August 19, 2007

BUNGE; Somo la uraia limepotea..

MOYO KABLA YA SILAHA......
Hakuna asiyefahamu kwamba hivi sasa habari za mbunge Zitto Kabwe zinarindima kila kona ya nchi kwani kusimamishwa ubunge imekuwa kama wanachochea nguvu ya raia kukubali kwamba bunge letu limepoteza somo mahiri la uarai.

Hivi tatizo ni lipi hasa hadi tunaogopa kuwa na tume hiyo aliyopendekeza?
kwani kujua ukweli uko wapi kwa porojo za siku hiyo zinaweza kumaliza nguvu za chama tawala? kushushwa hadhi maana yake nini?kwani ukishushwa hadhi unaweza kufa?

Haya mwingine alishatanguliza adhabu kabla hata Big bunge hajatoa uamuzi,bila shaka alipangwa huyo,wazee wetu hawatujali tena ni wakati wa mapinduzi sasa,ewe kijana simama usiogope,umasikini wako si tija bali nguvu zako na hekima zako zikuondoe katika utumwa,pesa si kila kitu bali moyo wa huruma kwakizazi kinachokuja.

Tuache ushabiki kwa suala hili;kwanini mkataba usainiwe wakati Rais alishasema kwamba hakuna kufanyika hilo hadi mikataba mingine ipitiwe upya?Nini maana ya kwenda kusainiwa London? Haijalishi kwamba ilikuwa hotelini au wapi ilahoja kwanini ilifanyika huko?.

Toa maoni..uspitwe
uhuru daima

No comments:

Post a Comment

Maoni yako