March 01, 2018

NGOMA ZETU

MIAKA mingi enzi za babu zetu kulikuwa na ngoma maarufu iliyoitwa GEUZA. Hakukuwa na Ligambusa kama ilivyo sasa walisafiri kutoka Lundu kwenda Mbaha au Hinga kucheza Geuza usiku nyakati za Mbalamwezi na wakarudi nyumbani.
 
Kwa upande wa Ngoma ya Mganda, Maboma yaliyoka hadi sasa ni Mawili na yenye upinzani wa Kama vilabu vya soka. LICHUMA LINDU na LIHEGHELYA KONI majina hayo ni kama yanajibizana .Ni ngumu kuona mshiriki wa boma moja kwenda boma lingine nyakati za mazoezi utafukuzwa na kuonekana kama umeenda kuiba stepu(mtindo Wa uchezaji).

Kihoda ndo kimetia fola nyakati za nyuma Lundu ilikuwa na maboma mawili tu yaani Maji na Uamuzi. Lakini kutokana na ongezeko la watu kikafanya kuonekana wanawake wako wengi na wote wanataka kuonyesha uwezo wao wa kusakata ngoma. 

Ndipo maboma mengine yakazaliwa. Boma Maji limafanikiwa kuzaa boma linaloitwa Upendo ambao wao wanchezea pale nyumbani kwa Mzee Matamelu. Huku wenyewe Maji wakiwa pale nyumbani kwa Mzee Nduru Cosmas au kwa Lipambeka (maeneo ya Kunkwachu).

Pia kuna boma ambalo limezaliwa kwa kuwamega wachezaji toka Maji na Uamuzi ambalo linaitwa Kisiwani ambalo wanachezea kwa Mzee Lendela. Lilianzishwa mwakajana na wakaita kihoda. Linajumuisha watu wote Wa mlimanani na kitongoji cha maliwa..

Boma uamuzi amemzaa boma Amani lililopo Kitongoji cha Likwambe na wengine walipunda boma la kisiwani. Hivyo maboma ya kihoda yapo 5 hadi sasa.

Ligambusa na kindeku zinakuwa bado ngoma za kwenye sherehe kama ilivyokawaida yake. Ila wameongeza matumizi ya ligambusa hadi katika mkesha Wa mwaka mpya lazima lipigwe ili watu waburudike.

©HONORIUS MPANGALA

No comments:

Post a Comment

Maoni yako