NA KIZITO MPANGALA
DUNIANI kuna ubunifu wa namna
mbalimbali unafanyika katika teknolojia ili kurahisisha shughuli mbalimbali
katika maisha yetu ya kila siku. Ubunifu wa kiteknolojia umekuwa ni lulu
mojawapo katika ulimwengu huu wa Sayansi na Teknolojia hasa katika umeme na
elektroniksi, ingawa upo ubunifu mwimgine nje ya uga huu wa umeme.
Kiti cha magurudumu manne ni
kifaa cha muhimu sana kwa wagonjwa katika hospitali mbalimbali duniani. Na ubunifu
mbalimbali hufanyika ili kuboresha utendaji wa kiti hiki. Kiti hiki kwa sasa
kina magurudumu manne ambapo makubwa mawili na madogo mawili na hutegemea nguvu
za mgonjwa kama anaweza kukisukuma yeye mwenyewe na kama hawezi basi anasukumwa
na mtu mwingine.
Tofauti na baiskeli ya
magurudumu matatu, kiti hiki kina ukubwa ambao unatosha kwa mtu mmoja tu kuketi
na anayesukuma hulazimika kuembea. Vilevile hakichukui nafasi kubwa. Hakiwezi
kutumika kama njia mojawapo ya usafiri barabarani kama ilivyo baiskeli ya
magurudumu matatu inayotumiwa na walemavu wengi duniani kote.
Kiti hiki kilianza kubuniwa
nchini China mnamo karne ya tano na baadae nchini Ugiriki mnamo karne ya sita
ambapo kilibuniwa kwa ajili ya kubebea watoto na wazee wasioweza kutembea na
kisha kuwasukuma ili kuwafikisha sehemu waliyokusidia. Nchini China awali
walikuwa wakitumia matoroli kwa ajili ya kuwabeba wazee wasioweza kutembea na
pia vilema na vilevile kubebea mizigo mizito. Michoro ya kiti cha magurudumu
mawili iliyochorwa nchini China ilionekana mwaka 525 B.K huko Ulaya.