Showing posts with label Sayansi na Teknolojia. Show all posts
Showing posts with label Sayansi na Teknolojia. Show all posts

March 02, 2018

KUTOKA CHINA HADI CHUO CHA TEKNOLOJIA DAR ES SALAAM (DIT)

NA KIZITO MPANGALA
DUNIANI kuna ubunifu wa namna mbalimbali unafanyika katika teknolojia ili kurahisisha shughuli mbalimbali katika maisha yetu ya kila siku. Ubunifu wa kiteknolojia umekuwa ni lulu mojawapo katika ulimwengu huu wa Sayansi na Teknolojia hasa katika umeme na elektroniksi, ingawa upo ubunifu mwimgine nje ya uga huu wa umeme.
Kiti cha magurudumu manne ni kifaa cha muhimu sana kwa wagonjwa katika hospitali mbalimbali duniani. Na ubunifu mbalimbali hufanyika ili kuboresha utendaji wa kiti hiki. Kiti hiki kwa sasa kina magurudumu manne ambapo makubwa mawili na madogo mawili na hutegemea nguvu za mgonjwa kama anaweza kukisukuma yeye mwenyewe na kama hawezi basi anasukumwa na mtu mwingine.
Tofauti na baiskeli ya magurudumu matatu, kiti hiki kina ukubwa ambao unatosha kwa mtu mmoja tu kuketi na anayesukuma hulazimika kuembea. Vilevile hakichukui nafasi kubwa. Hakiwezi kutumika kama njia mojawapo ya usafiri barabarani kama ilivyo baiskeli ya magurudumu matatu inayotumiwa na walemavu wengi duniani kote.
Kiti hiki kilianza kubuniwa nchini China mnamo karne ya tano na baadae nchini Ugiriki mnamo karne ya sita ambapo kilibuniwa kwa ajili ya kubebea watoto na wazee wasioweza kutembea na kisha kuwasukuma ili kuwafikisha sehemu waliyokusidia. Nchini China awali walikuwa wakitumia matoroli kwa ajili ya kuwabeba wazee wasioweza kutembea na pia vilema na vilevile kubebea mizigo mizito. Michoro ya kiti cha magurudumu mawili iliyochorwa nchini China ilionekana mwaka 525 B.K huko Ulaya.

February 10, 2018

‘LOCATION’ YA WANAMUZIKI WA BONGOFLEVA ASLAY NA NANDY


Unaupata wimbo unaobamba sana katika vituo vya redio, kwenye magari ya abiria, bodaboda na Bajaj wa “SUBAKHERI MPENZI” ulioimbwa na wanamuziki wawili; ASLAY na NANDY?

Sasa hii pikipiki niliyokaa ambayo inamuundo wa aina yake imetumika katika video ya huo wimbo, maana ina usukani kama gari na makorombwezo ya mfumo Wa gari. Cratch inakanyagwa kama ya gari. Subiri kile ambacho wenye maeno yao wanavyosema pale inapotokea msanii anafanya video ya wimbo au kazi nyingine ya Sanaa kama filamu wao wanavyojisikia na namna gani wananufaika kupitia Location za hizo video zinazochukuliwa.

 Honorius Mpangala,

Matimbwa, Bagamoyo

November 15, 2017

HALI YA ZIMBABWE MCHANA HUU



1.Waziri wa Fedha wa Zimbabwe Ignatius Chombo amekamatwa na Jeshi la Zimbabwe. Pia wanajeshi wameua walinzi watatu wa waziri huyo. (Chanzo: PaZimbabwe).
2. Jeshi hilo pia lilitembelea nyumbani kwa Profesa Jonathan Moyo ambaye ni waziri wa elimu ya juu, amekamatwa (Chanzo: NewsDay)
3.Baadhi ya mawaziri wameripotiwa kutoroka, wakiwemo Saviour Kasukuwere  na Makamu wa rais Phelekezela Mphoko anayedaiwa kukimbilia Afrika kusini.

November 09, 2017

MAMBO 50 YA KISAIKOLOJIA YATAKAYOKUACHA KINYWA WAZI

NA VITUS MATEMBO, MBAMBA BAY 
Mwonekano wa ufukwe wa Mkwakwa katika Ziwa Nyasa.
Hii ni kweli hata kama ulikua hujui kubali tu, maana ndio ukweli uliopo.
 
1. Mtu hufanya ishara nyingi za mikono akiwa anazungumza ukweli. Azungumzae uongo mikono yake huwa imetulia zaidi.
2. Sikiliza kwa makini namna mtu anavyozungumzia watu wengine akiwa na wewe, na ndivyo atakavyokuzungumzia wewe akiwa na watu wengine.
3. Ndoto zako zinabeba ujumbe mhimu sana. Asilimia 70 ya ndoto zako zina ujumbe wa siri.
4. Kwa kawaida watu huwa waaminifu na wakweli mwili ukiwa umechoka, na ndio sababu hutubu na kutoa siri zao kwenye mazungumzo yatekeayo usiku wa manane,

October 16, 2017

CHUO CHAANZISHA SHAHADA YA WADUDU

NAIROBI, KENYA

KITUO cha Elimu na Utafiti kinachofadhiliwa na Benki ya Dunia kimeasisiwa katika Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Jaramogo Oginga Odinga na kinasubiri ruhusa ya kuanzishwa kwa programu za Uzamifu na Uzamili kuhusu wadudu wanaoweza kuliwa.

Taasisi hiyo inapania kubuni njia za kuzalisha wadudu hao kwa wingi bila ya kuharibu mazingira ili kukidhi utashi mara baada ya wazo hilo likifanywa kuwa biashara.Wadudu wanaoliwa sana maeneo ya Magharibi mwa Kenya, ambao wana wingi wa madini ya protini na Zinki watafanywa kuwa biashara ili kuimarisha uwepo wa chakula cha kutosha, na kuondoa dhana mbaya katika kula wadudu. 

October 06, 2017

ALFRED NOBEL: MHANDISI MWANZILISHI WA TUZO YA NISHANI YA AMANI YA NOBEL.


NA KIZITO MPANGALA, 0682 555 874

ALFRED NOBEL ni mtu aliye wazi masikioni mwa wengi lakini akifahamika zaidi kwa jina lake la mwisho yaani Nobel kutokana na tuzo aliyoianzisha katika amani, lakini kwa sasa tuzo hiyo imepanuliwa zaidi, haipo katika amani tu, bali ipo katika uga mwingi duniani na washindi wanapatikana kila mwaka kulingana na uga husika ambayo hubebwa na jina lake la mwisho yaani Nobel. 

Nobel alizaliwa Oktoba 21, 1833 jijini Stockholm nchini Sweden. Alikuwa ni mvumbuzi, mtaalamu wa Kemia, mfanyabiashara, mwanaphilanthropia na mhandisi katika viwanda mbalimbali ambavyo kati ya hivyo vipo vilivyomiliki yeye mwenyewe kikiwemo kiwanda cha Bofors ambacho kilikuwa kinajishughulisha na kufua vyuma na vyuma vya pua.
Alfred Nobel.
Alizaliwa katika familia ya kipato cha chini ambapo baba yake Mzee Emmanuel Nobel alikuwa mhandisi pia. Katika malezi yao Alfred Nobel na wadogo zake watatu walisalimika kuishi miaka mingi zaidi wakati wenzao waanne wakipoteza uhai kwa sababu mbalimbali. Hivyo kati ya watoto nane wa Mzee Immanuel Bernhard Nobel, bwana Alfred alijihusisha na kazi ya baba yake. Alijiunga katika mafunzo ya uhandisi katika himaya ya Mwanasayansi wa Sweden bwana Olaus Rudbeck ambapo alipendelea zaidi masuala ya milipiko (explosives) jambo ambalo alianza kulipenda kwa kujifunza misingi yake alipokuwa na baba yake nyumbani.