November 30, 2017

SAFARI YAO YA MAISHA


Kuna dhiki na shida. Safari yao ina milima na mabonde. Sauti zao hazisikiki kokote. Hawajui itikadi zenu bali wanatafuta shibe zao. Mazingira yao hayavutii, lakini hawachokii kuyatumia kupata matumaini na kipato. LAKINI wanaishi kwenye nchi yenye utajiri pomoni. Hawana amana benki watakuwaje na amani?  Hawana chakula nyumbani watakuwaje na utulivu?
Tafakari makuzi ya mtoto huyu....
 Tafakari mwelekeo wake na hitimisho lake. Atarudishaje faida kwa jamii iliyomtenga kiasi hiki? Nani anajali hisia zake? Nani anajali hatima yake? Nani anagusa moyo wake?
Sauti zao zisikike!

©Picha kwa hisani ya Musa Makongoro. Imepigwa katika eneo la Mburahati, jijini Dar es salaam

No comments:

Post a Comment

Maoni yako