Showing posts with label zana. Show all posts
Showing posts with label zana. Show all posts

October 21, 2017

MBUNGE WA CHEMBA AONDOA HOJA YA KUONGEZA MUDA WA UBUNGE

NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM

MBUNGE  wa Chemba Juma Nkamia (CCM)amesema ameondoa kwa muda kusudio lake la kutaka kuwasilisha muswada binafsi wa mabadiliko ya Katiba unaohusu kuongeza ukomo wa Bunge. 
JUMA NKAMIA
Nkamia ambaye aliwasilisha kusudio hilo  katikati ya mwezi uliopita mjini Dodoma kwa mujibu wa kanuni ya 81(2) ya kanuni za Bunge toleo la 2016,kupitia barua yake aliyoisaini Septemba 12  iliyokuwa ikipendekeza kuongeza muda wa bunge kutoka miaka mitano hadi saba na kupunguza wa uongozi wa vijiji kutoka miaka mitano hadi minne.

Kupitia ujumbe mfupi aliouandika katika mtandao wa kijamii wa WhatsApp,alisema ameamua kuondoa kusudio hilo  baada ya mashauriano  na maelekezo kutoka kwa viongozi wa juu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM).

“Ndugu viongozi wenzangu naomba kuwataarifu kuwa baada ya mashauriano na maelekezo  ya viongozi wa juu wa chama(CCM) na hali ya kisiasa  katika nchi kadhaa za Afrika  Mashariki  nimelazimika kuondoa kwa muda hoja yangu binafsi ya ukomo wa Bunge niliyokusudia kuiwasilisha katika bunge lijalo,”aliandika Nkamia.

Mbali na andiko hilo gazeti hili pia lilimtafuta Nkamia kupitia simu yake ya kiganjani ili kumuuliza kama  na sababu nyingine zaidi ya alizozitaja kupitia ujumbe  huo mfupi na lini atakuwa teyari kuwasilisha tena muswada huo alisema.

“Naomba ibaki hivyo hivyo kama ilivyo kwenye meseji  sina cha kuongeza,kuhusu ni lini nitapeleka tena nayo subiri kwa sababu nimesema nimesitisha kwa muda maana yake nitawasilisha tena nitakapokuwa teyari,”alisema Nkamia.

Hoja ya  Nkamia ambayo ilianzia  katika Bunge lililopita ilikuw aikipingwa na wanazuoni pamoja na wanasiasa wakongwe akiwemo Spika Mstaafu wa Bunge Pius Msekwa.

Msekwa ambaye alikuwa akiongea na televisheni ya Azam  mwishoni wa wiki hii alisema  chama cha CCM hakiwezi kukubaliana na maoni au mpango wa kuongeza muda wa kiongozi yeyote kutoka kipindi cha miaka mitano kilichopo kikatiba kwa sasa.

Msekwa alisema kwa uzoefu wake bungeni tayari anaona kuna tafakari nyingi zilizofanywa kabla ya Taifa kuamua kipindi cha utawala kuwa miaka mitano na si vinginevyo.

Alisema hoja hiyo inabidi iangaliwe kwa umakini mkubwa kutokana na ukweli kuwa, iwapo kiongozi atakuwa mbaya, maisha yanaweza kuwa ya mateso kupitia kiongozi huyo na kuongeza kuwa hilo hata Hayati Baba wa Taifa, Julius Nyerere aliliona hilo.

“Ni kwamba miaka kumi tu inatosha, ili kama mtu ni mbaya tuvumilie kwa hiyo miaka kumi, na siyo kwamba haikufikiriwa. .na sidhani kama CCM itakuwa na nafasi ya kujadili hilo kwa sasa” alisema Msekwa. Mbali na Msekwa wasomi wakiwemo Dk.Benson Bana nao walimpinga huku akisema kuwa lengo lake lilikuwa ni kujipendekeza kwa Rais Dk. John Magufuli ili ampe uwaziri.

September 22, 2012

DELVE TECHNOLOGIES INAKUTENGENEZEA TOVUTI BOMBA

DEAR CUSTOMER!

DELVE TECHNOLOGIES, HAVE A SPECIAL OFFER THIS SEASON:
ORDER YOUR YOUR WEBSITE NOW AT ONLY 550,000/= AND GET A FREE DOMAIN AND 1  YEAR HOSTING.

CONTACT: 0762 589791

April 05, 2010

NATUMIA HUDUMA HII

Baada ya kipindi fulani kutumia huduma za Zantel ambazo kidogo zilikuwa zikikasirisha kwa mambo kadhaa ikiwemo usumbufu fulani. Nilivumilia lakini yakanishinda.

Nakubali hudma ya Zantel katika mtandao wa Tarakilishi ni nzuri na rahisi unaweza kusafiri nayo kwenda popote huku tukuwa na Tarakilishi ndogo.

Lakini sasa natumia huduma hiyo hapo juu, huduma hii unaweza kupata mtandao wa Tarakilishi kwa njia ya simu ya mezani,simu na Flash diski, haya ni mapinduzi katika teknolojia.

Ni huduma poa, ikinusumbua tu nawafuata katika ofisi zao na kufaytuka kwa huduma mbovu sitaki utani tena. Lakini niseme tu ukweli ni huduma ambayo imeniridhisha sana, nimeikubali naiona poaaaaa kabisa. Je wewe unangoja nini? Usipitweeeeeeeeeeeeee

January 17, 2009

Mseto,Teknolojia na Yasinta+Klayson

Gumzo lilikolea si haba, tukajiburudisha kwa utani wa hapa na pale. Lakini jambo la msingi ni matumizi ya blogu katika kuelemisha na kuwa na marafiki zaidi. Sasa gumzo lilipokolea ilibidi mambo ya teknolojia yaanze kujadiliwa. Mosi ilikuwa huduma poa ya NeoWORX Widgets.
Huduma hii inakuwezesha mambo mengi ikiwemo kujua idadi ya watembeleaji, hali ya hewa, picha na mambo mengine. Hii inamaana pamoja na Free NeoCounter (wageni wanaoitembelea blogu yako), NeoBoard, NeoEarth (hali ya hewa ya mahali unapotaka), NeoPod, NeoFlags( ukipenda bendera mbalimbali ziwepo katika blogu yako), NeoPlanet (mambo ya sayari) na NeoKube.
Huduma hizo ni pamoja na zile za malipo na za bure, sasa kama tunavyojua kwamba blogu zetu zinazidi kupewa kipaumbele kwani zote hizi nia yao ni kuboresha zaidi. Sasa gumzo na mseto wa mazungumzo ilikuwa huduma hizi, lakini binafsi bado najifunza hazijakaa kwenye medulla sawasawa ndiyo maana kuna NeoCounter pekee. Basi bwana Klayson akahoji huduma za bure huzipendi, ikabidi nimweleze mimi bado najifunza hizo kwahiyo polepole.

Mambo ya blogu zetu siku hizi ni mengi huduma ni nyingi mno ambazo Wanablogu inabidi tuzitumie, pia ipo ya Feedbliz , hii ni huduma ambayo kila unachoandika unawatumia wasomaji katika akaunti zao, hivyo wao huingia moja kwa moja kukuta mjadala uliowasilishwa au habari/picha. Hata hivyo ahadi zetu ni kwamba huduma hizi tutaweza kuzitumia iwapo tutajipa muda kuzielewa umuhimu wake. Blogu ni mambo yanayokwenda na mabadiliko sana kwani tayari wataalamu wamebaini siyo upepo wa kupita. Kivumbi cha Gaza blogu zimeweka video, picha na habari motomoto ambazo hutumiwa na mashirika kama BBC, DW, AP, Skynews n.k jamani blogu ni teknolojia ambayo sijui magazeti itakuwaje tuendako maana Thomas Friedman anasemaje katika kitabu chake 'The World is Flat', yanawezekana, AMKA anza WEWE ili tuibadili jamii. Gumzo lilikuwa tamu sana aiseh

January 11, 2009

CO.MMENTS + BLOGLINES= mambo mapya

Jana niliandika kuhusu huduma ya Aggregators/Bloglines kisha nikasema unaweza kurahisisha mambo kwa huduma hizo. Lakini nikatoa anuani ya kusoma zaidi mambo hayo ya www.mwongozo.wordpress.com Sasa leno niseme hii CO.MMENTS na BLOGLINES pia. Huduma ya CO.MMENTS ni tamu sana, nayo inakuletea habari mpya kuhusu maoni uliyoyaacha mahali/katika blogu uliyoacha MAONI.
Huduma hii inachofanya ni kukupa taarifa mpya toka sehemu ulizoacha maoni, mfano umetembelea blogu ya Koero kisha ukaacha maoni wakati huohuo unataka kujua wasomaji au wanablogu wengine watasema nini juu ya maoni uliyotoa, kawaida unachofanya ni kurudi pale ulipoacha maoni ya wengine kuendeleza mjadala.
CO.MMENTS inakusanya maoni yote mapya toka mijadala unayoshiriki na kukuletea katika akaunti yako. Kwetu TZ tunajua baadhi yetu tunategemea huduma za kulipia kwahiyo suala la MUDA ni muhimu sana, kwani unaweza kutembelea blogu 25 halafu hazina mambo mapya.
Huduma ya CO.MMENTS na BLOGLINES zinakusaidia kukusanya habari mpya na MAONI mapya toka kwenye idadi yoyote unayotaka hata 100 na kukuletea katika ukurasa mmoja.
Sasa hii huduma ya CO.MMENTS inakupatia fursa ya kujua blogu zote ulizopitia na kuacha MAONI wapo wasomaji au wanablogu wamechangia, kwahiyo maoni yao yanakuwa yanakusubiri uyasome ili kuendeleza mjadala.
Binafsi nimejaribu hiyo, na napata taarifa za maoni katika akaunti yangu kila ninapoacha maoni mapya katika blogu yoyote, na nimeanzia kwa dada Koero na mengine nitayapata. NB: ili kujiunga na huduma hii unajiunga na BLOGLINES kwa urahisi hapa www.mwongozo.wordpress.com nyingi sana kuhusu huduma hizo.

January 10, 2009

Aggregators+Bloglines =vikusanya habari

AGGREGATORS: ni moya teknolojia tunazoziita teknolojia za kutunza muda. Vikusanya habari vinatunza muda kwa kutuwezesha kujua BLOGU zipi zimeandika habari mpya/mambo mapya badala ya kuzitembelea BLOGU moja moja. Inawezekana pia ukatumia vikusanya habari kupata habari toka katika tovuti mbalimbali za habari na siyo BLOGU pekee.
Huduma ya AGGREGATORS ni kama huduma ya BLOGLINES, inachofanya ni kukusanya habari toka kwenye blogu mbalimbali unazozipenda na kuzileta katika ukurasa mmoja.
KAWAIDA; ukitaka kusoma blogu upendeleayo unachofanya ni kuzitembelea kwa kuandika anuani zake.
Lakini unaweza kutembelea blogu 10 halafu hazina habari mpya. Sasa hii BLOGLINES inakuletea mambo mapya yaliyoandikwa katika blogu uzipendazo. Fungua blogu yako ingia halafu bonyeza LAYOUT ili kuongeza ukurasa mwingine uupendao. Utaona orodha ya kurasa ambazo ungependa ziwepo, ndipo utakuta BLOGLIST bonyeza halafu utaona neno ADD kisha andika blogu unayoipenda kusoma habari zake. Sasa hapo kichwa cha habari kimeandikwa MY BLOGLIST unaweza kubadili kama ambavyo nimefanya, mfano: mimi nimeandika kikusanya habari(tazama kulia kwa blogu yangu).
Unaweza pia kusoma hapa; www.mwongozo.wordpress.com
NB ukiwa na tatizo, ni vema tukatafutana ukipenda, napatikana Sinza Kijweni ofisi za New Habari house siku za jumamosi ni poa sana

January 06, 2009

Vipi unatuonaje, angalia tena

kama napumzika na kazi ya uvuvi yaani unajipa maraha kama haya! taratiiiiiiiiibu kinyasa nyasa siyo mchezo mambo haya.

January 01, 2009

20009+ YASINTA+ Wanablogu


2009 Pamoja daima.Wanablogu wote Nawatakieni mafanikio mema zaidi.Na kudumisha maendeleo ya Blogu zetu.Nimefurahi zaidi kwani jana nilikuwa na mwanablogu dada Yasinta,na kupiga gumzo la hapa na pale.Anatuandalia kitu kingine;tanzaniaresan2009.blogspot.com
NAWATAKIA SAFARI NJEMA.
ZIDUMU BLOGU ZETU na WANABLOGU DAIMA

December 31, 2008

Wanaopuuza shauri yao


nimesoma maoni ya Koero katika shajara/blogu ya Bwaya kuwa wapo wanaotazama blogu kama upuuzi. Nimefarijika kuona dada Koero kawagundua watu hawa lakini anawashangaa wanasoma mambo ambayo wanasema ni upuuzi. Namshukuru kwa kuwabaini LAKINI naomba uwaaambie blogu siyo upepo wa kupita, hii ni hatu nyingine zaidi ya kusoma magazeti na kuangalia luninga. Hapa hatuhitaji wahariri wakuu wala waandamizi bali nidhamu imejenngwa na mtu mwenyee. Kwa hakika watu tunajikuta tunafanya mambo ya ajabu lakini kujipa muda angalau kufanya jambo linalokufanya uwe bize na kuepusha porojo za hovyo LAKINI watu wengine hawaelewi. Jamani nia yangu ni kwamba pamoja na kwamba wanasema ni upuuzi ambao wanausoma lakini wajue kuwa blogu siyo upepo. Nashukuru dada Koero amegundua hilo maana kuna watu ukiwaeleza hili jambo wanaona kama ujinga fulani, eeeeh shauri yao wanaopuuza tunajua hawaamini kuwa wasomaji wanaweza kuwa wahariri na wahariri wanaweza kuwa wasomaji. Hivi huamini tunaishi zama zingine za teknolojia? Wape maneno yao dada Koero asante kwa kutukumbusha wanaopuuzia blogu/shajara shauri yao.

December 30, 2008

wazee wa kazi ndiyo zetu

tunavua hivi na tunafanya hivi kama tupendavyo. kazi ipooooooooo

December 24, 2008

kazi+kumbukumbu

ninakumbuka enzi zile tukilima mpunga, ekari kibao na shangazi yangu pale Ngindo, yaani ilikuwa tka asubuhi saa moja hadi saa kumi na moja jioni. Duuh kwa mwendo wa kuchoka na kulegea kila kitu. nipumue siku hizi huuuuuuuuuuuuuuuuuu nalima kwa kompyuta

December 16, 2008

tunasaka kitoweo cha Noeli hii

nadhani haya mambo toka babu na bibi mpaka mjukuu anatumia tu hakuna matata. jamani hebu waangalie mazingira yao ya kazi, yanakufikirisha? mimi sijui bwana

December 08, 2008

kazi+juhudi+ubunifu+mapenzi=MAISHA

maisha tu haya kama utapenda nunua tu utakuwa umenisaidia sana maana mwanangu namsomesha kwa kutegemea hii kazi yangu. Nahiheshimu sana. Ni kama anasema hivyo

November 27, 2008

unapofurahia kunywa, ujue na kushughulika

naam mambo shughuli za kulima kahawa. hapo ni suala la kukausha si mnajua tunakausha kwa njia za asili au mnafanyaje ninyi.

November 19, 2008

zana za kazi zipo mapumzikoni

November 17, 2008

kuvua dagaa usiku


dagaa wa ziwa nyasa ni watamu sana, wananoga mno, ukila unajiumauma tu hamu na kuzidi kunogea. SASA ukitazama picha hii utaona KARABAI zimefungwa mtumbwini, hapo ndipo kazi inafanyika kwani ukisha funga hivyo kazi inaanza kwenda kilindini na anyavu ya kuvulia kusaka kitoweo kunoga na utamu kuliko chochote..... ebu taja kitu kingine kitamu kuliko dagaa? najua utataja nanii....... nini ile ...... sijui ebu inaitwaje!!!! aahaa tuache, hayo. haya ndiyo mambo ya nyasa na zana zao

kazini hakuna matata

kuvua samaki ndiyo zetu, ni kazi zetu ni shughuli zetu wala hatuachi kufanya hivyo. KARIBUNI NYASA

October 18, 2008

mume+mke = papo kwa papo

NA JOYCE JOLIGA, SONGEA
Ni kamba serikali ya halmashauri ya mkoa wa Ruvuma inajenga wodi ya uzazi(upasuaji. Wazazi wengi walikuwa wakijifungua katika chumba maalum na kurejeshwa katika wodi ya akina mama ambayo ilikuwa na kero nyingi. Lakini ufumbuzi huo umepatikana na waume zao wakuwa bega kwa bega katika kujifungua kwa wake zao. Hivyo kusudio hilo linafanyika baada ya kuona usumbufu wanaoupata akina mama kwa kujifungua. Waume watatakiwa kuwa karibu na wake zao hasa wale wanaopata uapsuaji wa uzazi/kujifungua kwa njia ya kupasuliwa. Maana yake sasa wanaume kushuhudia namna wake zao wanavyojifungua? Hapana bali ni kuwa karibu na wake zao hao baada ya kufanyiwa upasuaji.

NA HAPPY KULANGA, SONGEA
Wakulima wametakiwa kujiunga katika vyma vya ushirika ili kupata urahisi wa kununua matrekta madogo ya kulimia ili kuongeza tija katika sekta ya kilimo. Mkuu wa mkoa amewataka wakulima kufanya hivyo ili kuweka mazingira mazuri ya uzalishaji.

NB; unatakla kuwekeza katika Mkoa wa Ruvuma? Njoo wekeza ufaidike sasa usingoje

October 12, 2008

korido za Mv Ilala ambayo hufanya safari zake toka Malawi-Tanzania. hii ni mali ya Malawi na yapili kwa ukubwa baada ya Mv Mtendele

October 09, 2008

habari ndiyo hiyo

hapa hakuna la mnadi swala wala sauti za kanisa, mchezo ni kujiburudisha, mchezo kufurahi yanini kujibana wakati muda wenyewe robo eti tutakwenda peponi mmmm