March 09, 2013

GEOPOLITICS: ODINGA ALIJITAKIA KUSHINDWA


MTAZAMO WANGU KWA UFUPI; 
Odinga amefanya makosa kisiasa. Timu ya Odinga mwaka huu ilikuwa dhaifu kupindukia. Haikuwa na ushawishi wowote wenye maana. Kalonzo Musyoka anastahili kuheshimiwa lakini naye tumwambie hana ushawishi wowote ambao ungemsaidia Odinga. 
Hebu angalia timu ya zamani; Najib Balala, Charity Ngilu, Mudavadi, William Ruto, na wengine wengi. Odinga amejitakia kushindwa kwanza kabla ya kuangalia kwamba amekuwa kibaraka wa ubeberu. Angalia njia zake, angalia timu yake; AMEJITAKIA KUSHINDWA kabla ya kuwa kibaraka. Kama mtu anakumbuka timu ya NARC ilivyokuwa mwaka 2002, kisha ile ODM ya mwaka 2007, kisha kilichotokea katikati na kusambaratika kabisa kwa timu yenyewe kisiasa, basi hakuna shaka kabisa Odinga alijitakia kushindwa uchaguzi kabla ya kulalamika.

Loading .........

KWA BARRACK OBAMA, MAREKANI

kwamba Obama mwanzoni alimzodoa Uhuru Kenyatta, lakini baadaye nadhani alisoma upepo wa kisiasa na nguvu ya Wiiliam Ruto ilivyokaa vema na Uhuru. kwanza Obama sio raia wa Kenya hata kama mzazi wake anatokea Kenya. Obama akumbuke swali alilowahi kuulizwa na marehemu Hugo Chavez, "Mwanangu Obama unataka kupata kura za uchaguzi nchini kwako kwa kuwashambulia raia wangu wa Venezuela?" Lilikuwa swali zuri sana. Sasa Obama anatakiwa kutambua yeye sio Mkenya, na wakenya wameamua kile kinachofaa kwao bila kujali mashtaka ya Uhuru kule ICC. Na Obama hana sababu za kushinikiza suala la ICC, kwanza aifanye Marekani kuwa mwanachama wa ICC halafu tumkamate Geprge W. Bush. Kama akishindwa kuiingiza nchi yake kuwa mwanachama wa ICC, basi hana mamlaka pia ya kuwachagulia wakenya rais wao.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako