December 27, 2017

...KUMBUKIZI ZA MZEE MPANGALA NA WAMISIONARI WABENEDIKTINE LUNDU



Mwaka 1931 Wamisionari waliomba eneo la kujenga himaya yao ya kitawa kwa serikali ya kijiji cha Lundu. Baada ya pendekezo lao serikali iliwaomba wazee wawili kutoka Ukoo wa Mpangala ili kuwapa Wamisionari hao eneo la kujenga makazi ya Kitawa.
Alikuwa Mzee Machwembeli Mpangala (Baba yake Mzee Hansgary Mpangala au Waziri) na Lipondelu Mpangala (Babu yake Mzee Hubungu au Robert Mpangala).Mzee Machwembeli alikuwa anamiliki eneo la kuanzia kilipo kituo cha afya kuelekea kaskazini( Kwa wale wanao ifahamu Lundu) na Mzee Lipondelu alitoa kuanzia Hapo kituo cha afya kuelekea Kusini iliko nyumba ya mapadre.
1959 Walijenga machine ya kupump maji toka forodha ya Chivanga hadi eneo la misheni.Mzee alishiriki ujenzi Huo akiwa na Bruda Lambert. Ananiambia gari ya kwanza kufika kijijini kwetu ilikuwa ni 1954.
Asubuhi ya Leo alinipiga na salamu ya kijerumani nikabaki natoa macho tu.Uishi miaka mingi zaidi Mzee wangu.

Honorius Mpangala,
#Mtoto_Wa_Misheni

No comments:

Post a Comment

Maoni yako