February 19, 2013

SIASA ZA KITOTO; WAKUBWA NA WATOTO


                                             
Markus Mpangala
Ndugu zangu waungwana, kama kuna kitu tumejilemaza katika nchi yetu hii ni ile hali ya kujitumbukiza katika janga la kufikiria matatizo tu. Wapo watu wanafikiria kila kukicha na kusubiria tatizo litokee ndio wanakuwa wa kwanza kupayuka. Kuna mchezo mbovu katika sasa zetu unaendelea hapa nchini. mwanasiasa anahama chama kimoja kwenda kingine akiwa na lundo la TUHUMA. Mathalani mwanasiasa anahama CHADEMA anakwenda CCM. Au anahama CUF anakwenda ADC, au anahama CHADEMA anakwenda CUF.
Au anahama ADC na kwenda TLP. Kila siku utasikia eti nilitumika kuwadanganya watanzania au wapigakura. Kwa wale wataalamu wa kusoma tabia za watu wanabaki wanajiuliza, hii ni tabia mpya au udhiafu wa kutokomaa kifikra? Sababu mwanasiasa anapohamia chama kingine kisha anakuwa na kapu la TUHUMA ni moja ya udhaifu mkubwa wa ukomavu wake kisiasa. Ni udhiafu na tumekuwa tukijipongeza kwa upuuzi huu kwamba ndio ugangwe wa kuonekana ni wanasiasa weledi.

Haikatazwi kuhama chama, haikazwi kutoa TUHUMA. Lakini moja ya udhaifu wa mwanasiasa au mkoamavu kifikra, na aliyejipika akajiivisha kisha chama/siasa zikamfanya aive hawezi kutoa lundo la TUHUMA kwa chama anachohama. Ni utoto na siasa za kitoto kuanzia watoto hadi wakubwa. Hayo ni dhahiri yanaonyesha namna gani tumeshindwa kutengeneza wanasiasa wenye ushindani badala yake tumekuwa na idadi kubwa ya wanasiasa wapika majungu, wivu wa kujinga na kadhalika.

Nakiri ni makosa makubwa sana katika siasa zetu. Nitatoa mifano midgo tu, Tambwe Hizza alirudi CCM akitokea chama cha CUF. Wakati anarudi CCM alisema kuwa kule CUF alitumika vibaya na alidanganya mengi, ingawaje hakutaja alichotumiwa au alichodanganya. 

Kwa mkondo ule wanasiasa wanaorudi CCM wanasema hilo hilo. Akihama CHADEMA kwenda CCM, au akihama CCM kwenda CHADEMA anatamka ukakasi kuwa wapo watu ambao wanasababisha matatizo ndani ya chama na wkamba wao wanaamua kuhama. Utoto mkubwa umeenea na ni aibu sana kwa mwanasiasa kijana kuigia siasa za kikoloni ambazo zimekuwa na ubainafsi na kushindwa kutengeneza misngi. Angalia hii pia, Arcado Ntagazwa alipohamia CHADEMA alisema sababu ni maovu ya CCM.
Ni kwamba kwa mkondo uleule wa Tambwe Hizza ambaye aliamua kuondoka CUF kisha akakabidhiwa kitengo cha PROPAGANDA cha CCM, akidai alitumika vibaya. Hii nchi yetu inachekesha mwanasiasa anahamia chama kingine anakishutumu kile anachotoka. Kuna haja gani dada yangu mpendwa Juliana Shonza kumwambia mwenyekiti wa CCM kuwa alipokuwa CHADEMA alitumika vibaya? Natambua wapo wanasiasa shupavu, na Juliana Shonza anaelekea kuwa shupavu, lakini moja ya dosari alizokumbana na kuangukia kwenye tope la mtindo wa lundo la TUHUMA.

Nasema hilo sababu huyu ni mwanasiasa kijana na anakuwa msingi wa vijana kuchukua uamuzi wa kuhamia kwingine. Lakini ushauri wa msingi haifai kabisa kuhamia chama kingine ukiwa na shutuma ambazo zinakuweka katika darubini ya uangalizi huku watu makini ndani ya chama wanabaki wakitoa gego na fizi kwa kujiuliza, tumfanyeje mtu huyu? Je kama mwanasiasa alitumika vibaya atokako, ataweza kuaminika aendako? sichelei kusema hizi ni siasa dhaifu sana. Hakuna sababu ya kujaza orodha ya maovu ndio umahiri wa kuhamia chama kingine, nadhani ni siasa za kitoto.

Wazee wetu wamekuwa waasisi wa siasa za kitoto kama hizi, maana rcado Ntagazwa angeliweza kutumia weledi kuhamia CHADEMA. Profesa Abdallah Safari naye angetumia weledi kuueleza umma sababu za kuhamia CHADEMA. Mabere Marando angetumia weledi kuhamia CHADEMA.Vivyo hivyo ilipaswa kuangaliwa kwa wanasiasa wengine ili kuondokana na mtindo unaomea siku hizi eti ukihamia chama kipya unatakiwa kuonekana u mtakatifu na kutubu 'madhambi' ya utokako, lakini wale wanaokupokea kwanza wanapoteza imani juu yako.

Kisha wanachofanya kukukejeli na kukuona u mtumwa wa siasa na umekosa misingi. Muhimu tutengeneze wanasiasa ambao wanajua nini maana ya siasa, na nini ushindani wa kisiasa. Lau hata wakihamia vyama vingine wawe na uhodari wa hoja sio kutegemea kuwatusi au kuwatuhumu wengine. Aibu, acheni siasa za kitoto kwa wakubwa na watoto.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako