November 16, 2017

MBAMBA HILL KUWA HIFADHI YA PILI YA ASILI TANZANIA KUWA MJINI

NA MWANDISHI WETU 
MKOA wa Ruvuma unatarajia kupata hifadhi ya wanyamapori ya pili ya asili inayoitwa Kilima Mbamba (Mbamba Hill) ambayo ipo mjini Mbamba Bay makao makuu ya wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma. 
Hifadhi pekee Tanzania ya kwanza ya asili iliyopo mjini inaitwa Luhira iliyopo kilometa saba toka mjini Songea mkoani Ruvuma iliyoanzishwa mwaka 1974. Mkoa wa Ruvuma unapata hifadhi ya pili ya asili mjini. 


Akizungumzia hifadhi hiyo Afisa Maliasili na Utalii wa Mkoa wa Ruvuma Afrikanus Challe anasema mchakato wa kuendeleza Mbamba Hill unaendelea vizuri na kwamba ya tayari bajeti imepitishwa.

“Tumeshapima eneo lote la Hifadhi ya Mbamba Hill,lina ukubwa wa hekta 420,ndani ya hifadhi hiyo kuna wanyama kama nyani, nyoka, pimbi,chui na ndege wa aina mbalimbali’’, anasema Challe

Amesema bajeti ya kujenga uzio kuzunguka Mbamba Bay Hill imepitishwa na kwamba ujenzi unatarajia kuanza wakati wowote fedha zitakapoletwa na kwamba mara baada ya ujenzi wa uzio kukamilika wanyamapori wa aina mbalimbali wanatarajia kuongezwa.

Anawataja wanyama ambao wanatarajia kuongezwa katika hifadhi hiyo kuwa ni Swala, Fisimaji, mbuzi Mawe, Digidigi, Mbawala na kwamba wanyama watakaongezwa ni wale ambao wanaweza kuishi katika mazingira ya hifadhi hiyo ambayo imeungana na ziwa Nyasa.

©Albano Midelo, Ofisa habari wa Manispaa ya Songea.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako