Showing posts with label elimu. Show all posts
Showing posts with label elimu. Show all posts
March 07, 2018
KITABU KIPYA KUTOKA KWA MWANDISHI BEKA MFAUME
March 02, 2018
KUTOKA CHINA HADI CHUO CHA TEKNOLOJIA DAR ES SALAAM (DIT)
NA KIZITO MPANGALA
DUNIANI kuna ubunifu wa namna
mbalimbali unafanyika katika teknolojia ili kurahisisha shughuli mbalimbali
katika maisha yetu ya kila siku. Ubunifu wa kiteknolojia umekuwa ni lulu
mojawapo katika ulimwengu huu wa Sayansi na Teknolojia hasa katika umeme na
elektroniksi, ingawa upo ubunifu mwimgine nje ya uga huu wa umeme.
Kiti cha magurudumu manne ni
kifaa cha muhimu sana kwa wagonjwa katika hospitali mbalimbali duniani. Na ubunifu
mbalimbali hufanyika ili kuboresha utendaji wa kiti hiki. Kiti hiki kwa sasa
kina magurudumu manne ambapo makubwa mawili na madogo mawili na hutegemea nguvu
za mgonjwa kama anaweza kukisukuma yeye mwenyewe na kama hawezi basi anasukumwa
na mtu mwingine.
Tofauti na baiskeli ya
magurudumu matatu, kiti hiki kina ukubwa ambao unatosha kwa mtu mmoja tu kuketi
na anayesukuma hulazimika kuembea. Vilevile hakichukui nafasi kubwa. Hakiwezi
kutumika kama njia mojawapo ya usafiri barabarani kama ilivyo baiskeli ya
magurudumu matatu inayotumiwa na walemavu wengi duniani kote.
Kiti hiki kilianza kubuniwa
nchini China mnamo karne ya tano na baadae nchini Ugiriki mnamo karne ya sita
ambapo kilibuniwa kwa ajili ya kubebea watoto na wazee wasioweza kutembea na
kisha kuwasukuma ili kuwafikisha sehemu waliyokusidia. Nchini China awali
walikuwa wakitumia matoroli kwa ajili ya kuwabeba wazee wasioweza kutembea na
pia vilema na vilevile kubebea mizigo mizito. Michoro ya kiti cha magurudumu
mawili iliyochorwa nchini China ilionekana mwaka 525 B.K huko Ulaya.
Madhumuni
elimu,
Sayansi na Teknolojia
March 01, 2018
USHAURI KWA RAIS: NAKUOMBA KUBALI TUENDELEE KUCHANGISHANA
NA.HONORIUS
MPANGALA
KWANZA kabisa nianze na kukusalimia shikamoo
mheshimiwa Rais wangu, Dk. John Pombe Magufuli. Najua hii kazi ni ngumu kama
usemavyo wewe mwenyewe lakini sina budi kukuombea uione nyepesi ili uweze
kupata nguvu ya kututumikia vyema kama yalivyokuwa malengo yako siku unaenda
kuchukua fomu ya kugombea nafasi hiyo.
Mheshimiwa nikiwa safarini kuelekea makao makuu
ya nchi yetu Dodoma, katika gari nilipata tafakuri ambayo ilinifanya
nitoe kitabu changu cha kuandika kumbukumbu na kuhifadhi mawazo yangu ambayo
nimeona nikuandikie.
Hoja yangu kubwa ambayo ilikuwa ikizunguka katika
kichwa changu ni ile niliyokumbuka kauli yako ya kupiga marufuku wananchi
kuchangishwa mchango wowote katika shule za serikali.
February 26, 2018
ZAWADI YA VITABU KWA MARA NYINGINE
JUMAMOSI Februari 24 mwaka huu nilipatiwa
zawadi ya vita viwili kutoka kwa Bwana Ragin Mmbaga, kama vinavyoonekana
pichani. Vitabu hivyo vimeandikwa na Bwana Johne Wisse. Kuna kitabu cha TONE LA DAMU cha lugha ya kiswahili na THE BROKEN CAMPUS RULE cha lugha ya Kiingereza.
Ninawashukuru kwa kujali
kuwa visima vya maarifa. Hakika mwaka huu nimeanza kwa furaha kubwa kwani huyu
anakuwa mtu wa tatu kuniletea vitabu kibaruani kwangu.
Usomaji wa vitabu ndicho kitu
ninachokipenda zaidi. Ndicho kilevi au kitu ambacho kinachukua muda wangu wote
kuhakikisha nafurahi. Zaidi ya hapo navutiwa na mchezo wa soka. Vitabu ni kitu
muhimu sana. Namshukuru Ragin Mmbaga kwa niaba ya John Wisse. ASANTENI SANA
-MARKUS MPANGALA
February 12, 2018
LEVARDIS ROBERT MARTYN BURTON JR: MSEMINARI ALIYEUVAA UAFRIKA KWENYE FILAMU YA “ROOTS” KWA JIN LA KUNTA KINTE.
Na Kizito Mpangala
Ukimtazama hata kwa picha
utasema ni mzaliwa halali wa Gambia kutokana na mwonekano wake katika filamu
iliyomlazimu kuwa Mgambia.
Alizaliwa mwaka 1957 nchini
Ujerumani Magharibi (sasa Ujerumani) kwa wazazi Levardis Robert Martyn Burton
Sr na Erma Gene. Baba yake alikuwa ni mpiga picha wa jeshi la Marekani katika
kituo cha afya cha Landstuhl cha jeshi la Marekani nchini Ujerumani. Mama yake
alikuwa mwelimishaji wa jamii.
Burton Jr na dada zake wawili
walilelewa na mama yao katika mji wa Sacramento jijini Calofonia nchini
Marekani huku baba yao akibaki Ujerumani kikazi.
Burton Jr alivutiwa na kujiunga
na Seminari na hivyo akakubaliwa kuanza masomo katika Seminari ya Mtakatifu
Pius X katika kitongoji cha Calt jijini Califonia kwa lengo la kuwa padre.
Alipokuwa Seminarini, alipenda
kusoma vitabu vya falsafa na kufanikiwa kuwasoma wanafalsfa kadhaa Seminarini
hapo. Katika falsafa hizo, alivutiwa na kuwasoma kazi za wanafalsafa Lao Tzu,
Nietzsche na Kierkegaard ambazo zilimfanya awahoji walimu wake kama Ukatoliki
ndiyo dhehebu pekee kweli.
Alipofikia umri wa miaka 17
alihitimu katika Seminari hiyo na kuamua kujiunga na chuo kikuu cha Califonia
Kusini kwa masomo ya sanaa. Alitunumiwa shahada ya kwanza ya sanaa huku
akijikita katika uigizaji.
ANA KWA ANA NA MBUNGE WA VITI MAALUMU CHADEMA, NDUGU UPENDO PENEZA
Sisi katika blogu yetu tunakutana
na wanasiasa mbalimbali bila kujali itikadi zao. Au pia viongozi wa kila kada
tunazungumza nao bila kujali fani zao.
Madhali wengi wao ni marafiki
zetu maana ni watanzania wenzetu basi huwa tunazungumza nao mambo yahusuyo ustawi wa jamii yetu kwa ujumla wake. Tunazungumzia
maendeleo ya elimu, uchumi, siasa, utamaduni, afya na kadhalika.
Madhumuni yetu ni kuendelea
kuzungumzia maendeleo ya wananchi pamoja na furaha ya jamii. Tunajikita katika
maslahi ya taifa letu. Tanzania ni nchi yetu na hatuna kwingine. Tutailinda na
kuikosoa ikibidi.
Pichani; kutoka kushoto ni
Gabriel Mushi (mwandishi wa gazeti la RAI), mhariri wa Blogu hii Markus
Mpangala (katikati) na Mbunge wa Viti maalumu ndugu Upendo Peneza.
JOSEPHINA MARGARET BAKHITA: MTAKATIFU MWAFRIKA ALIYEPONEA MIKONONI MWA MAHAKAMA YA ITALIA.
NA KIZITO MPANGALA
JOSEPHINA Margaret Bakhita
alizaliwa mwaka 1869 mjini Darfur kitongoji cha Olgassa nchini Sudan
katika jamii ya kabila la Daju. Baba yake aliheshimiwa sana kwa kuwa alikuwa ni
kaka ya Chifu wa kabila hilo. Bakhita aliishi kwa furaha akiwa hajui mateso ya
kitumwa yanakuwaje.
Alipofikia umri wa miaka minane,
alitekwa na Waarabu wafanyabiashara ya utumwa ambao tayari walikwishamteka dada
yake miaka miwili kabla ya kumteka Bakhita mwenyewe. Alilazimishwa kutembea
mwendo wa kilometa 960 peku kutoka Darfur hadi El Obeid. Kabla ya
kufika El Obeid alikuwa ameuzwa mara mbili njiani.
Bakhita alipofikia umri wa miaka
12
alikuwa ameuzwa tena mara tatu na kisha kusafirishwa mpaka Uturuki. Huko alikumbwa
na mateso mengi na uchungu hali iliyompelekea kusahau jina lake la asili na
hivyo alilazimika kutumia jina alilopewa na Waarabu, Bakhita likimaanisha mtu
mwenye bahati. Kisha akasilimishwa.
Bakhita alinunuliwa na tajiri
wa biashara ya watumwa ambaye alikwa Mwarabu na kumtumikisha kama mfanyakazi wa
kuwahudumia binti zake wawili ambao waliishi nae vizuri. Alipokorofishana na
mtoto wa kiume wa Mwarabu huyo alipigwa na kufikia hatua ya kushindwa kutembea
kwa muda wa mwezi mmoja.
February 03, 2018
JOHN LANGALIBALELE DUBE: MWANAFUNZI ALIYEAMINIKA KUWA NA TABIA CHAFU CHUONI MWASISI WA CHAMA CHA ANC, AFRIKA KUSINI.
Na Kizito Mpangala
John Langalibalele Dube
alizaliwa mwaka 1871 kwa wazazi James Dube na
Elizabeti Dube katika kitongoji cha Inanda,kwa sasa ni mkoa wa KwaZulu Natal. Jina
lake la katikati yaani Langalibalele
alipewa na wazazi wake likimaanisha “mwanga
wa jua”. Baba yake alikuwa mchungaji katika kanisa la misheni ya Waamerika
walioishi katika jamii ya Wazulu.
![]() |
| John Langalibalele Dube |
Baba yake alikuwa kiongozi wa
kabila la watu wa Qadi katika jamii ya Wazulu na jina lake lilikuwa Ngcobo
Dube. Baada ya ujio wa Wamisionri alimua kujiunga na Ukristo na kisha
akabatizwa kwa jina la JAMES DUBE. Huo ndio ulikuwa mwisho wa kuliongoza kabila
hilo. John Langalibalele Dube alikuwa
Mwalimu, Mhariri, Mpigachapa, Mshairi, Mwanafalsafa, Mwandishi wa Insha, na
mwanasiasa nchini Afrika Kusini.
John Langalibalele Dube alianza
masomo katika kitongoji cha Inanda, na baadae akajiunga na chuo cha Adams (Adams College) kitongoji cha Amazimtoti
kusini mwa mji wa Durban nchini Afrika Kusini. Akiwa chuoni hapo, walimu
walipeleka lalamiko kwa wazazi wa John kwamba kijana wao ana tabia chafu chuoni
hapo ambayo haiendani na sheria za chuo. Ndipo Mchungaji William Cullen Wilcox
alipoteuliwa kuzungumza na kumkanya John Langalibalele Dube kwa tabia zake
chafu (haikuwewa wazi ni tabia zipi hasa alizokuwa akizifanya). John alifuata
nasaha alizopewa na kisha akabadili tabia.
Wamisionari wa Amerika
walioondoka katika kitongoji cha Inanda, John aliambatana nao na kujiunga na
chuo cha Oberline nchini Marekani. Aliambatana nao kwenda Marekani baada ya
kupata ruhusa kutoka kwa baba yake Mzee James Dube ambaye alikuwa mchungaji na
kiongozi katika chuo cha Adams. Wamisionari hao walikubali kwa sharti kwamba
hawatamhudumia chochote kifedha, hivyo Mzee James Dube alipaswa kuingia mwnyewe
mifukoni mwake.
GARETT AGUSTUS MORGAN: MJASIRIAMALI ALIYEVUMBUA TAA ZA KUONGOZEA MAGARI BARABARANI.
Na Kizito Mpangala
Garett Morgan alizaliwa mwaka 1877 katika
kitongoji cha Claysville mjini Kentucky nchini Marekani akiwa na asili ya
Afrika yaani. Baba yake alikuwa mtumwa aliezaliwa katika kitongoji cha
Huntsville mjini Alabama. Baba yake alikuwa mtumwa kwa kurithishwa na wazazi
wake waliokuwa watumwa. Miaka kadhaa baadae baba yake, John Morgan akawa Luteni
Kanali wa jeshi la Marekani, Brigedia Jenerali katika jeshi la Kentucky kwa
lazima. Mama yake Garett Morgan pia alikuwa mtumwa kama mume wake.
Garett Morgan alipofikia darasa
la sita katika shule ya Brach Elementary mjini Claysville akiwa na umri wa
miaka 16 alikwenda katika kitongoji cha Cincinnati mjini Ohio kutafuta kazi
itakayompa ujira ili kupata mahitaji yake. Aliajiriwa mashambani.
Kama ilivyokuwa kawaida ya
watoto wengi nchini Marekani wakati huo, Garett Morgan alilazimika kuacha shule
akiwa darasa la sita na kuamua kufanya kazi katika mashamba kutwa nzima. Kutokana
na bidii yake katika kazi, aliletewa mwalimu awe anamfundisha hapohapo shambani
ambako ndiko yalikokuwa makazi huku akiendelea na kazi za shambani huko.
Alifundishwa ufundi na baadae
akawa fundi mahiri wa kutengeneza mashine za kushonea nguo yaani cherehani. Uzefu
huo wa kutengeneza cherehani aliuheshimu na kujifunza zaidi jinsi mashine
zinavyofanya kazi. Kazi yake ya kwanza kuvumbua ilikuwa ni cherehani inayotumia
mkanda kama cherehani za sasa. Alivumbua cherehani hiyo tofauti na za mwanzo
zilizokuwa zikizungushwa kwa mikono.
GEORGE CRUM: MPISHI MASHUHURI ALIYEVUMBUA CHIPSI YA VIAZI
NA KIZITO MPANGALA
Alizaliwa mwaka 1824 katika
mji wa Saratoga, sasa ndilo jiji la New York
nchini Marekani. Alijishughulisha na uwindaji na upishi katika migahawa ilikuwa
katika milima ya Adirondack. Alifanya shughuli hizo kwa bidii lakini baadae
alielekeza nguvu zake zaidi katika upishi. Jina lake lilikuwa ni George Speck. Kutokana
na jina la uchepe kushamiri zaidi ambalo ni Crum, aliamua kujiita George Crum.
Baba yake aliitwa Abe Speck
ambaye alikuwa mhamiaji kutoka Kentucky kwenda Saratoga. Akiwa Saratoga alimuoa
mwanamke mwenye asili ya India ambapo baadae George alizaliwa.
Bidii yake ilipoonekana zaidi,
alichukuliwa na tajiri mmoja katika mgahawa ulioitwa Moon’s Lake House, karibu
na maporomoko ya maji ya Saratoga. Mgahawa huo uliaminika kuwa ndio wenye
gharama za juu za chalula. Hapo ndipo ujuzi wake wa upishi ulipofahamika na
watu wengi zaidi. Licha ya kuwa na gharama za juu katika mgahawa huo watu
walipenda kufika kwa wingi kutokana na umahiri wa George Crum katika upishi
wake.
Bada ya kufanya kazi kwa muda
mrefu katika mgahawa huo, George aliamua kumchukua dada yake ili wafanye kazi
pamoja kutokana na ukata ulioikumba familia yao. Walikuwa ni wenye rangi
mchanganyiko.
February 02, 2018
MFUMO WA UFUNDISHAJI NCHINI UNATAKIWA KUBADILISHWA
NA KIZITO MPANGALA
KILA
mara inapofanyika mitihani kidato cha pili, nne na sita matokeo yanapokuwa
mabaya wanaolaumiwa ni walimu. Matokeo yakiwa mazuri wanapongezwa walimu.
Tunakumbuka
matokeo ya kidato cha nne yamewahi kubatilishwa wakati wa uongozi wa serikali
ya awamu ya nne. Ilibidi NECTA wafanye usahihishaji upya ili kuja na matokeo
mazuri kutokana na awali kuwa mabaya kwa nchi nzima.
Mwenendo
mzima wa sekta ya elimu mara nyingi Walimu wamebebe lawama nyingi. Lakini ipo
haja ya watendaji wakuu (yaani serikali yetu) kubadilisha mfumo wa ufundishaji
unaotumiwa hapa nchini.
Nasema
hivi baada ya kufanya utafiti na kubaini kuwa ili mtu awe amebobea kwenye
ufundishaji lazima awe na uwezo mkubwa katika somo fulani. Kwahiyo naongelea
namna ya kuwabadilisha watu ili kuleta manufaa ya elimu, uwezo wao na
kuwasaidia wanafunzi.
Ingefaa
kila mwalimu hapa nchini awe anafundisha somo moja tu na kwa madarasa mawili tu
kwa siku nzima. Somo hilo moja ndilo liwe hilo tu hadi atakapostaafu. Mbinu hii
itasaidia ubobezi mzuri wa somo husika kwa walimu wetu.
Isiwe
mwalimu wa Historia alazimike kufundisha tena somo la Uraia. Mwalimu wa
Biolojia alazimike tena kufundisha somo la Kemia. Mwalimu wa Hisabati alazimike
tena kufundisha somo la Fizikia. Mwalimu wa Kiswahili alazimike tena kufundisha
somo la Kiingereza kwa kuwa tu eti anajua sana kuidadavua fasihi. Mwalimu wa biashara(Commerce)
n alazimike tena kufundisha uhasibu (Accounts) ingawaje masomo haya
yanashabihiana kwa namna fulani.
Madhumuni
elimu
January 31, 2018
UCHAMBUZI WA KITABU: "AMEZIDI"
MWANDISHI: SAID AHMED MOHAMED
AMEZIDI ni tamthiliya iliyopgwa
chapa na East African Educational Publishers (Nairobi, Kampala, na Dar es
Salaam) ambapo chapa ya kwanza ilitolewa mwaka 1995. Kitabu
hiki kimesajiliwa kwa namba za usajili ISBN 9966-46-752-1.
MCHAMBUZI: KIZITO MPANGALA
Tamthiliya hii imegawanyika
katika maonyesho kumi ya jukwaani ambapo kila onyesho lina ujumbe ambao
unailenga jamii ya Afrika kwa ujumla hasa katika suala la maendeleo ya
liuchumi, kielimu kijamii na kadhalika. Wahusika wakuu wa tamthiliya hii ni Ame
na Zidi. Maonyesho haya yote na tamthilya yenyewe kwa ujumla ni cmhezo wa
mawazoni tu!
Ame na Zidi wanajikuta katika
umasikini mkubwa katika bahari iliyojaa mali. Katika hali hii ya uhitaji
wanatambua kuwa hawana lingine la kufanya ila kuomba misaada ili wayatosheleze
mahitaji yao. Msaada unapokuja unaleta madhara mengi zaidi.
Onyesho la kwanza linaonyesha
Zidi akiwa anamwamsha nduguye Ame aliyekuwa amelala kukiwa kumeshakuchwa. Zidi
anamwonyesha Ame mihogo miwili aliyotoka kuitafuta ili wapate kuila.
Onyesho la pili linaonyesha Ame
na Zidi wakiwa katika kasri lao wanalisifia kasri hilo lililojaa samani nyingi
kutoka Paris (Ufaransa) na vito mbalimbali pamoja na mazuria kutoka Iran.
January 26, 2018
TUNAPOKOSEA NI PALE TUNAPOCHANGANYA ELIMU,SIASA
NA HONORIUS MPANGALA
Japokuwa nimekuwa mtu nisiyependezwa
na na hili neno “Wananchi wa hali ya chini”' lakini najiuliza hao wa hali ya
juu ni akina nani, wanafanya nini kutokuwa na hali ya chini na njia zao zikoje
ili tuwaambie wa hali ya chini wajifunze kwenda huko juu?
HISIA zangu zimenifanya niwe
mtu tofauti kabisa kuhusiana na matumizi ya baadhi ya maneno hapa nchini. Mengi
hutumiwa na viongozi wa ngazi za juu kuwaona wale waliopo chini au wasio na
vyeo kama wao kuwa wenye kiwango fulani
cha dhiki kinachostahili kuitwa cha chini. Ni hapo ndipo nakuwa na hisia
tofauti sana juu ya kutumia maneno fulani dhidi ya kundi jingine hasa lile ninaloongoza
au viongozi wanaloliongoza.
![]() |
| Makala hii imechapishwa katika gazeti la MTANZANIA toleo la leo |
Suala elimu katika nchi yoyote
ni muhimu na linatakiwa kupewa kipaumbele sana. Kiuhalisia mazingira ya
wanafunzi kwa shule nyingi zinazomilikiwa na serikali zimekuwa na changamoto
kubwa na kupelekea hata matokeo mabaya kwa shule hizo.
Lakini unakuta baada ya kutazama wapi walipojikwaa wao wanakawaida ya kulaumu mwendo Wa aliyedondoka kuwa hatazami vyema au hatembei vyema.
Lakini unakuta baada ya kutazama wapi walipojikwaa wao wanakawaida ya kulaumu mwendo Wa aliyedondoka kuwa hatazami vyema au hatembei vyema.
Tangu iliposemwa elimu bure maisha
ya wanafunzi yamekuwa na changamoto zake na wazazi waliipokea katika mitazamo
yao hii hoja. Kutokana na kuzoea kupewa pewa tangu zama za wakaloni, waafrika
wengi wamekuwa wavivu wa kujitafutia wao na kutatua changamoto wao huku
wakitegemea tusaidiwa kama ilivyokuwa katika maisha ya ukoloni au kwa wale
waliokuwa wanaishi karibu na Taasisi za kidini zilivyokuwa zikitoa misaada.
UCHAMBUZI WA KITABU: SAFARI YA YERUSALEM KUTAFUTA AMANI
NA MARKUS MPANGALA
BOUTROS Boutros Ghali aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kati ya mwaka 1992 hadi 1996 amefariki dunia Februari 16 mwaka 2016 akiwa na miaka 93.
BOUTROS Boutros Ghali aliwahi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kati ya mwaka 1992 hadi 1996 amefariki dunia Februari 16 mwaka 2016 akiwa na miaka 93.
Leo
tunachambua kitabu chake cha “Egypt's Road to Jerusalem:: A Diplomat's Story of
the Struggle for Peace in the Middle East” kilichozindualiwa rasmi Mei 20,
1997. Kitabu hicho kina jumla ya kurasa 366, kimechapishwa na Random
House(1997) na kikiwa katika lugha ya kiingereza. Boutrous amekipatia namba
ISBN-10: 0679452451.
Boutros
Ghali anatuelezea miaka minne ya uzoefu wake katika utawala wa aliyekuwa Rais
wa Misri, Anwar as-Sadat. Anatuonyesha namna alivyochaguliwa kwenye uwaziri wa
mambo ya nje mwaka 1977 na kifo cha rais Sadaat mwaka 1981.
Katika
kitabu hiki Boutros Ghala anadhihirisha umahiri alioonyesha katika masuala ya
diplomasia wakati wa kusaka amani ya mashariki ya kati. Ikumbukwe eneo la
mashariki ya kati limekuwa kwenye migogoro ya muda mrefu kiasi kwamba ufumbuzi
umekuwa mgumu.
Ni
eneo ambalo mwandishi wa kitabu hicho anatukumbusha hatua kwa hatua walizokuwa
wakichukua katika kuhakikisha amani inarejea mashariki ya kati. Anatuonyesha
namna ambavyo Misri na Israel zilivyokuwa zikifanya juhudi za kumaliza uhasama
wao.
January 23, 2018
ZOLILE HECTOR PIETERSEN: MTOTO ALIYELAZIMU KUANZISHWA KWA KUMBUKUMBU YA MAUAJI YA KIMBARI AFRIKA KUSINI, TAREHE 16 JUNI KILA MWAKA.
Na Kizito Mpangala
Zolile Hector Pietersen
alizaliwa tarehe 19/08/1963 mjini Soweto nchini
Afrika Kusini wakati falsafa ya ubaguzi wa rangi ikiwa imepamba moto. Falsafa
ya ubaguzi wa rangi ilikuwa ikijulikana kama Apartheid, ambayo ilikuwa ikiendeshwa na makaburu waliokuwa
wakitawala nchi ya Afrika Kusini.
![]() |
| Zolile Hector Pietersen akiwa amebebwa na Mbuyisa Makhubo baada ya kupgwa risasi. kushoto ni Antoinete Sithole, dada yake Zolile Hector Pietersen akilia. |
Jina halisi la ukoo wake ambalo
lilikuwa likitumika na familia yake ni Pitso,
lakini fdamilia hiyo ililazimika kubadili na kuwa Pietersen ili kuendana na falsafa ya Apartheid, na kujihisi kama wao ni makaburu ilhali wakiwa ni weusi.
Familia hiyo iliamaua kufanya hivyo ili kukwepa dhuruma za makaburu. Hata jina
la Zolile lilifutwa kwa muda ili apate nafasi ya kusoma.
January 22, 2018
UCHAMBUZI WA VITABU KILA IJUAMAA
Kwa mwezi safu hii inachambua vitabu vinne (4). Kwa mwaka inachambua vitabu 48. Ni safu maalumu kwa uchambuzi wa vitabu pekee. Ni safu iliyodumu kwa miaka minne sasa ndani ya gazeti hili. Ni safu inayopendwa na kampuni za uchapishaji wa vitabu, waandishi na wasomaji pia. Ni safu inayotanua masimulizi au maarifa yaliyomo.
Una kitabu chako wataka
kichambuliwe? Wenzako wanakuja, kwanini wewe usubiri u! Ongea nasi, uwafikie
wadau wengi…..
January 21, 2018
ERATOSTHENES WA KIRENE: MWANAHISABATI ALIYEISHI AFRIKA NA KUKADIRIA MZINGO WA DUNIA KWA KIVULI CHA MWANZI.
Na Kizito Mpangala
Eratosthenes alizaliwa mwaka 276 KK
(Kabla ya kuazaliwa Yesu Kristo) mjini Kirene, Libya ya sasa. Kirene ni mji
mashuhuri ulioundwa na Wagiriki wa kale walioishi Afrika ya Kaskazini hasa
Libya ambako ndiko ulikokuwa mji wa Kirene maeneo ya Tripolitania ( sasa ni
Tripoli), na Misri maeneo ya Alexandria ilikokuwa maktaba mashuhuri iliyotumiwa
na wataalamu wengi wa Ugiriki ya kale.
Alikuwa akifanya mazoezi mbalimbali ya viungo kila siku asubuhi na jioni. Alijifunza kusoma, kuandika, na kuhesabu. Ni kama vile falsafa ya elimu ya msingi inayotumiwa nchini Tanzania yaani KKK (Kusoma, Kuandika na Kuhesabu). Pia, alijifunza uandishi wa mashairi na vilevile masuala ya muziki.
Alikuwa akifanya mazoezi mbalimbali ya viungo kila siku asubuhi na jioni. Alijifunza kusoma, kuandika, na kuhesabu. Ni kama vile falsafa ya elimu ya msingi inayotumiwa nchini Tanzania yaani KKK (Kusoma, Kuandika na Kuhesabu). Pia, alijifunza uandishi wa mashairi na vilevile masuala ya muziki.
January 19, 2018
TAITU BETUL: MALKIA JASIRI ALIYEASISI MJI MKUU WA ETHIOPIA, ADDIS ABABA.
Na Kizito Mpangala
Taitu Betul alizaliwa mwaka
1851 nchini Ethiopia ambayo wakati huo ilikuwa ni Milki ya Ethiopia kabla ya
kuwa Jamhuri. Neno Taitu kwao
lilimaanisha “mng’ao wa jua au jua”, hilo ndilo lilikuwa jina lake la
asili.
Baada ya kubatizwa katika
kanisa la dhehebu la Orthodox aliitwa Walatta Mikael, lakini baadae alilirudia
jina lake la asili yaani Taitu Betul. Baba yake alikuwa aliitwa Betul Haile
Maryam ambaye alikuwa na uhusiano na ukoo wa Mfalme Sulemani. Lakini baba yake
huyo hakufahamika sana kama alivyofahamika mjomba wake aliyeitwa Dejazmach Wube Haile Maryam, ambaye
alikuwa mtawala wa Ethiopia Kaskazini miaka ya 1840.
Familia ya baba yake Taitu
ilikuwa imeweka makazi yake katika mkoa wa Semien ambao ulikuwa ukitawaliwa na
Mfalme Susenyos I. Baba yake alikuwa ni mjukuu wa Ras Gugsa ambaye alikuwa
mshirika wa familia iliyotawala eneo la Yejju iliyokuwa na asili ya kabila la
Oromo. Baba yake huyo alikuwa Muislamu na baadae akabadili dhehebu akajiunga na
Ukristo.
Taitu Betul alikuwa na nafasi
kubwa ya kuwepo katika ngazi za juu katika maeneo hayo kutokana na ndugu zake
wengi kuwa katika nafasi za milki mbalimbali hasa katika ngazi za mikoa.
Taitu Betul aliolewa mara nne
na kuachwa kabla ya kukutana na Mfalme Menelik wa Shewa kama mke wa tatu. Muda
mfupi baadae, baada ya kuolewa na Mfalme Menelik wa Shewa, Mfalme huyo
akatawazwa kuwa Mfalme wa Milki ya Ethiopia (Ethiopian Empire). Taitu Betul
akiwa kama Malkia pamoja na mumewe Mfalme Menelik II walikuwa wanamiliki
watumwa elfu sabini (70,000).
Madhumuni
elimu,
Historia,
kumbukumbu
January 15, 2018
ELIMU BURE INAVYOTESA WATOTO WA WANANCHI WA HALI YA CHINI
NA HONORIUS MPANGALA
KITAALUMA na hisia zangu
zimenifanya niwe mtu tofauti kabisa kuhusiana na matumizi ya baadhi ya maneno
hapa nchini. Mengi hutumiwa na viongozi wa ngazi za juu kuwaona wale waliopo
chini au wasio na vyeo kama wao kuwa
wenye kiwango fulani cha dhiki kinachostahili kuitwa cha chini. Ni hapo
ndipo nakuwa na hisia tofauti sana juu ya kutumia maneno fulani dhidi ya kundi
jingine hasa lile ninaloongoza au viongozi wanaloliongoza.
Japokuwa nimekuwa mtu nisiyependezwa
na na hili neno “Wananchi wa hali ya chini”' lakini najiuliza hao wa hali ya
juu ni akina nani, wanafanya nini kutokuwa na hali ya chini na njia zao zikoje
ili tuwaambie wa hali ya chini wajifunze kwenda huko juu?
December 30, 2017
VITABU 50 NILIVYOSOMA MWAKA 2017
NAWASILISHA orodha ya vitabu
nilivyosoma mwaka 2017. Ukitazama orodha zangu za usomaji vitabu utabaini kuwa
ya mwaka imeongezeka. Nimesoma vitabu 50 na kuna mabaki kadhaa hayaguswa
kabisa.
Mwaka 2017 nimejikuta nikiwa nimeongeza
uwezo wa kusaka maarifa zaidi kutokana na ongezeko la vitabu ingawa sina
desturi ya kupanga idadi yake.
Kwa mwaka 2018 ninatarajia
kuongeza maarifa zaidi katika vitabu vya biashara na uchumi, lakini haina maana
nitasoma vingi kuzidi ‘ala za roho” (riwaya). Pamoja na changamoto za majukumu
na mengineyo, suala la vitabu limebaki kuwa nyeti maishani mwangu.
Subscribe to:
Posts (Atom)














