December 19, 2012

HALI YA WAVUVI NA UVUVI KATIKA ZIWA NYASA WILAYANI NYASA

Mvuvi akiwa na zana zake za kazi. 
PICHA: kwa hisani ya kaka Francis Godwin

UHABA wa samaki ziwa Nyasa upande wa Tanzania unaochangiwa na vifaa duni vya uvuvi umepelekea baadhi ya wanaume wa tarafa ya Mwambao wilaya ya Ludewa mkoani Iringa kutelekeza familia na kwenda nchini Malawi kufanya shughuli za uvuvi kama njia ya kukwepa changamoto za uchumi zinazoendelea kuwa kikwazo katika wilaya hiyo.
Uchumi wa wananchi wa tarafa yaMwambao ambao ulikuwa ukitokana na ajira ya uvuvi kwenye ziwa Nyasa nao umezidi kuporomoka kwa kasi kubwa na kupelekea hata biashara za wananchi wa maeneo hayo ambazo zilianzishwa kutokana na wingi wa wageni waliokuwa wakifika kujumua samaki kwenye ziwa hilo pia kuathirika kwa kiasi kikubwa.
Kama inavyofahamika kuwa uvuvi wa samaki kwa wananchi wa tarafa ya Mwambao wilayani Ludewa ndio shughuli kubwa ya kiuchumi ambayo imekuwa ikitegemewa na karibu robo tatu ya wakazi wa tarafa hii ya Mwambao na ndio shughuli iliyopelekea tarafa hiyo kuwa na mzunguko mkubwa wa fedha hasa kipindi cha nyuma japo kwa sasa imeanza kubaki historia pekee. 
Bonyeza kiungo;    SOMA ZAIDI HAPA

No comments:

Post a Comment

Maoni yako