September 27, 2008

kwa wanaotaka kwenda majuu - III

kila la heri mnaotaka kwend majuu ila mjue wala sichukii na wala sina kinyongo. Msidhani nawaonea wivu kwani najua kimsingi wivu humuua mtu mjinga. Mbinu za kutaka misaada na yale ya BRAIN DRAIN saswa tu hakuna maneno msidhani nawashambulia.Sina uuwezo wa kuwashambulia mimi binadamu mwenye nafasi ndogo katika maisha yako.Ninachosisitiza ni kwamba nenda ughaibuni kwa mipango,jiandae,kuwa mkamilifu,soma tamaduni zao,kuwa mwangalifu,amini kwamba mipango,jiwekee malengo huko uendako,usidanganyike na wapenzi/mapenzi/mpenzi..lakini kuwa makini kwa kila hatua.

2 comments:

  1. nakubaliana nwe ni kweli lazima uwe na malengo unaenda kufanya nini sio tu eti naenda ulaya je unakazi au kwani jamani ulaya ni jina tu ulaya kuishi ulaya au kwenda ulaya hakuna lolote si mnaona wenyewe walivyojaa Afrika yetu kwa nini? Ndiyo kwa sababu maisha rahisi, kwa sababu tuna ukarimu ambao wao hawana. Najua wengi wenu mtasema we si unasema tu kwa sababu mwenyewe upo huko. Ni kweli lakini ndo nawaambieni ukweli kwani kila siku naona watu wanavyoteseka kupata riziki zao za kila siku. Huku ndugu zanguni hakuna kusaiidiana, Nasema kama alivyosema kaka Markus sio kwamba nawatisha au nawonea wivu au wengine watasema anataka afaidi yeye tu HAPANA. Pia nasema kila la heri.

    ReplyDelete
  2. unakumbuka mateso ya mababu hawa?

    ReplyDelete

Maoni yako