November 04, 2017

TANZANIA YATAJWA KUONGOZA KWA MARADHI YA KIPINDUPINDU


NA MWANDISHI WETU

SHIRIKA la Afya Duniani imeitaja Tanzania kuwa  miongoni mwa nchi kumi kinara kwa watu wake kuugua ugonjwa wa kipindupindu. Mataifa  mengine yaliyotajwa ni pamoja na India ambayo ndio inayoongoza. Nyingine ni Haiti, Jamhuri  ya  Kidemokrasi  ya  Congo, Tanzania, Bangladesh, Uganda,  Msumbiji na Kenya, ambayo ilikumbwa na mlipuko mkubwa wa maradhi hayo kwa nyakati tofauti mwaka huu.


Katika ripoti yao iliyotolewa hivi majuzi, imesema kuwa sababu kuu ya kuandamwa na maradhi hayo ni kukithiri kwa mazingira machafu katika mataifa hayo.

Ripoti hiyo inasema kuwa watu bilioni 1.2 sawa na moja ya sita ya watu wote duniani wako hatarini kukumbana na maradhi hayo hatari.Wakati Bara la Afrika likikumbwa na kadhia hiyo kutokana na unywaji wa maji yasiyofaa, hali ni tofauti kwa  Ulaya na Amerika ya Kaskazini ambako mifumo imara ya maji taka imeyafanya mabara hayo yawe huru na kipindipindu kwa miongo mingi sasa. Lakini watu zaidi ya bilioni mbili wamebakia bila maji safi na mifumo ya maji taka.

Hivyo, kipindi pindu kinaendelea bila huruma kuathiri watu masikini zaidi duniani na ndani ya kila nchi athirika. Kwa sababu hiyo, Shirika la Afya Duniani (WHO) limeunda Kikosi Kazi cha Kudhibiti Kipindupindu Duniani (GTFCC), ambacho kinazileta pamoja taasisi zaidi ya 50.

Lengo la GTFCC ni kuongeza juhudi za kuimarisha ushirikiano wa kupunguza vifo kutokana na maradhi hayo kwa asilimia 90 ifikapo mwaka 2030. WHO limeeleza matumaini yake ya kupunguza kwa kiasi kikubwa maambukizi ya ugonjwa huo na idadi ya vifo vitokanavyo ifikapo kipindi hicho.

Mkurugenzi anayehusika  na masuala  ya dharura katika  shirika  hilo, Dk. Peter  Salama  alipokuwa akizungumza  na  waandishi habari  mjini  Geneva, Uswisi hivi karibuni,  alisema  shirika  hilo  lingeweza kuchukua  hatua  za  haraka  na  kutuma  chanjo  zaidi  ili kupambana  na  ongezeko  kubwa  la  maambukizi  ya ugonjwa  wa  kipundupindu nchini  Yemen  mwaka  huu.

Lakini pia ameeleza matumaini  yake kwamba, ‘tunakaribia  kufikia lengo,’ kuhusiana na ugonjwa  huo  unaoweza  kuzuilika, ambao umefikisha maambukizi  ya  watu  700,000  na  kusababisha  zaidi  ya vifo  vya  watu 2,000 mwaka  huu.

Lengo  ni moja  kati ya malengo makubwa ya WHO  kuutokomeza  kabisa ugonjwa huo ama kuupunguza  kwa kiasi kikubwa.Juhudi kama hizo tayari  zinafanywa dhidi ya ugonjwa  wa  kupooza, malaria, surua, na Ukimwi. 

Hivi  sasa, ugonjwa wa tete kuwanga ni pekee unaoelezwa umekwisha tokomezwa katika uso wa  dunia na hivyo kubakia katika vitabu vya historia.
India na nchi zilizoko Kusini mwa Jangwa la Sahara Afrika  zinakabiliwa na  changamoto ya muda mrefu ya kupambana na kipindupindu.

Maeneo kama Yemen inayokabiliwa na vita, ama Bangladesh, ambayo iliwapokea zaidi ya wakimbizi 500,000 Waislamu wa  Rohingya kutoka Myanmar, inakabiliwa  na  hali  ambayo  haitabiriki kwa  urahisi.Kwa sababu hiyo, mpango  huo  wa kimataifa unalenga  katika  kupambana na maeneo yanakozuka mlipuko wa ugonjwa huo  kila mara, ambako kila  mwaka  katika  wakati  ule ule, ugonjwa  huo hutokea. 

Mpango  huo  unalenga  kuboresha  usafi  wa maji na mifumo ya maji safi na maji taka pamoja na kutumia  chanjo za kunywa. Mkakati  huo unaweza  kusaidia  kutokometa  kipindupindu katika mataifa  20 yaliyoathirika  ifikapo mwaka 2030, kwa mujibu  wa  WHO. 

Hata hivyo, Shirika la WaterAid limeitaja nchi ya India  kuwa imeathirika kwa  kiasi kikubwa ikiwa  na  zaidi  ya kesi  za  maambukizi 675,000 kila mwaka.
Pia  ina idadi  kubwa  ya  watu  wanaoishi  bila  ya kuwa  na uwezo  wa  kupata  maji safi na  salama na  wengi wanaishi  bila  kuwa  na  vyoo sahihi.

Maeneo ya mijini yakiwa na maji machafu, ambayo yanaweza kuingia katika vyanzo vya maji na kusababisha magonjwa nchini Msumbiji,
Ethiopia na Nigeria,  ambazo  zinafuatia katika  nafasi ya pili na  tatu pia zina  idadi ya juu ya pili na  ya  tatu ya  watu  wanaoishi  bila  maji  safi.
Miongoni mwa waathirika walikuwa askari polisi zaidi ya 30, ambao walijikuta wakilazwa hospitali baada ya kula kile kinachodaiwa chakula xchenye mambukizo katika moja ya migahawa ya jeshi hilo

No comments:

Post a Comment

Maoni yako