November 15, 2017

MFAHAMU NDEGE ANAYEJENGA NYUMBA NA KUPANGISHA

NA MWANDISHI WETU

KAMA ulidhani ni binadamu pekee anajenga nyumba na kupangisha utakuwa unajidanganya kwa kuwa mwambao mwa ziwa Nyasa katika Kijiji cha Mtupale kata ya Chiwanda,kuna aina ya ndege anayeitwa Fundichuma (Hamerkop) ambaye anajenga nyumba na kupangisha kwa ndege na viumbe wengine kama mijusi.
Afisa Maliasili na Utalii wa Mkoa wa Ruvuma Afrikanus Challe ambaye pia ni mzaliwa wa mwambao mwa ziwa Nyasa anasema ndege huyo anapenda kuishi jirani na ziwa au mto kwa sababu chakula chake kikuu ni samaki.


Challe anabainisha kuwa Fundi chuma ni ndege wenye uwezo wa kujenga nyumba kubwa yenye vyumba vingi juu ya mti na kwamba ndege hao jike na dume wanapendana sana na kwamba huwa hawaachani hadi mmoja anapokufa.

Kwa mujibu wa Challe,ndege hao wanajenga nyumba kubwa na kukaribisha ndege wengine na viumbe wengine ambao hupenda kuishi katika nyumba hizo kutokana na ulinzi wa ndege hao.

Hata hivyo Challe anasema kwa utamaduni wa makabila ya watu wa mwambao mwa ziwa Nyasa ndege huyo wanamheshimu sana kutokana na ustarabu wake hivyo wanalinda makazi yake ili yasiharibiwe na kwamba wanyasa wanaamini ukimua ndege huyo utapata laana.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako