November 11, 2009

VITUKO VYA WANYASA NA SANAMU LA ASKARI DAR ES SALAAM


Nakumbuka nikiwa mdogo, simulizi za snamu la skari huyu zilinitihs akuona mji huu siyo wa kuishi. Nakumbuka waliowahi kufika huko Dar es alaam wakisifia na kutisha kuhusu mji wenyewe. Nakumbuka wengine waliwahi kusimulia kuwa hapo zamani kulikuwa na mzee fulani MNYASA aliwahi kukaa hapo kwa kuombeleza asamehewe makosa yake kwani hakujua kama anavunja kanuni za mji.
Na kosa lenyewe lilikuwa kushangaa ghorofa zilizojipanga katikati ya mji tangu alipokuwa akiishi Upanga. Na kwakua alikuwa mgeni basi aliamua kujipa jukumu la kuyajua mazingira kwakuwa alizowea mji kiasi chake. Basi akaijikuta maefika katika sanamu la askari huyu, mzee wa watu akapiga magoti kuomba msamaha sana kwa makosa ya kushangaa majumba makubwa watu wanaishi angani kama FIDEGE tena wale mbayuwayu...nawapenda sana hawa ndege.
Mzee huyo inasemekana alilia kwa nguvu zote kwa kudhani atasamehewa kosa la kushangaa majumba makubwa, yenye watu wasiotosheleza ubongo hadi wakawa walarushwa wakubwa na kuita TAKRIMA. Basi mzee huyo akaangua kilio hapo lakini hakuna aliyejali sana kuhusu hilo kwani alidhaniwa kua ni kichaa tu.
Lakini kama ujuavyo wabongo kwa kunusanusa udaku wakamsogelea mzee wa kinyasa na kumhoji inakuwaje anaongea na sanamu kwani amekuwa kichaa? Lakini mzee akasisitiza kuwa askari yule amemweleza atamdhuru kwanini ameshangaa maghorofa wakati anajua yanalipiwa? watu wakacheka inasadikika hivyo, wakamweleza huyo askari ni samanu tu hivyo kumtaka arejee nyumbani, ndipo mzee alikubalina lakini kwa sharti la kusindikizwa.
Alipotoa rai hiyo basi waungwana wakafanya hivyo hadi mtaa wa Undali na akaonyesha anapoishi kisha wenyeji wakajitokeza. Ndipo ikaulizwa kulikoni? Mzee akasimulia kisa na kudai jamaa wamemwokoa.... hee wenyeji wakaangua kicheko ikawa usiku ikawa mchana ......simulizi zimeendelea vizazi hadi vizazi vya mzee wa Lundunyasa alisimuliwa.....na hapo kale alikuwa akikataa kuja mji huu sababu hiyo ingawaje baadaye alikubali tu shauri ya elimu siyo sababu ya askari sanamu. Na akitimiza agano mzee wa Lundunyasa lazima arejee agano lake la nyasa. Vituko vya wanyasa na sanamu hilo jamani nilikuweo enzi hizo wakitusimulia yatokanayo

No comments:

Post a Comment

Maoni yako