January 05, 2013

CHADEMA WANACHEZA NGOMA ZA CCM

 Na Markus Mpangala
Tangu kumalizika kwa uchaguzi mdogo katika maeneo mbalimbali nchini kuna mwenendo wa kisiasa za mabadiliko kwa kila upande. Chadema walisimamisha harakati za mikutano ya hadhara ya M4C iliyokuwa ikifanyika maeneo mbalimbali nchini.
Kimsingi kwenye ushindani lazima apatikane mshindi, na asiyekubali kushindwa siyo mshindani. Katika kila tukio ama masuala ya kisiasa yanayotokea hapa nchini, tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu mwaka 2010, Chadema ilionekana kwua mshindani mkali wa CCM



Uchaguzi huo mdogo unalipomalizika katika kata 29, ilishuhudia CCM ikipata ushindi wa Kata 22, huku Chadema ikiambulia Kata 5. Baadhi ya wapinzani wa Chadema wanadhani hilo ni pigo kubwa kuliko yoyote yaliyowahi kutokea katika siasa za ushindani baina ya CCM na Chadema.
Kila jukwaa ambalo waliweza kupita wana chadema walifanikiwa kujigamba kutokana na hali iliyojitokeza kwenye matokeo ya uchaguzi. Licha ya mgombea urais wa Chadema kutoapata ushindi wa kiti hicho lakini alileta changamoto kubwa kwa CCM.
Kuanzia hapo CCM wakawa wanavutwa kila jambo na Chadema. ilikuwa rahisi kubaini kuwa Chadema walikuwa wkaiongoza nchi kutokana na siasa zao za ushindani na namna walivyoweza kusimamia hoja. Hili lilijitokeza bungeni na katika majadiliano mbalimbali.
Chadema ilikuwa inaasisi hoja amabzo baadaye CCM ilionekana kufuata nyuma. Hata hivyo kuna mambo yamebadilika katika kipindi fulani cha mwaka huu katkati.
Kwanza suala la Meya wa iji la Arusha, kisha malumbano ya kawaida kuhusu Mbunge Maswa, John Shibuda ambaye alidaiwa kutamka kunuia kuwania urais, kisha suala la Zitto Kabwe kuwa miongoni mwa wa kero za chama bila kujali uanachama wake.
Pengine hayo hayakuweza kuitikisa Chadema kwani viongozi wake walikuwa makini na walijua katika siasa hakuna kanuni moja ya kuweza kufanikiwa. Suala la Mbunge wa Arusha mjini nalo lilikuwa moja ya mambo yaliyisababisha Chadema izungumzwe zaidi.
Lakini mahakama ya Rufaa imemrudishia Ubunge wake, Mheshimiwa Godbless Lema. Nadhani huu ni ushindi mwingine wa kwa Chadema. aidha, pamoja na ushindi huo kuna suala jingine lililoibuka tangu kumalizika kwa uchaguzi mdogo uliohusisha Kata 29.
Kuanzia wakati huu ndipo CCM wameamka na kuanza kupata mwanya wa kuzungumza kwa ushindani dhidi ya Chadema. ikumbukwe CCM walipoteza ubunge wao katika jimbo la Igunga ambapo mbunge wake Dk Dalily Kafumu alivuliwa Ubunge na Mahakama Kuu kanda ya Tabora.
Hayo yalitokana na jitihada za Chadema kupinga ushindi wa CCM. lakini kuna mambo yamebadilika kwa kiasi kikubwa baada ya chaguzi ndogo.
Suala la madiwani wa Ilemela mkoani Mwanza nalo linaweza kuwa sehemu ya hoja za CCM ambao wameweza kuzinduka kutokana na ushindi wa Kata 22 kote nchini. Sababu baada ya hapo CCM ilikuwa na chaguzi za ndani katika jumuiya mbalimbali.
Pia CCM iliweza kuchaguana katika Sekretarieti mpya ya kuendesha chama chao. Ujio wa Abdulrahman Kinana na Philip Mangula unaonekana kuwa moja ya nyenzo ambazo mwenyekiti wa CCM, Jakaya Kikwete amejaribu kurejesha imani kwa wanachama na wapigakura wao.     Kama nilivyowahi kuandika katika safu hii kuwa tunaona wazi kabisa, Jakaya Kikwete anairudisha CCM kwa wakomunisti kwa kutengeneza njia zilezile ambazo zilitumika na akina Mao Zedong.

Zitto Kabwe, mbunge wa Kigoma Kaskazini. 


Tangu kumalizika kwa chaguzi za ndani za CCM na kuteuliwa kwa Sekretarieti hiyo ninaona kabisa mabadiliko ya kimantiki kuhusu ushindani wa vyama hivi viwili, kwamba Chadema badala kuifanya CCM ifuate njia zake, sasa Chadema ndio inafuata mengi yanayosemwa na CCM. 

Hayo yanayosemwa bila kujali yana maana au yamejaa upuuzi. Kuna upepo fulani umevuma ghafla kuelekea kipindi cha mwisho wa mwaka huu. upepo huo umekifanya Chadema kuwa na hali ya kutafuta tafakari nyingi kuhusiana na mwenendo wao wa kisiasa. Wapo wanasiasa wenye mtazmao finyu ndani ya CCM waliweza kuihusisha M4C na zile Pick-Up za waasi wa Benghazi. Hayo yaliendelea sehemu mbalimbali nchini iwe kwenye vyombo vya habari ama mitandao ya kijamii. 
Hali hii iliachwa, na matokeo yake wapow aliofanikiwa kuwarubuni wananchi kwamba harakati za M4C zilikuwa na lengo la kuvuruga amani. Jambo jingine ambalo limebadilisha upepo huu ni mgogoro wa chinichini baina Chadema na Jeshi la Polisi.
Maandamano ya Morogoro yalisababisha maafa. Maandamano ya Iringa yalisababisha kifo cha Daudi Mwangosi. Kisaikolojia pekee mtu atauliza kwanini kifo kimetokea. Jibu lake litakuwa ni katika mkutano wa Chadema bila kujali muktadha wa kifo hicho.
Kwa mantiki hiyo hii ilikuwa inaleta ghasia kwa wananchi wa kawaida lakini kwa werevu walijua mwenendo wa siasa za harakati una faida zake hivyo licha ya mapungufu mbalimbali bado Chadema walipaswa kuheshimiwa.
Jambo zuri ni kwamba Chadema wamekiri kuwa wanalazimika kuachana na siasa za Harakati, hivyo kujipanga upya tangu kusitishwa kwa M4C. hekima hii imekisaidia sana Chadema ili kupumzisha akili za wnaanchi kutiwa hofu na kasi ya vurugu baina yao na jeshi la Polisi.
Yapo mambo ya msingi ambayo Chadema na Jeshi la Polisi wanaweza kusaidia katika kukuza demokrasia na uhuru wa kujieleza. Lakini haitoshi tu kulalamika kwamba Chadema ilisababisha ama Jeshi la Polisi lilisababisha.
Kila upande ukichukua wajibu wake nina uhakika haliweza kutokea tena, na endapo litatokea basi sababu za kutokea kwa vurugu hizo kutakuwa na zaidi ya siasa za kawaida tulizozizoea.
Lakini kingine ambacho kinasababisha Chadema ielekee kucheza ngoma za CCM ni hatua ya Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye kusema baadhi ya vigogo wa vyama vya upinzani wanamiliki kadi ya CCM, kumejitokeza masuala mengi ndani ya Chadema.
Sio hilo tu bali hata taarifa mbalimbali zinaonyesha kuwa Chadema inapitia katika jaribio la kisiasa kutoka CCM. wakati CCM ikipima kina cha maji ya Chadema kwa kushambulia moja kwa moja kwenye ngome yao (Dk. Slaa), bado Chadema haijatoa majibu kwa hoja hizo zaidi ya mazungumzo ya hapa na pale.
Kisiasa hatua ya kutajwa Dk Slaa kumiliki kadi ya CCM kulikuwa na maana moja tu kutimiza falsafa ya aliyekuwa Rais wa Marekani Bill Clinton, kwamba ukitaka kumshinda adui yako basi shambulia ngome yake. CCM inaelewa aliyesababisha wakose kura nyingi kwenye uchaguzi wa mwaka 2010 alikuwa Dk. Slaa kutokana na kukubalika na wengi.
Pili CCM imejaribu kuzingatia hoja ya nani ashambuliwe kisiasa ili kuweza kuidhoofisha Chadema. kimsingi kufanya malumbano au mashambulizi yoyote dhidi ya Chadema kupitia Dk. Slaa nina imani ni kujaribu kushambulia ngome ya Chadema.
Kwahiyo shambulizi hilo kwa Dk. Slaa ni jaribio la kupima uzito wa majibu ya Chadema namna ainavyoweza kukabailiana na njia mpya ya kupambana na CCM.
Bahati nzuri Chadema wametulia, ingawa wanasiasa chipukizi wameambukizana hisia na kuanza kucheza ngoma za CCM. hatua za viongozi wa Bavicha huko Mwanza, Mbeya au manyara, ni mwanzo wa kuonekana ukosefu wa msingi wa kushghulikia mashambulizi ya kisiasa.
Njia nzuri ya kudhibiti mashambulizi ni kuacha wakati upite, huku wahusika wakiacha kutumia muda mwingi kulumbana kwa hoja zinazowasilishwa. Kwahiyo Chadema watacheza ngoma za CCM kwa muda mrefu kama hawataelewa kwanini kuna mashambulizi dhidi ya Dk. Slaa.
Kwa vijana wenzangu wa Bavicha na chama chao kama hawatagundua hila za kisiasa sina shaka wanaweza kudhani kile wanachoshambuliwa wanatakiwa kukijibu kwa mashambulizi ya papo kwa papo.
Lakini njia nzuri ya kupambana kisiasa ni kuhakikisha wakati unapita ndipo unachukua nafasi ya kujibu mashambulizi kwa namna nyingine.
Mathalani, wakati wa uchaguzi wa Marekani, Mitt Romney alifanikiwa kumshambulia Barrack Obama kwa nguvu sana kwenye mdahalo wa kwanza.
Lakini wakati wa mdahalo wa pili Barrack Obama aliweza kumwadhibu Mitt Romney vibaya sana tena kwa kumgusa kutokana na kampuni yake ya Bain Capital kuendeleza wimbi la kuwakosesha ajira wamaerkani kwa kununua makampuni machanga kisha kuyafilisi.
Jambo jingine, am ana ambalo Chadema wakitaka kuepuka kuendelea kucheza ngoma za CCM ni kujifunza jinsi Obama alivyoweza kumshambulia Romney kwa hoja na “timing” ya hali ya juu.
Labda ingelikuwa kwenye ndondi basi tungesema Barrack Obama alipiga konde la “Chop” ya nguvu ambayo lililomdondosha Romney. Obama alisema wakati Romney aliwa Gavana aliongoza jopo la wabunge kusitisha uchimbwaji wa Makaa ya mawe, lakini miaka michache baadaye kampuni yake ikawa inaongoza kuhitaji uwekezaji wa makaa ya mawe.
Hilo linaweza kuchukuliwa kama njia ya kupambana kiasa. Lakini kwa hulka ya Bavicha bila utafiti wa kina watajikuta wakilazimisha Chadema kucheza ngoma za CCM, bila kuelewa dhumuni la kutungiwa nyimbo za kumnanga Dl. Slaa.
Sio yeye pekee, ilizuka nyingine kwamba Zitto Kabwe alihusika na rushwa kule Bungeni. Lakini Ripoti ya Mheshimiwa Ngwilizi ikaeleza kuwa kilichosemwa ilikuwa ulaghai.
Kwa maana nyingine ndani ya Chadema kuna wanasiasa walikwua wakicheza ngoma za CCM bila kujielewa. Na kwa mtindo huu, tunafanga mwaka kwa kuona Chadema wakiwa watulivu na kupanga mikakati kwamba mwaka 2013 hakuna kulala.
Lakini watambue hakuna kulala kokote kusiko na msingi wake. Itakuwa mbaya zaidi wakicheza ngoma za CCM, kwa kila shutuma dhidi ya wanasiasa wao wa ngazi za juu. Ni mtazamo tu. Nimemaliza.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako