NA
MAUNDU MWINGIZI
LEO nimekumbuka moja kati ya matukio yaliyopata kuniumiza sana hapo zamani. Nakumbuka nilikuwa darasa la sita, Shule ya Mazoezi Mwenge, mkoani Tabora.
LEO nimekumbuka moja kati ya matukio yaliyopata kuniumiza sana hapo zamani. Nakumbuka nilikuwa darasa la sita, Shule ya Mazoezi Mwenge, mkoani Tabora.
Siku
hiyo, nikiwa nimeketi dawati la mbele kabisa darasani, lilizuka kama zogo
maeneo ya katikati ya darasa; wanafunzi wakawa wamesimama; wengine wakicheka,
wengine wakionekana kufadhaika. Kusogea eneo la tukio, nikamwona binti mmoja
(jina ninalihifadhi) akiwa ameketi juu ya dawati ilhali wenziye wakiwa wima
wamemzunguka.
Nikiwa
sijatanabahi juu ya kilichotokea, baadhi ya wasichana wakamwinua mwenzao, kisha
wakamfunga sweta kiunoni ili limsitiri sehemu ya nyuma. Aliposimama, ndipo
nikaona kilichotokea. Damu ilienea kwenye sketi yake huku nyingine ikibaki
kwenye dawati. Wenziye kadhaa wakaungana naye kumsindikiza nje ili kumpa nguvu.
Lakini mambo ya kitoto, bila kujua hofu na fadhaa vilivyomuathiri kisaikolojia
mwenzetu, baadhi (hususan wavulana) wakawa wakishangilia na kumcheka.

