2009-11-18

KICHWA CHINI, MIKONO NYUMA

Fredy Macha namhusudu sana, kama ilivyo kwa Ndesanjo Macha ambaye ni kiini cha mimi kuanza kublogu. Nakumbuka nilikuwa nasoma sana kazi zake katika gazeti la Mwananchi, nikawa nakata ile sehemu ya safu yake na kuihifadhi-hadi leo ninazo sehemu hizo katika makataba yangu ya kijijini na hapa mjini. Nakumbuka mengi kwani wakati nataka nilimjulisha ananiambia ukitaka kublogu usifikirie mbali sana, bali tafakari kawaida tu kwamba una kitu gani ambacho wenzako wanaweza kujifunza toka kwako.

Maneno haya ya Ndesanjo ndiyo ikawa msingi wa mimi kuanza kublogu ingawaje nilianzia katika programu za Wordpress. Nakumbuka alinihimiza ni lini nitakuwa tayari kublogu. Jawabu langu likawa muda nikiwa tayari nitakuhabarisha. Ikawa mchana ikawaq usiku hadi leo nablogu na kuandika mambo yanahusu nyasa ambayo mimi ni sehemu yake, na inabidi kuyaeleza. Alisema blogu siyo upepo wa kupita ni zama nyingine hii usipitwe. Somo likaingia, likakolea nikaanza kublogu kuhusu mkoa, lakini dhamira ilikuwa kuhusu nyasa yetu tamu.

Nashukuru moyo wake wa kujitolea kunijuza, nashukuru pia rafiki yangu Simon Regis kwa mwongozo, nikawa katika uimara ninaoutaka ingawa sijaridhika. Nikasema blogu yangu ni kujitolea.

Sasa kwa Fredy Macha kuna kitu kimoja anazungumzia mara nyingi. Na alipokuja mwezi mei mwaka huu alirejea neno lilelile pale Soma Cafe(mgawahawa wa vitabu-mikocheni). Nilimweleza maendeleo ua utunzi wa vitabu, nikajaribu kumdodosa dhana ya maendeleo. Jibu lake kwangu ndilo linalonifanya niweke picha za aina hiyo kuhusu nyasa, yaani zile zenye kuonyesha uduni,ulalahoi n.k lakini naelewa nianza kufagilia mambo ya nyasa hapa hapatatosha. Ningeweza kuandika mambo mengi kuhusu jamii za Wajerumani wakiwa LUNDU na hususani wialaya ya Mbinga kwa uzoefu wangu. Ningeandika mengi kwani ni sehemu ya maisha yangu.

Ndiyo maana nakumbuka maneno ya Fredy Macha kwamba UKITAKA KUPATA MAENDELEO LAZIMA UJITAMBUE,UJIJUE. UJUE WAPI ULIKOTOKA, WAPI WAZAZI WAKO WALIZALIWA. THAMINI UTAMADUNI WAKO. KUWA NA NIDHAMU ILI UPATE HESHIMA. USIONE AIBU KUHUSU UTAMADUNI WAKO. UNA THAMANI SANA KWAKO.

Nikikumbuikamaneno hayo halafu ukitazama picha hiyo unaweza kudhani ninachofikiria unakifahamu. Hakuna kitu kikubwa kwangu kama AMANI YA MOYO. Nadhamini sana jambo hili bila kujali kitu chochote nilichonacho nje ya mwili wangu. SIWEZI KUTHAMINI KITU CHOCHOTE KILICHONJE YA MWILI WANGU, lakini suala ya utamdauni lipo kati yangu ndani mwangu nakihusudu sana.

Kwa bahati nzuri nimetembelea mwambao wa ziwa nyasa wote kwa upande wa Tanzania, na kwa upande wa Malawi kuna baadhi ya meneo ambayo nimeyatembelea, NAYAHUSUDU SANA KAMA VILE BANDARI YA CHILUMBA. Sasa thamni ya utamaduni wako ni kubwa hata kama watu wanaishi katika mazingira kama hayo. Unaweza kumtazama mtoto huyo halafu ukajifikiria ndiyo wewe unajijua sasa upo katika gali hiyo. Je utafanyaje? Ingawa kuna jambo la kufanya lakini jaribu kufikiria kama upo wewe.

Nadhani kuna jambo ambalo katika blogu yangu yanautofauti na maisha ya mjini. Kwanza mie siyo mtoto wa mjini, nimekulia kijijini na hata nilipokuwa nasoma nilipendelea kwenda kijijini, nimezoea misoto hata nikilosti mkwanja leo, sina maneno kwani nimefundishwa kuwa huru kifikra. Sasa wakati fulani nilimwuliza diwanmi wetu hivi unaonaje watoto wana[poshindwa kwenda shule shauri ya karo, ukachukua jukumu la kuwalipia? Alijibu UJAMAA UMEPITA. Nikamwambia mzee umekulia katika ujamaa mbona unabeza au maumivu sasa? Akasema ndiyo taabu ya wasomi.

Jawabu langu likawa kuwa mimi siyo msomi, mimi ni mwanenu mliyenilea hapa kabla sijahamia Mbinga pale shule ya smingi Kiwanjani. Naijua nyasa naelewa nyasa ninapenda sana kuliko chochote. Najua maisha hayao ya mtoto kama huyo pengine anamakamasi. Lakini ndivyo ilivyo, kwani wote hawakuumbwa na macho ya goroli, ndiyo maana wengine wanachongo.

Thamani ya utamaduni wako ni muhimu sana. Na naiona jamii za mijini kama zile alizozungumzia karl Marx kwamba jamii ambazo hazina utamaduni, na sifa moja kuu ni kwamba waafrika tamdauni zetu zinafanana. Kwakuwa Ndesanjo aliniasa unaweza kuandika kile ambacho wenzako hawakijui, na yale maneno ya mzee wangu Fredy Macha ni thawabu kwangu.

Nikiwatazama binadamu kama huyu aliyepichani ndipo ninapopata raha ya kuutibu moyo wangu kwamba ninapenda kuzungukwa na watu wenye hali hiyo ili tusonge mbele na kuiona dunia angavu ya ukwasi. Naweza kutembea KICHWA CHINI, MIKONO NYUMA, nikiwaza binadamu hawa. Mungu awe nanyi daima, awabariki wanaopigani hali zao na kuwalinda daima. MOYO KABLA YA SILAHA

NILIPOJIFUNZIA KUOPOSHA SAMAKI 'MANDONGO'


Hishangazi kukumbuka wakati nikiwa mdogo huku tukiamka mapema yaani kujalawa kwenda ziwani siku za mwisho wa juma. Hili eneo la Makoro au Pamuhumu, ambapo tulikuwa tunatumia sehemu ya mwisho katika kuoposha samaki aina ya Mandongo.
Nakumbuka wakati huo zoezi la kuoposha lilikuwa gumu kwangu lakini yote yalifanikiwa tokana na jitihada za aliyekuwa akinifundisha kuwa mkali kama pilipili. Nakumbuka ukikosea tu lazima utachapwa makofi. Ukiona samaki anajongelea katika chambo yako lazima umweleze ili akufindishe namna ya KUKWECHEKA yaani kumuopoa toka majini. Unatazama mwelekeo wake na namna alivyoikamata ndoana mdomoni kwake kisha unafanya mambo matamu.
Nakumbuka wakati ule mwalimu wangu alikuwa Edgar Chumila a.k.a Chipota alikuwa mkakamavu na mpenda mazoezi. Alikuwa mkali kwangu kuhusu suala la mbinu za kuoposha hata mbinu za kuogelea. Ndiyo maana nashangazwa na watoto wa mjini wanaogelea huku wameziba pua zao, nawaambia mbona hili ni zoezi rahisi sana kwa mahali pasipo na dhoruba? Nakumbuka kwetu hapa nyasa dhoruba kali ilikuwa kwetu furaha ya kuogelea na kuonyesha ufundi huku tukicheza mchezo wa CHIMPYALI yaani unamkimbiza mwenzako ndani ya maji hadi umguse ndiyo anatakiwa kumtafuta mwenzake naye amguse.
Ilikuwa pouwa sana. Nakumbuka wakati fulani mwaka 1993 Chipota alinikosa kwa kofi zito baada ya kunielekeza namna ya kumwoposha samaki aina ya Mandongo aitwaye LINDONGO NGOKU yaani lindongo kuku. Nakwambia huyu samaki anapatikana sana muda wa saa sit mchana, ni samaki jeuri asiye na mfano achilia mbali LINGOMBOLI. Huyu anaweza kukumalizia chambo zako buree hata usimpate.
Lakini siri moja kuu ni kwamba anahusudiwa na wengi sana tena sana. Kama ilivyo kwa Lindongo Ngaka maana ni samaki wadogo lakini watamu sana. Hata wale wavuvi wa zana za kisasa wanasifia ujanja wa samaki hawa. Tukirudi eneo la picha hiyo ni kwamba palikuwa mahali ufukwe wake ulikuwa mashuhuri na bado mashuhuri tokana na wageni wengu waliopendelea kupumzika nyasa yetu hususani Lundu.
Moja ya sifa ingawa ni mbaya, kuota kwa majini ya Bangi ambayo ilikuwa ni matokeo ya jamaa mmoja aliyeitwa Edgar, mzungu ambaye alikuwa yeye na bangi ni kama chanda na pete. Alikuwa fundi bomba, lakini alikuwa mvutani mzuri wa bangi. Sasa eneo hilo linanikumbusha mengi sana hasa kwa wazee wetu kupatumia kama mahali pa KULANGA HIPA yaani kutazama dagaa huku nyavu zikiwa zimetegwa.
Sualoa la uvuvi na uogeleaji wa wanyasa ni jambo rahisi sana, na nakumbuka hata waliokuwepo katika msukosuko wa meli zetu zile wanakwambia wao hawaogopi maji lakini watu watokao mijini wana misemo yao ambayo inalenga kukatisha tamaa eti hakuna aliyemtalamu wa maji katika kuogelea. Huo ni uwongo kabisa. Nimekumbuka sana eneo hili, nimekumbuka nitokako, napenda sana hilo.

2009-11-17

FIKIRIA SANA, USIAMINI SANA, AMUA WEWE

Mara ngapi umesoma kitabu au mahali ambapo panakupatia jawabu ambalo linaleta ukakasi kwako? Unaweza kufikiria lakini kama huwezi kufikiria basi jaribu kunisoma halafu fikiria kisha jipe jawabu kamili uone ukweli ulivyo.

1. Usiwe mwadilifu kupita kiasi unaweza kuwa mkiwa bureee maana mungu mwenyewe inadaiwa alisema hilo. Na kwakuwa kuna watu wanaamini kuwa dini za ukristo na Uislamu ni mwisho wa yote, hawajipi muda kuhoji, kwanini dini hizo za jamaa kutoka mashariki ya kati ambapo mmoja alikuwa akivaa misalaba mikubwa na mwingine alikuwa akifuga ndevu na kupka hina. Mbona kuna Wabudha, wahindu n.k angalia usiwe mwadilifu kupita kiasi.

2. Usiamini kitu chochote kwasababu tu kinasemwa na mtu mwenye busara. Pima mambo yako ewe mwanadamu usikubali tu kama ilivyo ndivyo bali unavyoamini ndivyo.

3.Usiamini kitu chochote kwasababu tu watu wengi wanaamini. Ndiyo maana sitaki kusikia dini ambazo zimejaa vimelea bya kutohojiwa, ambazo zinasadikisha ati ilikuwa lazima watakao hoji na wapingaji ukristo. Nimelelewa katika msingi wa dini zenyewe lakini ninachokiona katika ulimwengu wenyewe nashangaa tu. Kwani lile sanamu la mwanamke aliyepanda mnyama aliyepo pale nje ya bunge la ulaya ni nini kama siyo ushetani kwa mujibu wa UFUNUO WA YOHANA? soma tuulewe vema. Si mnadanganya na dini zenu kuwa Obama alikosea kuapishwa? wadanganyeni haohao ili mnyasa nisalie kuamini vile ambavyo naamini.

4.Usiamini kitu chcochote kwasababu tu vitabu vya kale vimeadnika. Yako mengi tu, mbona tunadanganywa Nostrodamus alitabiri vita vya dunia vya 3, alitabiri kuzaliwa kwa Adolfu Hitler na mengine mengi kama mapinduzi ya Ufaransa....lakini hatusemi kuhusu Mysters School ya Freemasons ambazo zilimfindisha kufundisha ushetani wake.

5 Usiamini jambo lolote kwasababu tu vitabu vitakatifu vimeandika. Hapo mie simo lakini unaamini kuwa simulizi za mambu wa mashariki ya kati ni chanzo cha kuwepo wa sisi. Alaah kumbe ilikuwaje aliyeletwa kwaajili ya Babeli na wayahudi akawa wa dunia nzima? Na historia ya Roma inaweza kunisadikisha kwamba niamini ndivyo ilivyo nisadiki tu bila kuhoji? Niamini anayekupiga kwenzi akuchape na mitama?

6. Amini jambo kwasababu wewe mwenyewe umelipima na ukaliona liko sahihi.

Ndiyo maana nasimimia hoja kwamba sihitaji kanisa wala msikiti wowote, sihitaji mchungaji wala ninachokiandika sikitumikii nakitumikia tangu mwaka 1996 hadi leo hii. Je unafikiri dini yako ni bora kuliko ya mwenzio? Unafikiria kanisa lako ni bora kuliko la mwenzio? Unafikiri sadaka yako ni bora kuliko ya mwenzio?

2009-11-15

HIVI PUNDE:.....kikao cha NYAZODE kimemalizika

Baada ya kutoka likizo mara vyuo vilipofungwa kwa muhula wa kwanza kumaliza. Na sasa kukiwa kumeshaanza muhuala mwingine hatukupata muda wa kuongea wala kujadili kwa kina kuhusu mradi wetu wa NYAZODE. Lakini leo hii jumapili HIVI PUNDE kumemalizika kikao hicho cha kwanza na maazimio kadhaa kupitishwa.

Mradi huu kwa hakika ukikamilika utawezesha wale walalahoi wenzetu wa nyasa kuamka wakiwa neema nzito maishani mwao. Ni hivi punde tumekamilisha masuala kadhaa muhimu ambayo yatawezesha mustakabali mzima wa NYAZODE.

Sasa mradi unapiga hodi katika ofisi ya Mbunge wa jimbo la Mbinga magharibi bwana John Komba ili apate taarifa maridhawa kuhusu mradi wenyewe. Na vilevile wazee kama Profesa Mihanjo, hivi punde atapewa maazimio na kuweza kufanya kile ambacho wengi hawakutarajia kufanywa na kundi hili la wazee wa nyasa. Ni hivi punde tu kumemalizika kikao hicho.

ASANTE KWA UHUDHURIAJI WENU NA KARIBUNI S ANA NYASA.

2009-11-13









Natamani Ningemwona,
Ili Nimjue Vema,
Nimwambie ya Maana,
Aziepuke Lawama,
Mficha Uchi Hazai,
Mtoa Uchi Hafai.


Lakini bahati Sina,
Karejea kwa karima,
Yuleyule maulana,
Mficha uchi hazai,
Mtoa uchi hafai.


Sababu isiwe haba,
Ahadi ijazwe kibaba,
Mtima wenye msalaba,
Mficha uchi hazai,
Mtoa uchi hafai.


Nenole Usilinene,
Jichole tena lisione,
Na sikio lisisikie,
Usiige kujua lolote,
Mficha uchi hazai
Mtoa uchi hafai.


Embe dodo natamani,
Kulila kwangu mdomoni,
Harara zangu za thamani,
Mficha uchi hazai,
Mtoa uchi hafai.


Nimelia sana maishani,
Katu siyashangai machozi,
Asilani liwazo si machozi,
Mficha uchi hazai,
Mtoa uchi hafai.


Maumivu yangu, huzuni yangu,
Tamaa yangu, furaha yangu,
Kipi kifaacho kwangu?
Furaha au huzuni yangu?
Mficha uchi hazai,
Mtoa uchi hafai.


Furaha na huzuni vi wapi?
Mwangu moyoni ama mwilini?
I wapi tofauti hii mpenzi?
Yako wapi yale mapenzi?
Mficha uchi hazai,
Mtoa uchi hafai.


Jamvi nalitandua,
Ukingoni nimetua,
Penzi sitolivua,
Kwako hakika nimetua,
Mficha uchi hazai,
Mtoa uchi hafai.

2009-11-11

VITUKO VYA WANYASA NA SANAMU LA ASKARI DAR ES SALAAM


Nakumbuka nikiwa mdogo, simulizi za snamu la skari huyu zilinitihs akuona mji huu siyo wa kuishi. Nakumbuka waliowahi kufika huko Dar es alaam wakisifia na kutisha kuhusu mji wenyewe. Nakumbuka wengine waliwahi kusimulia kuwa hapo zamani kulikuwa na mzee fulani MNYASA aliwahi kukaa hapo kwa kuombeleza asamehewe makosa yake kwani hakujua kama anavunja kanuni za mji.
Na kosa lenyewe lilikuwa kushangaa ghorofa zilizojipanga katikati ya mji tangu alipokuwa akiishi Upanga. Na kwakua alikuwa mgeni basi aliamua kujipa jukumu la kuyajua mazingira kwakuwa alizowea mji kiasi chake. Basi akaijikuta maefika katika sanamu la askari huyu, mzee wa watu akapiga magoti kuomba msamaha sana kwa makosa ya kushangaa majumba makubwa watu wanaishi angani kama FIDEGE tena wale mbayuwayu...nawapenda sana hawa ndege.
Mzee huyo inasemekana alilia kwa nguvu zote kwa kudhani atasamehewa kosa la kushangaa majumba makubwa, yenye watu wasiotosheleza ubongo hadi wakawa walarushwa wakubwa na kuita TAKRIMA. Basi mzee huyo akaangua kilio hapo lakini hakuna aliyejali sana kuhusu hilo kwani alidhaniwa kua ni kichaa tu.
Lakini kama ujuavyo wabongo kwa kunusanusa udaku wakamsogelea mzee wa kinyasa na kumhoji inakuwaje anaongea na sanamu kwani amekuwa kichaa? Lakini mzee akasisitiza kuwa askari yule amemweleza atamdhuru kwanini ameshangaa maghorofa wakati anajua yanalipiwa? watu wakacheka inasadikika hivyo, wakamweleza huyo askari ni samanu tu hivyo kumtaka arejee nyumbani, ndipo mzee alikubalina lakini kwa sharti la kusindikizwa.
Alipotoa rai hiyo basi waungwana wakafanya hivyo hadi mtaa wa Undali na akaonyesha anapoishi kisha wenyeji wakajitokeza. Ndipo ikaulizwa kulikoni? Mzee akasimulia kisa na kudai jamaa wamemwokoa.... hee wenyeji wakaangua kicheko ikawa usiku ikawa mchana ......simulizi zimeendelea vizazi hadi vizazi vya mzee wa Lundunyasa alisimuliwa.....na hapo kale alikuwa akikataa kuja mji huu sababu hiyo ingawaje baadaye alikubali tu shauri ya elimu siyo sababu ya askari sanamu. Na akitimiza agano mzee wa Lundunyasa lazima arejee agano lake la nyasa. Vituko vya wanyasa na sanamu hilo jamani nilikuweo enzi hizo wakitusimulia yatokanayo

NIMERUDI; ZAWADI YAKO DADA YASINTA


Nimerudi. Ndivyo ninavyoweza kusema, maana ni siku kadhaa zilitoweka bila kuaga hapa ingawaje sina kawaida ya kuaga bali kutangaza wapi nimeibukia. Na aktika kuibuka huko kumbuka usiaambie uhamiaji suala hili kwani unaweza kuleta utelezi katika jitihada za kudanganya too ili liweze kunifanikishia mipango ya ukubwa . Si unajua danganya toto ni uwongo? Pouwa msomaji wangu.
Pamoja na kusema hivyo utashangaa huyu mzee wa Lundunyasa alikuwa wapi? Usijiulize hilo ila kumbuka mambo ya elimu mtaani bongo poa ila magumashi kwahiyo vuta pumzi vuka boda hata kama ni masikini wenzetu. Nimerudi kwa mtind uleule wa kawaida kama ilivyo mambo ya nyasa, na inawezekana ikawa mwanzo wasafari zisizokwisha kama ambavyo wakoloni wa kiingereza wasemavyo TRAMP. Mmmhh! nakumbuka nilikuwa na begi lenye neno hilo sababu yule rafiki yangu alipenda kuniita hivyo kwakuwa nilikuwa mtu wa mizunguko isokwisha.
Nipo msomaji wangu, nimekuja tena kama kawaida ingawa nitakuwa nawe mara chache, bila shaka shule na mwendo wa kuongeza shule unandaliwa ndiyo maana natoweka. Mipango mingi na hapa ni nyumbani kwangu nyasa sitoweza kuwakimbia. Najua kaka Mzee wa Changamoto atanza zake za kazi kulea mwana........ Lol
ZAWADI SIYO? Ni moja ya michezo mingi ninayoicheza katika hii tarakilishi wakati mwingine natumia majina yenu na picha zenu wanablogu kutengeneza vitu ninavyovipendelea.....
Lakini hii ndiyo ilinipa hamasa zaidi kwani ndiyo nilianza kuitengeneza na madoido ya kingoni.
Ni maalum kwa dada yangu kipenzi Yasinta Ngonyani a.k.a Nangonyani..... si unajua watu dadangu MUHEKELA PANGENDE KUMOYO LUTIMBA LONGI! unaona dadangu haya mambo? usiwatajie wala nini lakini najua wadadisi watachokonoa kama wachokonozi.
CHUKUA ZAWADI HIYO KWAKO NA FAMILIA. MUNGU MKUBWA, AMANI IWE NAWE.
karibuni sana Nyasa, na karibuni Mitindo huru kijiwe cha makala zangu za sasa na zamani ingawaje bado sijaweka mambo mazito. Tungojee mengi.

2009-10-13

BURIANI FRED NDUNGURU

"Markus! nipo Makambako naelekea Mbinga, Fred amefariki dunia!"
Napoke ujumbe huu saa kumi na mbili na dakika 27, jana jioni. Ni Yasinta rafiki yangu kipenzi, anasononeka sana, uchungu umemjaa moyoni-anasafiri kwenda kumzika kaka yake FRED AUREUS NDUNGURU.

Baada ya taarifa hiyo navuta taswira ya Fred, namkumbuka nikiwa sekondari Lundo, nakumbuka upenzi wake katika kiondoko ya Hip Hop! nakumbuka falsafa zake ambazo zilambatana na msimamo thabiti. Nakumbuka wakati ule tukitumia muda mwingi kusikiliza santuri ya DUDUBAYA ya SASA NI SAA YA KUFA KWANGU. Nakumbuka hisia za mwanamuziki huyo Godfrey Tumaini au Dudubaya. tunatumia muda kukariri mashairi yake, tunacheka kwa harara na mashmsham!

Ingawa hakuwa mpenda soka kama mimi, lakini yeye alipenda kunywa kileo kidogo lakini kwangu kileo ilikuwa mwiko na mwiko hadi sasa. Nakumbuka pamoja na hayo urafiki wetu haukuweza kuvunjika. Nakumbuka sana soga,michapo,gumzo na mambo mengi tu mazuri. Mabaya yote namwomba mungu amsamehe sana.

Nimefadhaika na kuhuzunika sana kutoweka duniani kwa FRED NDUNGURU kijana mchangamfu, msomi na mwenye msimamo mkali ambao hata baba yake alikuwa akishangaa sana. Nakumbuka pamoja na mbwembwe zake lakini alikuwa mkali katika Fizikia,Kemia na hisabati(PCM). Alijua namna ya kukabiliana na changamoto, alikubali kubeba lawama kwa maamuzi anayochukua.

Kikubwa zaidi alikuwa karibu kwa kila mmoja wetu tena kwa msimamo mkali kama humpendi naye hakupendi ndiyo sera zake. Nakumbuka mengi tukiwa Lundo sekondari huku yeye akiwa kidato cha sita pale Meta high school. Aliweza kusimamamia msiamamo wake mara nyingi tu kuhusu mwenendo wake ambao ulimkwaza hata baba yake, lakini alieleweka vema.
BURIANI FRED NDUNGURU, mungu akulaze mahali pema peponi. Malaika wake wakulinde daima kaka, ulitupenda kwa mengi sana, umetuacha tukiwa hatujakulipa upendo wako. Nawe YASINTA AUREUS NDUNGURU usilie sana, kaka amekwenda mbele za haki.
SOTE TUNAMWOMBEA MEMA. amen.

2009-09-25

JE UNASADIKI KUNA UCHAWI?


Ndugu zetu wa Globalpublishers wametuwekea picha hii tangu habari hiyo ilipovumbuliwa na Knaisa la mama Lwakatare. Tunawashukuru kwalo.
Jambo moja la msingi ninaloongelea leo ni suala la UCHAWI/USHIRIKINA. Baadhi yetu tuliozaliwa ukanda wa nyasa siyo jambo geni wala halitishi kama ambavyo wengi wanavyotishika. Nakiri kwamba katika makuzi yangu nimekuwa nikisikia habari hizi na siyo mara moja nimezijua, nazielewa napengine nimeshuhudia matukio kadhaa.
Kwetu nyasa hapa, mambo ya uchawi yanasikika na unaweza kuambiwa familia ya fulani ni wachawi sana kwahiyo usioe wala kuolewa nao. Ni jambo la kawaida jamii kufikia kuamini kile kinachowazunguka. Kwani ndicho wanachokiona kila leo. Uchawi hapa nyasa ni suala ambalo limetamalaki na familia zinaweza kuogopana kwasababu ya uchawi. Hili utalikuta katika ngoma za utamaduni, soka, sherehe, uvuvi na mambo mengine. Siyo ajabu kukuta nyavu zinafungwa mafundo kadhaa yenye kila dalili za ndumba au kuona namna jambo fulani linavyohususishwa na wachawi.
TUKIO LA KUKUMBUKWA. Mwaka 1994 kulikuwa na kundi kubwa sana la watalii hapa kijijini kwetu LUNDU, kundi hilo ilikuwa ni kawaida katika miezi kama hii ya septemba na oktoba. Wazuungu wale walishangaza sana, walipokuwa ziwani pale walivalia vikaptura vya jeans, na wengine walikuwa wamevaa kawaida tu. Lakini tumezoea kuwa ifikapo saa 12 jioni wengi wao huondoka na kurejea pale Misheni yaani kama Monesteri za mapdre na masista kwa wanawake.
Wao hawakuondoka, wakatulia hapo hadi usiku wa manane, na kwakuwa ufukwe ule upo karibu makaburi basi wakaanza kufunga taa(umeme) kwa kutumia betri za gari. Wakafunga katika msalaba mkubwa uliopo katika ya makaburi yale na misalaba mingine. Baadhi yetu tuliokuwa karibu wamisionari tulijua kuwa hawa wageni wanataka kupiga picha za video ili wawanase wachawi. Ndivyo walivyofanya na inasadikika ilikuwa hivyo. Baadhi ya wafanyakazi wa wamisionari wale waliofanikiwa kuona video hizo wakataja baadhi ya watu wa familia fulani kuwapo katika mkanda huo. Je walikuwa wachawi kweli?
Dhana nyingine ikadaiwa kuwa wazungu wale nao ni wachawi, lakini hatukuweza kuthibitisha hilo. Lengo la kupiga picha zile ilikuwa kutaka kuwaonyesha wakazi wa kijiji chetu adhimu cha LUNDU. lakini kwa hekima za mwenyeji wao Padre Rainer alikataa jambo hilo na kuwaamuru kuwa wasionyeshe hapo bali wakafanye huko waendako. Ikawa hivyo...sijui kilichoendelea.
Vilevile katika kijiji chetu hiki eneo hilohilo la makaburi kuna miti mikubwa miwili ya mibuyu. Cha ajabu kuna mti mmojawapo kila ukiangua mabuyu yale wakati mwingine unaweza kukuta nywele ndani yake ay damu. Hilo linashangaza na linaendelea kushangaza sikusimuliwa nimeshuhudia mwenyewe hapa kwetu. Unaweza kuchuma mabuyu hayo lakini ukakinai kuyala. Tukirudi kwa wazungu wale walichofanya baada ya kuzuiliwa kuonyesha picha zile usiku uliofuata wakapiga kambi tena pale makaburini na kuanza kung'oa misalaba kadhaa na kuitupa. Wakaishia zao na kurejea kwao Bavaria-Ujerumani.(mji ambao baadhi ya wakazi wake ni wahudhuriaji sana hapa LUNDU) . Nikomee kwa hapa leo, kuna mengi ya kusimulia katika mjadala wa uchawi. Je wewe unasadiki kuna uchawi?

2009-09-15

KARIBUNI NYASA, KARIBUNI SAMAKI

Basi nikamwambia unataka kufahamu chakula nikipendacho zaidi? Hakuna kingine zaidi ya UGALI WA MUHOGO kwa smaki aina ya KAMBALE.... nikaona anacheka,,,, tena kwa harara utadhani amekamata lile jani au ile pombe mashuhuri hapa nyasa ya Myakaya. ha ha ha ha basi nikamkumbusha wale samaki aina ya MAGEGE nikamwambia utaniambia nini masika ifikapo? Nikajikumbusha raha za mji wangu niupendao wa LUNDU, nikamwambia naridhika na kutulia sana nikiwa hapa, nikamweleza zaidi kuwa labda anipeleke MBEYA mahali pengine ninapopapenda zaidi... halafu na pengine ni pale jijini LILONGWE kule kwa asili ya akina MPANGALA, kwa wajomba na mababu zetu, napazimia sana napahusudu sana mahali pale, vipi ile klabu ya soka ya Sivo service United huishangilii wewe?

Mi naihusudu bwana, si unaona ilivyojipangia mikakati? Halafu siku ile pale ulinizome ilipofungwa na MTL Wanderers, we haya tu bwana...... eti akacheka kwa mikogo ati. Ngoja na Mbinga magharibi sasa kuna mchakato wa kuifanya Mbinga magharibi kuwa wilaya rasmi.

Najua watagombania kati ya LIULI, MBAMB BAY na LITUHI wapi waweke makao makuu. Maana hata wiki jana nilikuwa na rafiki yangu kipenzi Raymond Ndomba..... kijana mcheza soka ninayemshangaa.... anaweza kucheza namba yoyote utakayo mpanga uwanjani tangu golikipa hadi winga wa kushoto....lakini shule imemfanya awekeze huko.......na sasa anawania kupata nini kile kinaitwa MASTERS. Huyu alinidokeza kuwa wazo la makao makuu la Wilaya Mbinga magharibi litakuwa shubiri maana kila mji unapenda iwe hivyo...nadhani LIULI wanaweza kupendelewa eti ni katikati ya wilaya yenyewe.

Tuache hayo, twende katika samaki wetu hawa watamu sana na adhimu duniani. Ni nyasa bwana wapi kwingineko utakako pata samaki hawa, ha ha ha ha raha sana. KARIBUNI NYASA, KARIBUNI SANA lakini neno langu siyo sheria au vipi waungwana? Pendaneni kwa mpango!

NKATA BAY: Bandari salama, lakini.....

Ha ha ha ha ha ha! Nayakumbuka niliyopita hadi kufikia uamuzi wa kuomba mnisamehe niliowakosea. Najua mapitio yale yalikwaza ndiyo maana simulizi ni nyingi hadi zikanifikia.........au vipi Babu? ha ha ha Pouwa ha ha ha ha ha ndiyo maana nimesema sina elimu ya FALAKI! Eeeehh! najua hayanihusu, nisielewe sana bureeeee!!!!!

Nkata Bay ni moja ya bandari iliyopo kaskazini kabisa mwa Malawi, ukiangalia pichani unaona Mv Ilala ikiwa bandarini. Kwa maana hiyo basi unaweza kujenga picha fulani kuwa ni eneo ambalo halina bandari nzuri ama kubwa kama ya Mtwara ama Lindi. Ni kweli, nilifika bandarini hapo kwa mara ya kwanza 1999 na mara ya pili ilikuwa mwaka 2oo1. Wakati huo tuliambiwa marekebisho makubwa yanakuja kwajili ya kuboresha huduma zake.

Hii ilitokana na suala la biashara kati ya TZ na Malawi. Lakini wakti huo kulikuwa na uongozi wa Rais Muluzi ambaye siyo siri aliwapenda na kuwapendelea sana waTZ, hilo lipo wazi kabisaaaaaaa. Lakini baada ya kuingia Rais Bingu wa Mutharika, mwanablogu mahiri tu ingawa ni mwanasiasa nakiongozi wa nchi, upendeleo ule umetoweka na hata wafanya biashara waliokuwa wakitumia sana usafiri wa meli wamepungua kama siyo kwisha.

Mv Ilala ni kubwa sana, kuna wakati kulikuwa na matatizo kwani bidhaa zilikuwa adimu huku meli likiwatia nanga Mbamba Bay ikiwa na mzigo kidogo. Hii yote ni kwasababu ya ujio wa Rais mwanablogu Bingu wa Mutharika. Simlaumu kwa lengo lake la kujenga uzalendo wa nchi yake.

Nkata Bay tatizo lake ni swa na pale bandari ya Manda, kwani kwa mujibu wa wachunguzi inadaiwa kuwa kuna miamba mingi chini ya maji-na sifa yake kubwa ni kina kirefu. Kwa uapnde wa TZ tunaringa kwa kuwa na maziwa mengi, lakini Malawi wanalitumia ziwa hilo kwa umakini sana, ukifika pale bandari ya Chilumba wanavua kwa zana za kisasa, na sheria kuhusu uhai wa samaki unalindwa sana.
Wavuvi wameelimishwa ipasavyo wanaelewa umuhimu wa kutunza mazingira na kuvua samaki bora.

Nkata Bay ni pazuri kama mji na bandari inapswa kuwa nzuri zaidi licha ya uzuri, changamoto kubwa kwetu ni TZ ni kuiboresha bandari ya Mbamba Bay au Liuli maana ile ya Chiwanda tuliambiwa mbali na hakuna kina kirefu, kweli nimeshuhudia hali ile na kuna upepo mkali sana ukielekea kijiji cha Kwambe ambapo ni jirani tu na Chiwanda. Bandari nzuri...lakini Rais Bingu apunguze "kuwafukuza" wabongo...... ila anatufukuza kwa kuwawezesha wamalawi...ndiyo hapo changamoto yetu ilipo.

2009-09-10

YASINTA NA JOHARI YA MATUMAINI (2)

YASINTA: we Markus uko wapi, mbona huonekani?

MARKUS: nakja bwana, nipo hapa jirani tu, tulia boli

YASINTA: uko karibu, pouwa nakusubiri basi.

MARKUS: nimeshafika hebu njoo dada yangu nipo hapa....

YASINTA: aaaaaah we dogo umekuja kwa usafiri gani tena?

MARKUS: Bajaj......(kicheko kidogo)

YASINTA: ha ha ha ha ha wewe Bajaj ndiyo nini tena?

MARKUS: huoni hicho kiberenge cha matairi matatu?

YASINTA: poa, lete stori mtu wangu, duh! hii kali, mzee kipara wewe kwanini umenyoa kipara?

MARKUS: aaah bongo joto kipindi hiki we huoni?

ERICK: (anaingilia gumzo) Mmmhh joto sana hapa, kweli

YASINTA: muone Erick utadhani unajua sawa sawa hicho kiswahili.

MARKUS: hee Erick kumbe Rasta? ha ha ha ha LoL

Msomaji unaweza kudhani simuliz fulani hivi kwani kama ujuavyo ZEE LA NYETI ninavyohusudu michapo na gumzo la hapa na pale. Lakini ghafla naona mtu kainamia meza anaandika kitu kwenye daftari nauliza niaje naambiwa naandika post ya leo kwenye blogu. Mi hee haya bwana. Huyu mtu ananipa maswali na mazungumzo yanakolea hapa na pale.

Msomaji mengine fikiria tu mwenyewe wala usisumbuke sana maana nimesitisha kuendelea nayo ili nisiandike mengi na kujiona namfahamu sana huyu mtu.... lakini sasa.... haya ngoja nikomee hapa........... ingawa skupenda kukomea hapo.... KWAHERI KWA LEO.

MNISAMEHE WATU WANGU, NIKIWAKOSEA

Najua uungwana ni vitendo ndiyo maana nasema hivi kwasababu kuna kipindi katika picha zangu za kuhusu wale jamaa wa RICHMONDULI a.k.a wakurichmondooooo kuwa nilikebehi imani ya wakristo. Naomba nieleweke kuwa sikukusudia kuwadhalilisha bali nilikuwa nawakilisha kuwa hapa tulipo kuna nini kwa wenzetu katika ulimwengu huu.

Kwahiyo kama waliokwazika na picha ile na hata wakaniandikia waraka pepe kuwa nimedhalilisha dini basi MNISAMEHE SANA nawaomba hilo. Vilevile kama kuna jambo nililoandika katika blogu hii limewakwaza na ambalo uandikaji wake siyo kwa nia ya mafumbo mafumbo na majungu ya muziki wa Taarabu naomba mnisamehe sana kwani siyo lengo langu katika blogu hii.

Pia kuna wale wanaoghadhibishwa na mwenendo wa blogu yangu wa polepole naomba mnisamehe sana kwani nawaheshimu wasomaji na wadau wangu LAKINI naipenda sana shule na wala sina haja ya kushika chupa za BIA ama misokoto ya akina LoL......... najua mnaokwazika mnanifundisha jambo. NAJUA pia nifanyalo ni kwa burudani za watu a nyasa na wanablogu wengine wahusuduo blogu yangu. NAWASHUKURU KWALO. jambo moja ni kwamba naweka tu kanuni kama nilivyoweka awali, naweka tu kwani naamini ni utaratibu wangu bila kujali ukaribu na umbali wetu.

Naomba wanisamehe woteeeee niliowakwaza kwa kuweka habari au gumzo ambalo kwa namna moja ama nyingine limewakwaza. Nachukua fursa hii kuwaambieni hivyo kwani maisha yangu siyo ya kuigiza na wala mimi siyo mwigizaji mzuri kama JORAM KIANGO katika MALAIKA WA SHETANI cha Ben Mtobwa anavyotuasa kuwa watu wanaigiza- maana huwezi kucheka na mtu ama kujifanya unazungumza naye mengiiii kwa raha na burudani za hapa naple halafu PEMBENI unafundo la GHADHABU. Naomba mnisamehe kwa yote nimejifunza- nitaendelea kujifunza mengi toka kwenu wanablogu na wasomaji wengine. Naamini kutenda kosa siyo kosa ila kurudia kosa. Nakiri makosa kwa yale niliyowakwaza wenzangu.

Pia wale walioniomba kuhusu kuweka matangazo katika blogu yangu, nitawajbu leo. Kwamba blogu yangu sihitaji tangazo la mtu la kibiashara ama lenye mlengo wa kufanya ubepari/biashara bali blogu yangu inajitolea kwa matangazo ya wale wanaohangaikia maisha yao kama nilivyofanya kwa VUNGA. hayo n aina ya matangazo niwekayo. Tangazo la kahawa ya Mbinga ni kujitolea kwangu kwani nilikwisha kuzungumza na mabwana wa pale na wakanielewa.
Blogu yangu haifumbi mtu na wala siyo ya ukoo wa akina HONORIUS MPANGALA bali ni kijana mpole tu Markus Honorius Mpangala na wala hatumii FALAKI ili aweze kuishi na kutambua makosa yake.

AMANI KWENU, TUPO PAMOJA NAWAPENDA NYOTEEEEEEEEE, KARIBUNI NYASA

2009-09-05

Mara ngapi umesahau kutumia Kondomu???

Ndugu wanablogu na wasomaji wangu, niwaombe radhi kwa kutoweka hapa bila taarifa. Ukweli nilikuwa na hali mabaya kiasi, hali kiafya ilitetereka sana maana kwa muda mrefu sikuugua kama hivi. Malaria yalinibana sana kiasi ambacho nikashindwa hata kuandika ama kuwajulisha watu wangu, marafiki zangu. Lakini natumaini tupo pamoja na sasa nimerudi niko kamili na afya yangu iko salama hata leo nimeanza mazoezi ya viungo pia mdomdo. Mungu mkubwa, na nimewasoma wanablogu katika blogu zao kwa njia ya simu yangu ingawa sikuweza kuchangia lolote.

Tukiacha hilo, kuna jambo mara nyingi naliwazia kulisema nalo ni kuhusu matumizi ya zana ya KONDOMU. Nasema hivi kwasababu kuu moja, Mama yangu alipoanza kuniuliza swali hili ilikuwa mara nilipomaliza kidato cha juu. Swali hili lilitokana na kitu kimoja tu, kwamba kuna usiku fulani pale kwetu Lundu nilichomoka zangu usiku (ilikuwa mwaka 2005, mwezi Juni) na kwenda kujiburudisha na uvunguni kwa kutumia kionjeo cha utamu. Sasa.... asubuhi ilipofika akasema......Markus jana usiku ulikwenda wapi na kitandani kwako hukuwepo?.... nilibabaika...kwani ni kweli niliruka zangu ukutu kisha huyoooooo kwenye madogoli... si unajua kijijini ngoma za usiku na ahadi tutakutana ngomani???

Basi mama yangu aliniuliza kwa njia ya utani, na amekuwa akifanya hivyo mara nyingi siyo kwangu tu hata wadogo zangu ambao nao ni waelewa wa mambo. Baada ya kuona sijajibu nilikuwa wapi usiku ule... akasema sikiliza mwanangu...mara nyingi unakataa mambo ya ulevi na tabia ambazo hazipendezi ama hazikubaliki hata kama hazina madhara...lakini nakuuliza swali kwamba MARA NGAPI UMESAHAU KUVAA KONDOMU? Mama yangu alikuwa makini kwani muda wote alikuwa akinitazama usoni, na anajua kama sijapendezwa na swali huwa nanyamaza au kuondoka eneo husika kuliko kuonyesha ghadhabu zangu.

Kitu nilichofanya ni kumweleza Mama kuwa kweli nilitoka na anisamehe kwani nilikuwa ngomani. Na kuhusu swali lake nilimjibu kuwa NIMEMWELEWA. Lakini Mama akasema kuwa kama unadhani nakuingilia katika uhuru wako basi sahau kujiona uko huru kuliko uhuru wenyewe hata kama utakuwa kwako... nitaendelea kukuuliza swali hilo....najua hujaoa na naamini unaye mtu unauhusiano naye. Nikamweleza Mama inatosha nimekuelewa. Siri moja ni kwamba iwapo katika pilika za kutafuta kupata utamu kwa kutumia kionjeo cha utamu akijua Mama yangu kuwa ninayemchungulia uvunguni ni fulani basi ilikuwa lazima nisitishe na mahusiano yanakwisha hapo. Nilijifunza jambo!

Linaloshangaza wengi ni kwamba katika familia yetu suala la kupimwa ukimwi siyo jambo la kubembelezwa ni lazima na hakuna ubishi katika hilo. Sasaaaa.....niliposhindwa kumjibu Mama yangu kuwa kama nasahau kutumia ama kuivaa kondomu nilijua anamaana gani, na tangu hapo nilijiuliza kwanini Mama yangu alisema hivyo? Siyo kwamba sivai au situmii kondomu, la hasha nimeishaitumia mara kadhaa. Na kwakuwa sijachungulia uvungu kwa muda mrefu... daima nalikumbuka swali hilo na naelewa tatizo linalotukumba sisi vijana kubeba kondomu mifukoni lakini tukifika dimbani hatuwezi kuhimili kuzivaa vema au kujaribu kuvaa.

Ninaamini udhaifu huu unatoka na KUONGOZWA NA HISIA bila AKILI. Najua kuwa idadi kubwa ya wanawake wanakumbusha suala la kondomu wakiwa dimbani hata kama vichakani dakika moja kabla ya kuchimbana mitaro. Nasema hivi kwani sihitaji kusimuliwa nilifanya uchunguzi mwenyewe kwani enzi hizo baadhi yao wanakuuliza kondomu iko wapi? Halafu wanajifanya kususia mpambano usio na REFA wala washika vibendera. Tunapofikia hapo tunabembelezana kwa maneno ya YAANI HUNIAMINI? MIMI NATAKA NYAMA KWA NYAMA NIJISIKIE KUNOGA NA KUFAIDI UTAMU WAKO! AU NAKUAMINI DIA WANGU WASIWASI WA NINI ..... HAYA TURIDHISHANE BASIIIIII. Ona sasa..... wizi mtupu!!!!

Unaweza kudhani napenda porojo ama ninachosema ndicho ninachofanya bali naona na hata mimi mwenyewe enzi zangu nilikuwa nabeba hizo kondomu halafu namsikilizia MWALI wangu anasemaje kuhusu matumizi. Hapo ndipo nilipoonza kulidharau tendo lenyewe na kuona wanaotembea wakiringia uzuri na kile walichonacho kumbe bureeee! Ndipo swali linaporindima daima .. hata nikaweza kukaa kipindi kirefu zaidi ya mwaka mmoja bila kuchungulia uvungu sababu naona sioni jipya hata kama kuna watamu kama sukari ama asali. Kinyaa tupu,............... wizi mtupu!

Siku zote naona sisi vijana tulivyochakaramu wa kuhusudu kuchungulia uvunguni, lakini tunaposimuliana kwa umahiri wa matumizi ya kondomu, kumbe ni 10 kwa mmoja wanaotumia hata kama maambukizi ya ukimwi yamepungua. Najua kile tunachokifikiria pale tunapokaribia kuitafuna Mbunye (samahani kwa mcharazo mkali). Na siku hizi wale washikaji zangu wanawabatiza wanawake wakubwa wenye miaka kuanzia 20 na kuendelea eti klabu ya AC MILAN ya Italia kwamba wazee damu haina moto. Ndiyo maana wanasema kuna mafataki ya kiume, lakini mimi nasema kuwa mafataki ya kike yako mengi tatizo tu yanajifanya kuja kwa vituko na ishara....sasaaaaa jitu kama mimi nakutazama na halafu nikikufiria ukiwa huna nguo katika ule muda hata kama umevaa ujue nimeshakutupa jalalani. Hili ni jambo linalohitaji ujasiri ...siamini kwamba tunashindwa kumiliki akili zetu hata tukashindwa kuivalisha kondomu ile NDUDE iletayo utamu.,,.... kwani uwongo? mifataki inayoniandama...halafu ngoja nitapiga mtu ngumi za jicho... LoL.............

Niliwahi kuhudhauria mafunzo ya matumizi ya kondomu mwaka 2006, nakumbuka wakati semina inaendelea ukazuka mjadala nani awe anabeba kondomu na matumizi ya kondomu za kike. Siamini kuwa wanawake hawawezi kubeba kondomu ama kuzinunua na kuvisha vionjeo vyetu vya utamu.... na ni jambo la usikivu mkubwa vinginevyo tunacheza mchezo wa hatari. Ndiyo maana daima nakumbuka swali la Mama yangu kuwa mara ngapi umesahau kuvaa kondomu? Hapo kuna maana mbili, aidha umekuwa mzinzi kupindukia hata kama unatumia kondomu hizo AU unatakiwa kutumia kondomu pale unapokutana na MWALI wako katika mshughuliko wa kushughulika na kujipatia utamu kwa kutumia kionjeo cha utamu.

Tunaweza kujifunza mengi kwa kukabiliana na jambo hilo, tunaweza kuongozwa na akili zetu na siyo HISIA ambazo zinakufanya ujutie katika maisha yako yote. Na unaweza kuachana na tendo la kuchunguliana uvunguni siyo lazima ukaombewe na wenye itikadi kali na imani kali. Unaweza kuhamishia mapenzi yako katika vitu vingi tu ambavyo vinakusahaulisha kuwazia Mbunye au mguu wa mtoto....LoL... Haina haja ya kudhani kuacha kushiriki ngono ni tiketi ya kujichua bin PUNYETO kama wale WALIOFILISIKA MAWAZO wanavyotulazimisha kuamini ukiachana na mambo ya MTALIMBO basi utakuwa una jingine kando.

Naamini kidogo unaelewa ninachomaanisha kwani nikisemacho kinaeleweka sana na hakuna wa kubisha kwamba wengi kondomu inakuwa msamiati mgumu. NAKUULIZA WEWE UNAYESOMA HAPA BILA KUJALI UNA NDOA YAKO AU LA, JE NI MARA NGAPI UNAPOTOKA NJE YA NDOA UNASAHAU KUVAA KONDOMU? AU NI MARA NGAPI WEWE MWENYE MABINTI WASIOHESABIKA UNASAHAU KUVAA KONDOMU?

AMANI KWAO, AMANI KWENU, tuwe sote... sasaaaa usiseme nimekataza kuchungulia uvunguni kwani NENO LANGU SIYO SHERIA ila tu nakuusia......mimi nimelipuuza tendo lenyewe kwanza kisha watu wenyewe...lakini usiseme kuwa sitamani......bali NAONGOZWA NA AKILI SIYO HISIA! LoL...................

2009-08-22

STANSLAUS KIGOSI yupo Songea leo!


Yupo Songea, anavinjatri hapa pale, nadhani unajua mambo ya kusafiri huongeza maarifa. Yupo Songea Leo Rafiki yangu huyu! kama unakumbuka msomaji niliandika kuhusu ndoto zake za kuwa CHACHAGE S. CHACHAGE. haya yupo hapa Songea anaburidika mambo mbalimbali. nadhani hata Ruhuwiko atatembelea, hata hivyo siku siyo nyingi naye ataingia NDANI katika Blogu, nadhani mtamkaribisha..... akiwa tayari atawaeleza mwenyewe!
Msomaji, jana nilikuwa na kaka Shaban Kaluse, tukapiga gumzo kidogo na mseto wa majadiliano kuhusu blogu zetu yuko poa sana! MWISHO WAJUMA MWEMA

2009-08-15

YASINTA NGONYANI NA JOHARI YA MATUMAINI

Nafungua anuani pepe nakuta ujumbe, najiuliza kulikoni ni nani huyu? Alaah kumbe mwana wa nyasa, aliye ughaibuni? Ni mwanzo wa kumbukumbu, furaha na burudani. Mzaha wa hapa na pale kustawisha gumzo. Mtandaoni kwa saa nyingi mazungumzo yasokwisha hamu? Hatimaye ndiyo huyu tupo uso kwa uso tunazungumza tunapiga gumzo hapa na pale najiuliza maswali kadhaa kuhusu huyu mtu lakini najua ni mungu ajuaye mengi.

Mawazo yangu yaavaa uhodari wa kujua na kutaka kuona kile ninachoamini. Siku zinapiga miezi, mwaka na saa zote. Nipo ghorofa ya pili, nasoma ghafla ujumbe mfupi unaingia katika simu, salamu toka ughaibuni, najiuliza nitende vipi kwa mwandada huyu? nafunika vitabu na daftari, namtazama mwenzangu pembeni ananikodolea macho anashangaa vipi naacha kusoma halafu nachezea simu? Namweleza kuna jambo, nataka kuongea na mtu kwanza.
Tayari tunajadili hili na lile najadili mambo kadhaa yenye maudhui ya nyasa, halafu tunakumbushana mambo ya Lundo na maisha kwa ujumla.

Inawezekana usinielewe msomaji wangu mpendwa, lakini mantiki yangu ni kukupa mwanzo wa YASINTA NGONYANI na MARKUS MPANGALA. Ni kama andiko la wakristo la yesu alivyowaambia msihangaike kwa lolote wala msibebe vyakula bali mwendako mtajaziwa. YASINTA ni kiumbe mwenye sifa ambazo kila siku naziwazia, najaribu kutafakari, nakumbuka stori zetu za hapa na pale, nakumbuka yale mambo ya WAOOOOOOOOOOO!!!!1 Hee kumbe hatuko peke yetu, tunatulia na kutafakari, tunaleta mzaha kidogo na kustawisha gumzo, mambo ya hapa na pale. Usisahau tupo umbali wa maili nyingi lakini ikawa dakika kuwepo ana kwa ana.

Mimi sinywi soda, situmii pafyumu, wala mafuta makali, siweki dawa nywele zangu daima ni rasta. Nauliza swali aaaahh ndiyo maana Erick naye anapenda sana Rasta siyo? Kicheko kidogo..., namtazama kwa shauku ya kujua mengi....LAKINI nagundua kama kile alichosema Koero kuwa YASINTA NGONYANI ni binti wa kitanzania. Sifa moja kubwa aliyonayo ni MAZOEZI na ukimtazama ni unaweza kubabaika ukasema umri wake ni 23 au 26 hivi kumbe huyooooo.

Hapa nyumbani nina bustani ya matunda na mambo mengi ya nyumbani wala siwezi kubabaikia hayo mambo ya wazungu. Mi hee unaweza kudhani mtu unayezungumza naye anatania lakini kukweli ni binti mwenye itikadi msimamo mkali. Nakumbuka nipo Mbeya, nikabandikwa maaswali lukuki, stori nyingi lakini kikubwa ni faraja za hapa na pale.
Msomaji wangu, huyu Yasinta nina mengi ya kumwelezea lakini nafupisha na kutoa vipande ili upate msingi kamili. Hata hivyo nimemlazimisha kucheza muziki wa KWAITO anacheza usipime kabisaa, majuzi nikamwambia ebu selebuka na MYEKE BABA ya Mandoza... akacheka kidogo.

Nikumbushe msomaji YASINTA ni mkarimu, mtulivu, mkali, mwenye upendo, smikivu, mdadisi ndiyo maana nilimwita Mama Maswali magumu, mchokonozi. Nakumbuka kuna kitu alinichokonoa lakini nikajua udadisi ukaanza.... tusijali hayo lakini nakwambia kama huwezi kuishi na YASINTA basi wewe ni kiumbe wa ajabu. Mara nyingi utamsikia Markus mdogo wangu unatakiwa kujali muda wa kupumzika, utulivu na kujenga afya kwa kufanya mazoezi....
Wakati mwingine inakuwa kama unaota kulala gizani na kulamba mchanga halafu huchafuki kumbe upo ukwelini na unawaza ukweli uleule wa siku zote.

Sikiliza mimi nataka kufanya kitu fulani katika blogu, nifanyeje? Ahh tunachapa gumzo tunafundishana haya na yale. Na fundsho letu kuu la mwisho lilikuwa pale ufkweni kuhusu NeoCounter. Ni mambo matamu ya teknolojia.
SWALI UNAJUA ALIANZAJE KUBLOGU NA KUIJUA BLOGU YA KARIBUNI NYASA?
Kuna kisa cha YASINTA katika blogu yangu hii ambayo naomba msomaji ukitafute. na mara nyingi amenihimiza kuandika tena kwani amevutiwa nacho.
Kumbe kuna siku alikuwa akitafuta akina YASINTA wenzake wapo wangapi duniani, .... ndiyo hapo akutana na KARIBUNI NYASA na kisa kile cha Yasinta mwenzake. vilevile nilimpatia kazi ya kuchoma samaki kama unakumbuka msomaji kuna TANGAZO LA KAZI NYASA, yeye ndiye alishinda. Ila anapenda sana kula MAEMBE halafu na tabia yake ya KUNYWA CHAI ISIYO NA SUKARI yaani CHINGAMBU ni moja ya vionjo vyake na ambavyo nakiri ni MTANZANIA.
Nikamwambia niseme au nisiseme kile kitu fulani....... aaaah Msomaji wangu utanichoka nadhani unaweza kudhani nafanya mzaha. Lakini kiini chake ujue tu ni binti ambaye naona tofauti yake na wengine ni mtazamo na misimamo yake isiyotetereka. Ni mdadisi sana huyu kiumbe, hachoki kujifunza kila mara lakini ndoto yake ilikuwa SISTA yaani wale watawa... utakumbuka ndoto yangu ilikuwa kuwa Padre lakini yamepita...SAHAU. Nakumbuka nikawa namlazimisha kumsoma kaka Ansbert Ngurumo....

Upendo wake na namna anavyoweza kujadili na watu ni kitu ambacho kinanifanya wakati mwingine nimwambie nina wivu sana, na hilo sifichi na nimesema daima ana anajua hilo. Mungu kamleta kwa kusudio la kupendwa na watu wala hana mengi. JE UNATAKA NIKUWEKEE PICHA TULIZOPIGA? aaaaaaahh msomaji nadhani hii stori ndogondogo ni habari kamili ingawaje imekaa mshazari. mtanisamehe kwa kutoweka picha tulizopiga.....
Watoto wake anawaeleza kabisaaa..... nakumbuka anasema na Camilla.... mwanangu funga kanga , lazima kutii utamaduni wetu sawa? Camilla huyoooo anatoka ndani ya bwawa... anaiendea kanga.... mrembo huyu anachukua na kuifunga mwendo wake wa maringo taratibuuu kama twiga najongea mezani. Pembeni Erick sijui kiswidi chao wanasema Irik au? Kijana mpenda mazoezi kama mamake... anafuga rasta.... lakini siku hizi kazinyoa bwana...... a ha ha ha ha!

YASINTA GERVAS NGONYANI.... ngoja nikutaji jina leke jingine..... aaaah hapana siyo ruksa ni mimi tu nalijua au vipi usitake kujua sana. Ni kweli Yasinta mpenzi wa lugha ya nyumbani na bahati nzuri ni mtundu wa kujua lugha za wengine, najua ni wachache wanamudu hilo... lakini ameweza kujifunza lugha za wanyasa wale wanaongea kama wamalawi.... zile MULIBWANJI.... halafu tunahamia mazungumzo katika kimatengo... kingoni chenyewe, kimanda, kimpoto.... kinyakyusa..... nk. ukitaka kufanikiwa maishani ni lazima ujue utamaduni wako na kuheshima na utajua wapi unatoka.....
YAKO MENGIIIIII SAANAAAAAAA............................... tutahabarishana siku nyingine.... manake kuna siri, mafanikio, shubiri na mwenendo mzima wa maisha yake.... harakati zake........ NITAKUMEGEA MAMBO MSOMAJI WANGU, na usisahau kumsoma pale kwa dada Koero( huyu naye subiri simulzi zake nimekuandalia ndugu msomaji na nitajibu maswali ya wanablogu fulani walioniuliza kuhusu YASINTA na hata huyu Koero) sawa? we tulia tuuuuuu
Mwisho wa juma mwema!!!

Watu wa Pwani Bwana!!!!!

Watu bwana cheki madume yalivyojipara, mauno kama dondora, dume zima shanga kiunoni. Eti guu la kushoto lavishwa cheni aaaah! kina dada chuchu njenje zote wanapenda. Chuchu wakipiga mbele na njenje wakipiga nyuma kote wanakwenda haina noma ilmardi waseme tu we choko utakulaaaaa eeeeh nitakula nikishiba nitalalaaaaaa.

Pwani bwana jioni watu wameketi jamvini mawazo chooni hawana soni wala haya, wao wanawaza na kuwazua kama walivyoparamia kuona ndogo kama nayo inaliwa bila kujali ni haramu eti nayo ni uvunguni au uvungu. lakini ukiwauliza swali kwanini mwakula haramu???

JAWABU LAO: VINGAPI NI HARAMU LAKINI VINALIWA?

watu wa pwani mimi sina maneno kwani nawatazama tu kama fungamaneno eeeehh usije ukaumia mbavu bureeeeeee maana hawajui umuhimu wa kujua kionjeo cha ndogo na kubwa ni hamu ya kama vile unafanya hadidu rejea.

2009-08-06

Toleo lijalo la CHACHAGE S. CHACHAGE?


Naam ni rafiki zangu, darasa langu, watu wangu kibingwa! Kutoka kushoto kweda kulia ni mtu wa nne, anaitwa STAN. Nimeandika kifupi tu ili ujue jila lake, ni rafiki yangu, kipenzi changu. Sikuo zote anaamini atakuwa Profes Chachage S. Chachage, nina hakika wewngi tunamfahamu sana kwa kazi zake tangu ALMASI ZA BANDIA hadi MAKUADI WA SOKO HURIA. Ngoja niwaibie habari basi, tayari kitabu chake kingine kinaandiliwa kinapikwa jikoni kwa wachapaji wa E nad D VISION PUBLISHING LTD, unajua kinaitwaje? ni hivi CHACHAGE, UCHAMBUZI WA SERA, UONGOZI NA MASLAHI YA WATANZANIA.
Ningeweza kuorodhesha vitabu vingi vya kampuni hiyo vijavyo ambavyo binafsi navisubiri sana hasa huyu Chachage. Basi rafiki yangu STAN ana matumaini hayo. na hao wote ni nondo kutoka chuko kikuu cha DSM. Au unaonaje msomaji wangu, unabisha kuwa hakuna Chachage mwingine ajaye? haya weee subiri mwenyewe halafu utaniuliza mbeleni.

NYAZODE, Kikao tarehe 9 Agosti hii

Ndugu zangu wananyasa na wengine, natumaini mko salama na mwenyezi hayuko mbali nanyi. Basi ni kwamba kile kikao kijacho kitafanyika tarehe 9 mwezi huu wa Nane, bila shaka tutakuwa pmaoja kwa kila hali, naamini kwamba kikao hiki ndicho kile ambacho kitaidhinisha wale wanachama wapya ambao siyo kwamba siyo wanachama bali wanajumuiya ya nyasa ambao kwa kila namna wanaguswa na hali ya huko. naamini kila siku mambo yanabadilika na mtazazmo unabdilika.

karibuni hakikufanyika kikao shauri ya mitihani ya baadhi yetu na majukumu ya hapa na pale. hata hivyo naamini kila kitu kinakwenda sawa na tutafanikiwa katika jukumu hilo. kama nilivyosema awali kuwa sisi ni watu tulioamua kufanya kile amabacho Wamrekani wamekuwa wakifanya kwa kukiita VOLUNTEER, na mara ya kwanza nilikiona pale Ng"ombo ambapo walikuja kufundisha mambo kadhaa kuhsu dini. nakiri wakti huo sikufahamu zaidi lakini sasa naona hakuna hata haja ya hao kuja kwetu tena.

Nakumbsha tu kwamba unaweza kuwasiliana na watawala wetu ambao wanajua kila jambo. nawashukuru wale walioniandikie barua pepe kuulizia jambo hili, kwakweli nawshukuru sana na natumaini kila kitu kitakuwa swa katika mstari wake. Naamini kwa pamoja tutafanikiwa na kuunda jeshi la mtu mmoja ambalo litakuwa na nia yenye manufaa zaidi.
Ni kwam,ba kikao hiki kitafanyika Mabibo Hostel, yaani hosteli za chuo kikuu cha Dar es salaam, na kama kuna madiliko basi tutafahamishana mapema. Jamani likizo ndiyo hiii na wengi wetu watakuwa katika ameneo yetu kama kawaida na tunafurahi tu kwamba mtazamo utazidi kupanuka.

KIBWAGIZO, hadithi za JORAM KIANGO bwana ni tamu sana. Nakumbuka enzi zile nilikuwa nikisoma juu juu tu katika gazeti la HEKO ama katika hadithi zenyewe. Lakini sasa nimeamua kusoma upyaaaaaaaaa yaani sitaki kupitwa maana najua sasa nimekomaa kweli kuliko wakati ni msingi, basi nimekusanya SALAMU TOKA KUZIMU, MALAIKA W SHETANI, NYUMA YA MAPAZIA na NAJISIKIA KUUA TENA.
Usifikiri nimemaliza hapo kwani najua nina deni la TUTARUDI NA ROHO ZETU, DAR ES SALAAM USIKU, ..................................... na vingine vyote vilivyoandikwa na hayati BEN MTOBWA.

jamani vitabu raha sana, halafu yaone maviongozi yetu yaliyopo madarakani kazi zao ni KUJAMBA NA KUJAZA VITAMBI MATUMBO MAKUBWA KAMA MABWAWA hawana hata kitabu cha kutusiulia japo jambo. mmmmmm samahani, HIVI umesoma vitabu vya Profesa Mbele? Mmmmmhhhh najua dada Yasinta ataanza na zake eti ndiyoooooooooo, haya bwana salamu zao hukoooo

2009-07-29

KUMRADHI WATU WANGU+KARIBU

Nimekuwa kimya sana, hii ni kutokana na majukumu pamoja na shule, muda wangu unaliwa sana na hawa jamaa. Ukimya wangu hauna maana kwamba nimeitosa, ni jambo gumu sana kuachanba na blogu kwani ndiye mke wangu, ndiyo kipenzi changu, ndiye faraja wangu kwa maana kila nikitazama na kusoma maandiko ya kaka Fadhy Mtanga, huku Kitutruru na kule yuko Mzee wa changamoto, angalia mzee wa fikra pevu Bwaya, angalia utambuzi wa Nyegerage(ingawaje alisindwa kunijibu maana na neno hilo wakati wa semina za Freddy Macha) angalia kazi za Kaluse. Dada zangu Yasinta na Koero, yuko Nuru, Subi na wengine ............................. nimeweka deshi ili ujaze jina lako kwa maana tupo pamoja sana.

Nadhani wakristo wanaelewa pale katika kitabu chao cha Mithali kisemapo KUNA WAKATI WA KUNENA NA WAKATI WA KUNYAMAZA. Lakini mimi naweza kunena na kunyamaza, ila sasa tuseme vitabu vinamaliza muda wangu pia maana nimeamua kukusanya simulizi za JORAM KIANGO zote za riwaya za BEN MTOBWA. Tayari SALAMU TOKA KUZIMU na MALAIKA WA SHETANI nimekwisha kuvisoma kwakuwa zamaniu nilikuwa mdogo halafu sikutilia umakini, sasa nakusanya tu, na mwezi ujao nitajinunulia vingine viwili. Unadhani nimesahau utamu wa vitabu vya Prof Mbele? ebu tafuta ujionee mambo kama hujasoma.

Nachukua fursa hii pia kumkaribisha kaka Deogratius Ndunguru katika mambo ya nyasa, maana yamemkuna sana tena hadi akakumbuka Chimate na zile simulizi za mzee wake mashuhuri KANG'OMA. Pia jana nilikuwa na BAHATI LINGALINGA, furaha sasna kukutana na watu ambao tangu tukiwa wadogo sekondari na sasa wakubwa kibingwa.
Natumaini mtanisamehe kwa kutoonekana na sasa naahidi kurejea kiasi na nikipotea nitasema jamani mwenzenu nimebanwa au vipi waungwana? kumbukeni kuna wakati wa kunena na kunyamaza.

Lundu +nyasa= lundunyasa

2009-07-06

Kwa Ajili Yako Mpenzi

Jambo la kweli kuhusu ukweli ni kwamba ukweli UNAUMA. Kwakuwa unauma, na kwakuwa tunapenda UTAMU badala ya uchungu, tunapenda uongo mtamu kuliko ukweli mchungu. Kadiri uongo unavyokuwa mtamu zaidi, na kadiri tunavyoupenda zaidi ndivyo tunavyopumbaa. Zipo njia mbili ambazo kupitia hizo tunaweza kupumbaa zaidi. Kwanza ni kuamini jambo ambalo si lakwqeli na pili ni kukaa kuamini lilele la kweli.

Kuna mambo ambayo sipendi kuyakubali, laikini sitoweza kuyakataa. Kuna mambo ambayo sitopenda kuyakumbuka, lakini sitoweza kuyasahau. Na kuna mambo ambayo sitokuwa na uwezo wa kuyalazimisha, lakini sitakuwa na hiari nayo. Kwa muda mrefu umekuwa ukidhani unaweza, lakini kwajili yako mpenzi pokea nasaha zangu.Kama ni upendo wangu ni mkubwa lkakini sitoweza kujizuia kuvuruga amani yako, na kwakuwa napenda uwe na amani kwahiyo itakuwa vigumu kukuvura na upendo wako.

Na kwakuwa unapenda kuona upendo machoni pako, basi tarajia kuuona ikiwa utaleta upendo wako. Nadhani uliamua mwenyewe kuamua, lakini kama ulikosea kuamua na sasa unaona kama makosa hayo ni makubwa, basi tafakari kwanini uliamua huku ukiangalia hao wanao. Waone kwa upendo, watazame kwa amani na mabaya yote ya mumeo yasahau. Kwakuwa nilikuwa napenda uwe karibu yangu lakini ukaamua uliyoamua basi hakuna sababu ya kulalamikia uamuzi wako.

Unapaswa kuelewa hakuna binadamu aliyekamilika, na hata kama kuna mtu anadhani atakupenda zaidi ya unavyopendwa na mumeo hilo sahau kwani huo ni unafiki. Na kama kweli unadhani upendo wake upo kwako na ndiyo maana hadi ametoa talaka, hilo mimi siliafiki tena natumaini kwako litakutokea tu kwani kama amefanya hivyo kwa mwingine, je itashindikana vipi kwako? Na kama anakupenda hata kuamua kuvuruga ndoa yake ili akuoe wewe jaribu kutafakari kwa kina. Mimi nilikupenda na nakupenda, lakini uamuzi wako wa kuolewa ni jukumu lako, halikuwa langu.

Kama mwanamke mwenzio ameachwa eti kwaajili yako, je wewe ungependa kutendewa hivyo? Je wewe haliweza kukuta hilo? Na mwanzo mpenzio ulimpendea nini? Na kwanini uliniambia nikushauri kuhusu kuolewa wakati uliamua? Nakupenda sana naomba tulia na ndoa yako kipenzi changu. Mungu akulinde pokea UA.

Markus Honorius Mpangala
Mbinga-Ruvuma
Tanzania

2009-06-18

Suala la Miguu Ya Koero!!!!!!

Wakati ninasoma kitabu cha DEBBIE DAVIS mwanamama mtaalamu wa masuala ya mapenzi nilikutana na suala la kuvutiwa na kiungo fulani cha mwili wa jisia nyingine. Nakumbuka rafiki yangu mmoja aliwahi kuniuliza ni kiungo gani katika mwili wa mwanamke nakipenda zaidi? Swali lake lilinikumbusha hoja ya baba yangu kuwa katika mwili wa mwanadamu hakuna kiungo kisichotegemea kingine.

Kwahiyo iwapo mwanaume anavutiwa na mguu wa mwanamke basi ni jambo la kujiuliza kwa makini. Basi miye nikatafuta picha nzuri yenye mguu ambao unaweza kuwakilisha maoni ya Debbie Davis. Lakini nikakumbuka picha hii hapo juu niliyopiga wakati najiaandaa kushinda na USAIN BOLT yule mkali wa mbio wa kule jamaika huku nikishindana na dada Yasinta katika kuwakilisha.
Pamoja na haoyo naona hoja yangu imehama kwakuwa kuna mguu unofanana na wa Koero, ila sijajua ni Koero yupi mnayemzungumzia hapa.

Sasa wakati najaribu kutafakari nikaona hebu niikumbuke hile picha yangu ambayo nilipiga mwezi januari, ili nione penine miguu yangu inafanana na nani sijui. Hivi kumbe kuna akina Koero wenye miguu ambayo inaweza kukufanya ukataka tu kujivinjari bila kupenda na kionjeo kikawa kinahangaika kukupa utamu na marudi yake ni makini na sahihi kuliko kwanza? Duh! nawaza tu, nakubali sana maoni ya kaka Simon Mkodo Kitururu maana najua nini alichomaanisha lakini usije ukaelewa sana kwani utamuia kichwa msomaji bureeeeee!

NAM nimewakilisha miguu yangu hapo, je inaweza kuwa tiketi ya kunogewa au? Maana kuna jinga moja hapa mtaani linatazama miguu yangu utadhani mishikaki, utadhani linataka kunimeza, lakini likubwa tena la mtu, na pete kidoleni.
Je suala la Miguu ya Koero na miguu ya wakware inatofauti na watazamaji wasiopenda kutekenya ukubwa wa ugali???????

Nani anapenda KISWAHILI chenu kichafu???

Kila nikipitia mitandao au kusoma magazeti nakutana na matumizi mabaya ya kiswahili, wengi tunatumia kiswahili vibaya, mtamshi mabaya, silabi mbovu, kanuni za lugha zimetupwa yaani kila kitu ovyoovyo tu.
Sina hakika kwanini jamo hili linasingiziwa kwa njia ya teknolojia lakini nidhahiri utandawazi ni nguvu ya utamaduni mwingine kwahiyoiwapo nchi inakuwa kama kundi la magabachori wale wasiojali hali za wengine na kukumbatia hali zao hata kama mbovu basi mambo ni juu ya mambo kuwa mabaya.

Yaani neno AAMINI= wanamaanisha HAAMINI
AMNA= wanamaanisha HAMNA
KUWA NA KUA= linatumika vibaya kwa kudhani ni maana moja
LISAA NA MASAA= wanamaanisha SAA
UJUI wanamaanisha HUJUI
UO wanamaanisha HUO.
ALAFU wanaamisha HALAFU

Nani kasema huo ndiyo ukweli wa lugha yetu adhimu? Kiswahili gani kibovu namna hii halafu mnasingizia zama mpya? Natamani kumezwa na ardhi yeoteee inifunike ili nikose kuyaona lakini natamani kuendelea kuishi. Badilikeni lugha iwe katika mhimili wake

2009-06-02

NYAZODE, ndiyo hii hapa sasa

Katika mkutano wetu wa jumapili ya jana kumefanyika jambo amabalo nimelifurahia sana. Kilichofanyika ni kuendelea kujitokeza hata wale ambao hawapo vyuo vikuu, bali hata kama yupo katika shughuli zake ilimradi tu anahusika na nyasa kwa kupitia elimu aliyoipata pale UNDO sekondari, kwahakika mambo ni mazuri.
Rasimu ya katiba inaandaliwa, kuwakaribisha wanachama yaani wanaoweza kutoa mawazo yao au kujumuika nasi katika lengo hili.

Sasa ni NYAZODE# hii ni NYASA ZONE DEVELOPMENT GROUP, tumebadili jina hilo ili kila anayejiunga asione yupo katika mkusanyiko bali yeye ni mwanakikundi ambaye anahitajika sana. Suala la katiba, uongozi na mambo muhimu yamejadiliwa, yanamalizika sasa. Kikao kijacho ni kuiweka vema rasimu yetu ya katiba na, mpango wa kufungua akaunti ya akiba ya NYAZODE.
Hii itasaidia hasa pale tutakapopitia baadhi ya shule za sekondari kuangalia wanafunzi wenye matatizo ya ulipaji karo hapa nyasa, na kuwaangalia katika michango mbalimbali. Pamoja na kusaidiana sisi wenyewe kama wanajumuiya hiyo katika mambo mbalimbali. Tumekusanya wengi na tutazidi kuwaelekeza wengi pia.

Hakika tunaweza CHANGE WE CAN BELIEVE IN *YES WE CAN
Tunashukuru pia Bwana Kapinga kutuunga mkono katika jukumu hili, maana Waraka wa kwanza wa Petro 3# 3-4> anasema NAYE NI NANI ANTAKAYE WADHURU MKIWA WENYE JUHUDI KATIKA MEMA?

KUSOMA> Mkononi ninaye YASSER ARAFAT

Pamoja na harakati au mchakamchaka wa maisha na shule kunibana kwa mitihani miiiiiiiiingiiiiii, lakini sijaweka kando jambo hili. Ninaye mkononi Yasser Arafat nakula nondo zake, najielimisha. Lakini bado kitabu cha Prof Mbele ninahamu nacho sana tena sana.
Sasa nadhani mambo ya mzee wangu Freddy Macha na semina za ujuzi zimekwisha, nimefaidika nimejifunza, tunmeongea mengi, tukafurahi na kupiga gumzo la hapa na pale. Vilevile mkononi ninaye TOM CLANCY katika THE CARDINAL OF THE KREMLIN. haya msije mkasema nimeacha kuvua samaki na kuvamia kusoma. Mimi na samaki ni kama mizizi na ardhi. KOERO mwana wa MKUNDI upo hai au umekumbwa na KIDELI maana siku hizi duuuh! haya mambo ya aiseh! ha ha ha ha

BURIANI> wana PAN AFRICANISM na PAN LOCALISATION

Tangu juma lililopita nilijulishwa na rafiki tangu wa karibu aliyeko nchini Kenya. Alinidokeza saa chache baada ya ajali iliyomwondoa mwanamapinduzi huyu na mwezeshaji wa MDs pale jijini Nairobi. Ni TAJUDEEN ABDUL-RAHEEM. kwa hakika nitazikosa kazi zake nyingi katika medani za uchambuzi wa mambo ya kiafrika, nitakosa na na kusikitika kama nilivyosikitika kwa muda wa juma zima huku nikitafakari kuwa kifo ni kitu gani. Lakini mwanafalsafa Socrates anatuonya kuhusu kuogopa kifo ni ujinga kwa kudhani tuna busara kuliko mungu.
Juma zima nilikuwa najaribu kuwaza kuhusu mwanamapinduzi huyu na ajali iliyomtoa duniani. Mungu mkubwa yupo nasi, kama ajali ni majaliwa yake basi hatuna neno,lakini kama siyo majaliwa yake basi tunazidi kumwombea mema. AMEN

2009-05-24

NYASA DEVELOPMENT ORGANISATION

Nilikuwa nimebanwa kidogo na semina za Freddy Macha, nikashindwa kuandika hapa, lakini nashukuru mungu nimerudi tena.
Ndugu zangu kimsingi jumuiya yetu hii ya Nyasa development organisation inaundwa na sisi vijana ambao kwa wastani kwa umri ni chini ya 27, tupo katika masomo tofauti kuanziia sheria, siasa, ustawi wa jamii, elimu, sanaa, kompyuta, na mambo mbalimbali yanayohusu elimu yetu.


Mradi huu ni ubunifu wetu kwamba kwa kiasi gani tunaweza kuibadili hali ya nyasa au maeneo yaliyopo katika jimbo la mbinga magharibi? hili lilikuwa swali kubwa sana kwetu, lilikuwa jukumu ambalo kama wanadamu tunapaswa kukabiliana nalo. kundi letu linaundwa na wanafunzi toka chuo kikuu cha dodoma, dar es salaam, IFM, na vingine vingi tu. kwani dhamira yetu ni kuwakusanya wenzetu ambao hawakuhudhuria awali tunaamini kuwa mchango wao ni muhimu sana,


Leo ni kikao cha pili, mazimio yatafikiwa na nitayaweka hapa. Tukumbuke huu ni mradi wa kujitolea, tumeamua kutumia nafasi tuliyopewa katika elimu na nchi yetu ili kuyabadili mazingira yetu. Mara nyingi namkumbuika sana Ndesanjo Macha, huwa nasisistiza kuwa ukitaka kuleta mapinduzi katika nyanja za kimaendeleo basi anza mwenyewe kwa kubadili sura ya mtaa wenu. Hilo ndilo lengo letu sisi vijana, maana tunaamini ni jukumu letu kuyaweka mapinduzi ya maendeleo katika ukanda wetu na hakika tuna dhamira kubwa sana, pia blogu yangu itakupasha mambo yote yanapohusu mradi huu na ikibidi kuanzisha blogu nyingine kama kutakuwa na umuhimu huo tutafanya hivyo mara mradi huu ukikaa ukiwa katika mhimili wake.


Nashukuru maoni ya mzee wangu Prof Mbele, kwa hakika umenipa faraja kubwa na kuona kwamba wapowatu wanaojali hali za wengine katika maisha. TUMEAMUA KWA DHATI, NA LEO HII NINAVYOANDIKA HAPA KUNA KIKAO KINGINE ILI KUIPANGA MIKAKATI ENDELEVU. tunakaribisha mawazo yenu ni muhimu sana.
kama unapenda kuwasiliana moja kwa moja na kiongozi wetu AMBROCE NKWERA, simu yake ni hii hapa 255-712514078, mawasiliano mengine tutayaweka hapa au niandikie katika barua pepe, lundunyasa@yahoo.com au jikomboe@gmail.com .
Leo ni kikao cha pili saa tisa katika ukumbu wa NewVenus pale mtaa wa Relini Tataba jirani na ofisi za gazeti la Mwananchi. KARIBUNI

2009-05-21

Kikao cha Dharura kuhusu NYASA

nilipotea kidogo, lakini nilikabiliwa na kikao kizito na muhimu zaidi kuhusu NYASA. Nambukuka mwanzoni mwa mwaka huu mzee wangu Profesa Joseph L.Mbele alinishauri kuhusu kuandika kitabu kuhusu nyasa. Nililipokea wazo lake kwa mikono miwili huku rafiki yangu koero akisisitiza jambo hilo.

Hata hivyo naweka wazi kwasasa kuna kikao kizito kuhusu nyasa, kikao ambacho kinaendeshwa na wanafunzi wa vyuo vikuu ambao wametoka katika ukanda wa nyasa. Kikao hicho kinazungumziaq maendeleo ya maeneo hayo na namna ya kuanzisha umoja ambao utawezesha jamii za nyasa kielimu,siasa, na uchumi. Jambo hili nashukuru linafanyika huku wazo la mzee Mbele likiwa mezani kwangu.

Jumapili iliyopita kulikuwa na kikao hicho, tulijaribu kuweka ama kuorodhesha kero na mambo mazuri ambayo nyasa tunayo na tunaweza kuwafaidisha wakazi wake. kikao hicho naweza kukiita NYASA DEVELOPMENT ORGANISATION. ni wazo ambalo tumeamua kwa moyo mmoja kujitolea kwa kuanzisha kikundi hiki kwa nia ya kuendeleza wananchi wa amaeneo yetu.

Kikao hiki cha kwanza kimefanyika huku wahudhuriaji wake ni BARAKA WANDAWANDA, HELLEN LOCHI. LAWRENCE EMANUEL, BONIFACE MNDALA, EMMANUEL NAMINGA, RICHARD MWANJA, VENANT KATOPOLANGA, SIMON HARRISON, FRANK NDOMBA, FRANK MAPUNDA, na LIBADA MAPUNDA pamoja na MARKUS HONORIUD MPANGALA.

Sisi siyo mwsho bali wenzetu wengine walikabiliwa na majukumu ya chuo, kwahiyo tunaamini kikao kijacho cha jumapili wiki hii kitakwenda katika mpangalio uleule. jitihada ni kubwa na ari yetu ni kubwa sana kwani kikundi hiki kinaundwa na vijana ambao wastani wa umri wetu ni chini ya 25. Tumedhamiria na tunahakika lengo letu litafanikiwa.

Mipango yetu ikiwa katika njia sahihi nitawahabarisha zaidi ili mjue dhamira yetu watoto wa kinyasa kuwa tunataka kufanya nini katika ukanda wetu na watu wetu. Kundi hili linakaribisha mwanachama yeyote ambaye anaweza kukiboresha na kusaidia mambo mbalimbali hususan mchango wa mawazo ambao ni muhimu sana. Vilevile ingawa ni suala binafsi sana lakini nawaomba Raiton Mbele(Ukraine), Robert Ngalomba(UK) na mzee wangu Mbele kuwa mchango wenu ni muhimu sana. Yasinta Ngonyani(sweden) nawe pia tunaamini kuwa upo pamoja nasi. Pia Mzee wangu Prof Mbele ningependa na nitakupendekeza uwe mlezi wetu iwapo nafasi itakuruhusu kwani mchango wako ni muhimu sana. Jumapili iyajo(juma hili) tunakikao cha pili ili kufikia maazimio yetu.
Tunakaribisha kila ya aina ya mawazo yenu wanablogu wote bila kujali ukanda wala mahali ulipotolea bali tunachofanya ni kujaribu kuwezesha jamii zetu. Sasa ninajikita katika kujitolea kwa jamii rasmi bila malipo. Tunawakaribisha sana nyasa.

2009-05-16

HAPPY BIRTHDAY MARKUS II

Nawashukuru wanablogu wenzangu, nawashukuru kwa kila namna yaani hadi chozi linadondoka, nawakumbuka zaidi ninyi kwani mnanifanya nijue kwamba wapo watu wanaonijali zaidi. Koero Mkundi uko wapi mziwanda wangu?, u hali gani huko mafichoni??????
Amini upendo mtamu
kama salamu tamu
kwakoFadhy wangu
Wanipa hamu hamu
Mtanga wangu, asante daima
Uso wapwita chozi,rabana ajua
Nionacho, u mwanamalenga
Hakika nakusujudia
Dhima yako idumu,milele
Maisha yangu kama tetere
Naishi bila kelele,nisonge mbele
U wapi koero wangu
U wapi pacha wangu
Kilio waona humu?
Nione kwa tonge au saumu.
Asante Changamoto, nipo mjini
jogoo la shamba mie,siwiki mjini
mtandaoni nipo,mjini nyingi dili
asilani sitokwacha,niamini
Nawasalimu kwa hamu
sina simile wala gubu
Nawapenda ninyi,mdumu
sijafunga kufuli,mlango u wazi
Jasho la majukumu, lakula muda bloguni
Wape hi Marekani na mashariki ya mbali
Waambie bongo twaishi mambo ni shwari
Asante Yasinta,kwa siku yangu
Kumbukumbu najivunia wangu
Usijali tupo sawi,tudumu
Asantedada weshi, ukarimu udumu
Usumbufu ulokubali,kunikirimu
Ahadi yetu itadumu,daima idumu
mungu mkubwa waungwana
Nimetembelea maduka ya vitabu pale Afrikasana kwa dada Weshi Lema kisha akanipeleka Mikocheni pale mtaa wa Regent, nikajipatia kitabu cha "PESA NA MAWE" kitabu kizuri nimekipenda, nashukuru kwa wote mliopo nami kwa kila dakika, kaka Simon mkodo Kitururu naamini tuko pamoja daima.
Nawashukuru nyote nawapendeni sana, hata kama sijakutaja najua hapa ................................. utaandika jina lako.
Dada Yasinta kwa kila dakika ya kunijulia hali na kujua siku yangu nashukuru sana. Digna, Manka na wengine. Nawapenda sana, upendo utadumu kama samaki na maji ingawa malaria yalinisumbua lakini sikuacha kwenda dukani kujinunulia kitabu. nitaandika kile nilichojifunza baada ya kwenda katika maduka hayo na ukweli wetu watanzania.

2009-05-15

"HAPPY BIRTHDAY MARKUS"


Hongera MARKUS HONORIUS MPANGALA, mwana wa nyasa umpendaye MALCOM X kila leo au JENERALI ULIMWENGU na JULIUS NYERERE, amani kwao watu hawa!
UPENDO UWE NANYI
Nashukuru baba na mama
Kwa kunileta hapa duniani
Nami najivunia kuishi ndani
Nashukuru sana wangu maanani
Kwani yupo nami kwa shida na raha
Kama machozi na majonzi naamini yanapita
Nashukuru ndugu waliopo hai
Na wale wasiohai, nawapenda kikweli
Upendo wangu, zaidi ya mshumaa
Nitawaangzia kwa uwezo wangu daima
Ningali nawajali, upendo usiopimika
Kwani ni tunu yake maulana
nawashukuru marafiki zangu nyote
Bila ninyi nikiri siyo mwenyewe
Najua imani yangu nimejaza kibaba
Naamini mola yupo nasi daima
Anajali,kutulinda na kutuhusudu
Ndiyo maana avumilia wetu utundu
Nawashukuru enyi wapenzi mlokuwa nami
Nawapenda kama amri ya mola
Kwani ni agizo la thamani daima
Nipo nanyi kwa mapenzi ya maulana
Nawashukuru maadui wote
Kwani mnanifanya niwe kama nilivyo
Bila ninyi sitokamilika, nawapa upendo
Mungu mkubwa.
Ni siku yangu ya kufurahia kuzaliwa kwangu, nashukuru wanablogu wote mliopo karibu nami. kwa pamoja tuseme waweke upanga au shoka au kufa ama kupona-mtaani tutabanana kwa pamoja tutafanikiwa kile kinachotakiwa kufanikiwa.
Na kwa yule mke/mchumba/mpenzi/demu n.k, ingawa nanua hujui kama wewqe ndiwe ninayekuhitaji. Labda hujui kama wewe ndiwe ninayependa uwqe demu/mchumba/mke wangu, lakini leo ujue ni siku yangu ya kuzaliwa.
Ingawa leo malaria yamenibana lakini nashukuru manesi ingawa wameshika matako yangu na kunidunga sindano. Najua kwa nia njema nitapona ndiyo maana ukichomwa sindano takoni unaambiwa poleeeeeee, ingawa nilisahau kumjambia ili nimwambia nami poleeeeee.
Najua kila mmoja anayozawadi yake lakini Koero Mkundi sijaona zawadi yako, unabifu na mimi au? Nashukuru Yasinta Ngonyani, zawadi yako nimeipenda sana1 daima tupo pamoja! OOOOhhh kwa wazee wangu nawaambia mjue mtoto wenu ni mwingi wa utani, mnivumilie ninaposema nesi amechezea TAKO langu. nadhani mnajua mambo ya kutaka uzima
LAKINI
atakayeweza anitunuku kitabu cha THE WORLD IS FLAT cha Thomas Friedman, nimtafuta hadi najamba. Mwenyewe ninacho mknoni JULIUS KAIZARI na CRYSTAL RAPTURE pia nakwenda duku la vitabu sasa kujinunulia zawadi. Bwaya, Kaluse,Kamala, na wengine naweka ..................................... ili ujaze jina lako kama nimesahau.
upendo daima, salama kwa mchumbangu usiyejijua kama ni wewe, naweka ........ andika jina lako

2009-05-01

Vuna pesa kupitia Blog yako

Dada Koero Mkundi, siku kadhaa alinidokeza kuhusu jambo hili. Yaani unavuna pesa kupitia blogu yako. hii ni habari nzuri na nyeti maana najua kuwa wale akina dada Asimwe walioulizia kama kuna malipo katika blogu.
Hata hivyo nadhani habari hii itasidia kidogo ili kuweza kujua namna ya kuweka ukurasa wa kujipatia pesa kwani wao wanachofanya ni kuweka kulingana na matakwa yako.

Isome habari nzima halafu ichanganue mwenyewe au kama kuna la zaidi usisite kuniandikia katika barua pepe/anuani pepe ili tuweze kufanya mambo makubwa. jamani blogu siyo ipepo wa kupita au siyooooo.

SOMA HII:

The Monetize tab in Blogger makes it easy to enable AdSense ads on your blog. Once enabled, Blogger will retrieve your AdSense earnings data directly from AdSense so you do not need to go to AdSense to get basic earnings information.
AdSense Reports
Once you start generating AdSense impressions, you will begin earning money when people click on ads that show on your site.
The earnings report (visible when you click on the Monetize link from your Dashboard, or the Monetize tab when viewing your blog while logged into Blogger) includes a drop-down bar with Today, Yesterday, Last 7 Days, This Month, Last Month, and All time.
Selecting an option will retrieve the relevant report directly from AdSense.
All time
If you are already an AdSense user, you will notice that Blogger created a new channel (with the URL of your blog) in your account. If you have had AdSense ads on your blog before using Blogger’s AdSense integration to insert ads into your blog, it is important to note that All time will retrieve data only from the time you connected Blogger to your AdSense account.
This in no way affects your overall AdSense reporting, available directly from AdSense.
Terminology
The AdSense report visible from the Monetize tab contains basic information about how many ads have run on your blog, how many clicks were generated, and how much revenue you have earned. Each term in the report is defined below:
Page impression: A page impression is generated every time a user views a page displaying Google ads. We will count one page impression regardless of the number of ads displayed on that page. For example, if you have a page displaying three ad units and it is viewed twice, you will generate two page impressions and six ad unit impressions.
Clicks:# The number of times an ad was clicked on in the given reporting period.
Page CTR (Clickthrough Rate): The number of ad clicks divided by the number of impressions for the page of ads that appears when a link unit is clicked.
Page eCPM (Effective Cost Per Thousand Impressions): Calculated by dividing earnings by number of page impressions and multiplying. This makes it easier to compare multiple sites to see which are performing better.
Earnings: Total revenue earned to date. More detail about earnings is available in the AdSense Help Center.

Nyasa, lakini sikuwahi kumwona


nimezaliwa na kuklia ukanda wa ziwa nyasa. ukiniambia mwamboa huo ni wapi sijawahi kufika toka Itungi pale bandarini Kyela hadi mwisho wa kijiji kuingi Msumbiji katika pale Chiwindi. Lakini yote hayo huyu mnyama sijawahi kumwona, zaidi nilichoona ni sehemu tu aliyokanyanga au kuona pua yake kwa mbaliiiiii akiwa majini, lakini nasikitka sijawahi kumwona.
lakini najivuni kuwa mnyasa jamani, karibuni

2009-04-26

Mjumbe hauawi jamani, nami nimeyakuta

nimeikuta hii picha katika kompyuta hapa ninapoandika hili jambo, kwahiyo ili kushirikiana na wenzangu naona ni vema nami nikaiwasilisha kwenu wadau. suala lenyewe ni RICHMOND ile kampuni iliyosababisha kutetereka kwa serikali yetu. sina mengi ila jionee mwenyewe, nani yuko katikati nani yupo kulia na mengineyo. imetengenezwa na jamaa wa Mzumbe chuo kikuu kama alivyoandika hapo juu. kazi kwenu

Nawapenda mkiwa kama hivi

Picha ka hisani ya watu fulani hivi ambao wanapenda kujuza wenzao mambo mazuri kama hivi. nawapenda mkiwa na mavazi kama haya, lakini hata mengine ilimradi hayaonyeshi mtikisiko wa matako kwa nyuma na zile nguzo zetu za kwanza kuvaliwa na za mwisho kuvuliwa. labada cha zaidi nawaza ni nani ataweza kufanya hivi katka jamii zetu za sasa????

2009-04-16

Yasinta+Wanablogu= MIMI NABISHA

Nilikuwa napitia mada mbalimbali ambazo nimezikosa tokana na kutokaa sana mtandaoni. Nimevutiwa na mada ya dada Yasinta kuhusu mapenzi. mada hiyo kilichonikuna ni maoni ya Prof. Mbele. kwamba tunatakiwa kutafakari kwa kina namna ambavyo tunaiga kila kitu. Kama ambavyo ameandika makala yake katika gazeti la KWANZA Jamii

Amejaribu kuhoji maendeleo ni nini na kwanini tunakubali kuitwa nchi zinazoendelea. Kimsingi kama ambavyo NABISHA kwamba magaidi pekee hawakulipua WTC mwaka 2001 bali kuna mambo yanaendelea.

Sasa katika maoni hayo nakubali kwamba yeye kama mimi nimekulia kijijini na nawaza kwa msingi wa kijijini, mtakumbuka niliwahi kundika kwamba ndege wangu amepotea. Hoja kuu ni yale yale ya kuonyeshana mbele za watu kwamba mnapendana, inawezekana kweli lakini sioni mantiki wala ulazima kama kuiga kila jambo toka kwa wazungu.

Nitaishi hivyo hata kama wapenzi wataona wamekutana mhafidhina kama rafiki zangu wanavyoniita daima. Kikubwa ni kwamba sisi kama binadamu lazaima tuwe na njia halisi za kuishi kama sisi. Lazima tukubaliane kwamba UTAMBUZI ni soma muhimu sana. ndiyo maana tunajiuliza sisi ni nani??????????? Ikiwa kama ambavyo dada Koero alivyosema kwamba siku hizi tunaiga kila kitu, nakubaliana naye akumbuke kwamba HAKUNA MTU ANAYEWEZA KUFANYA NGONO KIZUNGU au hakuna anayeweza kucheka kizungu bali utacheka kama wewe ulivyo siyo wao walivyo. Tabia hii ya kuiga kwamba ni lazima kama mwenzako anahuzuni kimapenzi umfariji imeshamiri lakini haina sababu za kutokea kwake zaidi ya kuiga tu. kuna mambo yanatia KINYAA namna ambavyo tunaiga. Naamini ipo siku tutaanza KUNYA, KUTAPIKA, KULEWA, KUOGA, KUKIMBIA kizungu tena kama akina BUSH, BLAIR nk.

Lakini msingi huo wa kuiga unatokana na HULKA ambayo tunajijengea kwamba kizazi chetu chenye kuhoji ukweli kinataka hata akiwa tegemezi kwa wazazi yaani awe na miaka 17 au 20 anataka kuleta boyfriend wake au girlfriend wake nyumbani kwa wazaziwe. AJABU hivi haya ndiyo mambo tunayoyataka au ni nini? Kuiga mambo ya kijinga kama hayo au kudai kwamba kumpenda mtu kwa dhati unapaswa kuonyesha hadharani huo ni UBATILI. Kumpenda mtu kwa dhati wala hakuambatani na KULAMBANA mitaani au kujidekeza eti uhudumiwe na mpenzio kwakuwa aonyeshe anakujali. Hivi unadhani kukujali kwa kuzoa matapishi ni lazima iwe mapenzini?? Usimfanye mtu kuwa kila kitu kwako maana siku akiondoka hutakiwa na kitu!!!

Nina mengi ya kuwajuza walimwengu, naweza kuongeza hata ujinga halafu nikashindwa kujieleza vema. HEKO mzee MBELE kwa kuonyesha uhalisia, ndiyo maana nahoji hata mantiki ya ndoa zilizopo hapa duniani kwa kisiingizo kwamba kilichofungwa na mungu binadamu asitenganishe halafu anayesema maneno hayo ni binadamu mwenzio ha ha ha ha ha ha ha ha nicheke mieeeeee.
Nini kudekadeka bwana, nini ulindwe na mwanaume bwana, jilinde mwenyewe, nini kufunguliwa mlango na mwanaume???? kwani wewe umekuwa kiwete??? nini kushikwa kiunoni bwana mbele za watu, kwani huko vyumbani hakutoshi????? kwani nini washkaji??? ha ha ha ha ha a ha ha ha nawaza tu
Msikilizeni sana EMINEM hasa pale asemapo katika wimbo wake wa JUST LOSE IT halafu niambieni yule jamaa kwanini alikuwa akiishi na vitoto ndani.

ha ha ha ha ha ha leo nimeamua kuwaza zaidi. haya mawazo tu wala msikasilike washikaji maana wakati mwingine NAFYATUKA na KUBWATA. ha ha ha ha ha ha ha ha ha ooooooooooiiiiiiiiiiioooooooooo ngoja nikavue mjanhahali ndo msimu wake huu bwana.
karibuni nyasa

HATIMAYE: Wamefika nyasa, wamefika Mbamba bay

Wamisionari,watawa au tuseme watu wa dini au vipi? lakini kumbuka usiwe na kicheko kile cha nyege za kutaka kujua kulikoni lakini tulia tu nikuhabarishe mambo ya nyasa. Chipole kuna sekondari inaitwa St Agnes ni shule ya watawa wale nadhani ni pamoja na wale wa Wabendictino wa Peramiho( dada Yasinta, sahihisha).

Wamekwisha kutua Mbamba bay na hii ndiyo hoteli yao ambayo inatwa MBAMBA BAY HOTEL. Nakumbuka yupo dada Anna pale tuliyecheza naye enzi za Mwalimu, enzi za wewe baba na mimi mama au vipi? lakini siku hizi najua amesahau hakumbuki shauri kavaa utawa jamani duuh!1 sasa habari yenyewe ndiyo hiyo kwamba wameanzisha hii hoteli au shirika la utawa ambalo ni shemu ya Chipole.
haya wageni na wwale wasiojua kuogelea na wanaogopa kama dada Yasinta(eti anaogopa mamba) Karibuni sana. tovuti yao http://www.chipolestagnes.org/ (kama sijakosea0.picha kwa hisani yao

2009-04-14

Nimewasikia+Nitawafikia= Tutaongelea

pasaka iwe bora kwenu nyote

2009-04-01

mjadala: waliberali vs wahafidhina

david frum ametuanzia mjadala fulani katika mambo ya utawala wa marekani. wakati huo jonathan darman naye kasema kile ambacho mwenzake kasema.
nakumbuka rafiki yangu anaiita mhafidhina kama magret thatcher. unajua huwa napenda sana mambo ya uhafidhina ndiyo maana sipendi kukubaliana na kila jambo ambalo waliberali wanasema kuhusu mabadiliko ya dunia.

katika orodha ya wahafidhina ambao wanamkosoa kwasasa rais obama ni jamaa wa kambi ya republican. ebu angali orodha yake ; newt gingrich,rush limbaugh, sean hannity john yoo, george stephanopou na wengine kibao.

wao anasema kwamba "liberalism will fail" lakini hawasemi kuwa obama atashindwa. wasema kwa maneneo yao hadi dihahaka ndani yake; soma " one the one side, the president ot united states is softspoken, and comciliatory,never angry, always invoking the recession and victims.

unsurprisingly women are trust him and admire, he is spoken about "responsibility" zaidi soma hapa

jamaa wamekandamiza humo ni balaa. lakini swali na mjadala mkubwa ni kwamba wao wanasema hawaoni kipya toka kwa liberalism na hata huyo obama.
je wanablogu tunasema kuhusu utawala wa washington kwa sasa na matarajio yetu kwa baadaye katika utawala wa obama?

mimi sijui ingawa kweli ni mhafidhina ambaye sikubaliani na rafiki yangu kuwa liberalism. bado sijarudi kikamilifu wanablogu wenzangu

2009-03-28

CHUPI: Nani alianza kuivaa?

Nimekaa na jamaa tunawatazama watu wakifurahia yao bahari, wakijimwaga majini kwa taha zao, wengine ndiyo wale wapendanao, wamekaa mikao ya kuwaniana. Wamekaa mikao ya kutakana na kupeana hamu. Lakini swali moja ninajiuliza inakuwaje mtu wangu hatujimwagi kama wao?
Lakini natamani kujimwaga majini ili nami niwe kati yao lakini mbona sipo kama wao maana wamejigawa wawili wawili halafu miye na mshikaji tupo 'kiugumu'. Lakini ugumu mwingine wa ajabu sana.

Sasa nawaza sana hivi CHUPI alianza kuvaa nani? Natafakari nawaona mabinti na wavulana huku wanawake na wanaume wamevaa CHUPI/VYUPI. Mimi nawaza tu najua nina CHUPI moja halafu namuuliza jirani kidogo kwamba umewahiku kuulizwa swali la kijinga? jamaa anacheka ghafla anakuja HANII wake bwana anasaula nguo anabaki na CHUPI namtazama hadi nahisi mate fulani yenye majimaji laini yaashiriayo kunogea kitu. si mnakumbuka KIONJEO jamani.

Inabidi ageuke na kunisalimia yule binti halafu anauliza mko wote shem? Najibu kama binadamu tuko wote ila kihisia na mawazi ya mazingira haya hatupo sawa maana wewe ushafika sasa! Jamaa anashangaa halafu anakumbusha vipi swali lako? Namwuliza hivi NANI ALIANZA KUVAA CHUPI? Nauliza tena je ADAM na EVA waliwahi kuvaa CHUPI? mbona picha zao zinaonyesha wamefunga misuli tu, vipi mle ndani nao walikuwa wanavaa CHUPI kama sisi au huyo shem hapo? au zile CHUPI zenye kamba moja ipitayo katikatu ya milima miwili ya nyuma yetu?

Binti akashangaa, nikamwuliza hujawahi kuvaa CHUPI? nauuliza huku naona kavaa lakini pengine siyo chupi ni bukta tu. Hata hivyo lengo langu ni kujiuliza nani aligundua utengenezaji wa CHUPI? wala sitaki kuingia mtandaoni ila nawaza mwenyewe tu ni kwanini aliona CHUPI ni kitu muhimu? Sijui labda nimechanganyikiwa! Eeeeeh ngoja nikomee hapa bwana mmmmhhhh Waone hao jamaa pichani na chupi zao

2009-03-12

Kwako dada ASIMWE, naongea na wewe

Kwanza niomba Radhi kwa wanablogu wenzangu, kwamba nimepotea sana katika kuchangia mambo mbalimbali katika blogu zenu. Nina hakika nimeelweka kwa wwale niliowaeleza sababu za kupotea kwangu. Lakini naamini tupo pamoja kila siku BADO NIPO NIPO KWANZA.
Pia najua wengi mnangojea jwabau la ombi la kaka Kamala kuhusu KUHARISHA.

Sasa namboa kuongea na dada Asimwe. Nimejaribu kutafakari kwa kina na kuhoji maoni ya dada yetu Asimwe kwa nduguye Koero. Nimemwandikia kuhusu msimamo wangu kuhusu VUKANI VUIKANI VUKANI VUKANI VUKANI VUKANI yetu (msisitizo). Naongea na wewe Asimwe kuwa BLOGU hatua nyingine baada ya kumiliki barua pepe, ndani ya blogu unaweza kujenga CNN,BBC,TBC,ITV yako bila kuulizwa na yoyote.

Nikupe siri hii kuwa katika uchaguzi wa Kenya kuvuja kwa matokea ya udanganyifu yalifanyika kupitia blogu, nakwambia blogu siyo upepo wa kupita kwani hatua ya juu zaidi kuliko magazeti ambayo unasoma kila leo. Magazeti ambayo Wahariri na matumbo yao makubwa kama wamemeza vifaru au wanabeba mizgo mithiri ya Guta wanajidai kukalia kiti cha kukulazimisha kile usichotaka kukifanya ili ufanye.

Katika blogu za Kenyan Unlimited ndizo zilimwumbua Kibaki na wizi wa kura nchini Kenya, pia kwa kipenzi changu Mugabe aliumbuliwa na Blgu lakini siyo hayo tu, nenda pale afrika kusini kuna mtoto wa mika 13 anamiliki blogu yake anafanya kile anachokipenda yaani kuchangamsha akili.
Rais Bingu wa Mutharika ana blogu yake ambayo inawapasha watu habri mbalimbali achana na hawa wavivu wa kufikiri wa bongo wanaodhani kuvaa suti na kusme amimi kiongozi ni mwisho.
Blogu inaweza kukufanya uwe mhariri mkuu, mwandishi au mwandishi kuwa msomaji.

Kutaka kuandika habari za urembo yaani zile chupi za kamba, suruwali, pedopusha, sidiria jeans, kucha za bandia, wanja lipustiki, na mengine mengi. Lakini kumbuka VUKANI linamaanisha nini jamaniiiii dada ASIMWE? Nakuomba sana tena sana, fikiria upya na tunakukaribisha katika uliwmengu wa blogu tena uje na blogu ya UREMBO lakini VUKANI tuachie vilevile.

Kujitolea ni jambo muhimu sana kwani binafsi sikujua kama biblia ilikoewa mara tatu kama siyo VUKANI. Kumbuka Italia watu wanaandikisha uridhi wa mali kwa mbwa,paka n,k lakini kwetu hakuna kitu kama hicho. Jaribu kutusaidia na kutusamehe sana hata kama Koero anashepu kama Miriam Odemba au macho kama Asia alcohlic kama Sista V, au akiwa gizani anang'ara.

IDUMU VUKANI

2009-03-06

Uzuri, Urembo au?


Nikiwa napitia habari za mtandaoni, kwa fundo la hasira kuona majitu toka afrika maghribi yanataka kuniibia kweupe, lakini yote tisa - kumi Mrembo huyu alikikuna kinoma yaani hadi sijisikii kuwasha tena. Nimependa sana urembo wake ingawa najua unahitaji uvumilivu

2009-03-03

Penzi, Mapenzi na Thamani ya Mtu

Unajua au umewahi kunisikia napenda, napendwa au nataka kupenda? Daima nashangazwa na mwelekeo wa upande mmoja. Mara nyingi utaona iwapo Mwanaume anamtongoza mwanamke, kuna vitu vinamwongoza hadi kufikia hatua hiyo. Inaweza kuwa tamaa yaani anahamu ya kualala na mwanamke ( kuchungulia UVUNGUNI). Usishangae jina la Uvunguni maana ndiyo maneno ya waungwana na mabadiliko ya tafsiri kwamba ni UVUNGUNI kati ya mwanamke na mwanaume wanapofanya kile wanachoona kitamu zaidi wakiwa SIRINI.

Jambo linalonishangaza ni hulka za wanawake kudai kwamba kuna wanaume wanaotongoza ili kuwachezea wanawake au kuna wanaume wanaotongoza kwa nia ya kuwachezea. Sijui undani wake lakini si haba mambo haya kusikia. Utasikia 'unanipenda kweli au unataka kunichezea tu? Lakini ukitafsiri dhana ya kuchezea ni pana kwani hakuna asiyemchezea mwenzake kwa namna yeyote ile hasa suala la mapenzi.
Wapo watu wanaona kwamba dhana ya kuchezea ni upofu tena nikiwamo mimi. Suala la kutongozwa halafu unasema anataka kukuchezea, kwani wewe humchezei mtu hata kama unaye katika uhusiano wa mapenzi?

Unaweza kubeza lakini najiuliza kwanini wanawake wanajiona wanathamani kuliko wanaume katika suala la kutongoza au kutongozwa? kwanini wanasema wanaume wanataka kuwachezea na siyo kudumu nao mapenzini? Kwani hakuna asiyemchezea mwenzake? Utona kwamba baadhi ya wanawake wanasema kabisa 'Mi nimechoka bwana, yaani unataka kunichezea hadi niweje?" Hili tunaweza kusema kwa wale ambao tayari wanachungulaina uvunguni.

Lakini kwa wale ambao wanatakana, wanahitajiana, wanataka kuanzana, yaani wanatongozana huku wengine hasa wanawake wakichukua muda mrefu kukubali ombi la kutongozwa. Hivi dhana ya kumchezea mwanamke ilianzaje, tulifikaje hapo? Kuchezewa nini hasa ambacho kina thamani kuliko utu wetu? Nini thamani ya penzi au mapenzi? Na nini kinachokamilisha mapenzi? Wengine mtasema SIYO LAZIMA TO DO? lakini ukiona watu wanajifanya hawapendi kuchunguliana uvunguni eti siyo lazima, waulize siku watakayofanya kuna jambo jipya litakalo kuwa nje ya PENZI au Mapenzi? Kwanini wanawake wanajipa thamani sana katika mwili wao hasa suala la mapenzi? KAZI MNAYO WAUNGWANA, JIULIZENI.

2009-03-02

Nakumbuka Mengi sana

Nayakumbuka mengi niliyoyaona na kuishi. Nakumbuka enzi zile kuvaa kandambili tu bonge la utajiri. Nakumbuka mbali kwa kweli, nakumbuka bibi akiwa mfinyanga vyungu. Nakumbuka kwakuwa wazazi wangu walikuwa na ahueni ya maisha basi hali hii niliepuka kidogo sana. Na kwakuwa kila jambo lifanyikalo lilionekana basi kila mtu anajua kwanini nina uchungu pia na msimamo mkali. Weka mapenzi kando, nipe hoja msingi! Ni wangapi mtanipenda nikiwa sina SHILINGI?????

Nikumbuka sana maisha yale, kuvaa viatu tu tulichukiwa eti watoto wa matajiri, lakini nikiangalia hali nyumbani eti kwakuwa nilikuwa na viti vizuri kama vya ofisini. Nakumbuka niliwahi kupigwa kwa kuitwa :najivuna" kwa hali yetu nyumbani, lakini nakumbuka tulikuwa tunakunywa chai isiyo na sukari tena kwa mihogo jamani.
Nikikumbuka muundo ule ndiyo maana wazazi wangu walipiga sana kelele hoja yangu ya kutaka kucheza soka tu bila kusoma shule. Nakumbuka baba yangu anaposema 'huna kitu hapa nyumbani, tafuteni vyenu kwani hivi ni vyangu na mke wangu"

Nakumbuka sana, yaani unaona wengi wanakuchukia sababu wewe kwenu kuna wageni wanakuja toka mbali, au kwavile ndugu zako wanasoma mahali. Jamani, mazingira yangu yananikumbusha na kunitoa machozi, yananifanya nione hakuna ninayeweza kumwamini kama siyo mimi ingawa wakati mwingine simwamini hata mimi mwenyewe..
Lakini leo najua wapi nilipotoka, wapi nilipoanzia na wapi niliposimama kabla ya kutembea na vidole katika blogu tena kabla ya kugeuka mtundu wa teknolojia niliyojifunza kupitia maandishi kama hadithi ya sungura na fisi. Nisije nikalia zaidi, najua wenzangu hawa wanaweza wakasema mbona umepata nafuu, tuokoe na nasi. NAWAPENDA SANA, SIJAIONA KESHO!!!!

2009-02-27

Markus Honorius VS Markus Mpangala (II)

Naam katika kujua Markus Honorius na Markus Mpangala ni nani, watu wangu hamjakosea, wala hamkwenda upogo, ni kweli, ni yuleyule mtu mmoja katika maisha ya aina mbili tofauti.
Nadhani kwa wale wanaojua kuwa ni mtu mmoja basi wanablogu nawapenda sana na ndiyo maana naona ni kama moyo wangu, nawajali kuliko chochote. Tupo pamoja kama samaki na maji. au kula mihogo na na wanyasa.


Kila ninpotafakari maisha ya Markus Honorius nakuta vioja lakini ukimtaja Markus Mpangala wanablogu wanafurahi kwa raha kwani wanajua sisi ni ndugu kwa shida na raha tumekuwa familia moja.
Katika kutaka kutoa maelezo kwanini najiuliza swali, bado sijui nijibu nini lakini wanautambuzi wanaelewa najaribu kufanya nini.


Kila dakika namwona Markus Mpangala anaishi kwa raha sana lakini nikimtazama Markus Honorius ametawaliwa na mambo ya ajabu, ingawa ni mtu mmoja katika mwili mmoja. Inaweza kuwa kama unaishi mbingu nyingine, yenye vioja na shubiri lakini vyote ni mali ya mwandamu. Unapoona mwili mmoja unakusudia kufanya mambo mawili, basi unahitaji kutafakari, unahitaji kujiuliza wewe ni nani?


Wewe ni nani katika ulimwengu mmoja? Wewe ni nani hasa hadi ukawa kama ulivyo? Hivi unatafakari kuwa kwanini umefanya jambo fulani, umejiuliza kuwa umefanya kama nani? Unajua wewe ni nani hadi ukafanya hayo? Unaweza kufikiri kwa kina, unaweza kufikiri vizuri lakini uzuri wa kufikiri usidhani ni lazima ufikiri mazuri! Usidhani kuwa kila MAARIFA lazima yawe na matokeo mazuri! Jaribu kujihoji, lakini usizidishe usije ukawa kituko, lakini jiulize unapohitaji MAARIFA ni lazima yawe mazuri au hujui kuwa MAARIFA mengine ni mabaya?


Labda Markus Honorius anaishi kwa njia ya bandia, siyo uhalisi wake au ndiyo maana wengine wanasema yupo kama shushushu, lakini wengine wanajua ni mwenye AIBU, MWOGA, MKIMYA lakini lazima analo jambo linalomfanya awe hivyo. Ukija kwa Markus Mpangala utaona anaishi kwa uhuru sana, tena wengi wanamfurahia akiwa katika blogu, anakutana wanablogu mbalimbali, ndani ya nchi na nje ya nchi, ameingia kupitia blogu hadi Brazil halafu akapokea wageni toka huko ulaya magharibi lakini maisha yake ni tofauti na Markus Honorius.


Acha kuwaza sana lakini huyu ni mtu mmoja mwenye maisha ya aina mbili. Sijui watu wanadhani ukiwaza sana ni lazima unaficha kitu, au ukiwa na mwonekano wa wema hutendi mabaya, au kama huongozani na wanawake si mpenda ngono au huna ashki. Pengine mali yako haifanyi kazi ndiyo maana uko mbali nao! Kumbe!!! kuwa karibu na wanawake ni sawa na kuwa karibu na wanaume tu, unaweza kuwa na marafiki sawaswa kwa kila jinsia. Kwani "hii kitu iliumbwa ya nini".

Heeee aise jamaa vipi, aaah watu vipi "USIIBE KABLA GIZA HALIJAINGIA".
NB; ngoja nikamsikilize Mpwa wangu EMINEM anasema "CRACK A BOTTLE" ni mpya hiyo: soma mistari yake

"Look, if you had one shot or one opportunity. To seize everything you ever wanted. One moment would you capture it or just let it slip"?????

2009-02-25

Markus Honorius VS Markus Mpangala

Usipojiuliza hawa watu wawili ni nani, basi jiulize wewe ni nani. Kma hujui huyu ni nani, basi jiulize hawa ni nani.
Lakini kama kombea la chuma linapata kutu basi nami kama binadamu naweza kufa au kukosea, pengine makosa ya wengine sipendi kuyasema, ndiyo maana unakufa na siri moyoni. Labada siri hiyo inaua familia za wen. Lakini aliye hai ni yule anayeongea kwa jashooooo halafu anakupa mistariya upendo. Pengine ukimya ni silaha ya kuficha maovu au labda umaarufu ni silaha ya kufunua maovu.
Labda wale wasotenda mambo hawakuzaliwa katika mambo. Na wasiofanya mambo basi ni wale wanaokalia kuti kavu huku wakifichiwa jambo. Labda mimi ni kati ya wale wasioju MARKU HONORIUS ni nani na MARKUS MPANGALA ni nani?
Yawezeakana kabisa huelewi lakini inawezeakana hujui maana ya kuwindwa kama sungura, lakini hata yeye sungura hushindw kumzidi kete mbwa.

Ni maisha ya MARKUS HONORIUS au MARKUS MPANGALA? Hapo ndipo lilipo swali, lilipo jambo la kutafakari au labda ni kama mwehu kutoka nyasa.
Na chazaidi kumbe wapole ni wenye visa na visirani kama mavi ya asubuhi na mengine nayo yameoprodheshwa katika sehemu mbalimbali.
Huyu ni mtu tofauti?

2009-02-21

TANGAZO: mambo ya A -TOWN

I would like to introduce to you the "VUNGA" wear.The product line:You may order a 'VUNGA' logo engrossed in different Tops and Tee Shirt colors. So far the colors available are, Blue, Black, White, Red, Green, Gray, Khakhi and White hoods for ladies.Availability and ordering:
Products are readily available in Arusha, Moshi, Dar and Mwanza (Tanzania).For prices and placing orders, please contact VUNGA products at : vungaa@gmail.com or call +255715268400
/ +255784893289In their own words:
...vunga'


simply means take it easy/chill or dont stress. This is a purposeful message to
the young generation! Unajua vipi eeh, siku hizi watoto hawajatuliatulia. Yaani
wasichana wa shule wadogo sana wanakimbilia madingi watu wazima kisa hela na pia
masela kujirusha 24/7 bila mpango - hiyo HAIFAI. Kwa mwendo huu mshikaji
utajikuta kwenye madawa ya kulevya, bangi na mambo kama hayo, ...kwa hiyo
"vunga" ni neno la mtaani A-Town linakupa "Tulia! (acha papara)"!



The founders.
VUNGA is a product of these entrepreneurs:
Ismail Lossini
Eddie Dan
Henry Minja/DX (Producer of The Noizmekah Productions)
Banx Minja
Benjamin (was in the MTV VJ search finals)

2009-02-20

Kikwete acha kupiga Mayowe


Nimetulia wala sijaandika maoni yangu kuhusu ujio wa Hu Jintao wa China. Nimtumiwa sms nyingi na waraka pepe kwamba ninaonaje ujio huo na kauli zako kuhusu Mkapa. Wengi wanadhani nimebadilika kimtazamo kwani kuna mambo siyajadili,sipendekezi au kuongoza njia.BADO NIPO SANA!
Wapo wanaolalamika kwamba nimeacha kujadili mada zangu za kuhusu bara la afrika, wanadai ninapwaya katika mada za nyumbani bongo. Lakini nasema kuna mambo yanaingiliana, kwasasa nakula darasa kali sana kuhusu mashariki ya kati na yanayowahusu, pia na shughuli zangu za maisha.
Sasa ninaandika hapa kama mwanzo tu kwani natarajia kuandika wazi zaidi. Sikubaliani na mtazamo au porojo za Rais Kikwete kwamba uwanja taifa ni juhudi za Mkapa na uzuri wake. Mimi nasema ni juhudi za watanzania, kwani hakubuni bali aliahidi kwasababu ni wajibu wake kuteda hivyo.
Sasa basi kutwambia kwamba hayo ni mazuri yake ni kutulazimika kunya mavi jamvini huku msosi upo tayari kwa kuliwa. Sikubali kwamba mambo machafu ayaliyoyatenda eti yamekuwa mazuri na kupakwa rangi au marumaru. Kwanza nitakumbusha BOT ujenzi wake.
Bodi ya wahandisi nakumbuka ilifanya tathmini na kusema kwamba ni bilioni 56 zingtosha kujenga BOT tena bila msaada wa nchi yeyote, lakini uwongo ukatungwa halafu tukaambiwa BOT imejengwa kwa milioni 700 huku mjenzi wake alitaka milioni 70. Je nini kilichofanywa hadi ikapandishwa bei kiasi hicho? Au unadhani uzuri wa mtu husemwa tu kama ufanywavyo wewe?
Huo uwanja wa soka nani amekwambia Watanzania hawajui uzuri wa mtu? Watakula uwanja na kunya uwanja? Ingawa kwa wapenda soka tunafurahi, lakini nguvu ya kushangilia tutoe wapi? Ni kweli kulikuwa na umuhimu wa kumpamba tena Benjamini? kwa sababu naamini ni jukumu lake na tulimtuma kufanya kazi kwa ajili yetu full stop! Sasa unapopiga mayowe eti jamaniiii mkapaaaa alijenga uwanja huuuuuuuu.
Nini thamani ya mgodi wa Kiwira ambao ulikuwa na Milioni 700 halafu wakijiuzia na Yona Milioni 70? Au unadhani kila mtu kipofu, haoni anakubali kuchekewa na kulishwa porojo kama zile ulizozitoa uwanja wa taifa. Unafikiri wenye kiona mbali tunajali kwamba eti Hu Jintao alikuja kuzindua uwanja? thubutu labda wajinga wajinga watachekelea mpaka kupasuka misamba ya midomo halafu wasijipe muda wa kufanya tafakuri.
Kwani nani hajui mashtaka mengi yaliyopo ni porojo na ngebe za uchaguzi? Unafikiri tunafundishwa uzuri wa mtu kwa hotuba au matamko? Sikiliza wahenga walisema 'mtoto acha kupiga mayowe, acha watu waone wenyewe'
'usiseme sana kwani tusiposema hatumaanishi hatuna ila tunakutazama tu ili tujue umahiri wako wa kuchanganua hoja.
Amka, hujasikia kama ni kizazi cha dhahabu cha Nyerere kinakuja, hujui. Zubaa uchekwe. Nitajadili zaidi nje ya blogu.

2009-02-18

Tunaweza kuishi bila Penzi au Mapenzi?

Tuishivyo ndivyo tufanyavyo. Na kama tufanyavyo ndivyo tuishivyo basi tunaweza kuangalia mwenendo wa maisha yenyewe. Sina hakika kama kuna tofauti kati ya PENZI na MAPENZI, maana inaweza kuwa kinyume kinyume halafu nikapotosha maana. Unampenda mtu, una hamu naye, roho yako inapwita,inahamanika,inachezhceza lizombi.

Sijui unajichukuliaje unampenda mtu fulani, au unataka penzi la fulani maana wapo wasemao nataka penzi lako bilakujiuliza kama umwambiaye naye anahitaji penzi lako au la! Unaweza kuhitaji penzinla fulani lakini kwa tafsiri ya haraka penzi ni ngono na kupeana utamu uupedwao. Lakini wapo wanaosema au kulalamika katika ndoa zao kwamba hawatosheki. Lakini ukiuliza hawatosheni nini wanasema PENZI bila kutoa ufafanuzi kwamba penzi wasilotosheka ni ngono au nini.

Inawezekana ukawa mmoja wapo kwamba ukasema mpenzi mbona leo umechemsha au umemaliza mapema? Lakini kila siku unalilia penzi ambalo unasema ni tofauti na mapenzi. Sijui inawezekana kuwa tofauti lakini HAMU ya kutaka penzi la mwenzako inatokana na nini? Na kama kweli utamu wa penzi ni ndoa, inakuwaje wengine wanarejea penzi lao la kwanza eti wamekumbuka UTAMU wa kale mavi ya kale hayanuki.

Kwanini uingie kwenye ndoa halafu usijiulize ndoa ni nini? Ikiwa utamu wa penzi ni ndoa na wale wanaoshikana mikono kwa raha na kuambatana kila leo kama kumbikumbi na kusema MAPENZI matamu au Penzi ni tamu wanapata wapi utamu ambao siyo halali hadi uhalalishwe kanisani na msiikitini eti sasa mnaweza kufaidi PENZI mtakavyo, kwani awali hamkufaidi mtakavyo na kujua utamu wa Mpenzio upo mahali gani au ukimtyekenya shemu fulani inampagawisha na kuelgea kama mlenda wa BAMIA?

Utakuta tunaweza kupenda kupendwa na kutamani au kunogea kufanya PENZI ambalo siyo tendo la ndoa mpaka lihalalishwe na wawakilishi wa imani. Ni imani gani unajua kama mpenzi wako ni bomba sana kwani PENZI akupalo ni lile litokalo Ghana au Nigeria? Inawezekana utamu huu ni sawa kama ule wa mnyasa na yule demu mkanada awawzaye umasikini wa waafrika. Je kwanini wengine wanataka penzi la dada zao na kaka zao au binamu nyama ya HAMU?

Jibu la Kitendawili, na pole kwa Yasinta

Wanazuoni, wapo hoi,wameomba jawabu limekuwa thawabu,hawanalo,wanataka ahueni lakini tuweke tu AFANALEKI ili tupaje jibu lake.
Pengine hongera SARA kwa kujaribu kuwa MANII ni jibu lako, lakini nilikupamaswali kadhaa ambayo unaweza kunipatia jibu la kitendawili changu. Jamani eeeeh hivi kweli mmeshindwa au mnanitega?
JIBU; nimehangaika na kitendawili hiki tangu mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka 2008, nilipewa,nikashindwa kisha nikajua hakuna shemu ya kusemea tena kama Blogu zetu maana kuna kila wajuzi wa mambo mbalimbali yatuhusuyo kila leo. LAKINI binafsi sina JAWABU ndiyo maana niliweka hapa ili tusaidiane, na kwahakika mwenye jibu atusaidie.

Kuhusu Yasinta, pole sana rafiki yangu, najua ni mabadiliko ya mazingira ndiyo maana imekuwa hivyo. Ninakuombea zaidi kwani nimevumilia kutoandika hapa, lakini naona lazima wanablogu wenzetu wajue kuwa unaumwa, toka uje bongo ni homa na afya kidogo kuzorota. Lakini naamini unaweza kubadilika, unaweza kurejea katika uhalisia wako.

Tupo pamoja,tunakuombea mema,tunangojea Tanzaniaresan irejee hewani kwa moto na makusanyo ya uhakika. Ni mungu pekee anayeuongoza kwa imani lakini miongozo tunayo mikononi mwetu. Ugua Pole Yasinta utarudi kama kawaida na kuwakilisha maofisini mpaka kwenye mageto, afrika na ughaibuni. Na wenye nia tunakuombea
Mnyasa.

2009-02-16

Kitendawili kimewashinda? Karibuni tule basi!

Nilikuwa nangojea waungwana mjitahidi kufunua bongo zenu, nilidhani kwa wanazuoni kama ninyi lazima jawabu lipatikane ..... lakini wapi bwana, maji yamezidi unga..... yaani tatu bila, tatu bila. Haya basi nimekuja na chakula hiki sijui tutashiba maana samaki mmoja, kwahiyo kula ni kula mbaya kukoimba mboga jamani. Karibuni mkekani, mlozowea mezani msahau kwa leo.

2009-02-11

Shindano! KITENDAWILI........

KITENDAWILI........................................., "Ni CHEUPE kama barafu na ni CHEUSI kama giza, KULIWA ni HARAMU na kunywa ni HALALI, kina herufi 5 na kinaanza na herfi M.
Kinatumiwa na WANAWAKE mara moja katika UMRI wao, na kinatumiwa na WANAUME mara tatu kwa siku.
Je, ni kitu gani hicho? Ukipata jawabu lake.

NB: ZAWADI NONO kwa mshindi

Hakuna kulala hapa

Vipi, unaonaje ukijiunga nao! Unaweza kweli mauno ya viuno kama Fifimoto wa Enomizizi au wewe ni laini yaani nyororo! Utaweza wewe mtoto wa geti kali mambo haya? Mtoto umekulia wapi kama siyo ndani kutazama kideo na propaganda za seleka za walami ughaibuni.
Nakumbusha umuhimuwa kunengua mitindo ya kwetu, hakuna kulala aiseh

2009-02-07

Katika kujua Umuhimu wa Kujamba maishani!

Unageuka kushoto, kulia, unangalia waliopo karibu yako, unaona hawakusikii. Unajua nini? Ijumaa nipo pale Upanga, ndani ya chumba tulivu cha kompyuta, natazama pembeni, watu wametulia na kompyuta zap, wameelekeza akili zao. Huku pembeni mwenzao nahaha, nimetahayari, nataka Kujamba. Lakini nawaza hivi kijambo changu kitakuwa na harufu ya nguchiro au?. Nikijamba, mjambo utatoa kiwambo?
Maana hiki chumba kilivyo halafu ukijamba DUH sauti kama mirindimo ya Piano. Je nikijamba, inzi watasogea? Vipi harufu ya mavi itanisonga na kuweka mnato katika suluwali!

Nikikumbuka kutoka nje, basi huko itasambaa zaidi. Fikiria hapo zaidi ya nusu saa hadi tumbo linanguruma kama radi, kijambio kipo hoi taabani kwa kubinya kujamba, kimechoka kujikaza tu.
Nikiachia Fyuuuuuuu! itakuwaje? Bila shaka mkutano wa inzi utajaa, sherehe itakolea, tena shangwe za mavi ya kijambo.
Nawaza, nijambe? Nawaza harufu je? Sauti au kiwambo cha mjambo toka kijambioni itakuwaje? Kumbuka hapo nimetulia tu lakini nahangaika. Cha Ajabu kuna Binti! mmoja muda mwingi anageuka huku na kule kutazama nilipo, anacheka. Anabadili mikao, anabana miguu! Namfahamu! mara namkonyeza, VIPI? anaguna! anasema kwa ishara na kukunja ndita, eti tumbo linanguruma kama radi anataka KUTAPIKA. Akaniambia twende nje! DUH! nikisimama tu nitajamba! Tena naanza vyuuuuuuuuuu! harufu kali! Namfuata yule Binti, tunakwenda nje anachechemea, kashikilia tumbo. KUFIKA NJE ghafla anabana miguu! anapumua oooooohhpsssiiii, kisha anasema.......
"Markus , yaani mwenzio nilitaka kujamba mpaka tumbo limaniumiza, kwahiyo kujambia mle noma aise lakini KAUSHA basiiiii. Nikajibu, mbona hata mimi pia!


NB:Uliyesoma hapa, maneno haya hayana heshima eti au? Lakini unajua umuhimu wa kujamba kweli katika maisha yetu?

2009-02-06

ndiyo maana nakupenda sana

Daima nawaza, nakumbuka enzi za uvuvi bwana,kabla sijajua kubonyeza niandikacho. Mmmmhh Koero aliagiza samaki, akadai anahitaji Kamongo, DUH! Pengine sijui hawa samaki wapo wapi lakini sijui kama ziwa letu lina Kamongo. Mmmhh labda nimesahau mambo yetu. Haya weeeeee tayarisha ugali mimi naandaa mboga, wala usilete kitu tofauti na ugali tena wa muhogo.

Katika kuwaza na kuwazua, ni kama nalamba mchanga gizani halafu sichafuki. Nawaza mengi kila nijionapo, maana najiona mimi kwani yanagusa maeneo niliyokulia.
Niliwaona wengi, nikawaringia kwakuwa nyumbani tunakula ugali kwa uma na visu, nikaringa ati tunakula mezani, halafu tulala mkekani. Hapo sijakwambia kitanda cha Demu wangu mmoja cha Teremka tukaze . Nakumbuka nilivyokuwa kikojozi hadi mama ikawa kila siku makofi, nakumbuka dingi alivyokuwa mkali utadhani mwandamizi wa jeshi la Hitler.
DUH! nakumbuka enzi zile tunakunywa chai (tunaita Chingambu) bila sukari ya Mtibwa, enzi za kula viporo vya ugali wa muhogo na dagaa usiku wa manane halafu tunajiona wajanja. Nakumbuka mengi niwaonapo wenzangu kama hawa, nawaza wakati ule tunalala kwenye mkeka tuliokojolea.
Nakumbuka mama alinipa adhabu ya kulamba sehemu niliyokojolea mkojo, nakumbuka jinsi nilivyokuwa nimebuka vumbi sababu ya soka langu. DUH! niwaonapo hawa najiona mimi, japo kwangu afadhali vipi wale wakuangalio kama hawa? Nakumbuka mengi sana sana sana sana nashindwa kunena zaidi EEH! Mola tuonyeshe Nuru

2009-02-05

sijui vipi, kwani wewe unaonaje hapo?


He we! mbona?
Mimi sijui wanafanya nini kwani macho yamegota,yamefunga,sijui yaonacho. Haya unaona vizuri ebu rudia tena! DUH!

2009-02-04

Rahaaaa sanaaaaa

Sijui labda unatupenda ila husemi.

Pengine unaweza kutuambia lolote, unaweza kutafsiri chochote lakini sisi ni kama wewe, tupo pamoja nawe daima! Vipi unawaza nini utuonapo, au kuna lolote unajifunza? Tulia mwenzetu ule kwa raha, usafiri kwa raha wala usitie shaka, kwani ile gari yako unaweka mafuta lita ngapi na kwa shilingi ngapi?
Maana hapa tunakula kwa dola moja siku nzima. Si unaijui BUKU au elfu moja, wenzio tunatumia kwa siku mpaka inabaki kwaajili ya kesho, siku ambayo tutaongezea nyingine ili itimie kama ile. Tunafurahi, tunaridhia maisha yetu, wala hatutaki kukaa eneo lenye maandishi '"mbwa wakali" au "eneo hili linalindwa kwa mitambo maalumu".
Wala kwetu hatuna walinzi tuwalipao kwa miezi 12. Pengine unadhani siye wanyonge! unajidanganya, tunauwezo kuliko wewe unavyodhani, tunaweza kutenda na kuenenda kama wewe lakini tumetulia kwa raha na tabasamu utuone kwanza! Vipi unaonaje!

2009-02-03

Ukishiba, msome Richard Wright

Kama utashiba bila mboga au kama imekwisha basi msome Richard Wright maneno yake haya " Hatari inayoukabili ulimwengu wa leo ni kusahau kile kiainishacho ubinadamu wetu. Maana halisi ya mahusiano, maana halisi ya mapenzi, hata ile heshima na hadhi ya maisha ya binadamu inaelekea kusahaulika. Kipimo cha utu si utu tena bali mienendo na tabia za kikatili na ufisadi.
Leo hivi mapenzi ni neno lililobadilika maana yake, sasa mapenzi ni uhusiano wa mtu na gari au mali yake.
Neno utu limebadilika kabisa maana yake na kuwa utukufu na ubinadamu ukawa ubwana damu hata damu imekosa thamani ya asili na utakatifu!

wale wasomi wetu vipi,inapendeza eeehee!!!

Vipi waungwana mwadhani nimepotea kilingeni kwangu? Duh1 nipo nipo sana, yaani nipo nipo kama vile ujuavyo nipo1 Lakini sijui unaonaje hii kitu, au nisme unaonaje haya maudhui ya picha. Haya weeeeee!!!

2009-01-30

Nimeibukia wapi? usiwaambie uhamiaji

Duh! nilidhani nikiwa katika linchi la watu nitapata muda wa kutosha, lakini kumbe jamaa kaniandalia ratiba ya kuzurura kama chokoraa??? Yaaani mara huku mara kule.... Halafu jana nilikuwa napekuliwa mpaka nguo za ndani..mmhh hujui chupi wewe au? Unajua nilikuwa nawaza sana mambo ya kuzamia lakini sikujua kama nitakamatwa(natania).
Basi katika mambo ya hapa na pale, nilikuwa kwanza pale Zimba baada ya kutoka kalonga. Mwendo ukiwa umekolea hadi kwa mwenyeji wangu nikaona jamaa limenuna ghafla halafu linaniuliza... ujinga "eti huku hakuna safari lager wala kilimanjaro, kwahiyo nijiandae kunywa pombe zao za Kuchekuche" Nakwambia nilibadilika na kuwa mwekundu ghafla hadi jamaa likashangaa. Kama kuna kitu sitaki nasema sitaki narudia sitaki kukitia mdomoni ni POMBE!
Mmmh samahani. jana wakati narudi nilibishana sana wale jamaa wa uhamiaji eti kwakuwa niliwaachia kitambulisho cha maktaba na kile cha lotto kitita cha akiba!
Nikaa nimejinafasi katika mgahawa mmoja hivi ili kutumia huu mtandao, eti jamaa wanakuja na kusema oyaa MTZ mbona unanunanuna? Nikaona wanasengenya kinyanja wakidhani sijui! Nakwambia nilipayuka kwa lugha hiyohiyo halafu wakaomba msamaha, duh!
Ngoja kuna jamaa hapa kando linachungulia lugha ya kiswahili, linanicheki toka nyayoni mpaka kwenye bichwa langu. Nimeliuliza we jamaa vipi? tena kwa lugha yao,limeshangaa na kuchekacheka.
Mmmh leo narudi tena kwa uhamiaji kuchukua vitambulisho vyangu vya Lotto na maktaba, aiseh asikwambie mtu, waafrika hatupendani wakati mwingine duh!
Ngoja mwenyeji wangu Mark Wood na Sonny Banda wananiangalia pia niandikacho, huku nimekunja uso kama nimekula pilipili. Eti jana walinipelaka kunywa kuchekuche na nyama choma. Sitaki kusikia kulewa hapa! Kwaheri kwanza!
wakati naendelea kuandika kuna toto la Kitasha limeingia lipo pembeni hapa, Duh! Toto limeiva limefunga kanga kama wabongo. Halafu linachungulia, nimelikonyeza kijicho, likaachia meno 32 nje, hiyo ndiyo salamu bwana. Mmmmmh ebu mcheki yupoje? Aiseh mmmmhh na BARIDI ya Mbeya nikikumbuka??????? halafu linaandika kwa spidi kali sana.

2009-01-26

Baridi sana, Nipo Mbeya

Duh! Hii hali bwana we acha tu! Nipo Mbeya jamani, mapumziko ya siku saba hivi lakini naamini kila kitu kinakwenda kama ninavyopanga na ninavyotaka bila kujali ni namna gani nakarahishwa na hii hali. Baridi inanikamata halafu hakuna hata chembe ya faraja, duh! labda kama alivyonipatia wimbo Keoro kuwa niskilize wimbo wa Ziggy Marley.
Jana nilikuwa njiani kuja hapa, mvua, kumbukumbu za maisha yangu ya shule, mitikasi na vioja vya hapa na pale. Mji umekuwa na mabadiliko ambayo naamini kama jiji limepiga hatua kiasi fulani tofauti na mwenendo wa maeneno ya Dar kwenu.
Vipi wanablogu mnaonaje kadiri siku ziendavyo mnafikiria nini kuhusu blogu. Najua wapo wajuaji wa blogu na wale wajuao mchanganuo wa hoja, huku wakipendacho kiwepo ndicho wafanyacho kwakuwa wanajua wafumbacho ni huishia ubongoni mwao! Aiseh!
Tafadhali usiwaaambie uhamiaji kama kesho naingia zangu Malawi kwanza kwa rafiki yangu. Duh! Hii inakuwa ngumu sijui lakini uhamiaji usiwaambie kwani nina kitambulisho cha maktaba tu sina kitu kingine.
Haya, lakini bado nawaza mambo ya mlimani akili imekufa ganzi. Kwaheri kwa leo jamani ila usiwaambie uhamiaji kama kesho navizia kuingia Kalonga kisha ndani ya nchi kabisa.
Pamoja daima! Baridi sana, mapumziko safi-nasonga kwa wajomba unyanjani.

2009-01-24

ndiyo kazi zetu, ndiyo utamduni wetu

Hii nayo ni kama vile ujuavyo kula na kulala au kupenda na kupendwa. Pengine unajua kuwa tunajua haya mambo. Jamani sijui unawaza nini, au mimi ndiyo nawaza nini. Sijui labda UA alangu, thubutu mmhh pengine. Lakini Koero aliuliza kuhusu picha fulani kuhusu mimi. Eti hii nayo vipi, kweli mimi nipo au? Sijui, lakini haya ndiyo maisha yetu tunatafuta shibe, furaha na pumziko. karibu sana.

2009-01-23

Asante Mkodo Kitururu

Nikiwa mawazoni, huku na kule, mara hapa na pale jamani kichwa chaniuma. Mnyasa nitakuwa safarini kidogo, nikapumzike sehemu zenye baridi. Siyo siri kaka Simon Mkodo Kitururu falsafa zake zanipa matumaini na ukweli wa maisha. Najua kuwa na akiba ya ya maumivu ni nzuri sana kwani ipo siku utalipiwa nayo.
Katika kuwaza na kuwazua, nikakumbuka Koero Mkundi na maoni yake kuwa maua yapo mtaa wa Samora, lakini alijua kuwa naugulia UA langu halipo tena nami. Najua kaka Mkodo kasema unaweza kutokea kwa mlango wa mwingine, mwenzenu nilijua haya mambo binafsi lakini naona bora kusema tu ili nipewa mafunzo. Nakumbuka niliususa mlango wa Canada, nikauvunjilia mbali kwa mikogo, nikasema mahaba ya kitasha basi, eti sasa duuuuh majonzi na kilio tu, inakuwaje?.

SASA hakika najua wanablogu tuko pamoja kama samaki na maji, mizizi na ardhi. Nashukuru mafunzo uliyonipa kaka Mkodo Kitururu, ingawa Koero alikuwa mwoga (anaficha nini?), kaka Fadhy Mtanga asante kwa shairi linipalo "Johari ya Matumaini" kama kitabu cha Barack Obama.
ASANTE kaka kwa Akiba ya Maumivu, nimeielewa mkuu, na hata ile ya Penzi la Pua na Kamasi, ni kweli kumpengesha mtu kamasi za penzi nako kunahitaji uwiano lakini uwiano huo hata kama unamizani za tufani,lazima lifike pwani. Naacha kwanza nimechoka kidogo ndiyo maana najipa likizo naenda mkoa wenye baridi ukanipe nguvu za ziada.
Dada Koero naomba unichagulie wimbo basi nijipumzishe kwa raha.

2009-01-22

tunaweza, ndiyo mapenzi yetu


hapa hakuna kuremba wala kuleta utata. Vipi unatuonaje tulivyo? Tunafanana na wengie au siyo, lakini kweli si unajua maisha ni tofauti au? poa basi angalia sana tena mpaka picha itoboke halafu nipe jawabu

2009-01-21

nimepoteza ua langu,nalia

Nimepoteza UA nilipendalo, nilisudulo daima. Nimepoteza UA langu kipenzi cha MOYO wangu, upepo wenye nguvu umenipora, wenye harara wamechukua kwa madai nilishindwa kulipenda UA na kulitunza. Najua nalipenda UA langu tena sina mfanowe lakini najuta mimi mwana wa nyasa, mhafidhina, Mnyasa aishie maisha ya kizamani, fikra za kale. Si wajua mahaba ya sasa, uwe kama kumbikumbi, UA langu nalia niwazapo nakonda, sijui nifanye nini waungwana nipeni pole, nishikeni mkono, nitaanguka.

Najua nalia, najua naumia, najua nakonda, najua chakula kibaya kwangu na mwili wangu watetereka, nahojiwa maswali, muungwana kulikoni? Mbona uso umejaa soni kama siyo huzuni? Najuta sana mimi, nalia sana mimi, najua ukimya wangu na mwenendo wangu hauna faida kwa maisha ya kisasa. Kweli nina kasoro zitajwazo, kweli najua ninazo lakini UA langu lijualo limepotea, UA lijualo udhaifu wangu limekwenda mbali nami kwa yule nimjuaye.

Ua langu lijualo kasoro hizo limekwenda ughaibuni, wengine wenye vipawa vya kuonjesha asali za huba wamenyakua bila suluba kwa tiketi ya mateso ili waepukane na maumivu. UA langu linaondoka leo ni siku ya pili, nakiri nilibaini kitambo ila ukimya kwangu silaha, nilijipa moyo licha ya kujua nimebaini. UA langu limetoweka, moyoni nasononeka.

Kwa hali hii, binadamu gani asoweza kurutubisha UA lake alipendalo? Kwanini ujualo ni kosa usilipatie tiba ikiwa yawezekana? Tiba ni kupeperuka, kuniswaga kondeni kwa mafarisayo na wayahudi waua wenzao? Tiba ya kidonda ni kukata mguu au kutibu kidonda, Aaaaaah nakumbuka maeneo ya wahenga, walotujuza kale kwamba ISHI kwaajili yako, furahia maisha yako. UA langu linanipa furaha lakini leo napata simanzi, sioni raha, najua sababu lakini kinywa kinapiga KITE wala AFANALEKI sizihitaji bali nataka UA langu, kikohozi changu. SWALI: Ukiwa na kidonda mguuni unakata MGUU au unatibu kidonda?

Ooooooooooohhhh UA langu limeponyoka, limekwenda mbali limechukuliwa na wenye uwezo wa kushaini HUBA, wenye vipawa vya HAMU. masikini mimi, nalia mwenyewe sina msaidizi UA langu limetoweka. Ukijua una homa, unafanyaje? Utajiua kwakuwa hutaki homa au utapata TIBA? Nakulilia UA langu, rudi kwangu, rudi nyumbani!
Natulia kidogo na wimbo wa IT'S NOT EASY

Jamani ile makala ya 'DINI INAPOTUMIWA KAMA KITEGA UCHUMI' imetoka jana jumanne januari 20./2009 katika gazeti la TAZAMA Tanzania

2009-01-19

naona upo karibu yangu

upo karibu au mbali, umewahi kufanya haya tufanyayo? Si mengine ni kuvua tu samaki na kuoposha vindongo hapa nyasa. Karibu nyasa, uwe nasi daima, unatuonaje sasa