November 04, 2017

KITABU CHENYE UTATA KUHUSU RAIS ZUMA CHAPIGWA MARUFUKU



PRETORIA, AFRIKA KUSINI

MAJASUSI wa Afrikia Kusini wanataka kufutiliwa mbali kwa kitabu kipya chenye utata kuhusu madaia yua rais Zuma kujilimbikizia fedha kimakosa ,wakisema kuwa kitabu hicho kimajaa makjosa na kinakiuka sheria ya ujasusi.

Shirika hilo la Ujasusi limetishia kwenda mahakamani iwapo wachapishaji wa kitabu hicho NP watakataa kukifutilia mbali kitabu hicho kwa Jina “The Presidency Keepers: Those Keeping Zuma in Power and Out of Prison''-Wale wanaomueka Zuma mamlakani na kutokwenda jela, kilichotungwa na mwandishi aliyeshinda tuzo la uandishi wa uchunguzi Jacques Pauw.

Kitabu hicho kinadai kwamba Rais Zuma kwa muda wa miezi minne alipokea mshahara kutoka kwa mfanyibiashara mmoja mbali na mshahara anaolipwa na serikali na kwamba hakuutangaza mshahara huo kwa watoza ushuru wa taifa hilo.

Baada ya nakala za kitabu hicho kuchapishwa siku ya Jumapili katika gazeti moja, msemaji wa bwana Zuma alitoa taarifa ,akikana makosa yoyote dhidi ya rais Zuma akidai kwamba alikuwa mwathiriwa wa kampeni mbaya ya kumchafulia jina.

"Maswala ya ulipaji wa kodi ya rais hayana makosa '',ilisema taarifa hiyo.
Nakala za kitabu hicho zinauzwa kwa kasi huku raia wakijaribu kukinunua kabla ya kuisha katika soko.

©BBCSWAHILI

No comments:

Post a Comment

Maoni yako