenda haki na sera yake ya kushawishi wasomi ambao ni wazaliwa wa Wilaya ya Nyasa au Mbinga na nyingine za mkoa wa Ruvuma kwamba ni vyema wakarudi nyumbani kuwatumikia wananchi wao kuliko kulalamikia wageni wanaotoka mikoa mingine kutopendelea kufanya kazi maeneo ya mkoa huo. Mabadiliko na maendeleo yatawafikia watu kwa watu kufanya jitihada za kufanya kazi kwa bidii. Hongera sana Mgosi wa Ndimba AMBROCE NKWERA.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako