February 14, 2018

AFCON 2019: TUSIJISAHAU MWAKANI SIYO MBALI.

NA SAMWEL CHITANYA.
 
MWAKA 2017 utabaki kuwa mwaka unaokumbukwa na Watanzania wapenda soka. Mwaka huo ni mwaka ambao timu yetu ya vijana Serengeti Boys ilishiriki kwa Mara ya kwanza mashindano ya vijana kwa Afrika tangu Tanzania iwepo. Ushiriki huo ulikuja baada ya miaka 37 tangu Tanzania iliposhiriki kwa Mara ya kwanza fainali za kombe la Mataifa ya Afrika maarufu kama AFCON mnamo mwaka 1980.
Kikosi cha Serengeti Boys
Ilkuwa ni Furaha kubwa sana kuwaona vijana wa Serengeti Boys wakiwa wanashindana na timu kama Mali,Niger, Congo na timu nyinginezo zilizoshiriki mashinano Yale. Ingawa hatukufanya vema sana lakini angalau nasi tulionekana kama tunaweza. Nani alikuwa hafurahii kumuona Ramadhan Kabwili akiwa langoni na wenzie kama akina Ally Nganzi, Nasho Naftari, Nickson kibabage, Abdi Suleiman, Said musa, Yohana Nkomola kwa kuwataja wachache. 

Hakika ilikuwa ni furaha na Faraja kubwa kwa soka la Tanzania. Tukiacha ujanja ujanja na kuamua kusimia soka kwa uhakika tunaweza fika tunakohitaji.
Mwaka 2019 Tanzania itakuwa mwenyeji Wa michuano ya mataifa ya Afrika kwa vijana walio na umri chini ya miaka 17. Tuliomba kuwa wenyeji Wa michuano hiyo maika miwili iliyopita. Ni jambo la kujivunia kuona mashindano makubwa ya vijana kama hayo yakifanyika katika ardhi yetu. Hii inaweza kuwa njia ya kuelekea kuomba kuandaa mashindano ya wakubwa maarufu kama AFCON. 

Bila shaka tunaweza kuandaa AFCON miaka kadhaa ijayo maana kama tunashindwa kushiriki fainali hizo kwa njia ya kawaida, kundaa ndio njia pekee itakayo tuwezesha kushiriki mashindano hayo. 

Tunaenda kuwa wenyeji Wa michuano ya vijana hapo mwakani lakina bado Nina hofu na ushiriki wetu katika michuano hiyo. Hofu yangu haiko katika viwanja vitakavyo tumika la hasha!! Kama viwanja tunavyo, tuna uwanja wa taifa, uwanja Wa Uhuru, uwanja Wa Gombani kule Pemba, uwanja Wa Amani unguja, Uwanja Wa Azam complex na Uwanja Wa Kaitaba pia. Hofu yangu iko katika ushiriki wetu uwanjani maana pale ndio sehemu pekee inayoonesha namna gani tumejiandaa. 

Soka ni mchezo unaochezwa hadharani na kila Mwenye uwezo Wa kuona anaona. Soka siyo bao au karaka usema utajificha mahali Fulani ucheze hapana. Hadi wakati huu sijasikia chochote kuhusu mashindano hayo nikiwa na maana ya maandalizi yetu kama wenyeji, kuanzia kwa Shirikisho la soka FFF, Serikali na wadau Wa soka kwa ujumla wake. Wote wako kimya. 

Sijasikia timu yetu ikicheza mechi za majaribio kujiandaa na mashindano hayo, au bado mapema??. Soka linahitaji maandalizi ya muda mrefu kama tunahitaji kushindana katika michuano hiyo basi tulikuwa hatuna budi kuanza maandalizi mapema Mara tu baada ya kupewa taarifa rasmi kama tumekubaliwa kuwa wenyeji wa michuano hiyo. 

Inawezekana Mimi ndio Niko nyuma pengine timu imekwisha andaliwa na iko kwenye mazoezi ya kujianda kwa michuano hiyo hapo mwakani sijui.  Kama tunania ya kushiriki hakuna shida tunaweza endelea na taratibu Nyingine. Maana kushiriki na kushindana ni mambo mawili tofauti. Lakini tukumbuke hakuna njia ya mkato kwenye kandanda, usipojiandaa vema utaumbuka tu. 

Tunatakiwa kujiandaa kushindana na siyo kushiriki, vinginevyo tunatolewa mapema na kuwaacha wageni wakichuana kwenye ardhi yetu jambo ambalo ni aibu kubwa, kwa muandaaji Wa mshindano kundolewa mapema. Rai yangu kwa Serikali na shirikisho la soka TFF tutumie muda huu uliobaki kuindaa timu yetu. 

Tusitegemee muujiza kama tutakuwa na maandalizi ya zima moto. Soka linahitaji maandalizi ya muda mrefu siyo kama muziki usema utaandika mashairi Leo, kesho ukarekodi,keshokutwa wimbo utoke na watu waanze kuuimba la hasha!!! 

Soka haliko hivyo.  Uchaguzi ulishamalizika, sasa ni wakati kusimamia soka letu ili kusogea mbele.  Mheshimiwa Rais wa TFF kama kuna jambo ambalo litakufanya usisahaulike miongoni mwa Watanzania wapenda kandanda basi ni Ushiriki mzuri Wa timu yetu ya Serengeti boys katika michuano ya Afrika hapo mwakani. 

Uongozi Wa Leodgar Tenga unakumbukwa na wapenda soka wote hapa nchini pamoja na kuifanya TFF kuwa taasisi inayoaminika na kujenga misingi bora ya utawala kuna jambo la ziada linalofanya uongozi ule uendelee kukumbukwa nalo ni ushiriki Wa timu yetu ya taifa katika michuano ya CHAN iliyofanyika mwa Mara ya kwanza mwaka 2009 pale Ivory cost. 

Uongozi Wa Tenga ulifanikisha hilo kwa kushirikiana na Serikali na wadau Wa soka na kuifanya Tanzania kuwa nchi iliyokuwa inaogopeka kwenye kandanda Afrika mashariki na kati yote na hata Afrika kwa ujumla. 

Hata mtangulizi wako bwana Jamal Malinzi pamoja na mapungufu yalijojitokeza kwenye uingozi wake, alijitahidi kuiweka Tanzania kwenye ramani ya soka kwa kufanikisha kuifikisha Serengeti boys kwenye fainali za mataifa ya Afrika kwa vijana wenye Wa umri chini ya miaka 17 naye anaheshima zake. Kipindi cha uongozi wake ndipo tulifanikiwa kupata uwenyeji Wa michuano hii hapo mwakani anastahili pongezi. 

Rais Wa TFF na kamati yako ya utendaji huu ni wakati wenu kuipaisha Tanzania kwenye kandanda kupitia michuano hii itakayo fanyika mwakani ambayo sisi ni wenyeji. 

Ushiriki mzuri wa Serengeti boys unaweza kuwa ni kampeni tosha katika uchaguzi ujao Wa TFF. Tujiandae kushindana na ikiwezekana kulibakisha kombe nyumbani kwa Mara ya kwanza tangu kuumbwa kwa dunia. Itawezeka endapo tu tutakuwa na maandalizi mazuri na kuwepo kwa ushirikiano baina ya TFF, Serikali na wadau Wa soka kwa ujumla. 

Watanzania wanapenda sana kandanda, pamoja ma madhaifu yote yanayojitokeza kwenye uendeshaji Wa mpira wetu lakini bado hawachoki kwenda viwanjani kuzitazama timu zao. Nawakumbusha TFF, Serikali na wadau Wa soka wote kuwa mwakani Tanzania itakuwa mwenyeji Wa fainali za kombe la mataifa ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17. Tuna miezi 12 tu ya kujiandaa. Wahenga walisema" Kiuangukacho majivuni hakiishi kupulizwa.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako