Showing posts with label Maendeleo. Show all posts
Showing posts with label Maendeleo. Show all posts

March 26, 2018

NGUZO ZA GATI LA BANDARI YA NDUMBI

March 01, 2018

USHAURI KWA RAIS: NAKUOMBA KUBALI TUENDELEE KUCHANGISHANA

NA.HONORIUS MPANGALA
KWANZA kabisa nianze na kukusalimia shikamoo mheshimiwa Rais wangu, Dk. John Pombe Magufuli. Najua hii kazi ni ngumu kama usemavyo wewe mwenyewe lakini sina budi kukuombea uione nyepesi ili uweze kupata nguvu ya kututumikia vyema kama yalivyokuwa malengo yako siku unaenda kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo.

Mheshimiwa nikiwa safarini kuelekea makao makuu ya nchi yetu Dodoma, katika gari nilipata tafakuri  ambayo ilinifanya nitoe kitabu changu cha kuandika kumbukumbu na kuhifadhi mawazo yangu ambayo nimeona nikuandikie. 

Hoja yangu kubwa ambayo ilikuwa ikizunguka katika kichwa changu ni ile niliyokumbuka kauli yako ya kupiga marufuku wananchi kuchangishwa mchango wowote katika shule za serikali.

February 28, 2018

NAFASI ZA KAZI MAMLAKA YA BARABARA VIJIJINI "TARURA" MKOA WA RUVUMA

 
 

February 13, 2018

JE, WAKALA WA MAJENGO NCHINI (TBA) WANAO UWEZO WA KUKIDHI MAHITAJI YA SEKTA YA UJENZI?


Jengo hili linalotakiwa kujengwa na TBA halijaisha hadi leo. Lipo Halmashauri ya Madaba, mkoani Ruvuma. Haifahamiki litajengwa lini au wakati gani. Hali hiyo inachochea baadhi ya mafundi kuondoka. Chanzo cha habari kimesema, “Hata kwetu Nyasa wapo tunatimua muda sio mrefu hao (TBA) sio wenyewe,”

DC SONGEA
Naye mkuu wa wilaya ya Songea amekasirishwa na utendaji duni wa TBA. DC huyo amesema, “DC SONGEA HAIWEZEKANI UJENZI WA GOROFA HATA KOKOTA HAKUNA TBA MNASUMBUA WATU,”

Mkuu huyo amewataka wakala wa uthibiti wa majengo TANZANIA TBA kuharakisha ujenzi wa ofisi ya mkurugenzi wa Madaba kwa wakati ili kusogeza huduma kwa wananchi. Katika wilaya ya Nyasa wanajenga ghorofa la ofisi ya Mkurugenzi, Chuo cha Veta, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya (DC) na Nyumba ya Mkuu wa Wilaya (DC).

February 12, 2018

ANA KWA ANA NA MBUNGE WA VITI MAALUMU CHADEMA, NDUGU UPENDO PENEZA


Sisi katika blogu yetu tunakutana na wanasiasa mbalimbali bila kujali itikadi zao. Au pia viongozi wa kila kada tunazungumza nao bila kujali fani zao. 
Madhali wengi wao ni marafiki zetu maana ni watanzania wenzetu basi huwa tunazungumza nao mambo yahusuyo  ustawi wa jamii yetu kwa ujumla wake. Tunazungumzia maendeleo ya elimu, uchumi, siasa, utamaduni, afya na kadhalika.
Madhumuni yetu ni kuendelea kuzungumzia maendeleo ya wananchi pamoja na furaha ya jamii. Tunajikita katika maslahi ya taifa letu. Tanzania ni nchi yetu na hatuna kwingine. Tutailinda na kuikosoa ikibidi.
Pichani; kutoka kushoto ni Gabriel Mushi (mwandishi wa gazeti la RAI), mhariri wa Blogu hii Markus Mpangala (katikati) na Mbunge wa Viti maalumu ndugu Upendo Peneza.

February 02, 2018

KAHAWA YA MBINGA, MABADILIKO NI HATUA

   Picha kwa hisani ya Maggid Mjengwa aliyepo mjini Mbinga.

Nakumbuka zamani tulikuwa tunatumia pumba za kiwanda cha kukoboa Kahawa Mbinga kufanya mazoezi ikiwemo kuruka sarakasi. Kiwanda hicho kipo mtaa wa Kiwandani unaopakana na Msimbazi. Zamani Kiwanda cha Mbinga kilikuwa kinajishughulisha na Kukoboa Kahawa peke yake. lakini sasa mabadiliko ni makubwa hadi kutengeneza Kahawa yenyewe kuweka kwenye paketi na kuziuza.
Mabadiliko ni hatua.

Markus Mpangala,
Dar es salaam

January 19, 2018

HAPO NI ENEO LA LWIKA KATIKA KIJIJI CHA LUNDO

Leo hii hakuna Mawasiliano ya Barabara toka Mbamba Bay to Kilosa....Bus zilizotoka   Mbinga na Songea Zimeishia shell pale Tambachi Kuna Calvart Limekwenda na maji watu wanahangaika hawajui cha kufanya.Hali ya mawasiliano kwa njia barabara ilikuwa mbaya sana siku ya tarehe 18/1/2017.

January 17, 2018

HALMASHAURI YA WILAYA YA NYASA INAO WAJIBU WA KUHUDUMIA BARABARA ZAKE

NYASA inahitaji matibabu kamili (kama dawa ya Mseto) sio kutuliza maumivu (Panadol). Matengenezo haya nimeyakuta mwezi Disemba 2017. Niliwaacha watengenezaji wakiwa kijiji cha Ndumbi, lakini yanaonekana yameanzia kijiji cha Amanimakolo (nako kunajazwa vifusi na kukarabati).
UJUMBE WANGU: Halmashauri ya Nyasa inao wajibu wa kuhudumia barabara zake wakati wote si kujaza vifusi kwakuwa Mheshimiwa Waziri Mkuu anapotembelea au kiongozi yeyote, au shughuli yoyote ya muda inapofanyika. Barabara ni nyenzo muhimu sana ya kukuza uchumi wa eneo lolote. Kila la heri wahusika. Tutaendelea kukumbushana.

January 15, 2018

ELIMU BURE INAVYOTESA WATOTO WA WANANCHI WA HALI YA CHINI

NA HONORIUS MPANGALA
KITAALUMA na hisia zangu zimenifanya niwe mtu tofauti kabisa kuhusiana na matumizi ya baadhi ya maneno hapa nchini. Mengi hutumiwa na viongozi wa ngazi za juu kuwaona wale waliopo chini au wasio na vyeo kama wao kuwa  wenye kiwango fulani cha dhiki kinachostahili kuitwa cha chini. Ni hapo ndipo nakuwa na hisia tofauti sana juu ya kutumia maneno fulani dhidi ya kundi jingine hasa lile ninaloongoza au viongozi wanaloliongoza. 
Japokuwa nimekuwa mtu nisiyependezwa na na hili neno “Wananchi wa hali ya chini”' lakini najiuliza hao wa hali ya juu ni akina nani, wanafanya nini kutokuwa na hali ya chini na njia zao zikoje ili tuwaambie wa hali ya chini wajifunze kwenda huko juu? 

January 12, 2018

JIMBO LA NYASA: KWANINI WANANCHI WA TARAFA YA RUHUHU WAMEACHWA UKIWA?

NA MARKUS MPANGALA
Ubovu wa Barabara katika kijiji cha Ndumbi.
RUHUHU ni miongoni mwa Tarafa zinazounda Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa. Wilaya hii ni miongoni mwa zingine kama Songea Vijijini, Songea Mjini, Mbinga, Namtumbo, Tunduru zilizopo mkoani Ruvuma. Wilaya ya Nyasa ilianzishwa rasmi mnamo Machi 2012 baada ya kugawanywa wilaya ya Mbinga. Eneo la wilaya ya Nyasa liko kando la Ziwa Nyasa.
Tarafa ya Ruhuhu ipo kwenye mwambao huo, ikiwa ni miongoni mwa maeneo yaliyoachwa nyuma kimaendeleo na kiuchumi. Tarafa hiyo inazo Kata za; Mbaha, Lituhi, Ngumbo na Liwundi. 
Kwa mujibu wa sensa ya mwaka wa 2012, Kata ya Mbaha ilikuwa na wakazi wapatao 6,972. Ni Kata ambayo ndiyo mwenyeji wa Shule ya Sekondari ya Monica Mbega iliyoanzishwa rasmi mwaka 2006. Jina la shule hiyo lilitokana na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Monica Mbega kabla ya kuondoka.
Wananchi wa Tarafa hii wanakabiliwa na changamoto nyingi mno hali ambayo inadhoofisha ukuaji wa uchumi. Changamoto hizo zinatokea katika nyakati tofauti na kuziba mianya ya kujipatia pato kutokana na huduma kadhaa wa kadhaa kuwa dhaifu. 

BENKI YA DUNIA YATOA MSAADA WA KUBORESHA KITUO CHA AFYA MKILI

NA MWANDISHI WETU
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Benki ya Dunia wametoa msaada wa shilingi milioni 400 kwa Kituo cha Afya cha Mkili kilichopo Kata ya Ngumbo wilayani Nyasa mkoani Ruvuma kwa ajili ya kuboresha utoaji wa huduma bora za Afya kwa wananchi kwa ujumla.

January 10, 2018

UJUMBE WA CHINA NDANI YA NYASA

Ni Mwenyekiti wa chama cha Wawekezaji kutoka China hapa nchini, Bwana Ding (Mwenye shati nyeupe), mbele ya Naibu Waziri Viwanda,Biashara na Uwekezaji, Injinia Stella Manyanya, ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nyasa mkoani Ruvuma.  Naibu waziri na mwenyekiti huyo walikutana katika tamasha la utamaduni la Nyasa linalofanyika kila mwaka Disemba 31/2017 hadi Januari 6, 2018 mjini Mbamba Bay. Mwenyekiti huyo amethibitisha kuhamasika kujenga Viwanda kwenye Wilaya ya Nyasa. Tuvute Subira.

PICHA NA GEORGE NDIMBO, DIWANI WA KATA YA KIHAGARA.

January 05, 2018

AMBULANCE YA HOSPITAL YA WILAYA NYASA ILIVYONUSURIKA KUANGUKA.

NA HONORIUS MPANGALA, LUNDU
AWALI niombe radhi kwa kukosa picha kwasababu nilipofika eneo la tukio simu yangu ilizima moto. Nakumbuka nilitumia simu yangu ndogo kumweleza kakangu Markus Mpangala kuwa narejea nyumbani lakini tumesimama mahali kuna gari inasaidiwa kunasuliwa toka ilikoegema. Ni mlima wa kwanza ukitoka kijiji cha Kihagara eneo la Camp, tulikuta hiyo Ambulance ikiwa imeshindwa kupanda mlima kwa uterezi na kuburuzika hadi pembezoni mwa barabara. Jambo la kuahukuru ni kwamba ilikuja kugota kwenye jiwe vinginevyo ingelala kwa ubavu katika kuta za barabara.
Barabara ya Lituhi kwenda Mbamba Bay  eneo la mtaa wa Likwambe katika Kijiji cha Lundu wilayani Nyasa.