December 02, 2017

FURAHA YA MAZEMBE ILIYOPORWA UWANJA WA NDEGE NA KABILA

NA. HONORIUS MPANGALA 
Rais Joseph Kabila ni mmoja ya marais wa Afrika ambao ni wamashabiki wakubwa wa mchezo Wa soka. Amekuwa akisapoti sana mchezo Wa soka Kwa timu yao ya taifa inayoitwa chui. Wadau wengi wa soka wanakumbukumbu ambayo aliiweka kwa kuwapa zawadi ya magari kila mchezaji na viongozi wote walioshiriki katika michuano ya CHAN iliyofanyika mwaka Jana 2016 nchini Rwanda. 

 Kabila ameonekana mara nyingi sana katika viwanja vya michezo akihudhuria mechi mbalimbali.Hata katika video ya ule wimbo maarufu 'Leopards fimbu na fimbu' ulioimbwa na Felix Wazekwa umemwonyesha rais akikabidhiwa kombe la Chan mwaka 2009 na Nahodha Wa wakati huo Tresor Mputu,ambalo Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo walilichukua baada ya kuwafunga Ghana katika uwanja wa Felix Houpout-Boigny pale Abidjan Nchini Ivory Coast.


November 25,2017 katika ardhi ya Afrika kusini klabu ya Tout Puissant Mazembe Englebert ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo walifanikiwa kunyakua ubingwa Wa Afrika kwa kutwaa kombe la shrikisho la soka Afrika Caf ambao walikuwa wanauchujua kwa Mara ya pili mfululizo.Ilikuwa ni wiki mbili tu baada ya kupatikana bingwa wa ligi ya mabingwa Afrika ambaye ni Wydad Athletic Club Casablanca. 

Mazembe walifanikiwa kupata ushindi katika chezo wa awali uliofanyika nyumbani kwao kwa magoli mbili kwa moja dhidi ya wageni Super sport United ya Afrika kusini. Mchezo wa marudiano katika uwanja wa Lucas Moripe jijini Pretoria unamalizika kwa sare ya bila magoli. Hatimaye Mazembe akatwa ubingwa.

Wakiwa Afrika kusini Mazembe walipambana kwa dakika zote za mchezo kuhakikisha wanalinda ushindi walioupata nyumbani na wanarejea na kombe. Walifanikiwa katika hilo na matarajio yalikuwa kikombe kitumike kuwasahaliulisha Wakongomani ambao kwa sasa wana machafuko ya kuhitaji kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa rais. Ni wazi maandamano yanayofanyika maeneo mbalimbali ya Kongo ni kushinikiza uchaguzi na Vyama Vingi vikiungana ili kumwondoa Kabila maradakani kwa kupitia boksi la kura.

Wakiwa nchini Afrika kusini klabu ya Mazembe siku ya November 27 jumatatu walitarajia kusafiri kwa ndege moja kwa moja hadi Lubumbashi ilipo maskani ya klabu hiyo. Kioja kilichotokea wachezaji na viongozi walisubirishwa kwa masaa kumi katika uwanja wa ndege wa Johannesburg wakisubili ndege waliyotakiwa kusafiri nayo. 

Huku nchini Kongo mashabiki wa Mazembe walifurika kuilaki timu yao wakasubiri kwa masaa mengi bila mafanikio. Ilibidi wasubiri hadi jumanne ya November 28, baada ya kupata ndege iliyoweza kuwafikisha katika uwanja wa Simon Mwansa Chapwepwe mji wa Ndola nchini Zambia na baadae msafara kuelekea Lubumbashi kuwa wa njia ya barabara.Mazembe walitakiwa kuwahi ili siku ya jumatano November 29 wacheze mechi ya ligi kuu ya Kongo dhidi ya Don Bosco.

Katika changamoto hizo walizokutana nazo Mazembe Mmliki wa klabu Alimlaumu waziwazi rais wa Kongo Joseph Kabila kuwa hayo yote yametokana na yeye kuwa sehemu ya Mazembe. 

Kumbuka Moise Katumbi Chapwe ni mmoja ya wanasiasa wenye nguvu nchini Kongo akitarajiwa kumpa changamoto kubwa Kabila katika uchaguzi ujao ambao Moise anaungwa mkono na vya vya upinzani taklibani tisa. Mosie aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa tweeter"mazembe ni bingwa wa afrika, ubingwa wa mazembe ni wakongo wote na sio wa Katumbi.

Nyakati zote nimekuwa nikisema Kabila ni mtu mbaya anayekiuka haki za binadamu" baadae akawashukuru mamlaka ya usafiri wa anga wa Zambia kwa huduma waliyowapatia na kusema "hii ndiyo afrika ambayo iko fair na inasapoti. Pamoja na kutua Ndola klabu hiyo ilitumia nafasi hiyo kuwafanya wachezaji wao wenye asili ya Zambia kushukuru sapoti waliyowapa kureje na Kuwaonyesha kombe lao. Ni Raniford Kalaba,Nathan Sinkala na Kabaso Chongo ambao hutokea Zambia wakihudumu katika klabu ya Mazembe.

Unaweza kusema Kabila alikuwa hana uelewa na suala la ka klabu kupandishiwa Bendera ya taifa inalotoka? Hajui kama klabu zinaimbiwa nyimbo za taifa za nchi zinatoka bila kujali kuwa na wachezaji wasio wa nchi husika?. Au ndo ubabe wa kisiasa wa kunyimana nafasi ya kuonyesha walicho nacho wapinzani wake kisiasa.

Msafara wa Mazembe ulishika barabara ya Ndola hadi Mpakani Kasumbalesa kupotia Kitwe,Chingola na Chililabombwe.
Kikundi maarufu cha ushangiliaji cha klabu hiyo ambacho husafiri kila mahali kusapoti klabu yao kinaitwa 100% 'cent pour cent' . kilirejea baada ya mchezo huku baadhi ya washangiliaji wa kikundi hicho ambao hawakusafiri waliendesha shamrashamra uwanja wa ndege wa Lubumbashi. 

Hata hivyo iliwalazimu kuelekea Kasumbalesa siku ya jumanne ili kuipokea klabu yao huku wakiwa na zama zote wanazotumia katika kushangili.Kutokana na Katumbi kutohudhuria mechi hiyo Afrika Kusini ilimlazimu kulipia tiketi elfu tano na kitoa magari ishirini ili mashabiki waemde kuishangilia timu yao.

Kwa Mara ya kwanza niliwaona asilimia mia moja wa Mazembe katika mchezo wa Simba dhidi yao mwaka 2011 katika uwanja wa taifa. Pia niliwaona tena mwaka 2016 juni 28 katika mchezo wa Mazembe dhidi ya Yanga,nadiliki kusema hakuna kikundi chenye kujua kushangilia mechi kama 'cent pour cent'. Ni kikundi kinachojua kushangilia wakati wote wa mchezo huo. Na kina watu maarufu kama ilivyokuwa kwa yule mshangiliaji maarufu wa Yanga marehemu Ally Yanga. Lakini katika kikundi kile kuna watu wawili ambao ni mhimili mkubwa wa kundi na wameliongoza kwa miaka mingi. Ni Nkolomoni almaarufu kama 'Ninja' na Mutamba Kelemuta kaka wa golikipa wa Mazembe Robert Kidiaba ambao waanzilishi kwa kundi tangu Mwaka 1983. Amewahi kukariri mmoja ya wanakikundi hicho alipokuwa akiongea na aliyekuwa katibu mkuu wa klabu hiyo Rex Mumba kuwa wao hawajali kuhusu matokeo bali wanajua kazi yao moja tu kuishangilia Mazembe.

Wimbo ambao unajukikana kama ndio wimbo wa klabu uitwao 'Ooh Mazembe Ooh Mazembe' ulitungwa na Young Kazadi almaarufu kama 'Chirika'.Pia wana wimbo ambao humsimamisha kila mmoja hata Katumbi bila kujali yuko jukwaa kuu unaitwa 'Okoyoko' maana mirindimo ya sauti na ngoma hakuna ambaye ataweza kumudu kukaa akaacha kusimama na kuimba pamoja 'Okoyoko' huku wakipiga makofi uwanja mzima na kuserebuka na 'outro' kama 'Tp yoyoyoooh Tp yoyoyooh'.

Kundi lina Wachezaji,waimbaji pamoja na wanamuziki. Kwa idadi yao wako wanakikundi 500 wenye umri wa mika kuanzia miaka 20 hadi 50,wanamuziki ndani yake wako 32 na bendi mbili Na uongozi wa kundi uko mbioni kuongeza wanakikundi vijana wadogo wa umri wa miaka 14 hadi 15 ili kuwapa changamoto wale watu wazima. Kwa aina yao ushangiliaji imekuwa ya kipekee na klabu kuona mafanikio yao nyuma yake wako 'cent pour cent'. Uundwaji wake ulikuwa kupeana upinzani na makundi ya Timu za Kinshasa.

Iliwahi kutokea katika moja ya mechi za Klabu bingwa ya dunia zilizofanyika Umoja wa falme za kiarubu, mechi kati ya Mazembe na Intacionale ya Brazil. Mashabiki taklibani elfu tano wa Brazil waliokuwa washangiliaji wa klabu yao walicheza Samba jukwaani na kuimba sana. Baadae 'cent pour cent' waliuwasha moto katika uwanja wa Abu Dhabi kwa Ngoma, filimbi, tarumbeta,kayamba,vinubi na nyimbo. Hali iliyoufanya uwanja kuwa na ndelemo za hali ya juu toka kwa wakongo. Huku wakicheza rhumba ,sebene na mitindo mbalimbali ya Ngoma za kongo, Wabrazil iliwabidi kutulia na kuwa wapole mbele ya 'cent pour cent' .

Aliwahi kunukuliwa aliyekuwa Kocha Mazembe Msenegal Lamine Ndiaye nilikuwa inamuwia vigumu kufikisha maelekezo yake kwa wachezaji kwasababu walikuwa hawamsikii kutokana na sauti zilizoko juu za 'cent pour cent' na hakuweza kuwaambia wapunguze kuimba kwani ile ndiyo kazi yao inayowafanya waifuate klabu popote inapocheza.

Kitendo cha kutotua katika uwanja wa ndege wa Lubumbashi kiliwasikitisha kwa kiasi kikubwa mashabiki wa Mazembe na Wakongo kwa ujumla. Usafiri wa gari walioutumia iliwalazimu 'cent pour cent' kufika hadi boda Kasumbalesa na kuwalaki mashujaa wao. 

Njiani katika Maeneo ya Whisky, Seventie Maile,Shamba la kabila,Lumata,Kashamata hadi Kisanga sehemu zote Wakongo walipungia mikono msafara wa klabu hiyo. Katika eneo la Kisanga ndipo anapotokea rais Kabila ndani ya Jimbo la Katanga ambalo zamani lilikuwa chini ya Gavana Moise Katumbi Chapwe.Shagwe za mashabiki wakikundi hicho wamekuwa na kawaida ya kuzunguka katika mitaa ya Lubumbashi kama Machipisha na Kigoma na misafara ya magari na pikipiki wakicheza na kuimba kwa pamoja.

Unaweza kujiuliza ni wakongo wangapi ambao wanaisapoti Mazembe na wakawa hawana furaha na kilichotokea baada ya klabu yao kutotumia usafiri wa ndege kutua Kongo. Wako ambao sio mashabiki wa mazembe lakini pia hawamuungi mkono Kabila lazima watalichukulia kwa mihemko ya juu kwasababu linaonekana ni jambo la kisiasa. Hata wale Mashabiki wa Fc Lupopo, Darling Club Motema Pembe,Don Bosco hata As Vita wataona kama kilichotokea kwa wapinzani wao sio 'fair' kwa taifa ambalo linajua nini maana ya soka.

Ifike mahali viongozi wa nchi watambue soka ni kama dini maana ni utamaduni ambao watu wameutithi Tangu miaka iliyopita. Wasiwe wanapenda kuitumia tu michezo kujitangaza katika kupata kura za wapiga kura wao pia watambue kama ni sehemu ambayo watu huwekeza na kutoa ajira kwa watu.
Hata hapa Tanzania tuliona mapema kabisa katika maandalizi ya msimu wa ligi kuu klabu ya Njombe Mji ilipata changamoto kutoka kwa viongozi wa kiserikali katika Mkoa wa Njombe waliposema rangi ya jezi zao inafanana rangi za bendera ya chama kikuu cha upinzani nchini. Na walikagaa kuhudhuria sherehe za utambulisho wa klabu hiyo kwa mashabiki na wadau wa soka Njombe.Hizo ndio fikra mgando mbazo zinafanya watu kama rais Kabila aone kuwanyima wasaa wa kuserebuka katika uwanja wa ndege mashabiki wa mazembe ni kumkomoa kiongozi wa upinzani.

Wanasiasa wamekuwa waharibuji wakubwa utamadumi na ustarabu wa soka letu Mara nyingi duniani kote. Hata sakata la Wakatalunya ni siasa tu ambayo almanusura itukimbizie 'el clasico' . soka ni zaidi ya kucheza uwanjani linarudisha imani ya waliokwazana na kugombana linawaweka pamoja wanasiasa wenye upinzani mkubwa kisiasa. Lakini ni hatari kama kiongozi mkuu kama kabila kuingia katika 'skendo' ya kuwanyima ndege TP Mazembe na kujikuta wakikaa uwanja wa ndege Kwa masaa kumi kisa mambo binafsi ya kisiasa. Hapo anajiharibia mwenyewe.

0628994409

No comments:

Post a Comment

Maoni yako