Salama
nimewasili, jirani kanipokea,
Mekaa
kwenye kivuli, upepo unapepea,
Nimekuwa
mdhalili, mengi yamenipotea,
Nimewasili
salama, jirani kanipokea.
Nilikotoka
najuta, watu wengi wamekufa,
Mazingira
ya utata, yamejaa nyingi nyufa,
Maadui
masalata, ni kama vile malofa,
Nimewasili
salama, jirani kanipokea.