NA.HONORIUS MPANGALA
MAISHA popote unaweza kusema hivyo kwani
waliofikiria katika hoja hii walikuwa na sababu za msingi zilizokuwa na maana
kiuhalisia. Wakati kipato ndio sababu hasa zilizopelekea kukawa na maneno kama
haya ambayo yanasadifu uhalisia wa maisha. Katika mazungumzo yangu na mmoja ya watanzania
waishio nchini Afrika kusini ilinifanya nistaajabu kile anachonieleza ambacho
ndio uhalisisa wa maisha ya huko.
Ni rafiki yangu na ndugu yangu Joseph Boimanda
alinifanya nistaajabu pale aliposema mtaji wa milioni hamsini za kitanzania
ukiwa Afrika Kusini sio lolote kwa serikali ya huko. Maisha yamekuwa yenye uhuru
na amani ya kutosha kwa raia.
Wakati nataka kuyajua haya ananieleza kuwa
mamlaka ya mapato ya huko haina muda wa kufuatilia mfanyabiashara wa kati.Kama
inatokea mtu anataka kulipa mapato serikalini basi ni hiari yake,hii ni kwa
wale wafanyabiashara wadogo na wa kati amabao mtaji yao ni kitu kidigo kwa
serikali yao.