Showing posts with label uongozi. Show all posts
Showing posts with label uongozi. Show all posts

March 01, 2018

NGOMA ZETU

MIAKA mingi enzi za babu zetu kulikuwa na ngoma maarufu iliyoitwa GEUZA. Hakukuwa na Ligambusa kama ilivyo sasa walisafiri kutoka Lundu kwenda Mbaha au Hinga kucheza Geuza usiku nyakati za Mbalamwezi na wakarudi nyumbani.
 
Kwa upande wa Ngoma ya Mganda, Maboma yaliyoka hadi sasa ni Mawili na yenye upinzani wa Kama vilabu vya soka. LICHUMA LINDU na LIHEGHELYA KONI majina hayo ni kama yanajibizana .Ni ngumu kuona mshiriki wa boma moja kwenda boma lingine nyakati za mazoezi utafukuzwa na kuonekana kama umeenda kuiba stepu(mtindo Wa uchezaji).

Kihoda ndo kimetia fola nyakati za nyuma Lundu ilikuwa na maboma mawili tu yaani Maji na Uamuzi. Lakini kutokana na ongezeko la watu kikafanya kuonekana wanawake wako wengi na wote wanataka kuonyesha uwezo wao wa kusakata ngoma. 

February 16, 2018

DK. SLAA ATEULIWA KUWA BALOZI WA TANZANIA NCHINI SWEDEN


December 07, 2017

KILICHOTOKEA KATIKA UCHAGUZI WA KATA 43 HAKINA TASWIRA NZURI 2020

NA HONORIUS MPANGALA 

TANZANIA ni nchi ambayo wananchi wake wamejengwa kwenye ushrikiano na mshikamano mkubwa sana katika aisha yao ya kila siku. Yawezekana misingi iliyowekwa na waasisi wa taifa hili ilikuwa haswa ambayo inatufanya hata wale wenye mitazamo tofauti kwenda sawa na wengine. 

Tumekuwa tukipata viongozi wetu kwa njia za uchaguzi kwa kuwapa nafasi wananchi kuchagua kiongozi wanayemtaka. Uhuru wa kuchagua ni moja ya vipengele vilivyoko katika Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano ya mwaka 1977 inayotumika hadi sasa. Katiba imeeleza kila mtu anauhuru wa kuchagua na kuchaguliwa.

Wananchi wa Kijiji cha Katumba Kata ya Ibighi
Katika uchaguzi mdogo wa madiwani uliofanyika katika kata 43 hapa nchini umenifanya nitafakari hatma ya Tanzania kwa yale ambayo nimepata kuyaona na kusikia toka maeneo tofauti. Hakika kuna mahali tumeteleza na tunapaswa kujisahihisha. Kuteleza ninakosema ni kwa yale matendo ambayo yamekuwa yakiibuka wakati wa uchaguzi mdogo katika maeneo tofauti.

November 12, 2017

NANA YAA ASANTEWAA: MALKIA WA MILKI YA ASHANTI ALIYEWAKINGIA KIFUA WAKOLONI WAINGEREZA.

Na Kizito Mpangala

Alizaliwa mwaka 1863 katika mji wa Besease katika jamii ya Ashanti yenye dhahabu nyingi, Ghana ya sasa, magharibi mwa Afrika. Kaka yake Nana Akwasi Afrane alikuwa ndiye Edweso (kiongozi, au chifu) wa milki ya Ashanti wakati huo. Nana Yaa Asantewaa akiwa bado binti alijishughulisha sana na kilimo. 

Kaka yake (chifu Akwasi) alipokuwa Edweso (kiongozi) alituma askari wake kwenda mapiganoni dhidi ya wakoloni. Baadae aliwekwa kizuizini na wakoloni katika visiwa vya Ushelisheli pamoja na mfalme Prempeh I. Akiwa kizuizini, Nana Akwasi Afrane alimteua dada yake NANA YAA ASANTEWAA kuwa malkia wa milki ya Asante. 

Mwaka 1899 gavana wa wakoloni Waingereza Frederick Hodgson aliitisha mkutano mjini Kumasi ili kulazimisha apewe kiti kilichotengenezwa kwa dhahabu tupu ambacho ni alama takatifu ya Ashanti ambapo askari wa kikoloni walishindwa kukipata kiti hicho, hii ni baada ya kufikiri kwamba ugumu wa kuwatawala Waashanti ungeisha baada ya kupata kiti hicho cha dhahabu. Nana Yaa Asantewaa alimteua mjukuu wake mkubwa kuwa mkuu wa miliki ya Ashanti mara baada ya kufariki kaka yake.