MIAKA
mingi enzi za babu zetu kulikuwa na ngoma maarufu iliyoitwa GEUZA. Hakukuwa na
Ligambusa kama ilivyo sasa walisafiri kutoka Lundu kwenda Mbaha au Hinga
kucheza Geuza usiku nyakati za Mbalamwezi na wakarudi nyumbani.
Kwa
upande wa Ngoma ya Mganda, Maboma yaliyoka hadi sasa ni Mawili na yenye
upinzani wa Kama vilabu vya soka. LICHUMA LINDU na LIHEGHELYA KONI majina hayo
ni kama yanajibizana .Ni ngumu kuona mshiriki wa boma moja kwenda boma lingine
nyakati za mazoezi utafukuzwa na kuonekana kama umeenda kuiba stepu(mtindo Wa
uchezaji).
Kihoda
ndo kimetia fola nyakati za nyuma Lundu ilikuwa na maboma mawili tu yaani Maji
na Uamuzi. Lakini kutokana na ongezeko la watu kikafanya kuonekana wanawake
wako wengi na wote wanataka kuonyesha uwezo wao wa kusakata ngoma.