October 17, 2017

UTAMU WA WIMBO WA TAIFA UKO KOMBE LA DUNIA.

NA. HONORIUS MPANGALA
 
ILIKUWA miaka Sita ya Ubabe wa soka barani Afrika kuanzia mwaka 2006 hadi 2012. Kila mpenzi wa soka alimfahamu Hassan Shehata,kila mpenzi wa soka alimfahamu Waile Gomaa. Ilikuwa nyakati za Misri kunyanyasa mataifa mengine ndani ya bara la Afrika. Ilimchukua Kameruni miaka tisa kulipiza manyanyaso aliyopata toka kwa Misri ya kiumeni mwaka 2008 pale Ghana.
Ni Misri ambayo iliipa hasara CAF kuunda kombe lingine la Afcon baada ya kulibeba lile awali Mara nne Mfululizo. Mwaka 2006 fainali zilizoandaliwa na Misri wakikutana na Ivory coast ya Didier Drogba.
KIKOSI CHA MISRI

Fainali ile iliisha kwa matuta na wenyeji kutwa taji. Licha ya kuwa na kikosi ambacho kilikuwa na vijana taklibani Saba wakitoka kikosi cha Al Ahly ambayo ilikuwa moto wa kuotea mbali. Hapa nawazungumzia Mohammed Barakat,Saeed Moward,Essam El Hadary,Ahmed Hassan,Hossam Hassan,Mohammad Mido,Mohammed Aboutrika na wengineo. Ilikuwa ni kikosi kilichojaa vipaji kikiwa na hamasa kubwa kutoka kwa kocha mzawa Hassan Shehata kiliwafanya wapinzani wafikirie Mara mbili zaidi.


Ukuta ulioongozwa na Waile Gomaa ilikuwa kama unakutana na Rio Ferdinand wa nyakati za Vodafone na Manchester Utd yake. Beki mmoja chuma halafu bedui anacheza kibabe kiasi kwamba hupati nafasi ya hata kumiliki mpira kama mshambuliaji. Kwa lugha za sasa za mtaani unaweza kusema 'ana kuvugaa' kama ulivyo.

Si mnakumbuka Zengwe la Hassan Shehata na Mido katika Nusu fainali ya afcon iliyowalutanisha Misri na Senegal 2006. Ilikuwa Senegal ya vipaji haswa. Kuna nyakati unaweza kukaa na kutoa majibu kuwa soka la kipaji limeondoka miguuni mwa wachezaji tunao watazama sasa. 

Lile zengwe ilikuwa baada ya Kufanyika mabadiliko yaliyomuingiza uwanjani Amri Zaki na kumtoa Mido. Mwarabu yule hakufurahishwa aligombana kwa maneno na kocha wake. Ajabu ya mwenyezi Mungu Zaki akafunga bao lililowapeleka fainali na kumwacha Mido akishindwa kushangilia huku Shehata akimwonyeshea kidole katika kichwa chake akimaanisha akili.

Licha matukio matamu yenye kusisimua kwa nyakati za zote za Ubabe wa Misri jambo pakee ilikuwa kizazi hicho hakikufanikiwa kufuzau kombe la dunia. Asikudanganye mtu hakuna raha kama kuimbiwa wimbo wa Taifa katika mashindano ya kombe la dunia.Misri walijaribu kuitafuta raha hiyo lakini wakaishia kuipata wanapocheza Afcon.

Mara ya mwisho kwa Misri kushiriki ko be la dunia ilikuwa mwaka 1990. Katika fainali zilizofanyika nchini Italia ikawa mwisho wao hadi sasa ambapo Mohammed Sarah anawapeleka Urusi mwakani. Ilikuwa nyakati za utawala wa Hosney Mubarak ndipo waMisri walipoimba kwa pamoja na wachezaji wao wimbo wa taifa pale Italia.

MOHAMMED SALAH

Wakiwa na nahodha na golikipa mkongwe Essam El Hadary Misri wanafuzu huku akiwa na wadogo zake ambao wametengeneza kikosi kilichoandika historia ya Misri tena. Matumaini ya kurudi katika Ubabe wa soka la Afrika yalianza kuonyesha matumaini katika michuano ya Afcon ya mwaka huu pale Gabon. Ukikitazama kikosi chao kina majina maarufu mawili yaani Mohammed Sarah na Mohammed Elneny katika dimba huku kaka yao El Hadary akihakikisha hakuna mpira unaompita na kutinga wavuni.
Juni 8 ilikuwa ya kihistoria kwao baada ya kufanikiwa kutinga faninali za kombe la dunia la mwakani. Magoli ya mawili ya Salah dhidi ya moja la Congo Brazzaville yaliwapaisha na kuwafikisha Urusi. 

Jambo pekee katika Mchezo huo ni goli la dakika ya 90+3 lililofungwa kwa mkwaju wa penati na Salah ndilo lililofanya Misri yote ilindime kwa Shangwe vifijo na ndelemo. Ilikuwa zaidi ya sherehe kila mmoja alijikuta akifurahia matokeo ya Timu ya taifa licha ya tofauti za kisiasa zinazolitafuna taifa hilo kwa maandamano na mapigano ya wanajeshi wa serikali na Waasi.

Ukitaka kujua raha ya kuimbiwa wimbo wa taifa kombe la dunia muulize Serey Die nahodha wa sasa Ivory Coast. Alitoa mchozi wakati wimbo wa taifa unaendelea pale Brazil katika Mechi iliyowakitanisha Ivory Coast dhidi ya Japan. Mchezo ambao wapenzi wengi wa soka ilibidi wasubili hadi kumi za usiku kwa masaa ya Afrika mashariki kumwona Die akiangua kilio.
WAEL GOMAA
Nawaona wamisri wakiangua kilio zaidi ya kile walichoangua pale Misri baada yachezo dhidi ya Congo Brazzaville. Ilikuwa kama ndoto kwa mkongwe El Hadary kutimiza ndoto za kuisaidia Misri kufuzu kombe la dunia. Vilio vya uchungu walivyolia Wamisri pale Sudan mwaka 2009 vimegeuka vilio vya furaha kwa mwaka 2017. Kuna wakati mnaweza kupitia mitihani mikubwa lakini kumbe Mungu anakuwa na maksudi nanyi. 

Ubabe wa Afcon kwa wamisri haukuwapeleka kombe la dunia lakini unyonge wao wa wakati huu unawafanya watimize ndoto na kwenda kuimba wimbo wao wa 'My country' katika ardhi ya Urusi. Utamu wa wimbo wa taifa mchezaji auimbe akiwa kombe la dunia.

Hakuna hoja yoyote ambayo inaweza kumfanya mtanzania akaona kama ni ya kujifunza Kwa kufuzu Kwa misri. Kama kufuzu Kwa Serengeti watanzania walichangiani je kwa Taifa Stars? Unajisikiaje Rais wa Misri kamwaga pesa Kwa vijana wake au unasikia Rais wa Panama kaamua siku moja kufanyika mpumziko ili kuwapongeza vijana wake. 

Misri mmepata mlichokitafuta kwa miaka takribani ishirini na sita. Nendeni Urusi mkawakilishe Wafrika ambao watakuwa wanawachukulia kama timua yao.

0628994409


No comments:

Post a Comment

Maoni yako