January 28, 2018

UTAFITI: SIGARA MOJA HUSABABISHA UGONJWA WA MOYO NA KIHARUSI

WATU watu wanaovuta Sigara angalau moja kwa siku wapo kwenye hatari ya kupata magonjwa ya moyo kwa asilimia 50, huku wengine wakiwa na uwezekano wa kupata ugonjwa wa Kiharusi kwa asilimia 30 kuliko wale wasiovuta kabisa.
 
Kwa mujibu wa utafiti huo uliofanywa na Taasisi ya Saratani ya Chuo Kikuu cha London, umeonyesha kuwa hakuna kiwango cha usalama kati ya uvutaji wa sigara na kupata magonjwa tajwa. lakini umeeleza kuwa mtu anayeachana na uvutaji wa sigara hayupo katika hatari ya kupata ugonjwa wa moyo au Kiharusi.
Wamesema, asilimia 48 ya vijana wanaovuta sigara wanakabiliwa na magonjwa ya kuganda damu, kuharibu mapafu, pamoja na matatizo ya mishipa mwilini.  Magonjwa hayo yanayotokana na uvutaji wa sigara ni hatari kwa afya ya mtu yeyote kwani husababisha hata kifo.


Utafiti huo umeongeza kuwa asilimia kubwa ya watu wazima nchini Uingereza wanaovuta sigara imepungua, lakini idadi ya watu wanaovuta sigara moja hadi tano kwa siku imeongezeka.

Uchambuzi wa utafiti wa taasisi hiyo uliochapishwa baada ya kuwachunguza watu 141, unaonyesha tabia ya uvutaji wa sigara kwa siku 20 inasababisha watu saba kuugua ugonjwa wa moyo au kiharusi katika kundi la watu 100 wenye umri wa kati. Lakini iwapo wataachana na uvutaji wa sigara kwa siku moja unaweza kusababisha watu watatu pekee kuugua magonjwa hayo. 

Watafiti wamesema wanaume wanaovuta sigara moja kwa siku wana uwezekano wa asilimia 48 kutengeneza dalili za ugonjwa wa moyo na asilimia 25 ya ugonjwa wa kiharusi. Kwa upande wana wanawake, watafiti wamesema ni asilimia 57 ya wanaovuta sigara wapo kwenye hatari ya kuugua ugonjwa wa moyo na asilimia 8=31 wataugua ugonjwa wa kiharusi.   

Profesa Allan Hackshaw wa Taasisi ya Saratani ya Chuo Kikuu cha London ambaye aliongoza timu ya utafiti, aliliambia Shirika la habari la BBC, “Utafiti unaonyesha zipo nchi chache zenye kupunguza kiwango kikubwa cha uvutaji wa sigara, hilo ni jambo zuri, ambalo linaweza kuzuia magonjwa kama Saratani. Lakini upo uwezekano mkubwa wa kupata magonjwa hayo mawili (Moyo na kiharusi) kuliko saratani. Wanapaswa kuacha uvutaji wa sigara,”

Watafiti hao wamesema kuwa wana matarajio makubwa kuona idadi ya wavutaji wa sigara ikipungua ili kuepusha magonjwa, kwani pia hata takwimu zao zinaonyesha kuwa ugonjwa saratani ya mapafu unachangiwa na uvutaji wa sigara. 

Hata hivyo wamebaini kuwa wanaume wanaovuta sigara moja kwa siku wapo katika hatari ya kupata ugonjwa wa moyo kwa asilimia 46 na asilimia 41 ya ugonjwa wa kiharusi kwa wavutaji wa sigara 20 kwa siku. 

Ni asilimia 31 ya wanawake wanaovuta sigara moja kwa siku wapo katika hatari ya kupata ugonjwa wa moyo na asilimia 34 ugonjwa wa kiharusi. 
Profesa Hackshaw amesema hatari ya magonjwa hayo inatokana na muda mrefu wa kuishi, lakini upo uwezekano wa kuyapata iwapo mtu atavuta sigara kwa miaka michache tu. 

Amesema habari njema ni kwamba wote wanaoacha kuvuta sigara wana uwezekano wa kupunguza hatari ya kupata magonjwa nyemelezi.

CHANZO; TOVUTI YA BBC. IMETAFSIRIWA NA MARKUS MPANGALA

No comments:

Post a Comment

Maoni yako