March 18, 2013

NAFASI ZA KAZI KWA VIJANA WA KIKE NA KIUME 20 KAMA "VOLUNTEERS" KATIKA RUAHA MARATHON..!!


Shirika la Mindset Empowerment waandaaji wa mashindano ya RUAHA MARATHON inawashukuru wasimamizi wa shughuli zake kwa upande wa DAR ES SALAAM, Markus Mpangala na Kambi Mbwana, pamoja na akina dada waliojitokeza kuwania nafasi ya kazi pale Mlimani City, Dar es Salaam. 

Nimepewa taarifa kuwa walijitokeza kwenye interview ni mabinti zaidi ya 50 na wamechujwa na kupatikana mabinti watano (5) ambapo mmoja kati yao atachukua nafasi hiyo na wanne kuwa reserve kwa majukumu mengine ndani ya Ruaha Marathon. Tunayo furaha kutangaza tena nafasi 20 za kazi za kujitolea (volunteers) kwa vijana wa KIUME na wa KIKE kwa ajili ya kufanikisha mashindano haya tarehe 25/May/2013, mkoani Iringa.

ENEO LA KAZI: Iringa mjini & Iringa vijijini, kwenye njia (route) za mashindano
MAJUKUMU: Kufanya kazi katika vituo vya marathon siku hiyo ya mashindano
UKOMO: Kazi hii ni ya kujitolea kwa siku moja TU (siku hiyo ya mashindano)
SEMINA: Wiki moja kabla ya siku ya mashindano kutakuwa na semina kwa volunteers wote, kwa ajili ya ujuzi wa kufanikisha majukumu yao.

FAIDA: Pamoja na posho (allowance) atakayopewa volunteer siku hiyo, vile vile atapewa cheti cha kimataifa kinachoonesha kujali, uzoefu na ushiriki wake katika miradi ya kijamii (Ikumbukwe kuwa Ruaha Marathon inafanyika mwaka huu kwa ajili ya kuchangisha fedha za ujenzi wa shule na kituo cha michezo kwa watoto walemavu, Tanzania). Volunteers wote watakuwa ni watu wanaofikiriwa kwanza (first priority) kila zinapotoea nafasi za kazi za kudumu katika Shirika la Mindset Empowerment.

VIGEZO: Yeyote anaependa kuwa volunteer anatakiwa awe anajua kungea na kuandika lugha ya kiingereza kwa ufasaha. Pia awe na ufahamu mzuri kuhusu mambo mbalimbali. Wafanyakazi pia Wanafunzi & wahitimu wa vyuo vikuu/vyuo mbalimbali na wengineo wanaoweza kufika, waliopo/au wenye makazi Iringa mjini wanahamasishwa wasipitwe na fursa hii adhimu

KUTUMA MAOMBI: Tuandikie email: nyalukemarathon@yahoo.com au tuma sms au piga katika +255 719 127 901. Unapoandika/kutuma sms zingatia: 1) Andika majina yako yote matatu, 2) Elimu yako/mahali unaposoma au unapofanyia kazi. 3) Umri wako 4) Jinsia yako. Baada ya kukutuma maombi yako; tutakujulisha hatua inayofuata. Maombi tunaanza kupokea leo tarehe, 17/March/2013

IMETOLEWA NA: Albert Nyaluke Sanga, Mratibu-Ruaha Marathon/Mindset Empowerment, 2013~(C)

No comments:

Post a Comment

Maoni yako