December 17, 2013

DMCT YAPANIA KUWAPELEKA WANAFUNZI WA FANI YA HABARI NJE YA NCHI




Na Mwandishi Wetu, Mbeya 

SUALA la elimu ya mawasiliano kwa umma linazidi kuchukua nafasi kubwa kuliko ilivyokuwa miaka ya nyuma. Hii inatokana na mabadiliko makubwa ya teknolojia  ambayo yamesaidia nchi yetu kunufaika kama nchi zingine duniani.
Miongoni mwa vituo vipya vya elimu hapa nchini ni Chuo cha habari cha Digital Media College of Tanzania, kilichopo katika jiji la Mbeya ambacho kimekuja na mikakati mbalimbali katika kuitikia wito wa kuboresha elimu ya habari kwa watanzania.

Akizungumza na mtandao huu jijini Mbeya Mkurugenzi wa Chuo hicho, Lucas Kulwa alisema kuwa mpango wa kuanzishwa chuo hicho ulibuniwa na kampuni ya Radio Consult Limited, ambayo inaendesha shughuli zake jijini Mbeya.
“Kwa kweli tulifikiria sana kufanya kitu kwa ajili ya watanzania na nashukuru serikali inatuunga mkono kwamba sasa hatutategemea waandishi wa habari au wataalamu wa masuala ya mawasiliano ya umma kusoma fani hiyo hapa Dar es salaam pekee.
“Tumeanzisha chuo hiki mjini Mbeya na tumeweka makao yetu eneo la Nanenane, sababu tulifanya utafiti na baadhi ya wataalamu kutoka nje ya nchi ili kujua ni eneo gani sahihi ambalo litatusaidia kuwafikia watanzania bila kutegemea kitovu cha nchi, yaani Dar es salaam. 

Alipoulizwa na mwandishi wa makala haya ni kwanini wametumia jina la Digital Media College of Tanzania, naye alisema, “Kwasasa kuna vyuo vingi sana hapa nchini vinavyofundisha kozi hizi za media ukiwemo uandishi wa habari na utangazaji, changamoto kubwa iliyojitokeza ni kwamba wahitimu wote wanaomaliza katika vyuo mbalimbali wengi wao wanakosa ajira na kibaya zaidi wanashindwa kutumia elimu yao waliyoipata hata kujiajiri kwa kuandika habari,
Lucas Kulwa, Mkurugenzi wa Chuo cha DMCT, kilichopo jijini Mbeya
“Pia wanashindwa hata kumiliki mitandao (websites), kuandika na kuhariri vitabu, kutafuta fursa mbalimbali kwenye mitandao, kujiunga katika vyama mbalimbali ulimwenguni vinavyojihusisha na masuala ya uandishi wa habari, kuandaa makala na kushiriki kwenye mashindao mbalimbali. Kuna mambo mengi sana ambayo mwandishi wa habari anaweza kuyafanya bila kuajiriwa yaani namaanisha kwa kujiajiri mwenyewe,

“Kwahiyo hii ndiyo sababu kuu ambayo chuo cetu cha DMCT kinapenda kuiangalia kwamba kwa mwandishi wa habari yeyote yule kuanzia ngazi ya chini kabisa hadi ya juu wawe na uwezo wa kujiajiri wenyewe. Kuna tofauti kubwa kati ya nchi yetu na nchi za Afrika Mashariki na Ulaya kwamba sisi mwandishi wa habari hutegemea ajira tu katika chombo cha habari na akikosa hapo anarudi kulala nyumbani na kulalamika hakuna ajira,

“Katika kutafakari ni kwa njia zipi tutazitumia kumsaidia mwanafunzi au mwandishi wa habari aweze kujiajiri hata pale anapokosa chombo cha habari cha kufanyia kazi, DMCT tumeona ni bora tufundishe kozi zifuatazo kwa mwaka 2014:- Certificate in digital Journalism ya mwaka mmoja, pamoja na Certificate in Radio Production kwa mwaka mmoja.

Anasem,a, “hii kozi ya Digital Journalism itawawezesha wanafunzi wote kuanza kutengeneza pesa hata kama ni kiasi kidogo wakiwa wanasoma kutokana na kazi za vitendo watakavyokuwa wanazifanya, kama kuandika habari na makala na kuziuza katika mitandao mbalimbali nje na ndani ya nchi.
“Pia watafundishwa masuala ya kumiliki mitandao (website/blog) kwa undani zaidi hali itakayowawezesha pia kuendelea kujipatia pesa. Vile vile kozi ya uandaaji wa vipindi ambayo itatoa waandaji wa vipindi wenye ujuzi wa hali ya juu ambao wanaweza hata kuuza vipindi vyao kwenye vyombo vya habari mbalimbali.

“Chuo chetu kimepania kufundisha somo la kompyuta kwa kiwango cha juu zaidi, kwani tumegundua eneo hili limekuwa kero kwa wanahabari na wananchi wengine watakaopenda kusoma kompyuta kama nyenzo ya kukabiliana na mabadiliko ya tkenolojia mpya,

“Uwiano wa mafunzo kwa vitendo, katika chuo chetu cha DMCT tunatarajia kutumia 70% ya mafunzo kwa vitendo na 30% mafunzo ya nadharia. Tunatarajia kutembelea chombo cha habari cha nje, kwa kuwa Mbeya ipo karibu na nchi za Malawi na Msumbiji tunatarajia kufanya mpango wanafunzi wetu wapate nafasi ya kutembelea chombo chochote kikubwa cha habari nchini Malawi au Msumbiji. Pale DMCT tuna studio ya kisasa itawasaidia wanafunzi wetu, ndiyo maana tukaanzisha na kozi hii ya Music Production, TV Production na ICT. Tuna malengo mengi, watanzania watuunge mkono tu,”

No comments:

Post a Comment

Maoni yako