December 17, 2013

MICROSOFT STUDENT ADVANTAGE NI MAPINDUZI KIELIMU



Na Mwandishi Wetu,Mbinga

WAKATI dunia ikiwa kwenye michakato mbalimbali ya kitaaluma ya elimu, hatimaye kampuni ya Microsoft Corpoartion imeanzisha Programu mpya ambayo itawawezesha wanafunzi kufanya mazoezi yote  wanayopewa shuleni kupitia mfumo wa teknolojia mpya. 

Kampuni hiyo imebuni programu mpya ya “Student Advantage” ambayo itawawezesha wanafunzi kupeana kazi za shuleni,mazoezi ya nyumbani, na masuala yote muhimu ya kitaaluma. 

Mpango huo ulitangazwa juzi, alhamisi na kampuni hiyo wakati ikitambulisha programu ya Microsoft Office 365 Education ambayo inakadiriwa kutumiwa na zaidi ya wanafunzi milioni 110 wa vyuo , idara na wahadhiri mbalimbali duniani.
Programu ya Microsoft Office 365 Education itawapa fura wanafunzi kutumia kupitia huduma zilizopo mfano Microsoft Word, OneNote, ambazo zinafanana na huduma za PowerPoint na Excel.
Mpango wa kutumia programu hiyo unatarajiwa kuanza rasmi desemba 1, mwaka huu huku Vyuo mbalimbali duniani vikipewa leseni ya Office 365 ProPlus kwa wanafunzi na wahadhiri pamoja na wakuu wa idara watakuwa wanatumia programu yenye leseni ya Office Proffessional Plus bila gharama zozote.
Huduma hizo zote zitawapa nafasi wanafunzi kupata maarifa mbalimbali kupitia Exchange Online, SharePoint Online na Lync Online, ambazo zipo kwenye programu hiyo ambayo ina vitu vingine vitakavyomwezesha mwanafunzi kuwasiliana na wengine kwenye vyuo mbalimbali duniani. 

“Wanafunzi watakaotumia huduma hii kila siku wataweza kufanya akzi zao nyingi za shuleni, na zile muhimu kwa kutumia programu hiyo mahususi. Hii itawasaidia wanafunzi kuwekana pamoja katika kazi zao za vyuoni na kuongeza ufanisi wao kitaaluma,” alisema Mark Chaban, Mkuu wa kampuni hiyo katika nchi za Afrika na Mashariki ya Kati.
Kwa mujibu wa taarifa ya Microsoft, wamefanikiwa kutembelea vyuo 30 binafsi na vya umma pamoja na wizara mbalimbali za elimu ili kutoa mafunzo namna ya kutumia programu hiyo.
Alisema mpango huo upo chini ya Intenational Data Corporation(IDC) ambayo itakuwa ikikusanya taarifa za maendeleo ya wanafunzi mbalimbali watakaotumia ili waweze kuwa tija katika soko la ajira na kuboresha maisha yao.
Kampuni hiyo imesema kuwa inakusudia kufuatilia uwezo wa wanafunzi katika kutumia huduma hiyo, ambapo watakaoonekana kuwa na kiwango cha juu watachukuliwa na kupelekwa kwenye makampuni mbalimbali na kulipwa mishahara minono.
Microsoft imepanga kutengeneza ajira kwa asilimia 28 ifikapo mwaka 2020 ambapo miongoni mwa wanafunzi milioni 11.5 wataajiriwa kwa vigezo vilivyowekwa.
“Walimu wanapaswa kubuni njia mpya za kufundisha wanafunzi wao ili kuboresha sekta ya elimu. Elimu ya mawasiliano ya teknolojia ni muhimu, kwani inarahisisha utendaji wa kazi, na kuongeza uwezo kwa wanafunzi wote watakaohitimu na kuingia kwenye soko la ajira sasa na baadaye,” alisema Kunle Awosika, Meneja wa Microsoft nchini Kenya.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya juhudi za mara wka mara kurahisha shughuli za elimu kwa wanafunzi ikiwemo tangu kufanikiwa kwa programu ya Microsoft Student 2009 DVD na nyingine ambazo zimesaidia kuboresha sekta ya elimu na wanafunzi pia. 

Student Advantage inatarajiwa kuwa huduma bora zaidi katika sekta ya elimu na kuwezesha ufanisi katika sekta hiyo ikiwemo kuwasaidia wanafunzi kuingia katika soko la ajira wakiwa na weledi wa kuosha.

Makala haya yameandaliwa kwa msaada wa vyanzo mbalimbali vya mashirika ya habari.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako