May 05, 2018

TAARIFA MUHIMU: TUMESITISHA KUWEKA TAARIFA MPYA ZA NYASA

MARKUS MPANGALA
SALAAM nyi wasomaji wetu wapendwa! 
Ni matumaini yetu nyote mna afya njema na Mwenyezi Mungu amewajalia hilo bila hiyana. Tumshukuru zaidi.
Kwa muda mrefu  nimekuwa nikitoa huduma ya habari za mwambao wa Ziwa Nyasa na yatokanayo na wilaya ya Nyasa, mkoani Ruvuma. Nimekuwa nikifanya hivi kama mapenzi yangu tu (bila kutafuta faida yoyote ya fedha). Sikulipwa chochote kwa kutoa huduma hiyo ya kutangaza vivutio vya utalii, utamaduni, changamoto na mambo mseto ya wakazi wa maeneo hayo. 

March 26, 2018

MWONEKANO WA ZIWA NYASA KATIKA KIJIJI CHA MBAHA WILAYA YA NYASA

NGUZO ZA GATI LA BANDARI YA NDUMBI

AFISA MTENDAJI MPYA WA KIJIJI CHA LUNDU

Mara baada ya kustaafu kazi ya utendaji wa kijiji, bwana Remigius Nyenyembe maarufu kama Remmy au Fish, Kijiji chetu cha Lundu hakikupata mtendaji kwa muda mrefu ikasababisha Afisa Maendeleo wa Kata kukaimu nafasi hiyo.
 
Sasa kijiji chetu cha Lundu kimepata Afisa Mtendaji ambaye amewasili kijijini kwetu hapa tayari kuanza kazi. Ni mwenyeji wa Arusha, kwa jinsia ni mwanamke. Tunawaomba wanakijiji wenzetu wa Lundu wampokee na kumkaribisha ajione kama yuko Njiro,Philips,Ngarenaro,Ngaramtoni,Usa river, Sinoni daraja mbili yaani namaanisha Arusha.
KIJIJI CHA LUNDU
Kwa wakazi wa kijiji chetu kama watamtumia vizuri basi atasaidia kuleta maendeleo kwenye kijiji chetu kwasababu hawa wataalamu siku hizi wana viwango vizuri vya elimu na wamesomea masuala ya Maendeleo ya Jamii katika vyuo vinavyotambuliwa na serikali kama vile Homboro na vyuo vikuu vingine.

Tumtumie vyema mtendaji wetu kwa manufaa ya kijiji chetu cha Lundu kupata maendeleo. Itapendeza sana kama suala la kulewa asubuhi litapatiwa ufumbuzi maana wanywaji wamezidi.

©Honorius Mpangala

SIMBA, YANGA WANAIMBA KIMUNGU WANACHEZA KISHETANI.

Na. HONORIUS MPANGALA 
Nilikuwa nchini Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo April 4, 2015 siku ya pasaka. Kulikuwa na mchezo wa wa mtoano kuelekea kwenye makundi klabu bingwa Afrika kati ya Tp Mazembe wenyeji dhidi ya Orlando Pirates. Mitaani kila uliyemwona alikuwa amevalia jezi ya Mazembe na akizungumza kuhusu Mazembe huku wakielekea uwanjani Estadio de Mazembe. 

Nilimuuliza mlinzi wa eneo nilioenda kuhusu mashabiki FC Lupopo hawawezi kwenda uwanjani? Akanijibu hata Mimi ni Lupopo lakini inapokuja uwakilishi wote tunakuwa wamoja. Akanieleza hata uwanjani huioni jezi ya Lupopo. Mechi ile ilimalizika kwa TP kupata matokeo ya goli tatu kwa moja yaliyofungwa na Ranford Kalaba,Mbwana Samata na Rogers Asale. 
SIMBA

Nilikaa na mlinzi yule tukisikiliza matangazo ya redio kwa lugha ya kifaransa naye alinitafsiria kwa kiswahili cha kikongo. Wakati magoli yote yanaingia katika lango la Orlando alikuwa akisimama na kushangilia. Huo ndio utofauti wetu na wao inapokuja suala la michuano ya kimataifa.
Sababu ya pili ambayo inapelekea timu zetu za kitanzania kuwa na wakati mgumu ni kwa upande wa wachezaji. Upande Huu unatokana na ile hali ambayo wachezaji wanaichukulia katika mchezo. Huweza kuingia uwanjani wakiwa wamejiamini sana lakini ni kelele za dakika chache toka kwa mashabiki wanao wafahamu zitawafanya wachanganyikiwe.

MIAKA 188 YA KIFO YENYE CHANGAMOTO ZA MAISHA NA MATUNDA YAKE YA HISABATI

NA KIZITO MPANGALA
MACHI 21 ilikuwa ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa gwiji la hisabati, Joseph Fourier, kutoa nchini Ufaransa. Imetimia miaka 250 tangu alipozaliwa mwaka 1760 kijiiini Auxere nchini Ufaransa. Yeye ni mmojawapo kati ya wanahisabati mashuhuri duniani.

Katika kazi zake mbalimbali, aliwahi kuandika maneno haya: "hakuna lugha ambayo ni bora sana au nzuri sana kushinda lugha zingine, vile vile hakuna lugha iliyo ngumu sana au rahisi sana kushinda lugha zingine, uchambuzi wa nadharia za hisabati ni mzito sana kama ilivyo asili yake."


Kazi zake nyingi bado ni msaada mkubwa kwa wataalamu mbalimbali hasa katika Sayansi na Teknolojia. Ni akili ya kawaida tu kama ilivyo kwangu na kwako msomaji, tunaweza kuwa na umahiri katika uga (field) tuupendao kila mmoja wetu kwa juhudi na maarifa. 

March 23, 2018

LAURA BASSI: PROFESA WA KWANZA MWANAMKE BARANI ULAYA.

Na Kizito Mpangala

Wanawake wanayo nafasi ya kufikia malengo ambayo wanakusudia, ni kwa juhudi na maarifa wataweza kufikia malengo hayo. Suala la kipaumbele kwa wanawake duniani kote limepitia hatua kadhaa za ushawishi na changamoto kadhaa ambazo hasa huwakabili wanawake wenyewe. Katika uga wa sayansi na teknolojia, ni wanawake wachache ambao wamefikia malengo yao ugani humo. Hata sasa uhamasishaji bado unaendelea duniani kote.

Haikuwa kazi rahisi kwa mwanafizikia Laura Caterina Bassi kufikia kiwango cha profesa wa Fizikia katika chuo kikuu cha Bologna nchini Italia.
Laura Bassi alizaliwa mwaka 1711 mjini Bologna nchini Italia ambapo baba yake alikuwa mwanasheria. Laura Bassi alifundishwa nyumbani na mwalimu aliyeajiriwa na familia yake kwa muda wa miaka saba. Alianza kufundishwa akiwa na umri wa miaka 13. Mwalimu wake, Gaetano Tacconi, alimwelekeza zaidi katika sayansi na hisabati ndipo Laura alipoingiwa na hamu ya kutaka kujua zaidi yaliyomo katika sayansi.

Kutokana na msukumo aliokuwa nao katika sayansi, Laura alivutiwa zaidi na somo la Fizikia ambapo alijifunza zaidi kuhusu Sayansi ya Newton (Newtonian Science) ingawa mwalimu wake alitarajia kwamba Laura atajikita zaodi katika hisabati, lakini haikuwa hivyo.
Laura Bassi, katika juhudi zake za masomo alilazimika kusoma pia hisabati ili kujiimarisha katika Fizikia. Hapa Laura alimuomba binamu yake, Padre Lolenzo Stegani, amfundishe hisabati. Padre Lolenzo Stegani alikuwa akijua hisabati na lugha ya kilatini. Kwa kuwa vitabu vingi viliandikwa kwa lugha ya Kilatini, Laura alipaswa kujifunza sarufi ya lugha hiyo na baadae akafundishwa hisabati kwa lugha ya Kilatini.

Baada ya kuweka juhudi zaidi katika elimu hiyo ya sayansi, mwaka 1732 Laura aliandika kazi yake ya kwanza ambayo aliitetea mbele ya hadhira katika mihadhara mbalimbali katika ukumbi wa Pazzalo. Hiyo ilikuwa dira yake ya mafanikio ya elimu aliyokuwa akiitafuta zaidi.

March 22, 2018

MRADI WA MITI KIJIJI CHA LUNDU


Mradi wa shamba la Miti la kijiji cha Lundu linalomilikiwa na Kanisa Katoliki Parokia ya Lundu na kufadhiliwa na Mfuko wa Misitu Tanzania.

WODI ZA KULALA WAGONJWA ZA ZAHANATI YA MTAKATIFU RAPHAEL KIJIJI CHA LUNDU

 

CHANGAMAOTO YA WAKAZI WA MWAMBAO WA ZIWA NYASA NI BARABARA

March 21, 2018

JE, JAMII IMECHOKA KUISHI KWA MAFUNDISHO YANAYOTOLEWA KWA MIFANO?

Na KIZITO MPANGALA

Mafundisho ni moja kati ya elimu ambayo haina mpinzani katika maisha yetu ya kila siku. Mafundisho hayo yapo kwa namna mbalimbali, kuna mafundisho ya jumla, kuna mfundisho ya kipekee ambayo hugusia katika uga husika kama vile mafundisho ya dini, mafundisho ya stadi za kazi, mafundisho ya maadili, mafundisho ya rika na kadhalika. Hayo yote husaidia kujenga jamii na kuiweka katika mwenendo unaokunalika na wengi na ambao una manufaa mazuri kawa jamii hiyo na pengine hata kuakisi kwa jamii nyingine mahali popote duniani.
Mafundisho ya kijinsia yana umuhimu mkubwa sana katika maisha yetu. Jinsia fulani ifundwe yale yanayopaswa kufanyika nayo ili kuendeleza maadili au jeme lipatikanalo kutoka katika mafundisho hayo. Ikiwa mtu wa jinsia tofauti ataifunda jinsia nyingine fundisho fulani, kinachotakiwa ni kufikiri kilichosemwa ili kubaini kama kina manufaa ya kurekebisha kitu fulani kwa jinsia iliyofundwa au kama kina maudhui mabaya dhidi ya jinsia iliyofundwa kishapo hukumu itolewe, iwe hukumu chanya au hukumu hasi.
Kitendo cha kutoa mafundisho kinaweza kuwa cha namna mbili. Huenda mafundisho yakatolewa kinagaubaga au kwa kutumia mifano ambayo inalenga kurekebisha jambo fulani katika jamii. Ikiwa hilo linafanyika, si vema kulalamika ghafla bila kufikiri lengo au dhamira ya mafundisho hayo. Na kwa sasa jinsi ilivyo rahisi kusambaza taarifa katika mitandao basi ndani ya dakika kadhaa dunia yote huenda ikajua kinachojiri na kisha kila aliyepata taarifa anatoa maelezo yake kadiri ya taarifa ilivyomfikia. Watasifu, watalaani, watahamasisha watu kuwa watulivu, watamshutumu mnenaji, watamtetea mnenaji na kadhalika.
Katika suala hili la kuishi katika mafundisho yanayotolewa kwa mifano, inawezekana mfundaji anakuwa na nia ya kuonya au kurekebisha jambo fulani lakini huenda akaeleweka tofauti na lengo la fundisho lake. Hii inatokea mara nyingi na pengine husababisha maandamano ambayo yanaweza kuzua madhara kwa waandamanaji wakiwa wanakemea fundisho wasilolikubali au kama limefikirirwa kuwa ni la kejeli kawa kundi fulani katika jamii.

March 19, 2018

UMUHIMU NA CHANGAMOTO MBALIMBALI ZA NYWILA (PASSWORD)

Na KIZITO MPANGALA

Kila mmoja anatamani kuendeleza siri kubwa ya taarifa zake katika simu yake au tarakilishi (kompyuta) yake ili zisijulikane na wengine. Ulizni wa taarifa hizo husaidiwa na nywila (password). Nywila (password) inaweza kuwa ya haerufu tupu, namba tupu au mchanganyiko wa herufi pamoja na namba na baadhi ya alama za uandishi kama vile mkwaju (/) na kadhalika. Nywila ina umuhimu mkubwa katika ulimwengu huu wa Sayansi na Teknolojia ingawa ilianza kutumika zamani ila siyo kwa kiwango kikubwa kama ilivyo sasa.

Kabla ya kuboreshwa kwa teknolojia ya mawasiliano, zamani password ilijulikana kama “passphrases.” Kwa hiyo nywila ni ufunguo unaolinda lango la kuingilia katika kuzijua taarifa zako ili zisivamiwe na wengine (hackers). Hii ni kwa ajili ya usalama wa mawasiliano yako. Kila mmoja duniani ambaye anatumia tovuti au kurasa mbalimbali hukutana na kipengele cha kuingiza password ili apate anachokihitaji. Malengo ya nywila (password) ni:

1.      Kukupa ruhusa ya kuingia kwenye akaunti husika unayaotembelea,iwe ya kwako au ya mtu mwingine au kikundi au kampuni.

2.    Kuipa ruhusa barua pepe ifunguke ili kuona taarifa zilizomo. Baruapepe inaweza kuwa ya kwako au ya mtu mwingine kadiri ya maelewano kati yenu.

3.    Kulinda vifaa vya kielektroniki ili visitumiwe na wengine ikiwa mmiliki hapendi vitumiwe na wengine. Vifaa hivyo ni kama vile simu, tarakilishi (kompyuta), tarakilishi mpakato (laptop), ubamba (tablets) na kadhalika.

4.    Kupata mtandao (network) ikiwa itahitajika kutumia password.

5.     Kulinda tovuti ili isiingiliwe na wengine (hackers)

6.    Ulinzi wa data binafsi, za kikundi au za kampuni fulani.

March 16, 2018

FURAHA, EASTERLIN PARADOX NA MARIANO ROJAS

NA EZEKIEL KAMWAGA
 
JANA, ripoti kuhusu utafiti wa kimataifa ulioonyesha kwamba nchi yetu ina hali mbaya kwenye kigezo cha furaha kwa watu wake ilizua mjadala wa aina yake. Kuna walioupinga utafiti huo moja kwa moja kwa hoja kwamba ziko nchi zina vita wakati huu na haiwezekani wananchi wake wakawa na furaha kuliko sisi. Wengine wakapinga tu kwa sababu huwa wanapinga. Wengine wakaunga mkono kwa sababu za kisiasa tu.

Kitu kikubwa ambacho nilikiona jana ni kwamba wengi wetu tulitoa maoni kabla hata ya kuisoma ripoti yenyewe. Na hili ndilo tatizo kubwa ambalo wengi wetu tunalo. Tunapenda kutoa maoni katika mambo ambayo ufahamu wetu ni mdogo sana. Nafurahi kwamba nilijipa muda kuisoma ile ripoti jana. Hapa chini ni mawazo yangu baada ya kuisoma. Nimeyagawa mawazo yangu katika pande mbili tofauti; kabla ya kuisoma ripoti hiyo na baada ya kuisoma.

KABLA YA KUISOMA
Mimi ni muumini wa dhana kwamba furaha ni jambo gumu sana kulipima kwa mwanadamu. Nimewahi kuandika humu mitandaoni kwamba kuwa na furaha si jambo unaloweza kulipima kwa sababu ya wingi wa mali au marafiki.

March 12, 2018

KITABU KUHUSU CHINA

Nimemsoma Rais Wa Jamhuri ya watu wa China Mh. XI JINPING katika kitabu chake "THE GOVERNANCE OF CHINA" -Nilichojifunza nakubaliana na mtendaji mkuu wa EPZ Kanali Mstaafu Simbakalia kwamba Chinese are prepared to learn from others but will always import and make that experience relevant to their conditions, traditions and values. That’s why they have Communism “with Chinese characterstics” and Market Economy “with Chinese Characteristics” and so on.
 The Chinese don’t buy the “copy and paste” stupidity of “best practice” from Europe that purports to know what is good and works for everybody (Nakushukuru Sana Comrade Hussein Mtoro kwa zawadi ya kitabu hiki-Hotuba za JINPING zina mafunzo mengi.

©MKUU WA MKOA WA SIMIYU,

ANTONY MTAKA

SASA MWATUGAWA KWA ITIKADI ZA KISIASA.

NA. HONORIUS MPANGALA
 
WAKATI aliyekuwa Rais wa awamu ya kwanza wa taifa hili la Tanzania alikuwa kiongozi aliyewaunganisha watanganyika, sasa mambo yamekuwa tofauti kiasi. Katika hili wako ambao wanashindwa kukemea kutokana na mitazamo ya namna gani wataweza kuonekana mbele ya wenzao kiitikadi.

Hatuko kama majirani zetu kwasababuya  misingi iliyowekwa na waasisi wa taifa hili ni mizuri na inayowafanya wananchi wake kuwa na hofu ya mungu.
Ni jambo la kawaida sana kumkuta mtanzania wa kabila la kisukuma akiwa na mifugo yake katika bondel la mto Lwika huko wilayani Nyasa akiipa malisho mifugo hiyo. Ni kutokana na kazi kubwa iliyofanywa na waasisi wa taifa letu kwa kuondoa suala la ukabila miongoni mwa watanzania.
 Tangu taifa hili liasisiwe hakuja wahi tokea ugomvi wowote uliohusisha makabila moja na jingine. Hii ni kutokana na kujaliana kwetu na kufuata ile misingi ya ugugu baina yetu kama taifa moja. Katika upande wa masuala ya kiimani iliwahi kutokea mara moja katika utawala wa awamu ya tano,mgomo wa wakristo na waisalamu ambao ulihusisha suala la kuchinja.

March 07, 2018

KITABU KIPYA KUTOKA KWA MWANDISHI BEKA MFAUME

JOSEPH BOIMANDA: MTAJI WA MILIONI HAMSINI SERIKALI HAWANA MUDA WA KUKUFUATILIA

NA.HONORIUS MPANGALA
MAISHA popote unaweza kusema hivyo kwani waliofikiria katika hoja hii walikuwa na sababu za msingi zilizokuwa na maana kiuhalisia. Wakati kipato ndio sababu hasa zilizopelekea kukawa na maneno kama haya ambayo yanasadifu uhalisia wa maisha. Katika mazungumzo yangu na mmoja ya watanzania waishio nchini Afrika kusini ilinifanya nistaajabu kile anachonieleza ambacho ndio uhalisisa wa maisha ya huko.

Ni rafiki yangu na ndugu yangu Joseph Boimanda alinifanya nistaajabu pale aliposema mtaji wa milioni hamsini za kitanzania ukiwa Afrika Kusini sio lolote kwa serikali ya huko. Maisha yamekuwa yenye uhuru na amani ya kutosha kwa raia.
Wakati nataka kuyajua haya ananieleza kuwa mamlaka ya mapato ya huko haina muda wa kufuatilia mfanyabiashara wa kati.Kama inatokea mtu anataka kulipa mapato serikalini basi ni hiari yake,hii ni kwa wale wafanyabiashara wadogo na wa kati amabao mtaji yao ni kitu kidigo kwa serikali yao. 

March 05, 2018

MAMBO 10 USIYOYAJUA KUHUSU BUSTANI YA MUNGU- HIFADHI YA KITULO.

1.Hifadhi ya Taifa Kitulo ndiyo eneo pekee Tanzania lenye ndege aina ya tandawala machaka (Denhams Bustard) wenye uwezo wa kuruka kutoka bara moja hadi jingine.
2.Hifadhi hiyo inayopita katika mikoa ya Mbeya na Njombe ilitangazwa rasmi kuwa hifadhi ya Taifa mwaka 2005 ikijumuisha sehemu ya eneo la shamba la mifugo, msitu wa Livingstone na bonde la Numbi.
3.Kitulo ina ukubwa wa kilometa za mraba 442. Awali ilijulikana kama Elton Plateau baada ya Mvumbuzi Fredirick Elton kupita eneo hilo mwaka 1870. Mwaka 1960 Shirika la Chakula na Kilimo (FAO) lilichukua eneo hilo kwa ajili ya ukulima wa ngano na ufugaji wa kondoo.
4. Ndege aina ya tandawili machaka hawapatikani sehemu nyingine yoyote hapa Tanzania zaidi ya Kitulo.
5.hifadhi hiyo ndiyo eneo pekee ambalo ndege hao hutaga mayai na kuzaliana kwa wingi kabla ya kusafiri kwenda mabara mengine.

March 02, 2018

MO IBRAHIM,INUKA JIPUKUTE VUMBI UENDE

Na.Honorius Mpangala
MABADILIKO ya bechi la ufundi katika klabu yoyote huja na matokeo chanya na hasi kulingana na mwenendo wa timu au klabu kwa ujumla.Katika hilo kuna mambo huenda yakawa tofauti kwa wachezaji walioonekana kupata sana nafasi kabla ya mabadiliko.Unayakumbuka maisha ya mchezaji wa Chelsea John Mikel Obi baaada ya kutumuliwa kwa Jose Mourinho pale klabuni.Ujio wa Guus Hindik ulirudisha kwenye hali ya kupata nafasi hadi kufikia hatua ya mashabiki wa kitazania walimpachika jina la Ombeni Sefue.

Kupachikwa kwa jina la Ombeni Sefue kwa Obi kulitokana na jinsi alivyoonekana kutotumika wakati wa Mourinhona alipofika Hidink akaanza kumpa nafasi.Hii ilifananishwa na Sefue wakati wa utawala wa awamu ya tano alivyokuwa hasikiki katika serikali hadi ilipoingia serikali ya awamu ya tano.


Mabadiliko ya makocha yanakuwa yenye kuleta mabadiliko katika vikosi kutokana na kila kocha hupenda kuja na falsafa zao.Hili ndilp lililomkumba mchezaji fundi wa mpira aliyepita katika mashamba ya miwa pale Manungu Turiani Mohammed Ibrahim.Hadi klabu ya Simba inafikia hatua ya kukubali uwezo wake na kumsajili ni kutokana na kile alichokuwa akikifanya akiwa na klabu ya Mtibwa Sugar.

Simba waliamua kufanya usajil ulijumuisha wachezaji watatu kwa pamoja toka Mtibwa sugar yaani waliwasajili Mzamiru Yassin,Shiza Kichuya nay eye Mo Ibrahim ambao walikuwa mhimili mkubwa wa klabu hiyo yeneye maskani yake katika mashamba ya miwa Manungu Turiani.

KUTOKA CHINA HADI CHUO CHA TEKNOLOJIA DAR ES SALAAM (DIT)

NA KIZITO MPANGALA
DUNIANI kuna ubunifu wa namna mbalimbali unafanyika katika teknolojia ili kurahisisha shughuli mbalimbali katika maisha yetu ya kila siku. Ubunifu wa kiteknolojia umekuwa ni lulu mojawapo katika ulimwengu huu wa Sayansi na Teknolojia hasa katika umeme na elektroniksi, ingawa upo ubunifu mwimgine nje ya uga huu wa umeme.
Kiti cha magurudumu manne ni kifaa cha muhimu sana kwa wagonjwa katika hospitali mbalimbali duniani. Na ubunifu mbalimbali hufanyika ili kuboresha utendaji wa kiti hiki. Kiti hiki kwa sasa kina magurudumu manne ambapo makubwa mawili na madogo mawili na hutegemea nguvu za mgonjwa kama anaweza kukisukuma yeye mwenyewe na kama hawezi basi anasukumwa na mtu mwingine.
Tofauti na baiskeli ya magurudumu matatu, kiti hiki kina ukubwa ambao unatosha kwa mtu mmoja tu kuketi na anayesukuma hulazimika kuembea. Vilevile hakichukui nafasi kubwa. Hakiwezi kutumika kama njia mojawapo ya usafiri barabarani kama ilivyo baiskeli ya magurudumu matatu inayotumiwa na walemavu wengi duniani kote.
Kiti hiki kilianza kubuniwa nchini China mnamo karne ya tano na baadae nchini Ugiriki mnamo karne ya sita ambapo kilibuniwa kwa ajili ya kubebea watoto na wazee wasioweza kutembea na kisha kuwasukuma ili kuwafikisha sehemu waliyokusidia. Nchini China awali walikuwa wakitumia matoroli kwa ajili ya kuwabeba wazee wasioweza kutembea na pia vilema na vilevile kubebea mizigo mizito. Michoro ya kiti cha magurudumu mawili iliyochorwa nchini China ilionekana mwaka 525 B.K huko Ulaya.

March 01, 2018

NGOMA ZETU

MIAKA mingi enzi za babu zetu kulikuwa na ngoma maarufu iliyoitwa GEUZA. Hakukuwa na Ligambusa kama ilivyo sasa walisafiri kutoka Lundu kwenda Mbaha au Hinga kucheza Geuza usiku nyakati za Mbalamwezi na wakarudi nyumbani.
 
Kwa upande wa Ngoma ya Mganda, Maboma yaliyoka hadi sasa ni Mawili na yenye upinzani wa Kama vilabu vya soka. LICHUMA LINDU na LIHEGHELYA KONI majina hayo ni kama yanajibizana .Ni ngumu kuona mshiriki wa boma moja kwenda boma lingine nyakati za mazoezi utafukuzwa na kuonekana kama umeenda kuiba stepu(mtindo Wa uchezaji).

Kihoda ndo kimetia fola nyakati za nyuma Lundu ilikuwa na maboma mawili tu yaani Maji na Uamuzi. Lakini kutokana na ongezeko la watu kikafanya kuonekana wanawake wako wengi na wote wanataka kuonyesha uwezo wao wa kusakata ngoma. 

USHAURI KWA RAIS: NAKUOMBA KUBALI TUENDELEE KUCHANGISHANA

NA.HONORIUS MPANGALA
KWANZA kabisa nianze na kukusalimia shikamoo mheshimiwa Rais wangu, Dk. John Pombe Magufuli. Najua hii kazi ni ngumu kama usemavyo wewe mwenyewe lakini sina budi kukuombea uione nyepesi ili uweze kupata nguvu ya kututumikia vyema kama yalivyokuwa malengo yako siku unaenda kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo.

Mheshimiwa nikiwa safarini kuelekea makao makuu ya nchi yetu Dodoma, katika gari nilipata tafakuri  ambayo ilinifanya nitoe kitabu changu cha kuandika kumbukumbu na kuhifadhi mawazo yangu ambayo nimeona nikuandikie. 

Hoja yangu kubwa ambayo ilikuwa ikizunguka katika kichwa changu ni ile niliyokumbuka kauli yako ya kupiga marufuku wananchi kuchangishwa mchango wowote katika shule za serikali.

February 28, 2018

RIWAYA YA NYASITIKI


Nyastiki ni kitabu cha Riwaya kinacho mzungumzia binti aliyefeli mtihani wa darasa la saba na baadae anarudi darasani kusoma.
Nyastiki anakutana na vikwazo vingi lakini hakati tamaa,pia kwenye kitabu cha Nyastiki kimezungumzia namna kina mama wa kambo wanavyotesa watoto hao wa kambo,
Pia namna kina baba wanavyotelekeza familia zao na kuwaachia wakina mama mzigo wakulea familia peke yao.
Nakala ya riwaya hii inapatikana kwa tsh 5000/= tu
Weweza kukipata kupitia

+255712640303
+255767640303
AU email adress
maria.mihanjo@gmail.com