NA VITUS MATEMBO, MBAMBA BAY
MELI mpya ya mizigo iitwayo Mv.
Njombe imetia nanga kwa mara ya kwanza katika bandari ya Mbamba Bay tangu kukamilika
kwa ujenzi wake uliofanyika katika bandari ya Kiwira wilayani Kyela mkaoni
Mbeya. Meli hiyo itafanya safari zake katika Ziwa Nyasa.
Meli hiyo ni moja kati ya ahadi
za serikali ya awamu ya nne iliyoongozwa na rais mstaafu Jakaya Kikwete. Taarifa
zinasema meli hiyo itafanya safari zake katika ziwa hilo ili kurahisisha
usafirishaji wa mizigo mbalimbali ya wafanyabiashara ambao walikuwa wakipata
shida ya usafiri wa mizigo.
Aidha, imeelezwa kuwa kuanzia
wiki ijayo meli nyingine mpya ya abiria iitwayo Mv Ruvuma nayo itaanza safari
zake katika ziwa Nyasa.
No comments:
Post a Comment
Maoni yako