December 17, 2013

JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI YAANZISHA BARAZA LA AMANI NA USALAMA


KAMPALA, Uganda
 
VIONGOZI wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wametia saini kuanzishwa rasmi Baraza la Usalama la Jumuiya(East African Peace and Security Council) ambalo litashughulikia mambo mbalimbali ya ulinzi na usalama kwa nchi wanachama wa Afrika Mashariki. 

Viongozi hao kutoka Uganda, Tanzania, Kenya, Rwanda na Burundi wamefikia uamuzi huo juzi jumamosi wakati wa mkutano wao uliofanyika mjini hapa. Uamuzi wa kuanzisha Baraza la Usalama la Afrika Mashariki ni kutokana na kitisho cha kusambaa kwa ugaidi kama ambavyo yalivyotokea Dar es salaam(1998), Nairobi(1998 na 2013), na Kampala(2010).

Akizungumza mbele ya viongozi  waliohudhuria katika mkutano Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Richard Sezibera, alisema “Nathibitisha uamuzi uliofikiwa katika mkutano huu kuanzisha Baraza la amani na Usalama kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ikiwa na lengo la kuhakikisha ulinzi na usalama wa eneo hili dhidi ya tishio lolote litakalotokea,” 

Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanakabiliwa na tishio la ugaidi unaofanywa na kundi la Al Shabab ambalo lina uhusiano na Al Qaeda. Kwenye mkutano huo, nchi wanachama wamekubaliana kukabiliana na tishio la ugaidi kwa pamoja ili kuepusha matukio kama yaliyokea mjini Nairobi katika maduka ya Westgate ambapo zaidi ya watu 60 wasio na hatia walifariki dunia na wengine 175 wakiwa majaerhu. 

Mwaka 2010 kundi la Al shabab lilidaiwa kufanya mashambulizi katika jiji la Kampala na kusababisha vifo vya watu 70 baada ya mabomu mawili ya kutegwa ardhi kulipuka.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako