September 22, 2017

USHAURI WA BURE KWA TFF

NA SAMWEL CHITANYA

MOJA kati ya nchi za Afrika ambazo raia wake wanapenda sana mchezo wa kandanda  duniani ni Tanzania. Watanzania wanaupenda sana mchezo Wa kabumbu. Ni mchezo unaopendwa na watu wengi duniani kote. Unaongoza kwa kupendwa.

Bahati mbaya sana pamoja na Watanzania kuupenda mchezo huu bado hawana mipango madhubuti ya kuufanya mchezo huu uwe wenye tija kwao. Mipango yao mingi ni yakucheza mpila na Siyo Mpira kama wenzetu wanavyo Fanya.

Timu yetu ya taifa huwa inashiriki katika kupigania nafasi ya kushiriki mashindano mbalimbali kama vile Kombe la dunia, kombe la mataifa Afrika na kombe la Mataifa ya Afrika kwa wachezaji Wa ligi za ndani.

Timu yetu hushiriki kikamilifu katika kuwania nafasi zote hizo. Tunajiamini kuwa Tuna timu bora ambayo inaweza kufanikiwa kufuzu mashindano yote hayo. Kujiamini siyo jambo baya lakini jitazame na uwezo wako kwanza.
Mara ya mwisho Tanzania kushiriki fainali za kombe la mataifa ya Afrika ilikuwa mwaka 1980. Miaka thelathini na saba(37) sasa imepita tangu tushiriki mashindano makubwa zaidi ya soka katika bara letu.
Kiungo mkabaji wa Taifa Stars, Himid Mao Mkami 


Tangu wakati huo hadi Leo hii tumebaki kuwa wasindikizaji tu ambao tunakamilisha ratiba tu. Hatujiulizi kwanini tunashindwa kufuzu tena kucheza fainali hizo. Kupanga ni kuchagua tusidharau maneno ya wahenga. Walio fanikiwa wote walipanga na baadae wakachagua kufanya moja ya Yale waliyoyapanga kwa utaratibu na hatimaye kufikia lengo. Ndio maana wahenga walisema kupanga ni kuchagua.

TFF wanaweza kupanga sasa na kuamua wapi tuelekeze nguvu zetu katika mashindano haya matatu, Kombe la dunia, Kombe la mataifa Afrika(AFCON) na Kombe la mataifa ya Afrika kwa wachezaji Wa ndani(CHAN). Tupange na kuamua Mashindano gani tunayahitaji kwa sasa na siyo kupambana kupata nafasi katika mashindano yote, hatutaweza fanikiwa kamwe. Na lazima tuanze na mashindano ya ndani ya bara letu kwanza yaani AFCON na CHAN.

Mashindano yetu makubwa kushiriki kwa mara ya mwisho yalikuwa ni CHAN mnamo mwaka 2008 pale Côte D'ivoire. Mashindano Yale yalikuwa yanafanyika kwa mara ya kwanza yakishirikisha timu nane tu kutoka kanda mbalimbali za kisoka. Congo DR ikawa timu ya kwanza kuchukua ubingwa Wa CHAN baada ya kuwafunga Ghana katika fainali. Kipindi hicho kocha Wa Timu ya Taifa alikuwa Marcio Maximo.

Nawashauri TFF tuanze na mashindano ya kombe la Mataifa Afrika kwanza(AFCON). Sisemi kama CHAN haina umuhimu la hasha!! CHAN angalau tumeshiriki miaka tisa iliyopita kwa mara ya mwisho. Tunatakiwa kuwa na mipando madhubuti na AFCON ndio iwe shabaha yetu kubwa. 


Tunaweza andaa timu kwa ajili ya kupambana kufuzu kucheza AFCON kwa miaka mitatu au minne ijayo. Timu yetu inashiriki mashindano ya COSAFA kama waalikwa na CEFAFA pia (ingawa mashindano yenyewe hayana ratiba maalumu). Tunaweza itumia michuano hiyo kuwa sehemu ya kuandaa timu imara yenye uwezo Wa kupambana na kupata nafasi ya kucheza AFCON baada ya kipindi kirefu kupita. 

Kocha wa Taifa Stars, Salum Mayanga

Wakati huo tukiwa tayari tumeshapeleka barua Kule CAF kujitoa kuwania nafasi za kufuzu mashindano yote makubwa barani Afrika kwa kipindi cha miaka mitatu au minne.Kwa kufanya hivyi naamini tunaweza kupata nafasi ya kucheza fainali za kombe la mataifa ya Afrika baada ya muda tutakao jiwekea. Njia mbili zilimshinda fisi, tukubali kuelekeza nguvu zetu zote katika mashindano ya kombe la mataifa ya Afrika.

Timu itakayo andaliwa tuhakikishe inapata mechi nyingi za kujipima uwezo ndani na nje ya nchi. Tuombe kukutana na timu za mataifa makubwa kisoka hapa Afrika siyo kila siku iwe Uganda, Kenya, Malawi, Zambia, Msumbuji, Rwanda au Burundi hapana. 

Kipindi cha Maximo timu ilikuwa inasafiru nje ya nchi na kuomba kucheza mechi za kirafiki pia kipindi hicho timu yetu ilikuwa inacheza mechi za kirafiki na timu za mataifa makubwa kisoka hapa Afrika tunaweza tumia mfumo huo ili kujenga timu yetu. Tuhakikishe mechi za kalenda ya FIFA tunazifuatana vilivyo na ziwe mechi zenye tija ili kujenga timu yetu.

Tunaweza tukadhani uchache Wa wachezaji Wa kitanzania wanao cheza soka nje ya nchi ndiyo sababu la hasha!! Tatizo letu hatuna michuano maalumu ambayo tunaihitaji. 

Botswana, Venezuela ni funzo tosha kabisa. Venezuela wamefanikiwa kufika fainali za kombe la dunia kwa vijana chini ya umri Wa miaka 20 mwaka huu 2017 na kupoteza kwa goli 1-0 dhidi ya England. Kabla ya kufika hapo waliandaa timu yao ya vijana kwa muda mrefu na ilipata mechi za kujipima uweo zaidi ya arobaini. Hatimaye wakafanikiwa kutinga fainali.
Kwa Taifa changa kisoka kama letu hatuna budi kuelekeza nguvu katika shindano moja.

Tukiamua tunaweza, kuongeza timu za ligi kuu kwa madai wachezaji wetu wapate mechi nyingi ilikuwa na timu ya Taifa imara hiyo peke yake haitoshi. Tuamue sasa mashindano gani tunayahitaji na tuanze kujindaa nayo mapema na kuelekeza nguvu zetu zote huko.Bila kufanya hivyo tutaendelea kuwa kichwa cha mwenda wazimu siku zote. Wahenga walisema Ukiona vya Elea ujue vimeundwa.

0674721910.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako