February 18, 2009

Jibu la Kitendawili, na pole kwa Yasinta

Wanazuoni, wapo hoi,wameomba jawabu limekuwa thawabu,hawanalo,wanataka ahueni lakini tuweke tu AFANALEKI ili tupaje jibu lake.
Pengine hongera SARA kwa kujaribu kuwa MANII ni jibu lako, lakini nilikupamaswali kadhaa ambayo unaweza kunipatia jibu la kitendawili changu. Jamani eeeeh hivi kweli mmeshindwa au mnanitega?
JIBU; nimehangaika na kitendawili hiki tangu mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka 2008, nilipewa,nikashindwa kisha nikajua hakuna shemu ya kusemea tena kama Blogu zetu maana kuna kila wajuzi wa mambo mbalimbali yatuhusuyo kila leo. LAKINI binafsi sina JAWABU ndiyo maana niliweka hapa ili tusaidiane, na kwahakika mwenye jibu atusaidie.

Kuhusu Yasinta, pole sana rafiki yangu, najua ni mabadiliko ya mazingira ndiyo maana imekuwa hivyo. Ninakuombea zaidi kwani nimevumilia kutoandika hapa, lakini naona lazima wanablogu wenzetu wajue kuwa unaumwa, toka uje bongo ni homa na afya kidogo kuzorota. Lakini naamini unaweza kubadilika, unaweza kurejea katika uhalisia wako.

Tupo pamoja,tunakuombea mema,tunangojea Tanzaniaresan irejee hewani kwa moto na makusanyo ya uhakika. Ni mungu pekee anayeuongoza kwa imani lakini miongozo tunayo mikononi mwetu. Ugua Pole Yasinta utarudi kama kawaida na kuwakilisha maofisini mpaka kwenye mageto, afrika na ughaibuni. Na wenye nia tunakuombea
Mnyasa.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako