June 02, 2009

BURIANI> wana PAN AFRICANISM na PAN LOCALISATION

Tangu juma lililopita nilijulishwa na rafiki tangu wa karibu aliyeko nchini Kenya. Alinidokeza saa chache baada ya ajali iliyomwondoa mwanamapinduzi huyu na mwezeshaji wa MDs pale jijini Nairobi. Ni TAJUDEEN ABDUL-RAHEEM. kwa hakika nitazikosa kazi zake nyingi katika medani za uchambuzi wa mambo ya kiafrika, nitakosa na na kusikitika kama nilivyosikitika kwa muda wa juma zima huku nikitafakari kuwa kifo ni kitu gani. Lakini mwanafalsafa Socrates anatuonya kuhusu kuogopa kifo ni ujinga kwa kudhani tuna busara kuliko mungu.
Juma zima nilikuwa najaribu kuwaza kuhusu mwanamapinduzi huyu na ajali iliyomtoa duniani. Mungu mkubwa yupo nasi, kama ajali ni majaliwa yake basi hatuna neno,lakini kama siyo majaliwa yake basi tunazidi kumwombea mema. AMEN

No comments:

Post a Comment

Maoni yako