Showing posts with label Huduma. Show all posts
Showing posts with label Huduma. Show all posts

February 14, 2018

TAULO ZA KIKE

NA MAUNDU MWINGIZI
LEO nimekumbuka moja kati ya matukio yaliyopata kuniumiza sana hapo zamani. Nakumbuka nilikuwa darasa la sita, Shule ya Mazoezi Mwenge, mkoani Tabora.

Siku hiyo, nikiwa nimeketi dawati la mbele kabisa darasani, lilizuka kama zogo maeneo ya katikati ya darasa; wanafunzi wakawa wamesimama; wengine wakicheka, wengine wakionekana kufadhaika. Kusogea eneo la tukio, nikamwona binti mmoja (jina ninalihifadhi) akiwa ameketi juu ya dawati ilhali wenziye wakiwa wima wamemzunguka.


Nikiwa sijatanabahi juu ya kilichotokea, baadhi ya wasichana wakamwinua mwenzao, kisha wakamfunga sweta kiunoni ili limsitiri sehemu ya nyuma. Aliposimama, ndipo nikaona kilichotokea. Damu ilienea kwenye sketi yake huku nyingine ikibaki kwenye dawati. Wenziye kadhaa wakaungana naye kumsindikiza nje ili kumpa nguvu. Lakini mambo ya kitoto, bila kujua hofu na fadhaa vilivyomuathiri kisaikolojia mwenzetu, baadhi (hususan wavulana) wakawa wakishangilia na kumcheka.

September 18, 2017

WAKIMBIZI WA BURUNDI WAREJEA KWAO


Maofisa wa uhamiaji wa Burundi wakiwapokea wakimbizi wa nchi hiyo waliokuwa wakiishi Tanzania.


 PICHA; Honorius Mpangala

June 27, 2014

RADIO CONSULT LIMITED



RADIO CONSULT LTD

Ni kampuni inayotoa huduma za ushauri wa kitalaamu kwa masuala ya radio. Moja ya huduma tunazotoa ni kama ifuatvyo:-
Tunatoa huduma zifuatazo:-
1. Wanaotaka kuanzisha kituo cha radio, tunatoa huduma zote ikiwemo kuandika maandiko ya uombaji wa leseni TCRA.
2. Tunauza vifaa vya radio kwa order (Transmitter, mixer, microphones, Hybrid Telephones, antenna, STL n.k)
3. Tunadesign studio za mazoezi kwenye vyuo vya unadishi wa habari kwa bei nafuu. 4. Kuandaa ratiba za vipindi vya radio (scheduling&Planning)
5. Media Research
6. Kuandika maandiko (Business Plan, Strategic Plan, Editorial Policy, Feasibility Study n.k)
7. Tunatoa mafunzo mbalimbali (Uandaaji wa vipindi, Management, Marketing, ICT for radio, Internet Radio, Journalism n.k)
8. Tunachuo cha media pia www.dmctanzania.org. Kwa huduma zaidi fika ofisini kwetu Nanenane Mbeya, jengo la Chai (RSTGA) au tupigie simu namba 0768188429 au 0759307280 au tuandikie email: consultancy@radiotz.com zaidi tembelea www.radiotz.com Facebook: www.facebook.com/radiotz