January 11, 2009

CO.MMENTS + BLOGLINES= mambo mapya

Jana niliandika kuhusu huduma ya Aggregators/Bloglines kisha nikasema unaweza kurahisisha mambo kwa huduma hizo. Lakini nikatoa anuani ya kusoma zaidi mambo hayo ya www.mwongozo.wordpress.com Sasa leno niseme hii CO.MMENTS na BLOGLINES pia. Huduma ya CO.MMENTS ni tamu sana, nayo inakuletea habari mpya kuhusu maoni uliyoyaacha mahali/katika blogu uliyoacha MAONI.
Huduma hii inachofanya ni kukupa taarifa mpya toka sehemu ulizoacha maoni, mfano umetembelea blogu ya Koero kisha ukaacha maoni wakati huohuo unataka kujua wasomaji au wanablogu wengine watasema nini juu ya maoni uliyotoa, kawaida unachofanya ni kurudi pale ulipoacha maoni ya wengine kuendeleza mjadala.
CO.MMENTS inakusanya maoni yote mapya toka mijadala unayoshiriki na kukuletea katika akaunti yako. Kwetu TZ tunajua baadhi yetu tunategemea huduma za kulipia kwahiyo suala la MUDA ni muhimu sana, kwani unaweza kutembelea blogu 25 halafu hazina mambo mapya.
Huduma ya CO.MMENTS na BLOGLINES zinakusaidia kukusanya habari mpya na MAONI mapya toka kwenye idadi yoyote unayotaka hata 100 na kukuletea katika ukurasa mmoja.
Sasa hii huduma ya CO.MMENTS inakupatia fursa ya kujua blogu zote ulizopitia na kuacha MAONI wapo wasomaji au wanablogu wamechangia, kwahiyo maoni yao yanakuwa yanakusubiri uyasome ili kuendeleza mjadala.
Binafsi nimejaribu hiyo, na napata taarifa za maoni katika akaunti yangu kila ninapoacha maoni mapya katika blogu yoyote, na nimeanzia kwa dada Koero na mengine nitayapata. NB: ili kujiunga na huduma hii unajiunga na BLOGLINES kwa urahisi hapa www.mwongozo.wordpress.com nyingi sana kuhusu huduma hizo.

3 comments:

  1. Mkuu naona unaendeleza darasa.
    Kazi nzuri sana.

    Keep it up!

    Blessing......

    ReplyDelete
  2. now I see it!

    ReplyDelete
  3. в конце концов: благодарю. а82ч

    ReplyDelete

Maoni yako