September 22, 2017

MV. NJOMBE YATIA NANGA MBAMBA BAY LEO

NA VITUS MATEMBO, MBAMBA BAY

MELI mpya ya mizigo iitwayo Mv. Njombe imetia nanga kwa mara ya kwanza katika bandari ya Mbamba Bay tangu kukamilika kwa ujenzi wake uliofanyika katika bandari ya Kiwira wilayani Kyela mkaoni Mbeya. Meli hiyo itafanya safari zake katika Ziwa Nyasa. 

Meli hiyo ni moja kati ya ahadi za serikali ya awamu ya nne iliyoongozwa na rais mstaafu Jakaya Kikwete. Taarifa zinasema meli hiyo itafanya safari zake katika ziwa hilo ili kurahisisha usafirishaji wa mizigo mbalimbali ya wafanyabiashara ambao walikuwa wakipata shida ya usafiri wa mizigo.
Aidha, imeelezwa kuwa kuanzia wiki ijayo meli nyingine mpya ya abiria iitwayo Mv Ruvuma nayo itaanza safari zake katika ziwa Nyasa. 



No comments:

Post a Comment

Maoni yako