Showing posts with label kinyaa. Show all posts
Showing posts with label kinyaa. Show all posts

December 27, 2017

NYASA; DISEMBA 20 ILIPONIREJESHA MIAKA 13 ILIYOPITA

NA HONORIUS MPANGALA, LUNDU
TULIANZA safari yetu na dadangu kijijini kwetu Lundu na kuelekea Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Mbamba Bay. Changamoto za barabarani hazikukosa kwasababu ya mvua zinazonyesha. Tukifika na kukamilisha yaliyotupeleka huko. 

Saa kumi jioni nilipofika kituo cha mabasi cha Mbamba Bay sikukuta gari ya kugeuza kwenda kwetu Lundu. Ikatulazimu tupande ya kuishi njiani, gari iliyotoka Mbinga kwenda Kihagara. Nikiwa nawaza namna ya kutoka Kihagara hadi Lundu lakini nikapanga jambo kuwa bodaboda ziko kila eneo sikuhizi,na sikutoa nauli ya yangu na Dada nikamwambia waambie natoa Mimi. Nikamwambia konda natoa Kihagara kuna mtu anatusubiri,nilifanya Kwa maksudi.

November 04, 2017

TANZANIA YATAJWA KUONGOZA KWA MARADHI YA KIPINDUPINDU


NA MWANDISHI WETU

SHIRIKA la Afya Duniani imeitaja Tanzania kuwa  miongoni mwa nchi kumi kinara kwa watu wake kuugua ugonjwa wa kipindupindu. Mataifa  mengine yaliyotajwa ni pamoja na India ambayo ndio inayoongoza. Nyingine ni Haiti, Jamhuri  ya  Kidemokrasi  ya  Congo, Tanzania, Bangladesh, Uganda,  Msumbiji na Kenya, ambayo ilikumbwa na mlipuko mkubwa wa maradhi hayo kwa nyakati tofauti mwaka huu.

August 24, 2013

HEKA HEKA ZA WILAYA YA NYASA

HII MELI YA MV.SONGEA naihofia sana. Nahisi ipo siku yatatokea yaleyale ya MV.BUKOBA. Meli imechoka sana japo inaburuzwa kila siku. Meli toka 1988. Kila siku Gereji na Kupakwa RANGI.

DARAJA LA KULIPIA AMBALO LINAUNGANISHA KIJIJI KIMOJA NA KINGINE. HUU NI UBUNIFU WA VIJANA WAKAZI WA KIJIJI KIMOJA WILAYANI NYASA, MKOANI RUVUMA KUTOKANA NA UKOSEFU WA DARAJA HIVYO WANANCHI WAKIVUTA HAPO WANALAZIMIKA KULIPIA SHILINGI 500/-


January 11, 2013

UCHAWI: DHANA INAYOANGAMIZA JAMII YETU



Na John Chitanya, Nyasa

Mei 4, 2012 yalifanyika maandamano makubwa sana katika wilaya mpya ya Nyasa iliyogawanywa kutoka wilaya ya Mbinga. Nyasa ni wilaya ni kiserikali, lakini katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi inafahamika kama jimbo la Mbinga Magharibi. Maandamano yaliyofanyika yalilenga kuishinikiza serikali kumruhusu Mganga wa Kienyeji apewe  kibali cha kufanya kazi yake ya kuwaumbua wachawi wilayani hapa.
Maandamano yale yalionyesha na televisheni ya TBC1  wakazi wa mji wa Kilosa nje kidogo ya mji mdogo wa Mbamba Bay, kwa hakika ilikuwa fedheha kubwa kwa wananchi wa ukanda wa ziwa Nyasa na maeneo mengine yanayounda wilaya hiyo kwa upande wa mashariki ambayo yanakaliwa na jamii ya Wamatengo.
Kwa mtazamo wangu kama kuumbuana na kushika uchawi  wameshikana sana,  sasa tunataka maendeleo sio kuimba nyimbo za wachawi kuwanyima maendeleo baadhi ya watu.  
Watu wengi wanaamini kuwa kuna kasoro pale inapotokea jambo fulani likawa baya, basi linazungumzwa kuwa linatokana na kurogwa na wachawi.
Mganga wa kienyeji
Niliwahi kushuhudia tukio moja kwa moja ya familia iliyokuwa ikiendesha kikao cha kifamilia, kwamba binti mmoja wa shule ya msingi alishindwa kusoma na kuandika hivyo walipanga kwenda kwa Mganga wa Kienyeji ‘kumfungua” kwa madai alifungwa na watu wabaya(wachawi) asiweze kujua kusoma na kuandika.
Hakika suala hilo lilileta mtafaruku kwa wale waliofanikiwa kwenda shule, wakadai kuwa hilo ni suala la mwanafunzi mwenyewe wala halina uhusiano na kufungwa kwa misingi ya uchawi. Lakini ilishikiliwa uchawi ndio umemfunga binti yule. Hadi naandika makala hii juhudi za kumfikisha mwanafunzi yule kwa Mganga wa kienyeji zilikuwa zimesimishwa ila sina shaka zitaendelea kwani nia yao ipo na wanaonekana kuamiani sana uchawi umetumika kwa binti yule.
Matukio ya uchawi yamekuwa yakitangazwa sana hata wakati uchaguzi unapofanyika, kwani wagombea mbalimbali wanadaiwa kuwategemea waganga wa kienyeji, wapiga ramli na kuamua hatima ya harakati zao. Kwenye michezo ya mpira wa miguu na mingine suala la uchawi limekuwa likichukua nafasi kubwa bila kutegemea sayansi ya kuleta mafanikio.
Hatua za vigogo kuhangaika na kuwategemea waganga wa kienyeji inaleta ujumbe kuwa jamii yetu inakabiliwa sana na janga la uchawi na kutoamini nguvu zilizomo kwenye akili na miili yetu.
Leo hii ni vigumu kufanya jambo la maajabu kwa kutohusisha uchawi. Hapa ndipo mimi siku zote huamini mapinduzi ya maendeleo ya wilaya ya Nyasa na yale yenye kasumba za kutegemea wachawi yanapaswa kuanzia katika fikra zetu. Tuna mambo mengi ya kuyafanyia maandamano katika nchi hii, mfano umeme, bandari, barabara isiyoisha na mengine mengi, lakini wananchi wameshikilia na kuamini kuwa uchawi umesababisha wawe na maisha duni.
Hata hivyo tukio la mji wa Kilosa, waliohamasishwa mapema mwezi Mei, ili Mganga wa kienyeji kutoka Tanga walikamatwa na mamlaka zinazohusika. Mganga huyo alihamasisha vijana wa Mbamba Bay wafanye fujo kushinikiza apewe kibali ili atoe uchawi kwenye nyumba za watu, basi wale vijana wakavunja ofisi za serikali na kuchoma moto, huku  wakalazimisha kila familia kuchangia shilingi 5000.
Mamlaka zinazohusika zilifanikiwa kuzima jaribio hilo, na kuwakamata baadhi ya vijana waliohusika. Baadhi ya vijana yao ni mabinti watatu waliokamatwa kwa kosa la kuandamana bila kibali na kufanya vurugu, walishikiliwa mjini Kilosa, Mbamba Bay. Tukio hilo linaturejesha kwenye mjadala hivi masuala ya uchawi yanachukuliwaje kama turufu ya kufanya uhalifu au uvunjifu wa amani? Uchawi umekuwa ukizungumziwa sana katika jamii zetu.
Wafanyabiashara wanategemea uchawi, watu wa kawaida wanategemea uchawi, ina maana hata masuala yenye kuhitaji utaalamu yamepewa dhana ya uchawi. Jamii yetu imeshikilia dhana ya uchawi kama nyenzo ya kupata mafanikio. Wengi hushikilia sana kupiga ramli, wamekuwa wakishindwa kujielemisha na kupata ufumbuzi wa matatizo ya familia na jamii huku wakiamini matukio hayo yanatokana na uchawi. 
Idadi ya wapiga ramli nayo inaongezeka kila kukicha. Ulimwengu unatuacha nyuma, na kila mwenye mafanikio maishani anaweza kutazamwa kwa namna mbili; mosi aliiba mahli na pili amefanya uchawi. Hakuna watu wanaoamini kuwa juhudi hizo zimefanywa na mhusika. Kuna masimulizi mengi sana kwa wana jamii ya wilaya ya Nyasa kuhusiana na uchawi. Magari yakipinduka husemwa uchawi, hakuna anayesema kuwa barabara ni mbovu, wote husikilia uchawi.
Kuna mambo mengi yanatisha na bila juhudi za serikali kusambaza elimu kila jambo lingeonekana kwua uchawi. Na serikali yetu haiamini uchawi hivyo ni kosa la mtu kufanya fujo kama vijana wale kwa kisingizio cha uchawi. Sio hapa tu, hata Afrika Kusini, aliyekuwa kocha wa timu ya taifa ya nchi hiyo, Pits Mosimame aliwahi kukaririwa na vyombo vya habari akijibu swali kwanini Bafana Bafana haijashinda mechi nyingi tangu achukue madaraka.
Naye  alijibu kwa urahisi kuwa shirikisho la soka la Afrika Kusini halijamlipa Sangoma (mganga wa kienyeji) tangu michuano ya kombe la dunia. Hali hiyo inaonyesha namna gani jamii imetawaliwa na uchawi. Kila kitu tunachofanya kinaonekana kimetokana na uchawi. Wachawi wamekuwa vikwazo kwenye mafanikio ya jamii yetu.
Dhana hii ya uchawi itaendelea kutuangamiza ikiwa juhudi za makusudi hazitachukuliwa. Kwa mtazamo wangu, naona uchawi ni sumu kali sana, lakini kama uchawi wa kisayansi basi nitasema kila nchi inao uchawi.
Nasema kila nchi inao uchawi kwa maana ya kisayansi kutokana na mila na desturi za nchi hiyo. Ujerumani walileta utabiri wa Pweza Paul, akatabiri ushindi kwa wahispania. Nao ni uchawi kama wapiga ramli za kisayansi sio mazingaombwe. Zipo nchi zinatumia uchawi wa kisayansi kwa njia ya maneno hususani katika dini,  “kuapishwa” au “kusimikwa”, kinachotendeka ni uchawi, ni mila na desturi za nchi husika na tamaduni zao. Mikoa ya kanda ya ziwa inakabiliwa na dhana hii ya uchawi imesababisha hofu kwa ndugu zetu albino, na wazee wenye macho mekundu. Wazee hao huuawa kwa kisingizio eti wachawi. Nionavyo uchawi uliosababisha watu wa mji wa Kilosa waandamane mapema mwezi Mei mwaka huu ni sumu kali sana, na kawaida sumu haiwezi kutibu ugonjwa mwingine, kwani huua.

John Chitanya ni mwandishi na mwalimu wa Miracle Center, mjini Songea. Niandikie: 0718 005557

March 09, 2010

NIAZIME KONDOMU, NIPO BAGAMOYO

Hakika nakuomba msomaji wangu, watu wangu NIAZIMENI KONDOMU usifanye mchezo nimezidiwa kiasi ambacho inanilazimu kuomba msaada wa kondomu. Haya ni maisha ya huku sasa, maana kila mmoja anafanya kile anavyojisikia, ingawaje ni kawaida sana.

Sasa mimi nasema naomba msaada wa kondomu maana usiku nilivyoupitisha, nimeletewa MAKAHABA wawili, halafu kahaba wa pili akaomba kondomu ili amsadie kahaba mwenzie kwakuwa dume lake halikuwa na kondomu.

Siku zote naamini utafiti wakati mwingine inabidi uingie mwenyewe ushuhudie, na mchakato wangu wa kitabu kile ni lazima niingie maeneo magumu yenye vishawishi adhimu. BASI jana usiku nilikuwa na rafiki zangu, na kwakuwa hawa jamaa wamekuja na Wapennzi wao, wakaanza kunishambulia eti nitajiuuuuu(ulikuwa utani) wakati tukiendelea na porojo akaja mzee wa mapokezi akaniambia 'mjukuu usipate taabu wewe sema tu sasa hivi utapata, huu ni mji wa kimataifa bwana'.

Ikabidi nitulie kisha nikamjibu hebu niletee binti mmoja nimchungulie kidogo. Wakati nipo sehemu ya chakula, chumba changu nimekifunga, kumbe yule mzee akampigia simu kahaba mmoja hivi, nadhani anafahamiana nao. Akajiingiza hapa kwenye nyumba tuliyopo, lakini mlango wangu ukawa umefungwa(sikuwepo).

Punde niliporejea, nikaona mzee ananilaumu mbona binti alikuja, ila ameahidi kuwa atakuja tena. Kweli zilipita dakika 15 hivi, nikiwa chumbani naongea na rafiki zangu, mara mlango ukagongwa na yule mzee, nikawaambia jamani waungwana nendeni chumbani kwenu. Mzee akanikabidhi binti tuelewane......
Akakaa kitini na kuniambia anisikiliza, ikabidi niulize inakuwaje mbona unanijia? Akaniambia kuwa alielezwa na mzee kuwa nahitaji kupunguza ngare.

Nikauliza bei gani bila kondomu na bei gani kwa kondomu. Duh! jamani niazimeni kondomu .......tafadhali sina huku Bagamoyo. Yule binti bila kusita akaniambia kuwa hawezi kulala hapo kwangu kwani mtoto wake yuko nyumbani, kwahiyo bila kondomu 10.000 na tukitumia kondomu 5000.

Upo hapo? nikauliza swali inakuwaje mtoto aachwe nyumbani halafu yeye yuko hapo? Nikajibiwa hayanihusu, bali tufanye kazi(ku*******) kisha atimue zake. Nikatoa amri moja 'nenda kwenu kapumzike na mwanao, siwezi kulala na wewe wakati mwanao yuko mpweke hana mapenzi ya mama. Jamani akaniambia labda sina haja, nataka kumchezea tu kwa muda wake, nikafungua mlango nikamwabia hamna noma wewe nenda tu................

Kumbe yule mzee anakuwa na kigawo chake baada ya shughuli maana alinilalamikia vipi mjukuu unanikosesha kipato? Nikamwambia tafuta mwingine, huyo amezaa kwahiyo mimi na huyo ni mwiko.
Nikaletewa mwingine, huyu ndiye aliniacha hoi kwamba atalala hadi asubuhi hii ninavyoandika hapa, ila suala la kondomu au bila kondomu ni chaguo langu ila bei 10000. Dakika hiyo amekaa kitandani, na mzee ananiambia bei ndiyo hiyo kwahiyo kazi kwako.

Nikasema asante, waweza kwenda binti. Kitu nilichojifunza ni kwamba, niliuliza swali kwa binti huyo na mzee wa mapokezi ni kwanini anadhani kumekuwa na wimbi la ukahaba katika miji mbalimbali duniani? Nilijibiwa ni MAISHA TU. Sijui wewe unayesoma unaelewa nini maana watu wamegeuza miili yao kuwa biashara. Nimejiuliza sana kwanini binti aseme kuwa suala la kondomu ni uamuzi wangu ila anachohitaji ni malipo yake.
Mwenzangu yakanishinda, nikaomba niachwe kama nilivyo... nikawafuata rafiki zangu nikawaambia ipo kazi hapo ni 'cleverness without wisdom'.

KITUKO KIKALI
Mzee wa mapokezi anaye mkewe, lakini siku ya jana amefumaniwa baada ya kuchukua mwanamke mmoja hivi akataka amfi**** unaona yaani nyu***. Sasa alikuwa anataka kumlipa huyo mwanamke 20000 ili afanikiwe kuachiwa nyu****. Lakini ugomvi ukazuka, nyumba nzima zogo, watu wakashituka kuna nini, kumbe jamaa analazimisha ataufune uvungu wa nyuma. Ili kumnusuru ilibidi baadhi wapangaji wamshambulie yule mzee ili kumwachia yule mwanamke, lakini haikuwa hivyo kwani baada ya kuitafuna ile ya kawaida jamaa akawa anataka atafune na nyingine ndogo***.

Mungu wangu makahaba wanaushirikiano, na wanamfahamu mke wa yule mzee ilibidi wachukue hatua za kwenda kumchukua....wakakodi pikipiki(hapa ndiyo usafiri wa haraka sana usiku)..... ili amfumanie mumewe.... halafu kumbe nyumba ndogo naye alikuwa akicheza karibu na sehemu ya tukio ili kujionea...... jamani nipeni kondomu hakika hali hiiiiiiii we acha tu.
Baada ya fumanizi yule mzee kwakuwa alitaka kumfi**** yule kahaba kwani haikuwa siri tena yule mwanamke alikuwa akipayuka na kuwaeleza watu anataka kinyumenyume.....akasimulia yaani jana nimelala saa sita usiku hivi duh!
Sijui nisemeje kwani hii hali inaonekana wazi kuwa inashamiri na sisi wanadamu tunaonekana utashi wetu unadidimia kila kukicha.

Lakini mimi naomba kondomu ili nami nijinufaishe hapa, na rafiki zangu wananicheka sana na kituko changu cha kumkataa kahaba aliyezaa, kisha kumkataa mwingine ambaye baadaye aliomba msaada wa kondomu. Ni mambo juu ya mambo yamenikuna sana, najikuna na kujifunza.......lakini naomba sana mnitumie kondomu maana hapa nilipo sina kwahiyo nahitaji sana msaada wenu waungwana. Karibu Bagamoyo tutalii kwa raha lakini msisahau kuniazima kondomu....

February 20, 2009

Kikwete acha kupiga Mayowe


Nimetulia wala sijaandika maoni yangu kuhusu ujio wa Hu Jintao wa China. Nimtumiwa sms nyingi na waraka pepe kwamba ninaonaje ujio huo na kauli zako kuhusu Mkapa. Wengi wanadhani nimebadilika kimtazamo kwani kuna mambo siyajadili,sipendekezi au kuongoza njia.BADO NIPO SANA!
Wapo wanaolalamika kwamba nimeacha kujadili mada zangu za kuhusu bara la afrika, wanadai ninapwaya katika mada za nyumbani bongo. Lakini nasema kuna mambo yanaingiliana, kwasasa nakula darasa kali sana kuhusu mashariki ya kati na yanayowahusu, pia na shughuli zangu za maisha.
Sasa ninaandika hapa kama mwanzo tu kwani natarajia kuandika wazi zaidi. Sikubaliani na mtazamo au porojo za Rais Kikwete kwamba uwanja taifa ni juhudi za Mkapa na uzuri wake. Mimi nasema ni juhudi za watanzania, kwani hakubuni bali aliahidi kwasababu ni wajibu wake kuteda hivyo.
Sasa basi kutwambia kwamba hayo ni mazuri yake ni kutulazimika kunya mavi jamvini huku msosi upo tayari kwa kuliwa. Sikubali kwamba mambo machafu ayaliyoyatenda eti yamekuwa mazuri na kupakwa rangi au marumaru. Kwanza nitakumbusha BOT ujenzi wake.
Bodi ya wahandisi nakumbuka ilifanya tathmini na kusema kwamba ni bilioni 56 zingtosha kujenga BOT tena bila msaada wa nchi yeyote, lakini uwongo ukatungwa halafu tukaambiwa BOT imejengwa kwa milioni 700 huku mjenzi wake alitaka milioni 70. Je nini kilichofanywa hadi ikapandishwa bei kiasi hicho? Au unadhani uzuri wa mtu husemwa tu kama ufanywavyo wewe?
Huo uwanja wa soka nani amekwambia Watanzania hawajui uzuri wa mtu? Watakula uwanja na kunya uwanja? Ingawa kwa wapenda soka tunafurahi, lakini nguvu ya kushangilia tutoe wapi? Ni kweli kulikuwa na umuhimu wa kumpamba tena Benjamini? kwa sababu naamini ni jukumu lake na tulimtuma kufanya kazi kwa ajili yetu full stop! Sasa unapopiga mayowe eti jamaniiii mkapaaaa alijenga uwanja huuuuuuuu.
Nini thamani ya mgodi wa Kiwira ambao ulikuwa na Milioni 700 halafu wakijiuzia na Yona Milioni 70? Au unadhani kila mtu kipofu, haoni anakubali kuchekewa na kulishwa porojo kama zile ulizozitoa uwanja wa taifa. Unafikiri wenye kiona mbali tunajali kwamba eti Hu Jintao alikuja kuzindua uwanja? thubutu labda wajinga wajinga watachekelea mpaka kupasuka misamba ya midomo halafu wasijipe muda wa kufanya tafakuri.
Kwani nani hajui mashtaka mengi yaliyopo ni porojo na ngebe za uchaguzi? Unafikiri tunafundishwa uzuri wa mtu kwa hotuba au matamko? Sikiliza wahenga walisema 'mtoto acha kupiga mayowe, acha watu waone wenyewe'
'usiseme sana kwani tusiposema hatumaanishi hatuna ila tunakutazama tu ili tujue umahiri wako wa kuchanganua hoja.
Amka, hujasikia kama ni kizazi cha dhahabu cha Nyerere kinakuja, hujui. Zubaa uchekwe. Nitajadili zaidi nje ya blogu.