April 03, 2013

STRAIN THEOTY/CRIMENOLOGY VS UDINI NA DINI=CUHUMI?



Wataalamu kama Robert Merton waliwahi kusistiza umuhimu wa uhalifu katika jamii. Lakini kwa wataalamu hao hao wanasema, ikiwa njia za kujipatia pato zikibanwa au zikibinywa uhalifu ni kitu kinachochukua nafasi ambapo watu hutafuta pato kupitia njia zozote zile ikiwemo uhalfu. 
 
Wakasema kuwa kuna umuhimu wa uhalifu sababu unaileta jamii pamoja. Jamii inakuwa kwenye kutafuta njia mwafaka kumaliza uhalifu, lakini lazima jamii hiyo ijitolesheleze ndipo tunaweza kuufanya uhalifu kumalizika. .......

Naam kama nchi yenu haiongelei suala la ukuzaji uchumi, itaongelea nini? Kama tumeshuhudia watu kule Mwanza wanauana kisa HAKI YA KUCHINJA na kuvaa mavazi ya DINI kisha kumwaga damu, nini tafsiri yako? Je, umewaona wanaoshiriki zoezi la kuuana ni watu wa namna gani? ....je wale wanawezaje kuachwa katika faili la UCHUMI? Hatuna uchumi imara lakini hatutakiwi kuacha kutafuta UCHUMI imara.   

@Nakupenda sana nchi yangu TANZANIA. 

Hatutendi haki hata kidogo kutoandika 'aya' za uchumi wetu ambayo ndio msingi wa taifa letu na kumwachia Rais wetu Kikwete akihutubia mambo machache. Labda afadhali hayo machache kuliko kukosa kabisa. Kama tunataka kujenga utamaduni wa kutomwambia basi tunajenga taifa la watu wasioweza kufikiri au taifa la watu wanaopendelea mambo mepesi. 

Hatukatai kuona kuwa hotuba ya rais wetu haiwezi kuwaridhisha watu wote, lakini mimi naona kuna haja pia kuwakumbusha wale wote wanaohusika kuwa, wajaribu na waweze kufanya kitu ambacho kinaakisi jamii yao. Kama tunakubaliana kwamba uhalifu ni kitu kinacholeta jamii pamoja, na kwamba lazima jamii ijitosheleze basi yatupasa kujiuliza itajitosheleza katika lipi na kwanini? 

Lazima tumfanye rais wetu awe 'mgumu' kwa maana mtu 'mzito' kwa hoja nzito. Kwahiyo tusitegemee kuwa Rais anaweza kufanya hilo pekee bali lazima tusaidie, lazima kumfanya awe bora sababu ni mali yetu na tunajivunia yeye. Lakini kama kuna watu wanadhani kukosoa hotuba ya Rais ni dhambi ati sio saizi yetu hatuba budi kusema labda akina sisi tunaokosoa tumechanganyikiwa na tunakaribia kuchojoa nguo. 

Ni jambo baya sana tunapoona kila mtu anadhani waandishi wa hotuba ya Rais wanajua kila kitu. Lakini wanayo fursa ya kupata tafiti za kisasa za uchumi, makabrasha na kadhalika ili kuweza kuelezea jambo la msingi kuhusu hali ya maisha ya watu wetu. 

Ni vigumu sana kuamini kuwa Rais wetu anaandikiwa hotuba nusu, labda wenzetu walisahau, ila nakumbusha kama huijui jamii yako basi unaelekea kuchanganyikiwa. Turuhusu waandishi wa hotuba ya rais wawe hodari kwa kuwajengea hoja zenye maana sio kuwatusi. Tuwape nafasi ya kujisahihisha sababu wao sio miungu hata kidogo..

No comments:

Post a Comment

Maoni yako