Showing posts with label Mahojiano. Show all posts
Showing posts with label Mahojiano. Show all posts

December 06, 2017

“NYASA INAWEZA KUJENGA KIWANDA CHA MATUNDA. HOTELI NAZO ZINATUDAI MAHITAJI MENGI WANYASA”

NA MARKUS MPANGALA

MAELFU ya vijana waliotokea Wilaya ya Nyasa mkoa wa Ruvuma wamesoma elimu ya Sekondari  katika shule ya Lundo iliyopo Kata ya Lipingo wilayani humo. Hata hivyo sio vijana wote wamepata elimu ya sekondari ndani ya Wilaya ya Nyasa au shule hiyo pekee, lakini idadi kubwa wamesoma hapo. Katika kipindi cha miaka 2000 kumekuwa na ongezeko la shule za sekondari, ambapo nyingi sasa hivi ni za Kata tofauti na awali. 

Miongoni mwao ni ALPHONCE KWENDE ambaye ni mwanazuoni wa masuala ya Kilimo hapa nchini.  Yeye ni mzaliwa wa kijiji cha Chinula, tukiwa tumehitimu pamoja shuleni.  Amejikita katika fani ya Kilimo na anaitazama wilaya Nyasa ikiwa na uwezo wa kujenga Kiwanda pamoja na watu kubadilika kuwa na mawazo ya kibiashara kupitia kilimo. 
SOMA MAHOJIANO KAMILI…..

SWALI:  Habari za mchana mtumishi. Hebu tueleze baada ya  elimu ya Sekondari  Lundo ulichaguwa kwenda shule gani?
ALPHONCE KWENDE: Yes, nilijiunga na Kibiti High School, iliyopo mkoani Pwani kusoma masomo ya kidato cha tano na sita.
Mwanazuoni KWENDE akiwa kwenye shughuli za Kilimo.

SWALI: Umewahi kujiunga na Chuo chochote baada ya kuhitimua ‘High School’?
KWENDE: Sikujiunga na Chuo Kikuu kingine zaidi ya SUA. Hiki ni Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, kipo mkoani Morogoro. Hapo ndipo nilihitimu Shahada yangu ya Kilimo kwa ujumla wake.

SWALI: Aaah! Ndiyo maana kilimo kimekushika sana? Nadhani ni msingi wa Lundo katika somo hilo. Nililipenda sana ila likafutwa. 
KWENDE: Ni kweli kabisa. Kabisa, Lundo walitengeneza msingi mzuri sana kwenye somo la Kilimo, ndiyo matunda yake niliyonayo sasa. Nilimalizana na elimua ye sekondari ya juu  High School, mwaka 2004. Kisha mwaka 2009 nilifanikiwa kuhitimu shahada yangu ya Kilimo pale SUA.

SWALI: Tutajie mambo muhimu ambayo unadhani yanaweza kuipaisha Wilaya ya Nyasa kiuchumi, Afya na Mengine.

KWENDE: Kujibu hilo inatakiwa akili iwe imetulia kidogo. Mimi ningependa sana kuzungumzia sekta yangu ya Kilimo na Ufugaji. Ujio wa Wilaya ya Nyasa unaibua hitaji kubwa sana la kuanza kufanya kilimo chenye tija na cha kibiashara maana mpaka sasa bado wilaya ya Nyasa inategemea Muhogo kama zao kwa chakula na biashara. Ingawaje jitihada zinaendelea kufanyika kuendeleza uzalishaji wa zao hilo ili lilete kipato cha kutosha kwa wakulima hao. Ujio wa Wilaya mpya unakuja na ujenzi wa Mahoteli ambako hakuna uzalishaji wa kutosha mpaka sasa wa mazao ya bustani ya uhakika kukidhi hitaji hilo hivyo kutakuwa na uhitaji wa mboga hizo na matunda kama Mananasi,Parachichi,Matango,Matikiti maji na kadhalika.
Mojawapo ya Hoteli iliyopo wilaya ya Nyasa.
SWALI: Bwana Kwende hapa unatudhihirishia kuwa fursa hii inawahitaji waliosomea fani ya Horticulture (kilimo cha mboga mboga na matunda), kwamba wanahitajika sana Nyasa?

December 29, 2012

SIKU NILIPOHOJIWA NA DANIEL R. GINGO


Daniel Gingo akionyesha moja ya kitabu alichoandika.
NB: Wiki kadhaa zilizopita rafiki yangu huyu aliamua kujadiliana nami jambo muhimu kuhusu sekta ya habari hapa nchini. Haya ndiyo tuliyoongelea japo kwa ufupi kutokana na muda mchache. Karibuni........
DANIEL GINGO: Kuna huu mfumo ambao vyombo vyetu vinautumia kutuhabarisha habari za Ulimwengu kwa mfano: Gazeti la The Gurdian, linaweza likawa na kurasa hata sita zilizosheheni habari kutoka Reuters, BBC, UPI, AP na Xinhua ya China.
TBC: inaweza kusheheni habari kutoka RT au Al-Jazeera, ITV inaweza ikawa na habari za CNN, BBC, na vipindi kibao ambavyo hatujavitengeneza hapa nchini, na wakati mwingine tunavilipia. Je, mfumo huu unavinufuaisha vyombo vyetu vya habari au tunakuwa victims?
MARKUS MPANGALA: Nadhani kila TV inakuwa na makubaliano na kituo cha nje. Kuna mikataba ya kurusha matangazo baina ya TV zetu na za nje.
Kama STAR TV na DW. .....kimsingi hii ni moja hasara kubwa tunayopata katika sekta ya habari na jamii yetu. Sababu CNN, DW, BBC, RT na wengineo hawana muda wa kuonyesha vipindi vya TV zetu.
Hili ni tatizo kubwa sana nadhani TCRA inatakiwa kuwa na mchakato wa kupiga marufu au kupunguza muda wa vipindi vya TV za nje. Channel Ten wao wana SKY NEWS.
Kwa kweli ni hasara sababu badala ya kumuonyesha mkulima wa kisasa sisi tunaonyesha Beckham akiwa mitaa na watoto wake.
Kwa kweli mimi hata DIRA YA DUNIA nimeshindwa kukiangalia sababu malengo ni yale yale kuwa afrika chafu na makamasi.
DANIEL GINGO: Hasara inakujaje kwetu hapo?
MARKUS MPANGALA: Kwanza, tunapoteza nafasi ya kuhabarisha habari nyingi za kwetu. Pili, tunashindwa kuzitangaza habari zetu kupitia hao hao tunaokubaliana nao kurusha vipindi vyao.

Markus Mpangala katika tafakari zaidi kabla ya kujibu maswali.
DANIEL GINGO: Na wao wanafaidikaje?
MARKUS MPANGALA: Lazima tuchukue nafasi ya kuonyesha mambo ya kwetu, sio kuhamisha tu ya nje na kuyaleta.
Kwa mfano kama TV inakuwa na saa 4 za kuonyesha mambo ya Russia. je Russia wanatumia saa ngapi kuonyesha ya kwetu?
Kwa maana nyingine sisi kazi yetu ni kubebeshwa tu habari za CNN, BBC na kuzirusha huku, lakini wao hawana muda na habari za mkulima wa viazi kule mbeya.
DANIEL GINGO: Tena wakati mwingine tunazipokea bila hata kuzihariri, zikiwa za uongo wanazirusha hivyo hivyo. Nikuulize swali la nyongeza?
MARKUS MPANGALA: Na ukweli kabisa huo. Ili kupunguza lazima TCRA ichukue hatua, wengi wanadhani China ni wajinga kuzuia CNN, BBC, Facebook na mengine kujaza habari zao kule China. Lakini naona walikuwa na hekima zaidi. Siku hizi habari zingine mbovu kabisa kwenye hizoTv za nje basi tu.
DANIEL GINGO: Lakini. Ikiwa TCRA watafanyia kazi ushauri huo, unadhani tunaweza kumudu kujaza nafasi zilizoachwa wazi na CNN, BBC, Hollywood nk?
MARKUS MPANGALA: Tunaweza kabisa. tunayo mambo mengi nchi hii hayatangazwi. Mfumo wetu wa habari bado unategemea, sio kujitegemea kuendesha mambo.
Ninaposema kutegemea ni ile hali ya kungojea matukio au habari fulani, badala ya kujitegemea kwakuwa na vipindi vingi vyenye tija kwa taifa.
Nina uhakika CNN au nyingine haiwezi kuwa kila kitu nchini. Hakika nakuambia, tunaweza kuwa na habari nyingi iwapo vyombo vyetu vya habari vitaanza kujitegemea.
DANIEL GINGO: Ninamaanisha hivi: Je, vyombo vyetu vya habari vina pesa na nyezo za kutosha kwenda Rubili kule Kagera, Rusumo kule Ngara, Kizorogoto kule Morogoro, Makiungu kule Singida, Kilindi kule Handeni, Kerenge kule Korogwe nk kwa ajili ya ku-cover matukio?
MARKUS MPANGALA: Naam ndio maana nimesema vyombo vyetu vinaendeshwa kwa Kutegemea sio Kujitegemea. Kwahiyo kujitegemea ni kama hivyo unavyosema, je vitaweza kwenda ku-cover story kule? Mimi nadhani inawezekana, na kilichokosekana ni msukumo.
Hawa Mwananchi kuna mtindo fulani wanaufanya kwa upande wa magazeti yao. Wana kitu fulani wanakionyesha lakini najua inahitaji gharama sana.
Hata hivyo ukitaka kuleta ufanisi katika vyombo vyetu lazima bajeti zao ziwe za kutosha kwa kuwekeza kwa ku-cover story sio posho na mengineyo. Tulichokosa ni Dhamira. Matokeo yake, Tunajikuta tunategemea tu.