December 17, 2013

NDUGU ZANGU WANYASA NAWAPENI CHANGAMOTO



Na Bahati Chiombe, ARUSHA

WAHENGA walisema kuuliza si ujinga na aghalabu aulizaye anataka kujua. Wilaya ya Nyasa ni mpya na bila shaka yoyote inahitaji nguvu za wanyasa wenyewe katika kuleta maendeleo. 

Ningependa kuwauliza vijana wanawake kwa waume mmejiandaa vipi kupokea fursa uwekezaji? Nasaha zangu mjitahidi kuwa waaminifu kwa sababu Wanyasa waishi mijini watakapoitikia na kuwekeza ktk sekta mbalimbali UVUVI, KILIMO, UFUGAJI, UJENZI n.k atakuwa anatuma pesa kwa ajili ya mradi mliokubaliana kwa hiyo inahitajika uaminifu wa kina na taarifa za kweli.

Wengi huzongwa na kazi au shughuli za mijini na muda wa kuja huko mara kwa mara wanaukosa.Na kama kweli huko Nyasa wengi watakuwa waaminifu naamini wengi watajitokeza kuwekeza Nyasa na mzunguko wa pesa utaongezeka na uchumi kukua siku hadi siku.

Osati mtaji ndi faida vhonje vithela kumoa ndi kumadaba wachikazi asano asano.Zhikom sitimapezane mawa tulo sazino.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako