nimeikuta hii picha katika kompyuta hapa ninapoandika hili jambo, kwahiyo ili kushirikiana na wenzangu naona ni vema nami nikaiwasilisha kwenu wadau. suala lenyewe ni RICHMOND ile kampuni iliyosababisha kutetereka kwa serikali yetu. sina mengi ila jionee mwenyewe, nani yuko katikati nani yupo kulia na mengineyo. imetengenezwa na jamaa wa Mzumbe chuo kikuu kama alivyoandika hapo juu. kazi kwenu
Showing posts with label ushenzi. Show all posts
Showing posts with label ushenzi. Show all posts
April 26, 2009
Mjumbe hauawi jamani, nami nimeyakuta
nimeikuta hii picha katika kompyuta hapa ninapoandika hili jambo, kwahiyo ili kushirikiana na wenzangu naona ni vema nami nikaiwasilisha kwenu wadau. suala lenyewe ni RICHMOND ile kampuni iliyosababisha kutetereka kwa serikali yetu. sina mengi ila jionee mwenyewe, nani yuko katikati nani yupo kulia na mengineyo. imetengenezwa na jamaa wa Mzumbe chuo kikuu kama alivyoandika hapo juu. kazi kwenu
Madhumuni
habari,
kumbukumbu,
siasa.,
ushenzi
February 20, 2009
Kikwete acha kupiga Mayowe

Nimetulia wala sijaandika maoni yangu kuhusu ujio wa Hu Jintao wa China. Nimtumiwa sms nyingi na waraka pepe kwamba ninaonaje ujio huo na kauli zako kuhusu Mkapa. Wengi wanadhani nimebadilika kimtazamo kwani kuna mambo siyajadili,sipendekezi au kuongoza njia.BADO NIPO SANA!
Wapo wanaolalamika kwamba nimeacha kujadili mada zangu za kuhusu bara la afrika, wanadai ninapwaya katika mada za nyumbani bongo. Lakini nasema kuna mambo yanaingiliana, kwasasa nakula darasa kali sana kuhusu mashariki ya kati na yanayowahusu, pia na shughuli zangu za maisha.
Sasa ninaandika hapa kama mwanzo tu kwani natarajia kuandika wazi zaidi. Sikubaliani na mtazamo au porojo za Rais Kikwete kwamba uwanja taifa ni juhudi za Mkapa na uzuri wake. Mimi nasema ni juhudi za watanzania, kwani hakubuni bali aliahidi kwasababu ni wajibu wake kuteda hivyo.
Sasa basi kutwambia kwamba hayo ni mazuri yake ni kutulazimika kunya mavi jamvini huku msosi upo tayari kwa kuliwa. Sikubali kwamba mambo machafu ayaliyoyatenda eti yamekuwa mazuri na kupakwa rangi au marumaru. Kwanza nitakumbusha BOT ujenzi wake.
Bodi ya wahandisi nakumbuka ilifanya tathmini na kusema kwamba ni bilioni 56 zingtosha kujenga BOT tena bila msaada wa nchi yeyote, lakini uwongo ukatungwa halafu tukaambiwa BOT imejengwa kwa milioni 700 huku mjenzi wake alitaka milioni 70. Je nini kilichofanywa hadi ikapandishwa bei kiasi hicho? Au unadhani uzuri wa mtu husemwa tu kama ufanywavyo wewe?
Huo uwanja wa soka nani amekwambia Watanzania hawajui uzuri wa mtu? Watakula uwanja na kunya uwanja? Ingawa kwa wapenda soka tunafurahi, lakini nguvu ya kushangilia tutoe wapi? Ni kweli kulikuwa na umuhimu wa kumpamba tena Benjamini? kwa sababu naamini ni jukumu lake na tulimtuma kufanya kazi kwa ajili yetu full stop! Sasa unapopiga mayowe eti jamaniiii mkapaaaa alijenga uwanja huuuuuuuu.
Nini thamani ya mgodi wa Kiwira ambao ulikuwa na Milioni 700 halafu wakijiuzia na Yona Milioni 70? Au unadhani kila mtu kipofu, haoni anakubali kuchekewa na kulishwa porojo kama zile ulizozitoa uwanja wa taifa. Unafikiri wenye kiona mbali tunajali kwamba eti Hu Jintao alikuja kuzindua uwanja? thubutu labda wajinga wajinga watachekelea mpaka kupasuka misamba ya midomo halafu wasijipe muda wa kufanya tafakuri.
Kwani nani hajui mashtaka mengi yaliyopo ni porojo na ngebe za uchaguzi? Unafikiri tunafundishwa uzuri wa mtu kwa hotuba au matamko? Sikiliza wahenga walisema 'mtoto acha kupiga mayowe, acha watu waone wenyewe'
'usiseme sana kwani tusiposema hatumaanishi hatuna ila tunakutazama tu ili tujue umahiri wako wa kuchanganua hoja.
Amka, hujasikia kama ni kizazi cha dhahabu cha Nyerere kinakuja, hujui. Zubaa uchekwe. Nitajadili zaidi nje ya blogu.
February 03, 2009
wale wasomi wetu vipi,inapendeza eeehee!!!
Vipi waungwana mwadhani nimepotea kilingeni kwangu? Duh1 nipo nipo sana, yaani nipo nipo kama vile ujuavyo nipo1 Lakini sijui unaonaje hii kitu, au nisme unaonaje haya maudhui ya picha. Haya weeeeee!!!
Madhumuni
falsafa,
kumbukumbu,
maisha,
siasa,
ushenzi
December 24, 2008
waambie ROHO yangu nzuri, AMA ZANGU AMA ZAO
nashangaa wananichukia bila sababu, sijawatendea madhambi lakini wananitumia ujumbe wa simu wataniua, eeeh ongezeni juhudi sitoacha kundika kile ninacho amini tena mimi mfuasi wa MALCOM X, kwangu Martin Luther King jr siyo shujaa! naamini hivyo licha ya kukubali umahiri wake, napenda ukali wa X kwani unaonyesha msimamo siyo kupewa sifa za upole na ustaarabu, waambie ROHO ni nzuri kuliko picha. Sijawatendea madhambi nashangaa wana chuki, wanataka kunihukumu, wamefanya kikao cha kumaliza roho yangu, nasema niueni anza hata sasa mimi sitishwi kwa ujumbe mfupi wa maneno ya simu eti sitowezi kuzuia kifo, eti wataniua kwsababu zao sijui nilichowakosea lakini SITISHWI na mtu yeyote wambie AMA ZANGU AMA ZAO hiki ni kima changu ama chao iwe mtaani maskani au mahali popote pale, kwani dunia nzuri kama picha hii hutoa taswira upendo na nafasi zetu. Waambie upendo wangu haupo kwa maadui, ndiyo kwani naogopa KUFA labda sijazaliwa waambie tena na tena ukiona uzuri na upole wa picha hii utadhani hakuna SHARI. Anzeni basi, kwani HATARI KITU GANI?
December 01, 2008
mauzo ya kondomu
Mara nyingi napenda habari mpya zenye vituko ambavyo vinanipa kazi ya kutafakari lakini sipendi vituko au habari za kunichosha ingawa sichoki mwili akili inagota.
SASA: Mauzo ya Kondomu huko Korea yamepnda sana tokana na watu hususani vijana wadogo kujihusisha na utamu wa ngoma ya kikubwa NGONO. Mauzo hayo ni kwa mujibuwa Dk Janet Hyde aliyefanya utafiti katika jamii za watu wa Korea toka chuo kikuu cha Wiscons. Anasema wingi wa Runinga, pamoja na mhusiano mabaya ya wazazi majumbani ni mambo ambayo yanaaminika kuchochea vitendo vya ngono kwa vijana wa umri mdogo.
Wengi wanaangalia vipindi ambavyo vinaashiria au kupandisha mzuka kama siyo midadi ya ngono na hawavai kondomu. Lakini hivi karibuni utafiti unaonyesha kondomu inanunuliwa sana tu ili kujiburudisha na majambozi ya kiutamu utamu!!!! Vijan wengi ni wale wadogo wenye umri wa miaka 13 na 15 ambao anadai wameshafanya ngono kama siyo kufaidi utamu huo katika umri mdogo. Mauzo yameongezeka sana kipindi hiki kuliko ilivyokuwa awali:Na maadili yamekuwa mabaya sana siku hzi huko KOREA
HIVI ndivyo vituko, lakini nafikiri unaweza kuwaza jambo. JE JAMII ZA KITANZANIA ZIPO VIPI? VIPI WALE WAPUMBAVU WANAODAI UTANDAWAZI huku hawana lolote katika utandawazi wenyewe? Je utandawazi hauna maadili? PAMOJA DAIMA!!!!!!
SASA: Mauzo ya Kondomu huko Korea yamepnda sana tokana na watu hususani vijana wadogo kujihusisha na utamu wa ngoma ya kikubwa NGONO. Mauzo hayo ni kwa mujibuwa Dk Janet Hyde aliyefanya utafiti katika jamii za watu wa Korea toka chuo kikuu cha Wiscons. Anasema wingi wa Runinga, pamoja na mhusiano mabaya ya wazazi majumbani ni mambo ambayo yanaaminika kuchochea vitendo vya ngono kwa vijana wa umri mdogo.
Wengi wanaangalia vipindi ambavyo vinaashiria au kupandisha mzuka kama siyo midadi ya ngono na hawavai kondomu. Lakini hivi karibuni utafiti unaonyesha kondomu inanunuliwa sana tu ili kujiburudisha na majambozi ya kiutamu utamu!!!! Vijan wengi ni wale wadogo wenye umri wa miaka 13 na 15 ambao anadai wameshafanya ngono kama siyo kufaidi utamu huo katika umri mdogo. Mauzo yameongezeka sana kipindi hiki kuliko ilivyokuwa awali:Na maadili yamekuwa mabaya sana siku hzi huko KOREA
HIVI ndivyo vituko, lakini nafikiri unaweza kuwaza jambo. JE JAMII ZA KITANZANIA ZIPO VIPI? VIPI WALE WAPUMBAVU WANAODAI UTANDAWAZI huku hawana lolote katika utandawazi wenyewe? Je utandawazi hauna maadili? PAMOJA DAIMA!!!!!!
November 26, 2008
BREAKING NEWS: inaendelea.......
Kila mtu amesikia kuhusu mashtaka ya mawaziri wa zamani wa serikali ya Mkapa, bwana Dani Yona na Basil Mramba. haya ndiyo mashtaka dhidi yao.
BASIL MRAMBA
( alikuwa waziri wa fedha katika utawala wa Rais Benyamini Mkapa)
ANASHTAKIWA KWA MAKOSA YAFUATAYO:
1.KUISABABISHIA SERIKALI HASARA.
2.KUDHARAU MAPENDEKEZO YA TRA(mamlaka ya mapato)KUTOTOA MSAMAHA WA KODI
KWA KAMPUNI YA MS/STEWART YA UINGEREZA OKTOBA 10 2003 ALITOA NOTISI YA SERIKLI YENTE NAMBA 423 MWAKA 2003.
3.OKTOBA 15 2004 ALITOA NOTISI NAMBA 424 DESEMBA 19 2003 YA MSAMAHA WA KODI KWA KAMPUNI HIYO.
4ANATUHUMIWA KUTOA NOTISI YA SERIKALI NAMBA 497 MWAKA 2004 OKTOBA 15 ILI KUOTOA MSAMAHA WA KDI KWA M/S ALEX STEWART KINYUME NA MAPENDEKEZO YA TRA.
5.NOVEMBA 15 2005 AKIWA MWAJIRIWA WA SERIKALI ANATUHUMIWA KUTOA NOTISI YA SERIKALI NAMBA 377 YA 2005 KURUHUSU MSAMAHA WA KODI KWA KAMPUNI YA STEWART.
6.ANASHTAKIWA KWA KURUHUSU KUSHINDWA MAJUKUMU YAKE NA KUSABABISHA HASARA KWA SERIKALI SHILINGI 11,752,350,148.
7.ANATUHUMIWA KUTOA NOTISI NAMBA 423 NA 424 MWAKA 2003,NAMBA 497 NA 498 ZA MWAKA 2005 AMBAZO ZILIISAIDIA KAMPUNI YA ALEX STEWART KUTOLIPA KODI NA KUISABABSISHIA SERIKALI HASARA
8.DESEMBA 18 NA 19 MWAKA 2003 ALITOA NOTISI NAMBA 423 YA MSAMAHA WA KODI KWA KAMPUNI
HIYOHIYO
DANIEL YONA
(alikuwa waziri wa nishati na madini utawala wa Mkapa)
1.KUACHA UDHIBITI WA MADINI UFANYIKE KIENYEJI BADALA YA KUPELEKA KWA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI
2.UZEMBE NA KUISABABISHIA SERIKALI HASARA KAMA KWA BASIL MRAMBA.
3.KURUHUSU KAMPUNI YA M/S STEWART NA KAMPUNI TANZU YA M/S ALEX STEWART(ASSEYERS) GOVERNMENT BUSINESS CORPORATION KUSAINI UCHIMBAJI MADINI.
4.MATUMIZI MABAYA YA OFISI WAKIWA WAAJIRIWA WA SERIKALI.
5.KUTIWA SAINI KWA MKATABA WA NYONGEZA WA MIAKA MIWILI KWA KAMPUNI YA M/S STEWART KATI YA JUNI 14, 2005 HADI JUNI 23 JANA KINYUME CHA SHERIA ZA MANUNUZI YA UMMA NA SHERIA ZA MADINI.
6.MRAMBA NA YONA WANATUHUMIWA KUTUMIA VIBAYA MADARAKA YAO KATI YA MACHI 2005 NA MEI 2005 KUMWALIKA DK. ENRIQUE SEGURA WA KAMPUNI YA M/S STEWART KUKAMILISHA NYONGEZA YA MKATABA KABLA YA TIMU YA SERIKALI HAIJAANZA KUFANYIA KAZI SUALA.
NB; waungwana si mnakumbuka Mramba alisema tule NYASI ili ndege ya Rais inunuliwe, ha ha ha ha wala siwahurumiii. Na huyu Yona si ndiye aliyenunua Kiwira goldmine pale Kyela. hupajui? pale njia panda kituo cha ushirika.
ITAENDELEA ..............BREAKING NEWS USISHANGAE MNYASA NAPATA WAPI..... DUNIANI HATA UKIOGA BAFUNI TUNAKUCHUNGULIA TU..
BASIL MRAMBA
( alikuwa waziri wa fedha katika utawala wa Rais Benyamini Mkapa)
ANASHTAKIWA KWA MAKOSA YAFUATAYO:
1.KUISABABISHIA SERIKALI HASARA.
2.KUDHARAU MAPENDEKEZO YA TRA(mamlaka ya mapato)KUTOTOA MSAMAHA WA KODI
KWA KAMPUNI YA MS/STEWART YA UINGEREZA OKTOBA 10 2003 ALITOA NOTISI YA SERIKLI YENTE NAMBA 423 MWAKA 2003.
3.OKTOBA 15 2004 ALITOA NOTISI NAMBA 424 DESEMBA 19 2003 YA MSAMAHA WA KODI KWA KAMPUNI HIYO.
4ANATUHUMIWA KUTOA NOTISI YA SERIKALI NAMBA 497 MWAKA 2004 OKTOBA 15 ILI KUOTOA MSAMAHA WA KDI KWA M/S ALEX STEWART KINYUME NA MAPENDEKEZO YA TRA.
5.NOVEMBA 15 2005 AKIWA MWAJIRIWA WA SERIKALI ANATUHUMIWA KUTOA NOTISI YA SERIKALI NAMBA 377 YA 2005 KURUHUSU MSAMAHA WA KODI KWA KAMPUNI YA STEWART.
6.ANASHTAKIWA KWA KURUHUSU KUSHINDWA MAJUKUMU YAKE NA KUSABABISHA HASARA KWA SERIKALI SHILINGI 11,752,350,148.
7.ANATUHUMIWA KUTOA NOTISI NAMBA 423 NA 424 MWAKA 2003,NAMBA 497 NA 498 ZA MWAKA 2005 AMBAZO ZILIISAIDIA KAMPUNI YA ALEX STEWART KUTOLIPA KODI NA KUISABABSISHIA SERIKALI HASARA
8.DESEMBA 18 NA 19 MWAKA 2003 ALITOA NOTISI NAMBA 423 YA MSAMAHA WA KODI KWA KAMPUNI
HIYOHIYO
DANIEL YONA
(alikuwa waziri wa nishati na madini utawala wa Mkapa)
1.KUACHA UDHIBITI WA MADINI UFANYIKE KIENYEJI BADALA YA KUPELEKA KWA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI
2.UZEMBE NA KUISABABISHIA SERIKALI HASARA KAMA KWA BASIL MRAMBA.
3.KURUHUSU KAMPUNI YA M/S STEWART NA KAMPUNI TANZU YA M/S ALEX STEWART(ASSEYERS) GOVERNMENT BUSINESS CORPORATION KUSAINI UCHIMBAJI MADINI.
4.MATUMIZI MABAYA YA OFISI WAKIWA WAAJIRIWA WA SERIKALI.
5.KUTIWA SAINI KWA MKATABA WA NYONGEZA WA MIAKA MIWILI KWA KAMPUNI YA M/S STEWART KATI YA JUNI 14, 2005 HADI JUNI 23 JANA KINYUME CHA SHERIA ZA MANUNUZI YA UMMA NA SHERIA ZA MADINI.
6.MRAMBA NA YONA WANATUHUMIWA KUTUMIA VIBAYA MADARAKA YAO KATI YA MACHI 2005 NA MEI 2005 KUMWALIKA DK. ENRIQUE SEGURA WA KAMPUNI YA M/S STEWART KUKAMILISHA NYONGEZA YA MKATABA KABLA YA TIMU YA SERIKALI HAIJAANZA KUFANYIA KAZI SUALA.
NB; waungwana si mnakumbuka Mramba alisema tule NYASI ili ndege ya Rais inunuliwe, ha ha ha ha wala siwahurumiii. Na huyu Yona si ndiye aliyenunua Kiwira goldmine pale Kyela. hupajui? pale njia panda kituo cha ushirika.
ITAENDELEA ..............BREAKING NEWS USISHANGAE MNYASA NAPATA WAPI..... DUNIANI HATA UKIOGA BAFUNI TUNAKUCHUNGULIA TU..
Madhumuni
kumbukumbu,
siasa,
ushenzi
November 15, 2008
hatuchoki tunataka haki sawa hapa siyo longolongo
Madhumuni
kumbukumbu,
siasa,
ushenzi
Chuo Kikuu sehemu ya Mlimani
Tanzani ni migomo, maandamano kila mara. Chuo kikuu kimefungwa na kampasi zake zote WANAFUNZI wamegoma. Tunahitaji mabadiliko siyo uongozi wa mazoea HAPA. UONGOZI UMEKWAMA, UMEELEMEWA WANABAKI KUONGEA MPAKA MKOROMEA YANAKAUKIWA MATE
October 11, 2008
ni maisha tu kwani nani anajali hali hii
October 08, 2008
mwanamke auawa kwa kupigwa shoka
Na HAPPY KULANGA, SONGEA.
Watu wawili wameuawa kikatili katika matukio mawili tofauti yaliyotokea wiki jana.Kamanada wa polisi Falhum Mshana alisema jana kwamba katika tukio la kwanza agnes Kabanda aliuawa kwa kukatwa na shoka kichwani na hawara yake aliyehamika kwa jina la Ally Makinda. Kamanda huyo alisema tkio hilo lilitokea oktoba 3 saa 3:15 usiku katika eneo la Majengo Kisiwani ambako Makinda alimkata mpenzi wake shoka na kukimbia.
Taarifa z akufa zilitolewa na Hassan Salum(28) mkazi wa majengo C ambaye alikuwa akipita nyumbani kwake na kuona mwili wa marehemu ukiwa katika uwanja wa nyumba ya Makinda. Alisema chanzo cha mauaji ni ugomvi uliokuwepo baina ya marehemu na mtuhumiwa, ingawa alisema hadi sasa polisi bado hawajui ugomvi huo ulisababishwa na nini. Lakini uchunguzi unaendelea.
Pili, KILOSA MBAMBA BAY.
MkaZi wa Kilosa katika mji wa Mbamba bay Meshack Ngalima(62) amefariki dunia baada ya kudondokewa na mwembe aliokuwa akiuka. Tukio hilo lilitokea oktoba 3 saa 5 asubuhi mwaka huu. Meshack alifariki muda mfupi baada ya kufikishwa katika kituo kidogo cha afya Mbamba bay alikopelekwa na mdogo wake kwa ajili ya matibabu.
Watu wawili wameuawa kikatili katika matukio mawili tofauti yaliyotokea wiki jana.Kamanada wa polisi Falhum Mshana alisema jana kwamba katika tukio la kwanza agnes Kabanda aliuawa kwa kukatwa na shoka kichwani na hawara yake aliyehamika kwa jina la Ally Makinda. Kamanda huyo alisema tkio hilo lilitokea oktoba 3 saa 3:15 usiku katika eneo la Majengo Kisiwani ambako Makinda alimkata mpenzi wake shoka na kukimbia.
Taarifa z akufa zilitolewa na Hassan Salum(28) mkazi wa majengo C ambaye alikuwa akipita nyumbani kwake na kuona mwili wa marehemu ukiwa katika uwanja wa nyumba ya Makinda. Alisema chanzo cha mauaji ni ugomvi uliokuwepo baina ya marehemu na mtuhumiwa, ingawa alisema hadi sasa polisi bado hawajui ugomvi huo ulisababishwa na nini. Lakini uchunguzi unaendelea.
Pili, KILOSA MBAMBA BAY.
MkaZi wa Kilosa katika mji wa Mbamba bay Meshack Ngalima(62) amefariki dunia baada ya kudondokewa na mwembe aliokuwa akiuka. Tukio hilo lilitokea oktoba 3 saa 5 asubuhi mwaka huu. Meshack alifariki muda mfupi baada ya kufikishwa katika kituo kidogo cha afya Mbamba bay alikopelekwa na mdogo wake kwa ajili ya matibabu.
October 07, 2008
mbaroni kwa kumbaka mwanafunzi......
na HAPPY KULANGA, SONGEA.
Mkazi wa Mpandangindo mkoani hapa (Ruvuma) Filbert Ndomba(17) amefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Songea kwa kosa la kumbaka mwanafunzi wa darasa la kwanza mwenye umri wa miaka 8.
Mwendesha mashtka Inspekta wa Polisi Patrius Mlowe alieleza mbele ya hakimu mkazi Joseph Fovo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo septemba 16 mwaka huu, saa nane mchana, katika maeneo ya Mpandangindo ndani ya manispaa ya Songea mkoani hapa.
Mlowe alidai kuw mshatakiwa alimuingilia kimwili kwa nguvu binti huyo na kusababishia maumivu makali ambayo yalimfanya apige kelele zilizomshtua mwenye nyumba pamoja na wapangaji ambao walikwenda ndani kwa kijana huyo na kumkuta amemvua nguo zote mtoto huyo na kumbaka.
Mshtakiwa amekubali kosa na kudai kuwa mtoto huyo alimfuata chumbani kwake ndipo alipoamua kumbaka. Kesi hiyo iliahirishwa hadi leo oktoba ambapo hukumu itatolewa. Mshtakiwa alirudishwa rumande.
WAKATI HUOHUO, MBAMBA BAY.
Mkazi wa Mbamba bay Sevelina Komba(34) amefariki dunia baada ya kugongwa na pikipiki isiyofahamika na kuvunjika miguu. Sevelina alikuwa akitibiwa katika hosptali ya wilaya ya hapa Mbinga, mkoani Ruvuma. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi(Happy Kulanga) mjini hapa,kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma Falhum Mshana alisema tukio hilo lilitokea siku ya Idd Mosi, saa nne usiku katika maeneo ya hapa Mbamba bay.
Mshana alisema Sevelina Komba alifariki siku ya pili saa asubuhi katika hospitali ya wilaya Mbinga na kwamba aliymgonga hajafahamika baada ya kukimbilia kusikojulikana. Alisema mwili wa marehemu umezikwa jana na pia Polisi wanaendelea na uchunguzi sambamba na kumtafuta aliyemgonga marehemu huyo.
Mkazi wa Mpandangindo mkoani hapa (Ruvuma) Filbert Ndomba(17) amefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Songea kwa kosa la kumbaka mwanafunzi wa darasa la kwanza mwenye umri wa miaka 8.
Mwendesha mashtka Inspekta wa Polisi Patrius Mlowe alieleza mbele ya hakimu mkazi Joseph Fovo kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo septemba 16 mwaka huu, saa nane mchana, katika maeneo ya Mpandangindo ndani ya manispaa ya Songea mkoani hapa.
Mlowe alidai kuw mshatakiwa alimuingilia kimwili kwa nguvu binti huyo na kusababishia maumivu makali ambayo yalimfanya apige kelele zilizomshtua mwenye nyumba pamoja na wapangaji ambao walikwenda ndani kwa kijana huyo na kumkuta amemvua nguo zote mtoto huyo na kumbaka.
Mshtakiwa amekubali kosa na kudai kuwa mtoto huyo alimfuata chumbani kwake ndipo alipoamua kumbaka. Kesi hiyo iliahirishwa hadi leo oktoba ambapo hukumu itatolewa. Mshtakiwa alirudishwa rumande.
WAKATI HUOHUO, MBAMBA BAY.
Mkazi wa Mbamba bay Sevelina Komba(34) amefariki dunia baada ya kugongwa na pikipiki isiyofahamika na kuvunjika miguu. Sevelina alikuwa akitibiwa katika hosptali ya wilaya ya hapa Mbinga, mkoani Ruvuma. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi(Happy Kulanga) mjini hapa,kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma Falhum Mshana alisema tukio hilo lilitokea siku ya Idd Mosi, saa nne usiku katika maeneo ya hapa Mbamba bay.
Mshana alisema Sevelina Komba alifariki siku ya pili saa asubuhi katika hospitali ya wilaya Mbinga na kwamba aliymgonga hajafahamika baada ya kukimbilia kusikojulikana. Alisema mwili wa marehemu umezikwa jana na pia Polisi wanaendelea na uchunguzi sambamba na kumtafuta aliyemgonga marehemu huyo.
October 04, 2008
OKTOBA ni mwezi wa historia ya afrika
nadhani mwajua yanayojiri kwamba ni mwezi wa historia ya afrika huko Uingereza. Mwezi Februari ni huko Marekani. Lakini swali, JE HISTORIA YA AFRIKA IMEANDIKWA IPASAVYO? NI KWELI KWAMBA USTAARABU WA AFRIKA ULIANZIA MISRI, LAKINI NI KWELI KWAMBA MISRI HAWAKUISHI WATU WEUSI AU MAPIRAMIDI HAYAKUJENGWA NA WEUSI? tafakariJikomboe. Uhuru daima
Madhumuni
Hisia za moyo,
kumbukumbu,
siasa.,
ushenzi,
wageni
jamani vipi mmekwisha kusahau mwezi huu?
Jamaa huko ughaibuni wanasherekea historia ya mtu mweusi(waafrika) ndiyo ni huko uingereza kwa makamu mweyekiti wa viongozi wezi wa kura na waongo bwana Godi Blauzi sijui ni kinara mkuu wa uingereza.kumbuka mwenyekiti wa marais waongo na wezi wa kura ni Joji Kichaka kule washing..... huko majuu wanasherekea historia yetu watu weusi mwezi huu oktoba eti disko litakuwa huko Leicester sikwea na palase sijui. Historia yenyewe wanaipotosha kuhusu mtu mweusi tangu kule Misri. ndiyo maana nimeweka mtandano wa DAILY MOTION mjionee ukweli wetu watu weusi
Madhumuni
kumbukumbu,
siasa,
ughaibuni,
ushenzi
Subscribe to:
Posts (Atom)
