Showing posts with label uhai. Show all posts
Showing posts with label uhai. Show all posts
March 22, 2018
MRADI WA MITI KIJIJI CHA LUNDU
March 05, 2018
MAMBO 10 USIYOYAJUA KUHUSU BUSTANI YA MUNGU- HIFADHI YA KITULO.
1.Hifadhi ya Taifa Kitulo ndiyo
eneo pekee Tanzania lenye ndege aina ya tandawala machaka (Denhams Bustard)
wenye uwezo wa kuruka kutoka bara moja hadi jingine.
2.Hifadhi hiyo inayopita katika
mikoa ya Mbeya na Njombe ilitangazwa rasmi kuwa hifadhi ya Taifa mwaka 2005
ikijumuisha sehemu ya eneo la shamba la mifugo, msitu wa Livingstone na bonde
la Numbi.
3.Kitulo ina ukubwa wa kilometa
za mraba 442. Awali ilijulikana kama Elton Plateau baada ya Mvumbuzi Fredirick
Elton kupita eneo hilo mwaka 1870. Mwaka 1960 Shirika la Chakula na Kilimo
(FAO) lilichukua eneo hilo kwa ajili ya ukulima wa ngano na ufugaji wa kondoo.
4. Ndege aina ya tandawili
machaka hawapatikani sehemu nyingine yoyote hapa Tanzania zaidi ya Kitulo.
5.hifadhi hiyo ndiyo eneo pekee
ambalo ndege hao hutaga mayai na kuzaliana kwa wingi kabla ya kusafiri kwenda
mabara mengine.
October 16, 2017
CHUO CHAANZISHA SHAHADA YA WADUDU
NAIROBI, KENYA
KITUO cha Elimu na Utafiti kinachofadhiliwa na Benki ya Dunia kimeasisiwa katika Chuo Kikuu cha
Sayansi na Teknolojia cha Jaramogo Oginga Odinga na kinasubiri ruhusa ya
kuanzishwa kwa programu za Uzamifu na Uzamili kuhusu wadudu wanaoweza kuliwa.
Taasisi hiyo inapania kubuni njia za kuzalisha wadudu hao
kwa wingi bila ya kuharibu mazingira ili kukidhi utashi mara baada ya wazo hilo
likifanywa kuwa biashara.Wadudu wanaoliwa sana maeneo ya Magharibi mwa Kenya, ambao
wana wingi wa madini ya protini na Zinki watafanywa kuwa biashara ili
kuimarisha uwepo wa chakula cha kutosha, na kuondoa dhana mbaya katika kula
wadudu.
Madhumuni
habari,
Mafanikio,
maisha,
Sayansi na Teknolojia,
Teknolojia,
uhai,
Utafiti,
utulivu,
Vitabu
December 20, 2013
UTENGENEZAJI WA POMBE YA WANZUKI "VIPOROMBA" NYASA
Kwasasa pombe ya Wanzuki inazalishwa kwa wingi na akina mama pamoja na mabint wengi huku Nyasa. Vijana wanalewa asubuh asubuh kwa bei Rahisi sana. Pombe hii hutengenezwa kama Chai isipokuwa ongezeko la hamira.
ILA NAPATA MASHAKA NA NAMNA POMBE hiyo inavyotengenezwa
kwani mazingira yake. Vitambaa vya kuchujia havifai na makopo yake hayaoshwi. SAWA
NI AJIRA, ila sijui wewe Mnyasa mwenzangu una maoni gani?
Utengenezaji wa pombe aina ya Wanzuki
Pombe aina ya Wanzuki ikiwa imekamilika na kuwekwa ndani ya chupa
Pombe aina ya Wanzuki ikiwa tayari kuuzwa kwa wateja.
Madhumuni
afya,
kula,
kumbukumbu,
Nyasa,
uhai
Subscribe to:
Posts (Atom)
