Showing posts with label mafundisho. Show all posts
Showing posts with label mafundisho. Show all posts

March 21, 2018

JE, JAMII IMECHOKA KUISHI KWA MAFUNDISHO YANAYOTOLEWA KWA MIFANO?

Na KIZITO MPANGALA

Mafundisho ni moja kati ya elimu ambayo haina mpinzani katika maisha yetu ya kila siku. Mafundisho hayo yapo kwa namna mbalimbali, kuna mafundisho ya jumla, kuna mfundisho ya kipekee ambayo hugusia katika uga husika kama vile mafundisho ya dini, mafundisho ya stadi za kazi, mafundisho ya maadili, mafundisho ya rika na kadhalika. Hayo yote husaidia kujenga jamii na kuiweka katika mwenendo unaokunalika na wengi na ambao una manufaa mazuri kawa jamii hiyo na pengine hata kuakisi kwa jamii nyingine mahali popote duniani.
Mafundisho ya kijinsia yana umuhimu mkubwa sana katika maisha yetu. Jinsia fulani ifundwe yale yanayopaswa kufanyika nayo ili kuendeleza maadili au jeme lipatikanalo kutoka katika mafundisho hayo. Ikiwa mtu wa jinsia tofauti ataifunda jinsia nyingine fundisho fulani, kinachotakiwa ni kufikiri kilichosemwa ili kubaini kama kina manufaa ya kurekebisha kitu fulani kwa jinsia iliyofundwa au kama kina maudhui mabaya dhidi ya jinsia iliyofundwa kishapo hukumu itolewe, iwe hukumu chanya au hukumu hasi.
Kitendo cha kutoa mafundisho kinaweza kuwa cha namna mbili. Huenda mafundisho yakatolewa kinagaubaga au kwa kutumia mifano ambayo inalenga kurekebisha jambo fulani katika jamii. Ikiwa hilo linafanyika, si vema kulalamika ghafla bila kufikiri lengo au dhamira ya mafundisho hayo. Na kwa sasa jinsi ilivyo rahisi kusambaza taarifa katika mitandao basi ndani ya dakika kadhaa dunia yote huenda ikajua kinachojiri na kisha kila aliyepata taarifa anatoa maelezo yake kadiri ya taarifa ilivyomfikia. Watasifu, watalaani, watahamasisha watu kuwa watulivu, watamshutumu mnenaji, watamtetea mnenaji na kadhalika.
Katika suala hili la kuishi katika mafundisho yanayotolewa kwa mifano, inawezekana mfundaji anakuwa na nia ya kuonya au kurekebisha jambo fulani lakini huenda akaeleweka tofauti na lengo la fundisho lake. Hii inatokea mara nyingi na pengine husababisha maandamano ambayo yanaweza kuzua madhara kwa waandamanaji wakiwa wanakemea fundisho wasilolikubali au kama limefikirirwa kuwa ni la kejeli kawa kundi fulani katika jamii.

December 01, 2017

MACHO VITABUNI


NAAM! Mara kadhaa ninapotembelea jiji la Dar es salaam wengi hutuita  wageni kama “watu wa mikoani”. Lakini ninachokiona wakati mwingine ni kuzikali fursa ikiwemo ya kutembelea maduka ya vitabu.

Wahenga wanasema ni heri ukatekwa nyara, kushikiliwa mateka kwa muda fulani katika duka la vitabu kwani unakuwa umehiari mwenyewe. Pia wanasisitiza kitabu ni silaha. 

November 13, 2017

KWANINI SEKRETARIETI YA AJIRA HAINA MATAWI NCHINI?

NA MARKUS MPANGALA
MIAKA kadhaa iliyopita nilishindwa kuwaelewa kabisa watendaji wa Wakala  wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) hapa nchini. Nilikuwa siwaelewi kwa sababu siku moja niliwahushudia wafanyabiashara fulani kutoka Songea mkoani Ruvuma, wakizunguka vyumba vya ofisi vya taasisi hiyo kwenye jengo la Ushirika liliko Barabara ya Lumumba, Mnazi Mmoja jijini Dar es salaam kwa madhumuni ya kusajili kampuni yao.  
Jenista Mhagama

Pili,niliwahi kumsaidia rafiki yangu, Albert Nyaluke Sanga, ambaye ni mfanyabiashara mkubwa mkoani Iringa, ili apate leseni ya biashara. Haikuwa leseni yake binafsi, bali aliamua kumsaidia kijana mmoja aliyekuwa na ndoto za kuwa mfanyabiashara, lakini alikosa pa kunzia.
Rafiki yangu huyo anapenda kuwasaidia vijana wanaojishughulisha na ujasiriamali kwa sababu anaamini hiyo ndiyo njia pekee ya kuwakomboa, badala ya elimu yao na kuondokana na matembezi ya kusambaza bahasha za kuomba nafasi za kazi.

October 27, 2017

FELA ANIKULAPO KUTI: MWANAMUZIKI ALIYEASISI MTINDO WA PIJINI KATIKA MUZIKI NCHINI NIGERIA NA KUOA WANAWAKE 27.

NA KIZITO MPANGALA

TUNASIKILIZA muziki wa Nigeria mara kwa mara na pengine huenda uliwahi kujihoji aina lugha wanayotumia kuimba na hata katika mazungumzo ya kwaida ya wananchi wa Nigeria. Mtindo huo umejaa pijini kwa kiasi kikubwa hali iliyopelekea kuitwa NIGERIAN ENGLISH.

Fela Anikulapo Kuti alizaliwa  mjini Abeokuta nchini Nigeria mwaka 1938. Alipewa majina OLUFELA OLUSEGUN OLUDOTUM RANSOME ANIKULAPO KUTI lakini alifupisha na kuwa FELA ANIKULAPO KUTI. Mama yake alikuwa ni mwanaharakati wa haki za wanawake katika utawala wa kikoloni wakati huo, na baba yake alikuwa ni mwalimu na vilevile alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa kwanza mweusi wa chama cha walimu nchini Nigeria. Fela ni binamu ya Akimwande Oluwole Babatubde Soyinka maarufu kama Wole Soyinka.

Fela alisoma nchini Nigeria na baadae mwaka 1958 alikwenda nchini Uingereza kwa ajili ya kusoma Udakitari wa Dawa lakini alipofika huko alivutiwa na masomo ya muziki hivyo akasoma masomo hayo ya muziki katika chuo cha Trinity. Fela alikuwa mjuzi wa kupiga tarumbeta na Saxophone.

Alianzisha bendi yake iliyoitwa Koola Labitos ambayo ilipiga muziki aina ya jazz.  Huko alimuoa mwanamke aliyeitwa Remilekun Taylor na wakawa na watoto watatu. Mwaka 1963 alirudi nchini Nigeria na kuendelea na bendi yake aliyoianzisha na pia utangazaji katika shirika la utangazaji redioni la Nigeria.
Mwaka 1967 alihamia nchini Ghana na kuanzisha mtindo mpya wa muziki ambao uliitwa Afrobeat. Mwaka 1979 alisafiri kwenda Marekani na alikaa kwa muda wa miezi 10 jijini Los Angels, huko alibadili jina la bendi yake na kuitwa NIGERIA 70. Baadae alitimuliwa nchini humo pamoja na waimbaji wenzake kwa kutokuwa na kibali cha kufanya kazi nchini humo.

October 19, 2017

STEPHEN HAWKING: MWANAFIZIKIA MGONJWA WA MUDA MREFU.

NA KIZITO MPANGALA

STEPHEN HAWKING alizaliwa mwaka 1942 jijini Oxford nchini Uingereza kwa wazazi Frank Hawking na Isobel Hawking. Japokuwa familia yake ilikuwa na mtikisiko kifedha lakini wazazi wake walijitahidi kujiendeleza kielimu katika chuo kikuu cha Oxford. Baba yake alisoma udakitari wa dawa na mama yake alisoma Falsafa, Sayansi ya Siasa, na Uchumi katika chuo hicho.

Baba yake na mama yake walikutana kwa mara ya kwanza muda mfupi tu bada ya kuanza kwa vita ya pili ya dunia katika Taasisi ya Utafiti wa Dawa ambapo baba yake alikuwa mtafiti  na mama yake alikuwa katibu wa taasisi hiyo. Ndipo mapenzi yao yalipoanza na walibahatika kupata mtoto wa kiume ambaye ni Stephen Hawking.