March 26, 2018

AFISA MTENDAJI MPYA WA KIJIJI CHA LUNDU

Mara baada ya kustaafu kazi ya utendaji wa kijiji, bwana Remigius Nyenyembe maarufu kama Remmy au Fish, Kijiji chetu cha Lundu hakikupata mtendaji kwa muda mrefu ikasababisha Afisa Maendeleo wa Kata kukaimu nafasi hiyo.
 
Sasa kijiji chetu cha Lundu kimepata Afisa Mtendaji ambaye amewasili kijijini kwetu hapa tayari kuanza kazi. Ni mwenyeji wa Arusha, kwa jinsia ni mwanamke. Tunawaomba wanakijiji wenzetu wa Lundu wampokee na kumkaribisha ajione kama yuko Njiro,Philips,Ngarenaro,Ngaramtoni,Usa river, Sinoni daraja mbili yaani namaanisha Arusha.
KIJIJI CHA LUNDU
Kwa wakazi wa kijiji chetu kama watamtumia vizuri basi atasaidia kuleta maendeleo kwenye kijiji chetu kwasababu hawa wataalamu siku hizi wana viwango vizuri vya elimu na wamesomea masuala ya Maendeleo ya Jamii katika vyuo vinavyotambuliwa na serikali kama vile Homboro na vyuo vikuu vingine.

Tumtumie vyema mtendaji wetu kwa manufaa ya kijiji chetu cha Lundu kupata maendeleo. Itapendeza sana kama suala la kulewa asubuhi litapatiwa ufumbuzi maana wanywaji wamezidi.

©Honorius Mpangala

No comments:

Post a Comment

Maoni yako