Showing posts with label ughaibuni. Show all posts
Showing posts with label ughaibuni. Show all posts

November 23, 2017

FREDDY MACHA ALIVYOLIZUNGUMZIA JUKWAA LA KISWAHILI SOCIETY

NA MARKUS MPANGALA 
SWALI: Naam, shikamoo Mzee Macha?
FREDDY MACHA; Marahaba. Habari zako bwana! uko wapi wewe siku hizi? Maana tangu tuliposalimiana pale Soma Café,Mikocheni na baadaye Nyumba ya Sanaa, Dar es Salaam wakati wa warsha nilizoendesha huko.
SWALI; Nipo hapa Bongo naendelea vema tu. Ni kweli, kitambo hatujawasiliana, pia nilifaidika sana na warsha zako hata hivyo si neno, tutaongea kidogo leo.
Freddy Macha
 FREDDY MACHA; Asante. Nadhani leo unalo la kuongea zaidi. Karibu.
SWALI; Ni kweli, nahitaji mengi kutoka kwako mzee wangu. Kiu yangu ni huu mradi wa Kiswahili Society, kwani umeeleza mahala fulani nikasoma nami nimevutiwa ili niwaarifu wasomaji. Je mradi huu ulianza lini na wapi?
FREDDY MACHA; Umeanzishwa na wanafunzi na Wahadhiri wa Kiswahili pale chuo cha lugha cha SOAS (School of Oriental and African Studies) hapa London,Uingereza.
SWALI: Nini dhumuni la kuanzishwa kwa Kiswahili Society?
FREDDY MACHA; Kuunganisha Wazungumzaji wa Kiswahili duniani lakini hasa hapa Uingereza.
SWALI: Nashukuru sana. Ndugu Macha, wewe ni Mwanamuziki,Mwanafasihi,na Mwandishi mkongwe. Katika fani hizi kuna mambo mengi umejifunza kutoka bara letu la Afrika,Latin Amerika,Marekani na sasa Ulaya. Unadhani jamii za watu wa Ulaya hususani Uingereza zinaweza kuhamasika kukiendeleza Kiswahili? 

November 04, 2017

VITA YA KUGOMBANIA MAJI DUNIANI INAKUJA



NA MWANDISHI  WETU

SHIRIKA la Afya Duniani(WHO) linabainisha kuwa kuna watu bilioni 1.3 ambao ni moja ya tano ya watu wote duniani wanakosa maji safi na salama ya kunywa. Mwenyekiti wa Baraza la Maji Duniani Loic Fauchon anakiri hivi sasa hali ya upatikanaji wa maji duniani ni mbaya na kwamba watu wengi wanaweza kuangamia kwa kukosa maji safi na salama kutokana na uchafuzi wa vyanzo vya maji unaoendelea duniani kote.

November 03, 2017

UCHAMBUZI WA KITABU: IT CAN'T BE TRUE



KITABU: IT CAN’T BE TRUE
MWANDISHI: JOHN MWAKYUSA
MCHAMBUZI: MARKUS MPANGALA

HII ni mara yangu ya kwanza kusoma riwaya ya mwandishi John R.P. Mwakyusa, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam. Riwaya inaitwa “It Can’t Be True: A Story from Uganda-the Pearl of Africa”, na kuchapishwa kwa mara ya kwanza mwaka 2017 na kampuni ya Partridge Publishing ya India.

October 26, 2017

MWALIKO; WOTE MNAKARIBISHWA KWENYE MJADALA HUU


December 17, 2013

JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI YAANZISHA BARAZA LA AMANI NA USALAMA


KAMPALA, Uganda
 
VIONGOZI wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wametia saini kuanzishwa rasmi Baraza la Usalama la Jumuiya(East African Peace and Security Council) ambalo litashughulikia mambo mbalimbali ya ulinzi na usalama kwa nchi wanachama wa Afrika Mashariki. 

Viongozi hao kutoka Uganda, Tanzania, Kenya, Rwanda na Burundi wamefikia uamuzi huo juzi jumamosi wakati wa mkutano wao uliofanyika mjini hapa. Uamuzi wa kuanzisha Baraza la Usalama la Afrika Mashariki ni kutokana na kitisho cha kusambaa kwa ugaidi kama ambavyo yalivyotokea Dar es salaam(1998), Nairobi(1998 na 2013), na Kampala(2010).

Akizungumza mbele ya viongozi  waliohudhuria katika mkutano Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Richard Sezibera, alisema “Nathibitisha uamuzi uliofikiwa katika mkutano huu kuanzisha Baraza la amani na Usalama kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ikiwa na lengo la kuhakikisha ulinzi na usalama wa eneo hili dhidi ya tishio lolote litakalotokea,” 

Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanakabiliwa na tishio la ugaidi unaofanywa na kundi la Al Shabab ambalo lina uhusiano na Al Qaeda. Kwenye mkutano huo, nchi wanachama wamekubaliana kukabiliana na tishio la ugaidi kwa pamoja ili kuepusha matukio kama yaliyokea mjini Nairobi katika maduka ya Westgate ambapo zaidi ya watu 60 wasio na hatia walifariki dunia na wengine 175 wakiwa majaerhu. 

Mwaka 2010 kundi la Al shabab lilidaiwa kufanya mashambulizi katika jiji la Kampala na kusababisha vifo vya watu 70 baada ya mabomu mawili ya kutegwa ardhi kulipuka.

NDUGU ZANGU WANYASA NAWAPENI CHANGAMOTO



Na Bahati Chiombe, ARUSHA

WAHENGA walisema kuuliza si ujinga na aghalabu aulizaye anataka kujua. Wilaya ya Nyasa ni mpya na bila shaka yoyote inahitaji nguvu za wanyasa wenyewe katika kuleta maendeleo. 

Ningependa kuwauliza vijana wanawake kwa waume mmejiandaa vipi kupokea fursa uwekezaji? Nasaha zangu mjitahidi kuwa waaminifu kwa sababu Wanyasa waishi mijini watakapoitikia na kuwekeza ktk sekta mbalimbali UVUVI, KILIMO, UFUGAJI, UJENZI n.k atakuwa anatuma pesa kwa ajili ya mradi mliokubaliana kwa hiyo inahitajika uaminifu wa kina na taarifa za kweli.

Wengi huzongwa na kazi au shughuli za mijini na muda wa kuja huko mara kwa mara wanaukosa.Na kama kweli huko Nyasa wengi watakuwa waaminifu naamini wengi watajitokeza kuwekeza Nyasa na mzunguko wa pesa utaongezeka na uchumi kukua siku hadi siku.

Osati mtaji ndi faida vhonje vithela kumoa ndi kumadaba wachikazi asano asano.Zhikom sitimapezane mawa tulo sazino.

June 13, 2013

RAIS KIKWETE VS PAUL KAGAME; HAYA NI MAONI YA RAFIKI YANGU BEN SAANANE


Sijutii na sitajutia msimamo huu,ni msimamo wangu Binafsi.Ningekua Amiri Jeshi Mkuu leo hii nisingefanya jambo lingine zaidi ya kum-finance Jenerali Kayumba Nyamwasa kumpindua huyu Bloody Thirsty Dictator Kagame na kule Malawi ningeelekeza Nguvu kwa Prof.Peter Mutharika afutilie Mbali kibaraka mkubwa wa Mabeberu Joyce Banda(shame of Africa) wakati huo huo nikitumia vein tactic ya umuhimu wa Diplomasia

Kagame na Banda wakitaka kujua kuwa Watanzania tunaipenda nchi yetu waendeleze upuuzi waone tutakavyoungana kuwafutilia mbali.Hadi muda huu sijaona kauli kali ya waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe.Kauli za Kagame ni very undiplomatic na huwezi kukurupuka kutoa kauli kama zile wakati Kikwete alikua akiongelea kwa maslahi mapana ya ukanda huu.Pamoja na kuwa Tatizo la Congo Kinshasa,Rwanda na Burundi yana historia ya muda mrefu but there was nothing wrong in JK’s statement.Kenya na Uganda sasa walinywe maana ndiyo walikua makuwadi wa Rwanda katika kuhakisha wanapata admission EAC.Hata katika voting they always votes katika line ya Kenya na Uganda kwa gharama ya Tanzania kama Member State.

Namshangaa Kagame(one of the mastermind of Genocide) kwa kujifanya anayakoromea mataifa ya magharibi kinafiki hasa wanapojadili kuhusika kwake na mauaji ya kimbari,Yeye anawaita kuwa ni wakoloni na huku aki-enjoy matunda ya ukoloni kwa hiyo title aliyo nayo ya Urais.Hajui kwamba kama sio wakoloni waligawa eneo hili leo pengine angekua kama mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo tu maana Rwanda ingekua Mkoa wa Tanganyika hadi leo.

Tanzania tumezungukwa na majirani ambao ni hostile.Yule kibaraka wa kusini Joyce Banda anatia kinyaa,ndiyo maana hata ukanda wa SADC naona heri Bob Mugabe aendelee huko Zimbabwe kuliko Morgan Tsavangirai ambaye angezidi kuimarisha kambi ya vibaraka ukanda wa SADC.Hatuhitaji matusi ya Kagame ndiyo tujue JK ana mapungufu.SisiWatanzania ndiyo tunaojua na ndiyo maana Upinzani tuna hoja ya kutaka JK na Chama chake waondoke madarakani.Tusi la Kagame si kwa JK,ni tusi kwa watanzania wote.By the way,nakipongeza CCM na Kambi Rasmi ya Upinzani kujadili kwa uzalendo above party politics bajeti ya Wizara ya Ulinzi pamoja na kuwa na fungu kubwa.

Pamoja na umaskini wetu,tutumie raslimali zetu vizuri sasa kuimarisha maisha ya Watanzania na kuongeza millitary expenditure na ku-upgrade millitary software na hardware.Tuna majirani ambao wanaelewa lugha ya War Diplomacy zaidi kuliko lugha nyingine.Ukishakia na strong,Modern and formidable Millitary force kwa kawaida ina detterence effects kwa hostile Neighbours bila hata kuingia vitani moja kwa moja….Diplomasia kali inahitajika wakati kama huu.Tuendelee kuliunga Mkono Jeshi letu huko Goma DRC.

May 31, 2013

IJUE WILAYA YA NYASA KITAKWIMU



Na Vitus Matembo, Mbamba Bay
 Nyasa ni wilaya mpya ambayo inaongozwa na DC ERNEST KAHINDI. Kabla ya kwenda Nyasa alikuwa Dc wa Biharamulo.
..Nyasa inatarafa Tatu(3); Mpepo, Ruhekei na Ruhuhu.
..Nyasa inatakribani kata 18 ambazo ni;
*Lituhi: lituhi,kihune,mwera mpya,na ngingama.
*Mbaha;ndumbi,mbaha na lundu.
*Ngumbo; kihanga,ngumbo,mkili na Yola.
*Liuli; Liuli,puulu,Hongi,Nkalasi,Yumbu na Mkali.
*Kihagala;Mango,tumbi na kihagala.
*Lipingo;lundo,lipingo,Ngindo...
*MBAMBA BAY; mba bay,ndesule,ndengele,chinula na mbuyula.
*Kilosa;Kilosa,nangombo na likwilu.
*Kingelikiti
*Tingi
*Chiwanda; Chimate, Ng'ombo.
*Mtipwili;
*Luhangarasi
*Liparamba
*Liundi
*Mpepo
JUMLA YA WAKAZI kwa mujibu wa sensa 2012 ni WATU 146,000.
Shughuli yetu kubwa ni Kilimo,uvuvi,ufugaji na Biashara.
ZIWA NYASA NDIO NGUZO YETU YA KIMAENDELEO.