October 02, 2017

NI VIGUMU KUREJESHA ZAMA ZA RTC NA RELI KIGOMA.

NA. HONORIUS MPANGALA
WENGI wanapajua kwa jina la utani mwisho wa reli. Ni kigoma mkoa wa kanda ya Magharibi ukiwa na sifa kemkem katika kila nyanja iwe medani ya siasa,sanaa na hata soka. Kabila la Waha ndio wenyeji wa mkoa huo lakini yako makabila mengine. Wako wabembe na wanyema pia. Moja ya nyimbo bora za bongo fleva 'Leka tutigite' wa Kigoma All stars ni kati alama ambayo inatumika kuutambulisha mkoa huo.Hifadhi ya Gombe na Mahale ambayo ina sokwe ni miongoni mwa kivutio , pia meli kongwe duniani iliyoundwa na wajerumani mwaka 1913 katika maandalizi ya Vita ya kwanza ya dunia MV Liemba iko Kigoma na ingali inafanya kazi hadi Leo.
Umati wa wapenda soka mkoa wa Kigoma wakitazama mechi ya fainali ya mashindano ya kugombea ng'ombe katika uwanja wa Lake Tanganyika.

 
Historia ya Tanzania katika soka inakwenda sawa kama utautaja mkoa huo kwa kubainisha vilabu vilivyo wahi kufanya vyema zamani. Unaweza kujiuliza kwanini wakati huu ambapo soka linahamasa sana hawa watu hawana timu ligi kuu kwa jinsi walivyo na vipaji lukuki. Unapoitaja kigoma katika soka unawataja watu kama Saidi Suedi 'Scud', Makumbi Juma 'homa ya jiji', Edibily Lunyamila, na wengine wengi. Ukitaka mchezo wa ngumi huko ndiko alikotokea Japhet Kaseba.


Ukitaka Siasa huko ndiko alikotoka Zitto zuberi Kabwe na David Kafulila. Ukitaka kufahamu kuhusu muziki huko ndiko nyumbani kwa Ali kiba, Baba levo, Banana Zoro, Peter Msechu, Sunday Mjeda, 'Linex linenga', na Nasib Abdul 'Diamond'.

Wakati mkoa huo ukionyesha kuwa na vipaji lukuki jambo pekee linashangaza wapenzi wa masuala ya soka kwanini hakuna timu ya ligi kuu Kigoma. Nilifika Kigoma Mwezi sita na kuchikonoa hoja ya ukosefu wa timu ligi kuu na wadau na wapenzi walieleza mengi. Nikiwa nayapima maelezo yao nikaishia kutulia na kuhitaji muda tena. 

Nilifika tena Kigoma mwezi wa tisa huu, siku zangu tatu zimetosha kujua maswali yangu niliyouliza miezi mitatu iliyopita kwa watu tofauti na sasa nimejibiwa vilevile na watu tofauti. Msukumo wangu wa kujua haya yamekuja kutokana hali halisi iliyopo kutofanana na zama za Vilabu vya RTC Kigoma, Reli Kigoma katika soka la nchi hii. Nyakati zile ziliufanya mkoa huo kuonekana kuwa na timu ngumu na zenye vipaji halisi vya soka. Uwepo wa mashirikia yaliyojihusisha na soka ndiko kuliko itambulisha timu za shirikia la kibiashara kama RTC Kigoma,Kagera na Shinyanga.

Kwa kiasi kikubwa hamasa ya wadau na imani yao pamoja na kujitoa kwao kuliwafanya viongozi wa shirika kuona wanaweza kulitumia soka kama kutengeneza alama katika mkoa huu. Uwepo wa Afisa biashara na masoko wa mkoa mpenda soka ndiko kulikofanya timu kama RTC Kigoma kufanya vyema.
Haikuwa kwa RTC pakee bali kulikuwa na klabu ya Reli Kigoma iliyokuwa chini ya shirika la Reli Tanzania.Klabu hiyo iliyonunuliwa toka kwa klabu ya Kongo fc ambayo ilinunuliwa na kubadilishwa jina na kuwa Reli Kigoma. 

Utulivu wa nchi za Burundi na Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo ni kati ya mambo yaliyosaidi kuinuka kwa soka la mkoa huo . RTC walitegemea wafanyabiashara toka nchi hizo mbili katika masuala ya biashara ambayo yalifanya shirika kuimarika kiuchumi na kuwa na nguvu hata uuendesha timu. Uwepo wa Bandari na Reli ulifanya nchi jirani kutumia bandari ya Kigoma kama njia sahihi ya kupitisha mizigo yao na hilo lilifanya timu kutengeneza kipato na kuendeshwa vyema.

Mdororo wa kiuchumi kwa watu wa Kigoma kunatokana na hali ya nchi jirani na kufanya watu kutofikia malengo wanayojiwekea. Waliokuwa wakizamini na kutoa pesa kwa ajili ya vilabu kama vya Reli na RTC. Kukosekana kwa imani kwa viongozi wa soka nako ni sababu iliyofanya wadau kujiweka pembeni na kutokuwa na imani na viongozi wao.

Kwa asilimia kubwa watu wa mataifa ya Kongo na Burundi huitumia Kigoma kama sehemu ya kufanyia Biashara na kurudi kwao. Vilabu kutokana na kuwa vyenye kuhitaji michango toka kwa wadau na wapenzi wa soka. Mmoja ya wadau ananiambia "kigoma kuna uswahili sana ndo maana soka linatushinda miaka hii".

Hali ya uswahili inanifanya miweze kujua mengi ambayo yanachangia kutokufanikiwa kuwa na timu ligi za juu.Watu hupenda kuchuma matunda pasipo kushirikia katika kujenga vilabu vyao.Maendeleo ya soka katika eneo husika yanahitaji watu wanaojitoa kwaajili ya timu. Hali hii imekuea tofauti na wenyeji wa Kigoma kwa sasa.Jambo linalochukuliwa ni kutokuwa na imani na kila mtu anayejihusisha na soka kwani fikra za wengi ni kwamba watu hujinufaisha wenyewe pasipo kuzisaidia timu.

Uhalisia wa yanayoendelea Kigoma ndo hayo yaliyo ifanya klabu ya Mvuvumwa kuhama toka kigoma kwenda Dar Es salaam. Msimu uliopita klabu hiyo ikiwa katika ligi daraja la kwanza ilipata wakati mgumu kwa mechi zake za nyumbani. Uwanja wa lake Tanganyika kwao ilikuwa kama wako ugenini. Mashabiki na wenyeji wa mkoa huo waliizomea na kuzishangilia timu wageni ili klabu hiyo isisonge mbele.

Unaweza kushangaa kwanini usaliti wa klabu ya Mvuvumwa ulikuwa hivi. Lakini jibu lenye kueleweka masikioni mwa watu ni chuki zilizojengeka toka kwa viongozi wa soka kigoma pamoja na viongozi wa taasisi za kiserikali ambao kwa pamoja walikuwa na lengo la kuifanya Mvuvumwa iwe chini ya KRFA ikipata sapoti kubwa toka serikali ya mkoa na idara ya ulinzi na usalama ya mkoa. 

Matarajio hayo yaligonga mwamba kwasababu mmliki wa klabu alishajua kuwa wanataka kuochukua timu na kuifanya kuwa chini ya chama soka mkoa na mwisho wa siku I we kama kilichozikuta RTC na Reli Kigoma. Viongozi wengi wa soka la Tanzania katika ngazi ya klabu,mikoa na hata nchi wamekuwa na hali ya kutumia nafasi hizo kujinufaisha katika maisha yao. Hii ndiyo iliyokuwa 'target' namba moja ya watu wa kigoma kwa Mvuvumwa fc. Viongozi wakaamua kumwona mmliki wa Mvuvumwa kama ni msaliti wa maendeleo ya soka la kigoma na kufanya timu ichukiwe na mashabiki.

Hali hii imefanya timu hiyo kuhamia makao yake Dar es salaam. Na kwa kauli za wenyeji ambao ni wadau wakubwa wa soka la Kigoma wanasema hata kama Mvuvumwa ihamie ligi ya Kenya kamwe haiwezi kupanda daraja. Kauli hizo zinafanya nione kuna hali ya kutoitakia mema kwa kolote kwasababu ya mmiliki wa klabu kutotaka kuikabidhi klabu kwa viongozi wa soka mkoa.
Kwa lililomkuta Mvuvumwa halitofautiani sana na lililowakuta Jkt Kanembwa. Baada ya kuonekana uongozi wa klabu wote ni wa wanajeshi wale raia ambao wamekuwa waibua hoja nyakati zote wakaanza kuwataka wachanganye viongozi wa kiraia ili kuweza kuleta hamasa ya sapoti toka kwa mashabiki ambao ni raia. 

Wakiwa na mtazamo huo kumbe jambo lililojificha ni kwamba watu wanatafuta upenyo wa namna ya kuingia kwenye mfumo na kuwashawishi timu ishikiliwe na Viongozi wa chama cha soka mkoa. Na malengo makubwa yanakuwa yaleyale kuzitumia klabu kujinufaisha kimaisha.

Watu kama Said Sued 'Scud' walifanikiwa kuingia katika mfumo wa kiungozi ndani ya jkt kanembwa. Kilichoendelea ni klabu kuwa na mwenendo usiolizisha na watu kutumia klabu kama kitega uchumi na sasa inapambana ligi daraja la pili.Kilichotokea kwa Kanembwa ndicho kilichokuwa kikimpa wasiwasi mmliki wa Mvuvumwa anayefahamika kwa jina la Dk. Yared.

Licha ya kuwepo kwa hali ngumu kwa uchumi wa mtu moja mmoja na akaweza kuchangia katika klabu ili kuziinua na kuleta maendeleo ya soka lakini viongozi wamekuwa wasio aminika mbele ya mashabiki wao. Msuguano wa nani zaidi kati ya wale wadau wa soka wa maeneo ya Mwanga na wale wa maeneo ya Ujiji nayo ni saababu ya kutokupata mafanikio kwa vilabu vyao kwa miaka ya sasa. Hali hiyo inatokana na kila upande kuona wako bora katika kuufahamu na kusimamia vyema soka kitu ambacho kinaleta au kupitisha mianya ya figisu kwa upande wa pili.

Jambo pekee na lenye umuhimu mkubwa Kigoma wanahitaji mabadiliko makubwa ili kuondoa dhana iliyoko kwa wapenzinna wadau zidi ya viongozi wa soka la kigoma. Japo wako wanaoamini uchumi wao kushuka na watu kushindwa kuchangia maendeleo ya vilabu sababu ya mambo ya Mashariki mwa Kongo na Burundi. Napeleka fikra mbali zaidi mbona Sudani soka linachezwa vyema ilihali maeneo mengine kukifanyika mapigano.

Uimara wa viongozi na wenye kutaka maendekmleo ya vilabu vyao ndio jambo linalopaswa kuwa kichwani mwa viongozi. Soka la eneo husika husimamiwa na kupandishwa na wenyeji wa eneo hilo. Haiwezi kutokea mtu wa Singida akaenda kusimamia maendeleo ya soka la Kigoma. Inaweza Ndanda Kuwa na timu ligi kuu lakini Kigoma wakakosa kwasababu ya kupingana kwa fikra kati ya wadau na viongozi kuzalisha chuki miongoni mwao.

Soka halina njia ya mkato,linahitaji njia iliyonyooka na yenye kuekeweka uelekeo wake. Siasa inapitumika katika soka majibu yake ni kukosekana kwa imani miongoni mwa wapenzi na wadau wa soka.
 
0628994409

No comments:

Post a Comment

Maoni yako