December 27, 2017

NYASA; DISEMBA 20 ILIPONIREJESHA MIAKA 13 ILIYOPITA

NA HONORIUS MPANGALA, LUNDU
TULIANZA safari yetu na dadangu kijijini kwetu Lundu na kuelekea Halmashauri ya Wilaya ya Nyasa Mbamba Bay. Changamoto za barabarani hazikukosa kwasababu ya mvua zinazonyesha. Tukifika na kukamilisha yaliyotupeleka huko. 

Saa kumi jioni nilipofika kituo cha mabasi cha Mbamba Bay sikukuta gari ya kugeuza kwenda kwetu Lundu. Ikatulazimu tupande ya kuishi njiani, gari iliyotoka Mbinga kwenda Kihagara. Nikiwa nawaza namna ya kutoka Kihagara hadi Lundu lakini nikapanga jambo kuwa bodaboda ziko kila eneo sikuhizi,na sikutoa nauli ya yangu na Dada nikamwambia waambie natoa Mimi. Nikamwambia konda natoa Kihagara kuna mtu anatusubiri,nilifanya Kwa maksudi.

Tulipofika Mlima wa Yungu tukielekea Kihagara dereva akasema kuna dalili ya kunyesha mvua hivyo sitawafikisha Kihagara stendi bali nitaishia Camp yaani njia ya panda ya Kihagara na Malongo. Tulipofika Waliposema mimi nikatoa nauli pungufu ya elfu na mia tano nikagoma kutoa yote kwasababu sikufikishwa Kihagara.
Nilipowagusa bodaboda kutifikisha Mimi na dadangu Lundu waligoma,niliwabembeleza wakagoma. Nikamwambia Dada tutafanya mazoezi. Ilikuwa ni saa 2:05 tukitoka Camp tukaanza kutembea hadi Nindai kwa kupitia njia ya Malongo. Milio ya Wanyama kama Komba ndo ilikuwa mziki wetu,wadudu pori nao kama kawaida Kwa sababu ilikuwa ni milimani katika msitu.
Sista aliogopa nikamwambia hakuna jinsi nimevaa Rozari ambayo niliitoa na shingoni na kuvaa mkononi. nikaanza na kupiga vifungu pale safari ya kutembea ikaanza. Tulikutana na watu wawili eneo moja majira ya Saa tano na Nusu wakiwa wanatoka kulewa. Hapo Dada alinishika mkono nikaanza kucheka maana nilimwambia mbele yetu kuna watu wanakuja. Eneo tulilokuwa jumlisha usiku ule ndo kilichoogofya.
Nikamwambia hatuna jinsi lazima tufike nyumbani haraka iwezekanavyo kwasababu ya kile tulichokiendea kuwa na umuhimu mkubwa na thamani kubwa. Ni kama tulipewa dhamana na familia fikieni na kurejesha taarifa iliyotarajiwa.
Tukiwa tumeimaliza milima tunakaribia kufika kibao cha shule ya Liwundi saa 5: 55 usiku tukakutana na Mzee aliyebeba kafia akitoka ziwani. Nipogundua nikawa napita kwa ukaribu zaidi ili kuweza kutambua ni wa aina gani. Muda sio tatizo ila mashaka ni eneo lenyewe.

Dada akauliza hapa wapi nikamwambia hii Nindai punde tunaianza Yola. Tulitembea huku Dada akiwa ana kiu ya maji nami nikamkataza kunywa maji ya mtoni kwani yalikuwa machafu. Ilikuwa nampa matumaini kuwa utakunywa Hapo mbele. Kiujumla aliingia disko la kimasai kwa kusafiri na Mimi. Alichoka nikamwambia haya ndiyo majukumu uliyopewa na kilichobebwa kinahitajika na muhimu sana kwa mustakabali wa maisha yetu na ni haki yetu sasa usisikitike juu ya kusumbuliwa na changamoto kama hizi kwani utawasimuliwa wale wataotaka kujua ulifanikiwa vipi hili zoezi.

Tulipita shule ya Yola, palepale nikakumbuka nilipokuwa kule milimani kuna ‘comment’ ya kaka Atley Mpangala kuwa nikifika Yola niulize jambo. Licha ya kuwa usiku mkali wa saa Sita nikasimama na kuhesabu Fremu ambazo kaka huyu aliniagiza hapo nikajua zipo 12. Tukatembea kidogo tukakutana vijana wanne wanatoka ziwani kuvua dagaa sikuwasemesha. Tulipofika mbele kidogo nikaona nyumba wakazi wake wako nje wanashughulikia dagaa nikamwambia Dada twende ukanywe maji sasa.
Kutoka kushoto kwenda kulia, Honorius, Emma na Thobias Daudi.
Dada alipokunywa maji nami nikanywa, tukaulizwa swali mbona usiku mnaenda wapi nikajibu tunaenda Tughi alfajiri tutaenda Lundu, sasa tukishuka gari Camp na bodaboda walikataa kufanya biashara nasi ikabidi tutembee. 

Hapo Dada akaniambia ni saa 6:48 usiku. Nikamwambia mama mwenye ile nyumba kuwa naomba kujua mmiliki wa zile fremu pale shule akajibu Serikali ya kijiji. Nikamwachia agizo kuna kijana anahitaji kujua gharama za pango anaitwa Atley Mpangala yuko Dar es salaam. Akaniambia ile familia naijua kesho nikiamka nitamuuliza Mtendaji na nitapeleka jibu kwa nduguze ili wampigie simu. Alipouliza mbona unamtaja huyo kijana unamjua nikamjibu Mimi ni Mpangala na nawafahamu wenzangu pia.

Tukaendelea na kufika Mkili (Tughi) saa 7:13.Nikamwambia Dada gari hii tutapanda inayoenda mjini hivyo tupumzike. Tukaingia ndani ya gari na kusubiri kupambazuke gari ianze safari ya Songea kupitia kwetu. Huwezi amini gari ikaanza kuondoka saa 8:40 usiku daaaaa(Kuna watu wanapata changamoto halafu kuna anayejiita mbunge wao kudadadeki anakoroma tu mjini huko). 

Tulitembea nasi tukafika home saa 10:50 tulipofika home moja kwa moja tukapitilizia kulala ili asubuhi tufanye kazi iliyotufanya turudi home kwa changamoto lengo kufanya mambo kwa maagizo ya wale waliotuagiza.

Nawaonea sana huruma Nyie wapiga kura za wabunge wa maeneo kama haya. Bila kuwapigia kelele hakika hakuna kitakacho badilika. Hapa utagundua moja ya changamoto iliyojitokeza ni usafiri gari moja ikienda basi wewe utasubiri. Sasa ukiwa na uharaka wa kutatua yale yaliyombele yako utahitaji kulazimisha.
Bodaboda nao wakawa waoga wa kutufikisha tutakako kwasababu ya Usalama mdogo kwao kwani barabara ina changamoto sana. Tulichofanya na dadangu ni kuvaa ujasiri na kusema tutafika salama na mungu alijua hawa wamebeba msalaba wa wenzao acha niwalinde wafike.

Halafu mnasema hii serikali ya hapa kazi tu. Kazi gazi zinafanyika wapi hizo kazi mbona wengine hawazioni. Muulize mbunge anayejiita Injinia una pendekezo gani la kiwanda kupitia kwa uwepo wa Ziwa Nyasa na kustawi Kwa mazao ambayo yanaweza kufanya watu wakanufaika na kiwanda atao macho tu. Halafu unakaa bungeni kupiga makofi.  

Nimebahatika kufika mikoa 20 ya Tanganyika kila sehemu kuna changamoto zake lakini watu wanaongea wanapiga kelele ndo maana wanafanyiwa kazi ambazo wanaambiwa hapa kazi tu. Utafikiri tumelekezwa kuanzia serikali Kuu hadi za Mitaa. 

Maendeleo ya Nyasa ni kwa mwananchi mwenyewe lakini sio kwa huduma ambazo serikali inatoa kwa wananchi. Ndo maana sijashangaa kukuta Benki ya NMB hadi sasa kuendea kuhudumia kwenye gari pale mjini Mbamba Bay.

Inaumiza halafu watu wanaishia kusifiana tuu mbele ya kamera na kusema naunga juhudi za Fulani sijui... Hivi mnayajua Maisha ya wamachi kweli?  Eti Injinia Manyanya unataka kuniambia kwa huu nusu msimu wa uongozi wako kama mbunge umefikia nawe nusu ya ahadi zako? 

Tanzania ya nyerere tutaishia kuisoma katika makaratasi , umimi utabaki kuwa palepale....NIMESEMA. Nimechafukwa na nyongo balaa ngoja nimpigie simu wife kwanza!

No comments:

Post a Comment

Maoni yako