December 09, 2017

NIMEWASILI SONGEA, NAWASALIMU WACHEZAJI WA MAJIMAJI FC

Safari yangu ilianza katika Kituo cha Mabasi cha Morogoro.

Nikiwa na rafiki zangu Jerry Tegete na Six ndani ya uwanja wa Majimaji mjini Songea.
Nilianza safari yangu mkoani Morogoro kwenda Songea. Nimepitia njia ya Iringa, Mafinga, Njombe na kisha kuingia Songea. Baada ya kuwasili hapa Songea, kitu cha kwanza nimewatembelea rafiki zangu wawili ambao ni wachezaji wa klabu ya Majimaji FC ya mjini Songea wakiwa kwenye mazoezxi ya ya uwanja wa Majiamji. Ni Jerryson Tegete na Six Ally Mwasekaga.
Nitakuwapo hapa kwa siku kadhaa, kabla ya kuelelea Ziwani Nyasa. Tukutane ziwani kwenye ‘Show’ za ‘Cliff diving’.

Honorius Mpangala,
Desemba 12/2017
Songea, Ruvuma.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako